Makundi ya wanaopinga ndoa na maisha ya ndoa

Makundi ya wanaopinga ndoa na maisha ya ndoa

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Hali inazidi kuwa mbaya kwa vijana wetu hasa hawa wa kiume wanahamasishana kila kona na kampeni yao yenye hashtag #KATAA NDOA

Sababu wanazotoa zinachekesha mno na kwakweli hazina mashiko.. Kubwa ikiwa ni kuogopa kusalitiwa lakini pia kuna la uchoyo na kukwepa majukumu ila haya hawayasemi kwa uwazi

Hili jambo ni kama fasheni yenye mass hallucination ndani yake! Itapita lakini inaweza kuacha madhara kwa wengine hivyo hatuwezi kukaa kimya

Haya ndio makundi yao

1. Wasiojiamini
  • Hawaamini kama wanaweza kutunza mke kutokana na story za vijiweni
  • Hawaajiamini kama wanaweza kumridhisha mwanamke kitandani
  • Hawajiamini kama wanaweza kutulia kwenye ndoa bila kuwa na vimada
  • Hawajiamini kwamba watapendwa na hawawezi kusalitiwa!

2. Wenye kasoro za kimaumbile
  • Wanaojihisi ni vibamia
  • Wanaojihisi hawawezi kumpa mwanamke ujauzito
  • Wasiotahiriwa
  • Wagumba kwa ithibati

3. Waathirika kisaikolojia
  • Kutokana na makuzi mabaya
  • Kutokana na malezi mabovu
  • Waliolelewa na walezi katili
  • Walioathirika na punyeto
  • Walioumizwa kimapenzi
  • Waliosalitiwa

4. Wasela na wakaa geto
  • Maisha hayajasimama
  • Wanaishi kwa kuungaunga
  • Wasiopenda majukumu

5. Wenye kasoro za kijinsia
  • Mashoga wa kujificha (mchicha mwiba)
  • Madomo zege
  • Wenye ulemavu uliojificha

6. Wapenda kitonga, dezo
  • Wanaolelewa na wake za watu
  • Wanaotunzwa na mashangazi
  • Wanaopenda vya bure toka kwa yeyote
  • Wapenda shortcut
  • Wavivu wasipenda kujishughulisha
  • Wapenda starehe
7. Bendera fuata upepo
  • Wanashadadia tu kwasababu fulani kasema
  • Wanafuata mkumbo kwakuwa fulani yumo
  • Wanadhani ndio usasa na ndio ujanja
Washauri wao wakuu
  • Walioshindwa kuhimili changamoto za ndoa
  • Walioachwa, waliopigwa kibuti
  • Walioharibu kwenye ndoa zao
  • Wapotoshaji
Nisiandike sana ngoja niweke kituo hapa
 
Ndoa ni nini?

Ndoa ni muunganiko kati ya mwanamume na mwanamke, walio amua kwa ridhaa yao wenyewe kuishi pamoja kama mke na mume mpaka mwisho wa maisha yao ya ndoa.

Aina za ndoa kwa mujibu wa sheria

Kuna aina mbili tu za ndoa zinazotambulika na sheria ya ndoa Tanzania

Ndoa ya mke mmoja na mume mmoja tu.
Ndoa ya wake wengi.
Ndoa hizo zinaweza kusheherekewa kufuatana na misingi na taratibu za kidini, kimila au kiserekali, kushuhudiwa na watu wasiopungua wawili na kusajiliwa kwa mujibu wa sheria.

Hatua za kuchukua kabla ya ndoa kufungwa

Lazima taarifa ya nia ya kufunga ndoa itolewe siku 21 kabla ya ndoa kufungwa, kama kutakuwa na mwenye pingamizi budi litolewe itoe kabla ya ndoa kufungwa
Majina ya wale wanaotarajia kufunga ndoa, umri, majina ya wazazi wao na mahali wanapoishi yatajwe.
Tamko kwamba wanaotarajia kufunga ndoa hawana uhusiano unaokatazwa kisheria kufunga ndoa
KUSAJILI NDOA

Ndoa inaweza kufungwa Kiserikali au kwa madhehebu ya Kikristo au Kiislam au kufuatana na mila na desturi za wale wanaofunga ndoa.

Msajili wa ndoa atatoa cheti cha ndoa. Kila Ndoa inapofungwa lazima iwe na mashahidi wawili

Mambo ambayo sheria ya ndoa inakataza katika suala zima la kuoa au kuolewa

Mwanamke na au mwanaume kuolewa/kuoa bila ridhaa yake mwenyewe
Mwanamke na mwanaume wenye undugu wa damu kuoana
Mwanamke na mwanaume kuoana kabla ya kutimiza umri unaoruhusiwa kisheria (kwa mwanaume miaka 18 na kwa mwanamke miaka 18 au 15 kwa idhini ya wazazi/mlezi wake)
Kuoana watu wa jinsia moja
Mwanamke na mwanaume kutaka kuoana kwa mkataba wa kipindi maalum.
Haki za mume na mke katika ndoa

Wote wana haki ya kumiliki mali kama nyumba, shamba n.k. kwa majina yao binafsi;
Wote wana haki ya kutoa idhini katika uuzaji au kwa pamoja kuweka dhamana mali yoyote ya familia;
Wote wana haki ya kuishi katika nyumba ya familia iwapo mume/mke amemkimbia;
Mke ana haki ya kupewa matunzo yake na ya watoto wakati wa ndoa au iwapo mume amemkimbia, wameachana kwa amri ya mahakama. Na mume ana haki ya kupewa matunzo iwapo ana ulemavu hawezi kujiingizia kipato kutokana na ulemavu au ugonjwa wake;
Wote wana haki ya kutokupigwa na au kufanyiwa ukatili wa aina yoyote;
Wote wana haki ya kupeana unyumba;
Wote wana haki ya kutumia mali ya ndoa;
Wote wana haki kuomba amri ya talaka.
Ukomo wa ndoa Ukomo wa ndoa uko wa aina mbili:

Kifo cha mwanandoa mmoja wapo
Talaka ambayo imetolewa na Mahakama pekee pale inapojiridhisha kwamba kuna sababu ya msingi kufanya hivyo.
Baraza la usuluhishi la Ndoa

Baraza la usuluhishi la Ndoa, ni baraza lililoanzisha na kifungu 102 cha Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971, sura ya 29 kama sheria zilizopitiwa mwaka 2002, kwa madhumuni ya kusuluhisha wanandoa ambao wanaingia kwenye migogoro ya Ndoa. Kazi za Baraza la Usuluhishi la Ndoa:-

Kusuluhisha Wanandoa walioko kwenye Ndoa baada ya kupokea lalamiko toka kwa mmoja wapo wa Wanandoa
Kutoa hati maalum kuthibitisha kuwa suluhu imeshindikana na kuelekeza wanandoa kwenda Mahakamani kwa amri zaidi.
MUHIMU: Mahakama peke yake ndiyo ina mamlaka ya kutoa amri ya kutengana au talaka

Sababu zinazopelekea au kuishawishi mahakama kuvunja ndoa:-

Uzinzi kati ya wanandoa
Ukatili kati ya wanandoa au watoto wa ndoa
Dharau au kupuuza kulikokidhiri dhidi ya mwenzi
Kumtelekeza mwenzi kwa zaidi ya miaka mitatu Pale mwenzi anapofungwa kifungo cha maisha au kwa kipindi kisicho pungua miaka miaka mitano
Ikiwa mwenzi ameugua ugonjwa wa akili na imedhibitishwa na daktari kwamba hakuna uwezekano wa kupona.
Kubadili dini baada ya ndoa kufungwa pale wanandoa wote walikuwa wakifuata imani ya dini moja.
Haki za wanandoa zinazoambatana na amri ya talaka

Mgawanyo wa mali za ndoa /familia
Matunzo ya mke Hifadhi na matunzo ya watoto
Kizuizi cha kutobugudhiwa
Kuoa/Kuolewa tena
Fidia ya uzinzi
Gharama za kuendesha Shauri la Talaka
Haki ya Mgawanyo wa mali za familia/ ndoa Mali yoyote ambayo imepatikana wakati wa uhai wa ndoa na kwa nguvu na au machango wa pamoja wa wanandoa.

Iwapo mali iliyopatikana na mwanandoa mmoja wapo kabla ya ndoa au kwa nguvu zake mwenyewe lakini imeboresha/imetunzwa na mwanandoa mwingine mali hiyo itatambulika kama mali ya ndoa.

Lakini kama kuna mali yoyote ambayo mwanandoa mmoja amempa mwanandoa mwenzake kama zawadi, mali hiyo itakuwa ya yule aliyepewa pekee.

Aina za mchango

Kutekeleza kazi nyumbani hasa kutunza familia; mfano kuosha vyombo, kupika, kufua nguo, kubeba maji na kazi zingine zinazofanana na hizo kwa maslahi ya familia.

Kutunza mali za ndoa: mfano kufyeka, kulima, kuvuna shamba, kufanya marekebisho ya mali za ndoa kwa maslahi ya familia.

Mchango wa fedha wa mwanandoa katika kununua mali.

Haki ya Matunzo ya mwanandoa

Jukumu la kutoa matunzo kwa mke na watoto ni la mume, jukumu hilo litatekelezwa wakati wa uhai wa ndoa na baada ya talaka.

Haki ya Hifadhi na matunzo ya watoto

Hifadhi ya watoto hutolewa kwa mume au mke au mtu baki (mlezi) hasa kwa kuzingatia ustawi na maslahi ya wale watoto. Zaidi ya hayo, mahakama pia inaweza kuzingatia yafuatayo:

Umri wa wale watoto, mfano, watoto walio chini ya miaka saba kipaumbele cha hifadhi hupewa mama mzazi; labda kama kutakuwa na sababu za msingi za kuto fanya hivyo. Mfano kama mama mzazi ana matatizo ya kiakili, anaishi katika mazingira hatarishi.

Mazingira ya mahali watakapoishi watoto, mfano, kama mazingira ya upande mmoja ni hatarishi kwa ustawi wa mtoto, basi haki ya hifadhi atapewa mzazi mwingine bila kujali umri.

Matakwa ya wazazi wa mtoto nani kati yao angependa kupewa hifadhi ya watoto

Mila na desturi za jamii ambayo wanandoa wametokea.

Kama mtoto anaumri zaidi ya miaka saba na ana uelewa wa kutoa mapendekezo yake, basi matakwa/maoni yake yatasikilizwa zaidi.

Haki ya hifadhi ya mtoto haimnyimi mzazi mwenza haki ya kumuona na au kumtembelea mtoto/watoto. Haki ya hifadhi ya mtoto haiondowi jukumu la baba kutoa matunzo.
 
Wakataa Ndoa a.k.a Mchicha mwiba njooni huku.

IMG_20220914_180443_804.jpg
 
Binafsi siungi kampeni ya kataa ndoa,kwasababu ninaamini familia bora lazima iwe na msingi wa baba na mama,

ila hizo sababu ulizoziandika hapo juu itakuwa ni mtazamo wako tu,maana haujaandika kwa kuchambua kwa kina,umeandika kiushabiki ule wa simba na yanga,tegemea wapingaji wengi kwenye huu uzi wako tena kwa hoja za uzito,

kama kweli ulikuwa na nia ya kuwaelimisha watu kuhusu umuhimu wa ndoa hukupaswa kuandika kimipasho hivo kwa kutegemea uungwaji mkono kwa member wengi ambao wanaunga mkono kuhusu ndoa,

ulipaswa uelezee umuhimu na faida za kuwa kwenye ndoa pia ungeelezea hasara ya kutokuwa na ndoa
 
Mwanaume rijali hawezi kuthubutu kupinga ndoa isipokuwa yule mwenye vinasaba vya ushoga.
Unaishi dunia ipi? Urijali haupimwi kwa ndoa maana hata mashoga wanaoa. Urijali hupimwa kwenye tendo lenyewe (ambalo hupatikana kirahisi hata nje ya ndoa) na namna mwanaume anavyoweza kupambana kimaisha.

Hao wake zenu kutwa wanachapwa na madogo mtaani, kama mngekuwa marijali kweli si mngewatuliza!?

Tunawaona wengi wenu mliooa mnashinda Bar mpaka night kali, mnarudi makwenu usiku mnene kulala tu kama ndoa zingekuwa na hiyo raha mnayohubiri msingejificha Bar na kwenye vijiwe usiku mnene.

#NDOANISTRESS #NDOANIUTAPELI
#KATAANDOA
 
Back
Top Bottom