Mama amshauri mwanaye kuacha kazi kisa ndoa

Mama amshauri mwanaye kuacha kazi kisa ndoa

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, mama mzzazi amemshauri binti yake kuacha kazi ili kumfuata nume wake ambaye amehamishwa kikazi kwenda mkoa mwingine.

Kituko hiki kilitokea mnamo mwaka jana baada ya mume huyo kuhamishwa kutoka mkoa wa nyanda za juu kusini keenda mkoa wa kanda ya ziwa. Mume alipopata uhamisho, mke wake mwenye mtoto mmoja, ,aliyeolewa yapata miaka 3 iliyopita, alijaribu kuomba uhamisho ili kumfuata mumewe lakini waajiri wake walionekana kuchelewesha uhamisho wake wakati yeye aliomba kumfuata mumewe haraka iwezekanavyo.

Alipoona uhamisho unachelewa alimuendea mama yake mzazi kumuomba ushauri nini afanye. Bila kumumunya maneno, mama yake alimshauri kuacha kazi mara moja. 'Mume wako yupo kanda ya ziwa, wewe upo kanda ya nyanda za juu, hapo hakuna ndoa. Kama uhamisho wako unachelewa, acha kazi mara moja umfuate mumewe; shauri yako!' Alisikika mama akimshauri mwanaye.

Bila kusita, binti aliandika barua ya kuacha kazi yake ya uhasibu (senior accountant (CPA) na kumfuata mume. Sasa hivi ninapoandika uzi huu, huyo mwanamke ni mama wa nyumbani na hana namna ya kuajiriwa tena kwani umri wake umesogea.

MAONI YANGU
Hivi akina mama kuna wakati wanafikiri kwa kutumia kiungo cha chini tu au ni namna gani wenzangu? Inakuwaje mama amshairi senior accountant kuacha kazi na yeye kweli anamsikiliza mama na kuacha kazi? Akina mama wamerogwa na nani hasa?

Huu ushauri ungetolewa kwa mwanaume nina hakika angeupuuzilia mbali. Kwa kuwa akina mama alkili zao zinaishia kwenye urefu wa pua zao, ndio maana wanaweza kushawishika kuacha kazi kwa sababu tu ya kufuata m.b00 ambayo hata ichepuke kiasi gani haiishi.

Je, ingekuwa wewe mwanaJF ndiye umepewa ushauri wa aina hii, ungemsikiliza mama yako au ungetupilia mbali ushauri wake?
kwani Huko alikoenda amekwambia hatafanya kazi yoyote? Maisha Sio kukariri. Fursa ziko.nyingi ukichangamsha fuvu.
 
Kwahiyo wewe unaamini maisha ni kuajiriwa tu ?

Huyo mama yupo logically kukuzidi wewe katazama mbali na kaangalia the future of her daughter in long run benefits


Mimi Dada yangu aliacha Kazi na kutoka ulaya kumfata mwanaume Tz na Leo she is well of

So kuna wanaume ni potential Sana usiwe na fikra za kimasikini kuwa Kazi ni kuajiriwa serikalini tu.
Kiinglish logical or logically?
 
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, mama mzzazi amemshauri binti yake kuacha kazi ili kumfuata nume wake ambaye amehamishwa kikazi kwenda mkoa mwingine.

Kituko hiki kilitokea mnamo mwaka jana baada ya mume huyo kuhamishwa kutoka mkoa wa nyanda za juu kusini keenda mkoa wa kanda ya ziwa. Mume alipopata uhamisho, mke wake mwenye mtoto mmoja, ,aliyeolewa yapata miaka 3 iliyopita, alijaribu kuomba uhamisho ili kumfuata mumewe lakini waajiri wake walionekana kuchelewesha uhamisho wake wakati yeye aliomba kumfuata mumewe haraka iwezekanavyo.

Alipoona uhamisho unachelewa alimuendea mama yake mzazi kumuomba ushauri nini afanye. Bila kumumunya maneno, mama yake alimshauri kuacha kazi mara moja. 'Mume wako yupo kanda ya ziwa, wewe upo kanda ya nyanda za juu, hapo hakuna ndoa. Kama uhamisho wako unachelewa, acha kazi mara moja umfuate mumewe; shauri yako!' Alisikika mama akimshauri mwanaye.

Bila kusita, binti aliandika barua ya kuacha kazi yake ya uhasibu (senior accountant (CPA) na kumfuata mume. Sasa hivi ninapoandika uzi huu, huyo mwanamke ni mama wa nyumbani na hana namna ya kuajiriwa tena kwani umri wake umesogea.

MAONI YANGU
Hivi akina mama kuna wakati wanafikiri kwa kutumia kiungo cha chini tu au ni namna gani wenzangu? Inakuwaje mama amshairi senior accountant kuacha kazi na yeye kweli anamsikiliza mama na kuacha kazi? Akina mama wamerogwa na nani hasa?

Huu ushauri ungetolewa kwa mwanaume nina hakika angeupuuzilia mbali. Kwa kuwa akina mama alkili zao zinaishia kwenye urefu wa pua zao, ndio maana wanaweza kushawishika kuacha kazi kwa sababu tu ya kufuata m.b00 ambayo hata ichepuke kiasi gani haiishi.

Je, ingekuwa wewe mwanaJF ndiye umepewa ushauri wa aina hii, ungemsikiliza mama yako au ungetupilia mbali ushauri wake?
Mbona unaumia hivyo mke kumfuata mme wake? Ulikua unafukuzia?

Mama na mtoto wake wote wako sahihi asilimia zote.
 
Mkuu maisha na uchumi wa Norway huwezi kuyafananisha na maisha ya mchongo ya bongo. Huyu mama kampoteza mwanaye kwa kumshawishi kuacha kazi kwa ajili ya kutumikia m.boo. Hii ni mbaya sana.
Mafunzo ya ndoa yanasema, mume na mke ni mwili mmoja, njaa zetu zisitufanye kuwa watumwa tukavunja ndoa zetu. Bora uridhike na shilingi 10 kukiwa na utulivu ndani ya ndoa, kuliko kuwa na mamilioni na migogoro ya ndoa pamoja na maradhi.
Pia kuajiriwa wote ni utovu wa nidhamu kwa nini wasijiajiri? Pia hakuna tajiri aliyeajiriwa.​
 
Mtoa mada huyo mwanamke ni nani kwako mbona unaonekana umekwazika sana katika jambo lisilokuhusu? Ndoa ni ya wawili na wanamakubaliano iweje wewe uumie kiasi hicho??
 
Mtoa mada alitegemea supports,ila amejikuta kabanwa mbavu!halafu kumbe mleta mada ni kataa ndoa na age bado ya kitoto
 
MAONI YANGU
Hivi akina mama kuna wakati wanafikiri kwa kutumia kiungo cha chini tu au ni namna gani wenzangu? Inakuwaje mama amshairi senior accountant kuacha kazi na yeye kweli anamsikiliza mama na kuacha kazi? Akina mama wamerogwa na nani hasa?

Huu ushauri ungetolewa kwa mwanaume nina hakika angeupuuzilia mbali. Kwa kuwa akina mama alkili zao zinaishia kwenye urefu wa pua zao, ndio maana wanaweza kushawishika kuacha kazi kwa sababu tu ya kufuata m.b00 ambayo hata ichepuke kiasi gani haiishi.

Hofu ya vitu kama hivi kutokea

1723149405709.png
 
Kama familia yote inajiweza kwanini asiache kazi na kumfuata mumewe?.

Umasikini ndio chanzo wanawake kuwa watafutaji.
Muwe mnafikiria na mambo menginè. Maisha huwa yanabadilika, kuna kuachishwa kazi, biashara kuyumba, magonjwa,kifo, mke kuachwa ataenda wapi.
Muache ubinafsi wakati mwingine.
 
Mchawi ni wewe unaefuatilia maisha ya watu kwa kiwango cha lami na kuja kuwabeza JF
 
Kuacha kazi kunaweza kuwa chachu ya maendeleo na afya njema. Yumkini kazini kuna madhila mengi ambayo hayavumiliki. Utumwa uliofundishwa katika vitabu vya historia unafanywa makazini na viongozi wasio na utu na wanaojivisha ufedhuli na wasiojali utaalam na umuhim wa mtu. Kumfuata mume/mke ni kigezo cha uhamisho kwani uhai wa taifa lolote huanzia kwenye familia imara.
Pili, hii ni kwa wafanyakazi wote ikiwa alifanya kazi kwa ujuzi, anaweza kuibadili akili ileile na kufanya makubwa katika sehemu aliyopo. Fursa inatembea na mtu. Asiogope watu wanamuonaje.
 
We jamaa unaona kazi ndio kila kitu kwenye maisha yako

Pole sana
Sasa wewe mkuu unaona ndoa ni kitu cha kuchukulia umuhimu kiasi hicho? Ndo si ni utapeli tu?
 
Kwanza, hakukuwa na ulazima wa yeye kuharakia kuacha kazi badala yake angesubiri uhamisho hata kama ungechukua mwaka.

Watu mpaka mnafikia hatua ya kufunga ndoa mnapaswa kuelewa utafika wakati kutakuwa na utengano iwe kikazi au kiafya (ugonjwa n.k)
Hivyo suala la kuhamishwa mume kikazi sio la ajabu wala haliwezi kuonekana kama tatizo.

Vipi kama mume huyohuyo akipangiwa kwenda masomoni nje ya nchi? Hatoenda sababu ya ndoa?

Nafikiri ndoa ni uvumilivu, uaminifu na maelewano. Kuhamishwa kikazi ni jambo dogo sana mke kuacha kazi harakaharaka kumfuata mume.
Mkuu umemaliza kila kitu. Naomba nikutunuku PhD ya heshima Dokta Nifah .
 
Kumtunza mwanamke ni wajibu wa mwanamme.

Ni umasikini tu kwa mwanamke kufanya kazi kama mwanaume,yeye ni pambo la nyumba wakati wote anatakiwa awepo nyumbani.

Hana haja ya kufanya kazi.

Mama yupo sahihi.
 
Hapo ilitakiwa maamuzi ya busara sana kwa sababu mama ameona ndoa ni bora kuliko kazi, lkn swali je mume akifa ?

Je wakitalikiana?

, bint baada ya kushauliwa vile angeomba ushauli kwa ndugu wengine hasa kaka zake na angemshiliksha mumewe,

Hapo jamaa walitaka pesa,

Ndio maana huwa ninaambia vija wangu sio kila ushauli wa mzazi wa kuusikiliza unatakiwa utumie akili zako
 
Kama wanaishi vizur we unaumia nini? Au ndo ulikuwa mchepuko wake. A ndo ulikwamisha uhamisho?

Kazi zipo na yalianza Maisha kabla ya kazi

Familia ni bora kuliko mali
 
Back
Top Bottom