Mama Samia ameanza vibaya kwa kupuuza kuvaa Barakoa

Mama Samia ameanza vibaya kwa kupuuza kuvaa Barakoa

Dr John Pombe Magufuli hakua wa kufa leo wala kesho ; tatizo kubwa ni ile hali aliyoiweka na washauri wake kushindwa kuhakikisha Daktari wa Rais anakuwa na msimamo...
Niseme kwa ufupi tu mkuu Phillemon Mikael,

Tunao madaktari wazuri sana ndani ya nchi hii, tena wengi wao ni waliohitimu hapahapa nyumbani na kuendelea kufanya kazi kwenye mazingira ya ukosefu wa vifaa vya kuionyesha dhahiri umahiri wao.
Wapo wazuri kabisa, kama ilivyo katika nyanja zingine kote hapa nchini.

Tatizo kubwa sana, na kwa bahati mbaya, limekuwa ni siasa kuwa kila kitu.

Ukichunguza vizuri, utaona wakati wote wa uwepo wa Magufuli kwenye utawala, siasa ndiyo ilikuwa sauti ya mwisho kwa kila kitu.

Ukichanganya na kiburi chake, hata hao madaktari waliokuwa wamemzunguka wakawa ni wa kupima upepo wake unavuma kuelekea wapi.

Hebu fikiria haya mambo ya kujifukiza dhidi ya corona - Muhimbili na Mloganzila zikalazimika kuweka Sauna Spa, kila moja yenye gharama siyo chini ya milioni saba!

Ni daktari gani aliyethibitisha kwamba sauna inatibu corona?

Naungana nawe moja kwa moja kusema kwamba Magufuli kwa hali ya kawaida ya ugonjwa wake unaofahamika, hakuwa mtu wa kufa wakati huu.

Lakini unaona jinsi wanavyoendelea kuvungavunga na kuhadaa watu kwa kupindisha ukweli?

Sijui wanaendelea kufanya ujinga huu kwa manufaa ya nani hasa. Mtu aliyeshupalia jambo lenyewe hayupo tena. Wangetumia nfasi hii kuwahimiza wananchi kuchukua tahadhari juu ya ugonjwa huu.
Badala yake, wao wanaendelea kueneza ujinga.

Nililotaka kuanza nalo katika kujibu bandiko lako ni hili: Tanzania haiko mbali sana na jina la "Banana Republic."

Tunapodharau kutofuata taratibu; tukawa watu wa kujipigia tu bila mpangilio maalum, hali hiyo ni vurugu tupu.

Hili ninalolisema hapa unaweza kuliona hata katika mpangilio mzima wa maombolezi haya tuliyonayo sasa hivi.

Ni hali ya kuogopesha sana inayoweza kulikabili taifa. Omba sana tusikabiliwe na janga kubwa zaidi ya huu msiba tulioupata kabla hatujaanza tena kuwa watu wenye kufuata taratibu maalum katika utendaji wetu.
 
Ndio hali halisi kwa hiyo aje na suluhu au ushauri utakaomaliza au kubadili mindset za watu
Sio kulalama tuu
Unajuwa wazi ni nani mwenye wajibu huo.

Kwa hiyo inamaana hujaelewa hata swali moja nililokuuliza hapo juu, au huna uwezo wa kujibu chochote.
 
Unajuwa wazi ni nani mwenye wajibu huo.

Kwa hiyo inamaana hujaelewa hata swali moja nililokuuliza hapo juu, au huna uwezo wa kujibu chochote.
Mwenye wajibu huo umeamua kutumia njia nyingine basi mtumie njia sahihi kufanya nae mjadala au nanyi mumwache na maamuzi yake
 
Tarehe 19.05.2020 wakati Tanzania ikikabiliwa na wimbi la kwanza la janga la korona, nilichapisha uchambuzi wa kiintelijensia kuhusu mustakabali wa urais wa Magufuli kwa jinsi "alivyozembea" kushuguhulikia janga hilo...
Ushauri Mzuri Mtumishi wetu Jasusi.
 
Mwenye wajibu huo umeamua kutumia njia nyingine basi mtumie njia sahihi kufanya nae mjadala au nanyi mumwache na maamuzi yake
Uzuri ni kwamba hakuna namna - watu wengine hupenda njia ngumu katika kujifunza jambo rahisi.

Sisi tumeamua njia ngumu itakayotugharimu, lakini mwisho wa siku tutakuwa tumejifunza kwa gharama kubwa.

Uzuri ni kwamba wanaolipa gharama si wananchi wa kawaida tu..., kwa hiyo ni majonzi yetu sote.

Nisiendeleze mjadala nawe usioenda kokote; nimalizie tu kwa kuandika haya:
Samia na kundi lake lote hawana namna.

Ni swala la muda mfupi tu toka sasa, akili zitakuwa zimewaingia kichwani na mambo yatabadilika. Uvaaji wa barakoa ni jambo dogo sana, kama huko kusalimiana kwa kutoshikana mikono.
Wki mbili tatu zifuatazo uvaaji wa barakoa litakuwa jambo la kawaida tu kwa viongozi hawa, na wananchi wataiga kuanzia hapo.

Mama Janet tayari amekwishaonesha mfano.
 
Kwa kauli za huyu jamaa maana yake usipotambua covid lazima ikuue hii project kwa Tanzania nadhani wakubali imefeli waanzishe project nyingine
Usimpotoshe mama Samia jiwe kasepa. Alijifanya kichwa ngumu vovid imempeleka jehanamu.
 
Aendelee hivyohivyo kutokuvaa barakoa ili parapanda ziwe nyingi Tanzania tupate kuingia kwenye World Guinness Book of records , hapa tulipo kuna minister amerest in peace , but they didn't made it public .
 
Wote tunafahamu namna hayati John Pombe Magufuli rais aliyetangulia mbele ya haki alivyopinga au kukataa kukubali kuwa Covid-19 ni janga.

Nilipomuona mjane wake amevaa barakoa nikatia akilini. Tusicheze na dudu hili tutaangamia hasa tokana na mikusanyiko ya kuaga ambayo haina hata chembe ya tahadhari.

Hivyo, mama tangaza janga haraka uokoe wengi mama yangu nakuomba chonde chonde. Usiweke lockdown angalau uamrishe watu wavae mabarakoa.

Hilo ndilo ombi la mwananchi wako toka Kimanzichana mama yangu.
 
Kwa jinsi mikusanyiko inavyofanywa tena kizembe na kipuuzi bila kuvaa barakoa wala kuweka distance, zoezi hili kuanzia jana mpaka siku ya maziko itakuwa kasheshe.

Hongereni mliopamiana na kusukumana huko kwenye kuaga mwili wa marehemu bila kuvaa barakoa. Mwezi April mtauanza vizuri sana kwa nyungu/vitunguu/tangawizi na majeneza.

Ila kila ninae mdai ambae ameenda leo kwenye kuaga mwili wa marehemu, ntahakikisha week hii ananilipa kabla ya kufika April. Maswala ya kusamehe madeni kwa marehemu aliejitakia SITAKI HUO UPUUZI!!!
 
Si ilishatangazwa mwaka jana na shule zikafungwa?
 
Kwa jinsi mikusanyiko inavyofanywa tena kizembe na kipuuzi bila kuvaa barakoa wala kuweka distance, zoezi hili kuanzia jana mpaka siku ya maziko itakuwa kasheshe.

Hongereni mliopamiana na kusukumana huko kwenye kuaga mwili wa marehemu bila kuvaa barakoa. Mwezi April mtauanza vizuri sana kwa nyungu/vitunguu/tangawizi na majeneza.

Kila ninae mdai ambae ameenda leo kwenye kuaga mwili wa marehemu, ntahakikisha week hii ananilipa kabla ya kufika April. Maswala ya kusamehe madeni kwa marehemu aliejitakia SITAKI!!!
Vaeni kwa habari sio kulazimishana. Kama wewe unaamini barakoa ndio salama yako vaa acha na wengine waishi watakavyo. barakoa zimevaliwa sana huko kwa wenzenu na bado corona imepamba moto so tusipangiane maisha
mimi ninavaa lakini kwa hiyari na pia Kuna wengine hawavai, pia ni kwa mapenzi yao so kila mtu aishi atakavyo
 
Hii kauli aliitoa mke wa Bill gate mwaka jana mwezi Kama huu, hapa ulichofanya ni kurudia tu hamna jipya
Inawezekana huyo mke wa Bill Gates hakumaanisha variant ya sasa. Inawezekana wengi ni vijana wasidhurike ila wazazi wao na walio na magonjwa nyemelezi, bibi na babu kama wako karibu.

Pia inawezekana miili yao imeshapata kinga. Ndiyo maana nasema tusubiri.Inaweza kuwa ni recipe nzuri ya utafiti. Na si ajabu Mungu akalifuta hilo gonjwa hapa- si tunasali.

Sent from my SM-A505F using JamiiForums mobile app
 
Tumeambiwa ametangulia kwa sababu ya ugonjwa wa moyo. Hii hoja yako ya COVID utatuthibitishia vipi?

Nipo kwa ajili ya kujifunza.
Unaeleweka.
Kuanzia mwezi Mei mwaka 2020, hakuna Mtanzania hata mmoja aliyekufa kwa Covid.
Watanzania wanakufa kwa matatizo ya kupumua tu, hasa wale wenye matatizo ya magonjwa ya sukari na moyo, kama vile Balozi Kijazi na Rais Magufuli.
Tanzania hakuna Corona.
Swali lako ni uthibisho thabiti wa ujinga wa Watanzania.
Serikali imepiga marufuku kupima virusi vya covid-19, kauli za ugonjwa huo kuua watu zinathibitika?
Burundi ilikubali kuwepo kwa Covid-19 baada ya Rais wao kufariki.
Tanzania iko njiani kufuata njia ya Burundi.
Its just a question of time.
 
Evarist Chahali Kama hofu yako ni maambuki ya COVID 19 fanya kitu chochote kilicho ndani ya uwezo wako kutoa suluhu kwa hao watanzania unaowaongelea hapa akiewemo rais wetu. Kumbuka hakuna rais wa nchi bila wananchi

Na nikukumbushe makusanyiko ya watu bila barakoa wala sanitzer yapo nchi nzima. Hata ukimuuliza Tundu atakuambia alikua anaingia hadi kariakoo bila barakoa.

Labda sababu wewe na ukoo wako mnaishi ughaibuni ndio maana hujui. ila kama una ndugu huku waulize vile wanaishi watakusaidi labda ili uweze kulisaidia taifa lako

Kama nia yako ni COVID 19 acha kulalamika fanya kitu chochote kilicho ndani ya uwezo wako kutoa suluhu kwa hao watanzania unaowaongelea hapa.

Na kwa msaada zaidi nikukumbushe makusanyiko ya watu bila barakoa wala sanitzer yapo nchi nzima.

Labda sababu wewe na ukoo wako mnaishi ughaibuni ndio maana hujui..... ila kama una ndugu huku waulize vile wanaishi watakusaidi labda ili uweze kulisaidia taifa lako


Hii ni Kawe leo




Hii ni Mwenge leo




Kariakoo 5 months ago







Hii ndio hali halisi

Umemaliza kila kitu uzi utakiwa uishie hapa.
 
Back
Top Bottom