Mama Samia ameingia kwenye mtego wa wafanyabiashara kubembelezwa kulipa kodi, tumekwisha!

Mama Samia ameingia kwenye mtego wa wafanyabiashara kubembelezwa kulipa kodi, tumekwisha!

Maombi yangu siku zote ilikua mama asiingie mkenge wa wafanya biashara maana tunajua kitakachotokea.

Bahati mbaya mama ameuvaa mkenge wa wafanya biashara. Tusitegemee chochote cha maana kufanyika kwa miaka 4 ijayo. Mama mwenyewe amekiri kua kwa kauli yake makusanyo yatashuka, unajiuliza kwa nini yashuke?

Mama ana matumaini kua makusanyo yakishuka baada ya muda yatapanda, yatapandaje? Nini kitayapandisha?

Ukiona kiongozi hayuko firm and strong kwenye kodi, basi ujue hiyo nchi iko doomed to fail. Nashukuru hayati alikua wazi kwenye hilo, alikua wazi na firm kwenye hilo

Kodi ni jambo ambalo halihitaji kubembelezana, hakuna mfanyabiashara anaetaka kulipa kodi, awe tajiri mkubwa awe mdogo hakuna. Kipindi kile Magufuli anaingia kina Azam walikutwa wanakwepa kodi ya kutosha,itakuaje kwa wafanya biashara wadogo na wa kati? Hilo liko wazi kodi ni jambo ambalo hakuna mfanya biashara anataka kulisikia.

Hakuna mfanyabiashara atakaelalamika ikiwa mfumo wa kukusanya kodi ni dhaifu, hayupo. Maana mifumo dhaifu ya kukusanya kodi ni faida kwa wafanya biashara.

Siku zote wafanya biashara hawako tayari kulipa kodi kwani itawapunguzia mapato yao.

Hizo nchi za ulaya hawabembelezani kwenye kodi na kila mwananchi anajaza tax returns awe na kazi awe hana kazi. Nchi zote zilizoendelea hawana cha msalia mtume kwenye kodi.

Sisi tunabembelezana kuhusu kulipa kodi halafu tunaenda kuomba msaada na mikopo kwa watu ambao hawabembelezani kwenye kodi, hizi ni akili ama matope?

Tanzania nchi yenye watu 60m inaenda kuomba msaada Finland nchi yenye watu 5m wakazi wa Dar tu wanazidi wananchi wa Finland, ama Norway 5m ama Sweden 10m, hii ni akili kweli? Na sababu no moja tu, Finland kila mtu analipa kodi na hakuna kubembelezana na ukikwepa kulipa kodi unafilisiwa kabisa.

Mama ameanza kupenda cheap popularity, ameanza kucheka na nyani atavuna tu mabua.

Acha upotoshaji wa kijinga, usidhani hatujasikia alichosema huyo mama. Mama kasema hataki kodi ya dhuluma bali anataka kodi halali. Kinachokufanya upoteshe ni ili ufiche ukweli aliosema kuwa watu walikuwa wanabambikiwa kodi, na hilo limefanyika sana, na kasema kabisa kubambikia kodi kuna faida ya muda mfupi, lakini hiyo inaua biashara za watu. Kama ni kushuka kwa muda ni hayo mapato ya kubambikia na sio mapato halali. Na kwa approach yake kodi ya halali itapanda kwani biashara nyingi zitaamka na kuanza tena.
 
Kitu cha muhimu ni kupunguza wingi wa kodi...kuna msururu mrefu sana wa kodi
 
Mkuu wewe unaona sahihi mfanyabiashara anaambiwa alipe kodi ya miaka 5 iliyopita wakati miaka yote iliyofuata alikuwa anaenda kwenye ofisi zao na analipa kodi? Hiyo ya nyuma hawakuiona vipi?
Na hili la kujilipa kwenye akaunti za watu liko Ulaya pia?
 
Kodi sio sababu ya kwanza ya kukimbiza wafanyabiashara. Hii ni hoja ya watu wajinga ambao hawakwenda shule.

Huko ulaya kuna very strict laws za kodi, umeona kama wafanyabiashara wanakimbia ulaya?

Acha kuchanganya kodi na uporaji. Hakuna mwenye tatizo na ulipaji kodi wa halali. Watu wanaongelea kodi za kubambikiwa na kufunga account. Huo utoto wa kupora hela za watu kwenye account uko kwenye nchi gani huko ulaya, mpaka wafanyabishara wakimbie?
 
Mkuu wewe unaona sahihi mfanyabiashara anaambiwa alipe kodi ya miaka 5 iliyopita wakati miaka yote iliyofuata alikuwa anaenda kwenye ofisi zao na analipa kodi? Hiyo ya nyuma hawakuiona vipi?
Na hili la kujilipa kwenye akaunti za watu liko Ulaya pia?
Sio sahihi mkuu. Sio sahihi kabisa na wala siungi mkono hilo jambo.
 
Tanzania nchi yenye watu 60m inaenda kuomba msaada Finland nchi yenye watu 5m wakazi wa Dar tu wanazidi wananchi wa Finland, ama Norway 5m ama Sweden 10m, hii ni akili kweli? Na sababu no moja tu, Finland kila mtu analipa kodi na hakuna kubembelezana na ukikwepa kulipa kodi unafilisiwa kabisa.
Nilivyosoma hii para nimegundua hauna glimpse yoyote ya uchumi ila unageuka mchambuzi!! Suprising

Nani alisema population ina uwiano na GDP per capita au tax base? Ukiwa na watu million 5 na 70% hawana ajira na huko finlanda uwe na MNC 10 tu hivi unajua zinatosha kuingiza mapato kuliko population ya watu mamilion.

Hata Duniani 5% tu ya watu inachangia zaidi ya 60% ya mapato na hao ndio wameajiri mabilion ya watu duniani.

So population sio tija kwenye makusanyo.... Bali level of investment, per capita income, Balance of payment, Purchasing power parity, n.k
 
Wewe itakuwa ni mfanyakazi wa ofisi kubwa ya kiserikali na pengine ni ndani ya TRA.Hujawahi kufanya biashara na kuona madhara yake na pia wewe si mchumi hata chembe.
Kukamua wafanyabiashara kulipa kodi kama alivyoona hakuongezi kodi na kama ikiongezeka ni kwa muda mfupi.Kodi ya kunyang'anya watu ni haramu na haina baraka katika nchi.Watu wanaosononeka kwa kulazimisha wasichokuwa nacho dua zao zina madhara sana kwa watawala.
Maombi yangu siku zote ilikua mama asiingie mkenge wa wafanya biashara maana tunajua kitakachotokea.

Bahati mbaya mama ameuvaa mkenge wa wafanya biashara. Tusitegemee chochote cha maana kufanyika kwa miaka 4 ijayo. Mama mwenyewe amekiri kua kwa kauli yake makusanyo yatashuka, unajiuliza kwa nini yashuke?

Mama ana matumaini kua makusanyo yakishuka baada ya muda yatapanda, yatapandaje? Nini kitayapandisha?

Ukiona kiongozi hayuko firm and strong kwenye kodi, basi ujue hiyo nchi iko doomed to fail. Nashukuru hayati alikua wazi kwenye hilo, alikua wazi na firm kwenye hilo

Kodi ni jambo ambalo halihitaji kubembelezana, hakuna mfanyabiashara anaetaka kulipa kodi, awe tajiri mkubwa awe mdogo hakuna. Kipindi kile Magufuli anaingia kina Azam walikutwa wanakwepa kodi ya kutosha,itakuaje kwa wafanya biashara wadogo na wa kati? Hilo liko wazi kodi ni jambo ambalo hakuna mfanya biashara anataka kulisikia.

Hakuna mfanyabiashara atakaelalamika ikiwa mfumo wa kukusanya kodi ni dhaifu, hayupo. Maana mifumo dhaifu ya kukusanya kodi ni faida kwa wafanya biashara.

Siku zote wafanya biashara hawako tayari kulipa kodi kwani itawapunguzia mapato yao.

Hizo nchi za ulaya hawabembelezani kwenye kodi na kila mwananchi anajaza tax returns awe na kazi awe hana kazi. Nchi zote zilizoendelea hawana cha msalia mtume kwenye kodi.

Sisi tunabembelezana kuhusu kulipa kodi halafu tunaenda kuomba msaada na mikopo kwa watu ambao hawabembelezani kwenye kodi, hizi ni akili ama matope?

Tanzania nchi yenye watu 60m inaenda kuomba msaada Finland nchi yenye watu 5m wakazi wa Dar tu wanazidi wananchi wa Finland, ama Norway 5m ama Sweden 10m, hii ni akili kweli? Na sababu no moja tu, Finland kila mtu analipa kodi na hakuna kubembelezana na ukikwepa kulipa kodi unafilisiwa kabisa.

Mama ameanza kupenda cheap popularity, ameanza kucheka na nyani atavuna tu mabua.
 
Mkuu unaweza kua uko sahihi ama sio sahihi lakini namba nianze na hoja yako namba moja.

Kwenye mada yangu nimetolea mfano nchi kama Finland, Norway na Sweden. Wewe unasema nchi zilizoendelea zina walipa kodi wengi zaidi ya 10m.

Mimi kwenye mfano wangu nimetoa wa Finland yenye total population ya 5m, hiyo pia ina walipa kodi wengi?
Yaan we jamaa ni mjinga sana sasa unafananisha tanzania na finland nchi yenye population ndogo na ambayo 65% of population ni man power? Una akili kweli??

Finland nchi ambayo development of industries ni ya miongo mingi sana hivyo ina exportation kubwa kuliko importation

Halafu ndio uje ufananishe na tanzania ambayo about 65% ni dependent age which include jobless youth's , children's and lower percentage of elders over 60+ million of total population ??
 
Mkuu nime catch attention kwenye paragraph yako ya mwisho tu.

Umesema pwani wana vinasaba vya biashara, sasa hiyo biashara imewafikisha wapi wakati wanaongoza kwa umasikini? Mikoa ya Pwani, Zanzibar ni masikini wa kutupwa, hiyo biashara imewafikisha wapi?
Unatumia takwimu za wapi? Kaangalie takwimu za Taifa kuhusu umaskini. Mwanza ni mkoa wa 3 kwa umaskini. Dar ni ya kwanza kwa utajiri, ikifuatiwa na Kilimanjaro na Njombe. Na wewe unaelewa hivyo?
 
Sana mkuu jamaa hajawahi ata kuanzisha genge la mboga mboga!
Hajui TRA kodi zilipungua wakaanza kupora na kuwatengenezea watu makosa 'fake na kulazimisha kila mwezi mfanyabishara awe analipa kidogo kidogo!
Yaani pengine mzee alikufa kwa pressure baada ya kuona hafiki kokote maana biashara zimefungwa kupita maelezo!
Mtu yoyote akitaka kujua biashara zilivyo fungwa asipate taabu aende serekali za mitaa aulize watu wanao chukuwa barua za kufunga biashara kwa mwaka jana walikuwa wangapi!
Me nilienda nikijua ni mimi tu ninafunga duh adi nikaona huruma kwa Jamuhuri ya Muungano!!
Siku za karibuni, walikuwa wanakataa kufunga biashara baada kuona trend ilikuwa ikiitia aibu Serikali.
 
Acha kupotosha.
Nchi ya watu milioni 60 wanaenda kuomba Finland yenye watu milioni 5.5 kwa sababu hii nchi ina watu maskini wengi, ina watu tegemezi wengi, ina wakulima asilimila 70, ina wanyonge wengi(mama ntilie, boda boda na wamachinga), watoto wengi(na waliambiwa wazidi kufyatua tu na jiwe) ambayo wote hawa ni makundi yasiyolipa kodi na yanayotegemea yahudumiwe kupita kodi inayokusanywa kwa wafanyabiashara wachache.

Nchi hii ina ina mawaziri wengi, manaibu waziri, makatibu wakuu, wakurugenzi, wakuu wa mikoa na wilaya, MaRAS na MaDAS ambao wote hao wanatembelea mavieite, magari ya kifahari, mishahara na marupurupu mengine. Haya yote yanafanyika kwa kutegemea kodi za kikundi kidogo cha wafanyabiashara, hii ni tofauti na huko Finland ambako hakuna haya yote.
Maombi yangu siku zote ilikua mama asiingie mkenge wa wafanya biashara maana tunajua kitakachotokea.

Bahati mbaya mama ameuvaa mkenge wa wafanya biashara. Tusitegemee chochote cha maana kufanyika kwa miaka 4 ijayo. Mama mwenyewe amekiri kua kwa kauli yake makusanyo yatashuka, unajiuliza kwa nini yashuke?

Mama ana matumaini kua makusanyo yakishuka baada ya muda yatapanda, yatapandaje? Nini kitayapandisha?

Ukiona kiongozi hayuko firm and strong kwenye kodi, basi ujue hiyo nchi iko doomed to fail. Nashukuru hayati alikua wazi kwenye hilo, alikua wazi na firm kwenye hilo

Kodi ni jambo ambalo halihitaji kubembelezana, hakuna mfanyabiashara anaetaka kulipa kodi, awe tajiri mkubwa awe mdogo hakuna. Kipindi kile Magufuli anaingia kina Azam walikutwa wanakwepa kodi ya kutosha,itakuaje kwa wafanya biashara wadogo na wa kati? Hilo liko wazi kodi ni jambo ambalo hakuna mfanya biashara anataka kulisikia.

Hakuna mfanyabiashara atakaelalamika ikiwa mfumo wa kukusanya kodi ni dhaifu, hayupo. Maana mifumo dhaifu ya kukusanya kodi ni faida kwa wafanya biashara.

Siku zote wafanya biashara hawako tayari kulipa kodi kwani itawapunguzia mapato yao.

Hizo nchi za ulaya hawabembelezani kwenye kodi na kila mwananchi anajaza tax returns awe na kazi awe hana kazi. Nchi zote zilizoendelea hawana cha msalia mtume kwenye kodi.

Sisi tunabembelezana kuhusu kulipa kodi halafu tunaenda kuomba msaada na mikopo kwa watu ambao hawabembelezani kwenye kodi, hizi ni akili ama matope?

Tanzania nchi yenye watu 60m inaenda kuomba msaada Finland nchi yenye watu 5m wakazi wa Dar tu wanazidi wananchi wa Finland, ama Norway 5m ama Sweden 10m, hii ni akili kweli? Na sababu no moja tu, Finland kila mtu analipa kodi na hakuna kubembelezana na ukikwepa kulipa kodi unafilisiwa kabisa.

Mama ameanza kupenda cheap popularity, ameanza kucheka na nyani atavuna tu mabua.
 
Kodi sio sababu ya kwanza ya kukimbiza wafanyabiashara. Hii ni hoja ya watu wajinga ambao hawakwenda shule.

Huko ulaya kuna very strict laws za kodi, umeona kama wafanyabiashara wanakimbia ulaya?
Mkuu bado ahujakuwa kwenye ishu za biashara,
Hata uko ulaya hawakusanyi kodi kwa mabavu kama tulivyo kuwa tunafanyiwa na hawa TRA
Yaani ilikuwa upuuzi mtupu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ulaya watu wanalipa kodi barabara za mitaani ni za lami, miji inasafishwa, drainage systems zinajengwa, wanafunzi wanakaa madarasani sio chini ya miti. Hapa watu wanalipa kodi mtu anaenda kununua ndege kwa cash ambazo zinazalisha hasara tu, anajenga uwanja ndege na hoteli kijijini kwake , anatembea na maburungutu ya pesa anagawa hovyo barabarani!
Kodi sio sababu ya kwanza ya kukimbiza wafanyabiashara. Hii ni hoja ya watu wajinga ambao hawakwenda shule.

Huko ulaya kuna very strict laws za kodi, umeona kama wafanyabiashara wanakimbia ulaya?
 
Tuliwaambia tunataka KATIBA mpya longtime hamuelewi Mama tupige unavyotaka, fanya kwa utashi wako na atakayekuja aje na lake. Naombeni 2025 mnipe niwanyooooshe kwa utashi wangu pia
 
Hili sio swali.

Changamsha akili uulize swali la maana.
Be positive,usimlinganishe na kitu kingine au mtu .Kila mtu anafanya aonavyo na kwa njia tofauti.Tusubiri na kuangalia usilalamike kabla hata ya implementation nyie ndio watu mnaangalia ,mnachokonoa at the end of the day uoni kitu kwa sababau you have been negative about this
 
Kodi ikiwa rafiki hakuna ambaye ataacha kulipa maana kodi ipo kisheria,mimi nafanya biashara last time mwezi march mwishoni nilivyoenda TRA kufanyiwa makadirio yule afisa alikuwa so smooth aliniambia tu bwana mwaka huu utalipa hivi nikajitathmini kama naweza nikasaini paper ikapitishwa sasa nipo mtaani natekeleza.

Tatizo TRA officess wengine hupenda kubanana na mtu mpaka muanze kuulizana sauti za chini chini hapa tufanyeje wakati efd mashine inaonyesha uelekeo wa biashara ya mtu ndo maana watu huona bora wasiende,wasipoenda ndo haya kulaumiana ila ukweli kama kodi ni nzuri hakuna asiyetaka kuilipa.
 
Maombi yangu siku zote ilikua mama asiingie mkenge wa wafanya biashara maana tunajua kitakachotokea.

Bahati mbaya mama ameuvaa mkenge wa wafanya biashara. Tusitegemee chochote cha maana kufanyika kwa miaka 4 ijayo. Mama mwenyewe amekiri kua kwa kauli yake makusanyo yatashuka, unajiuliza kwa nini yashuke?

Mama ana matumaini kua makusanyo yakishuka baada ya muda yatapanda, yatapandaje? Nini kitayapandisha?

Ukiona kiongozi hayuko firm and strong kwenye kodi, basi ujue hiyo nchi iko doomed to fail. Nashukuru hayati alikua wazi kwenye hilo, alikua wazi na firm kwenye hilo

Kodi ni jambo ambalo halihitaji kubembelezana, hakuna mfanyabiashara anaetaka kulipa kodi, awe tajiri mkubwa awe mdogo hakuna. Kipindi kile Magufuli anaingia kina Azam walikutwa wanakwepa kodi ya kutosha,itakuaje kwa wafanya biashara wadogo na wa kati? Hilo liko wazi kodi ni jambo ambalo hakuna mfanya biashara anataka kulisikia.

Hakuna mfanyabiashara atakaelalamika ikiwa mfumo wa kukusanya kodi ni dhaifu, hayupo. Maana mifumo dhaifu ya kukusanya kodi ni faida kwa wafanya biashara.

Siku zote wafanya biashara hawako tayari kulipa kodi kwani itawapunguzia mapato yao.

Hizo nchi za ulaya hawabembelezani kwenye kodi na kila mwananchi anajaza tax returns awe na kazi awe hana kazi. Nchi zote zilizoendelea hawana cha msalia mtume kwenye kodi.

Sisi tunabembelezana kuhusu kulipa kodi halafu tunaenda kuomba msaada na mikopo kwa watu ambao hawabembelezani kwenye kodi, hizi ni akili ama matope?

Tanzania nchi yenye watu 60m inaenda kuomba msaada Finland nchi yenye watu 5m wakazi wa Dar tu wanazidi wananchi wa Finland, ama Norway 5m ama Sweden 10m, hii ni akili kweli? Na sababu no moja tu, Finland kila mtu analipa kodi na hakuna kubembelezana na ukikwepa kulipa kodi unafilisiwa kabisa.

Mama ameanza kupenda cheap popularity, ameanza kucheka na nyani atavuna tu mabua.
Yaani mama anadhani uongozi wa nchi ni kama Shehe kuongoza msikiti, hayo ni mambo tofauti. Hizo kauli zitaligharimu taifa
 
Maombi yangu siku zote ilikua mama asiingie mkenge wa wafanya biashara maana tunajua kitakachotokea.

Bahati mbaya mama ameuvaa mkenge wa wafanya biashara. Tusitegemee chochote cha maana kufanyika kwa miaka 4 ijayo. Mama mwenyewe amekiri kua kwa kauli yake makusanyo yatashuka, unajiuliza kwa nini yashuke?

Mama ana matumaini kua makusanyo yakishuka baada ya muda yatapanda, yatapandaje? Nini kitayapandisha?

Ukiona kiongozi hayuko firm and strong kwenye kodi, basi ujue hiyo nchi iko doomed to fail. Nashukuru hayati alikua wazi kwenye hilo, alikua wazi na firm kwenye hilo

Kodi ni jambo ambalo halihitaji kubembelezana, hakuna mfanyabiashara anaetaka kulipa kodi, awe tajiri mkubwa awe mdogo hakuna. Kipindi kile Magufuli anaingia kina Azam walikutwa wanakwepa kodi ya kutosha,itakuaje kwa wafanya biashara wadogo na wa kati? Hilo liko wazi kodi ni jambo ambalo hakuna mfanya biashara anataka kulisikia.

Hakuna mfanyabiashara atakaelalamika ikiwa mfumo wa kukusanya kodi ni dhaifu, hayupo. Maana mifumo dhaifu ya kukusanya kodi ni faida kwa wafanya biashara.

Siku zote wafanya biashara hawako tayari kulipa kodi kwani itawapunguzia mapato yao.

Hizo nchi za ulaya hawabembelezani kwenye kodi na kila mwananchi anajaza tax returns awe na kazi awe hana kazi. Nchi zote zilizoendelea hawana cha msalia mtume kwenye kodi.

Sisi tunabembelezana kuhusu kulipa kodi halafu tunaenda kuomba msaada na mikopo kwa watu ambao hawabembelezani kwenye kodi, hizi ni akili ama matope?

Tanzania nchi yenye watu 60m inaenda kuomba msaada Finland nchi yenye watu 5m wakazi wa Dar tu wanazidi wananchi wa Finland, ama Norway 5m ama Sweden 10m, hii ni akili kweli? Na sababu no moja tu, Finland kila mtu analipa kodi na hakuna kubembelezana na ukikwepa kulipa kodi unafilisiwa kabisa.

Mama ameanza kupenda cheap popularity, ameanza kucheka na nyani atavuna tu mabua.
Shusha kodi tengeneza walipa kodi wengi. hakuna mtu ambaye hatolipa kodi.
 
Back
Top Bottom