Mambo 30 usiyoyajua kuhusu utapeli wa Q-Net (Network Marketing)

Mambo 30 usiyoyajua kuhusu utapeli wa Q-Net (Network Marketing)

Kuna mmoja alikuja kunipa hilo somo...yeye ananambia kuwa nikijiunga basi fasta napata mapesa kibao aiseeee...nikamuuliza kama ni ya ukweli hiyo biashara, akajibu kuwa yeye ana uzoefu nayo muda mrefu so haina shida, nikamuuliza mbona yeye sasa hana hizo pesa anazonambia? Si amefanya muda mrefu? Tukabaki tunaangaliana hapo

Ndio wanavyoanza hivyo, wanaanza na kukushawishi kuwa utakuwa Tajiri, Qnet inafadhili timu ya Manchester United, usiwe na wasiwasi, yeye amenunua bidhaa ya milioni nne, nk..

Utapeli, Utapeli Utapeli..
 
  • Thanks
Reactions: Ctr

QNet formerly known as QuestNet has been banned in many countries. Countries consider it illegal and a form of fraud.

In order to cut the hassle, I am going to discuss below some of the countries it has been banned from and the reasons behind this shutdown.

Please feel free to check the references for further details.
1. Afghanistan (2008)
2. Rwanda (2009)

3. Iran (2005)

4. Sri Lanka (2004)

5. USA & Canada (2008)
6. Syria (2009)

7. India (2010)


*Dates indicate the year Quest was banned/shutdown.

For the following reasons:

Afghanistan

· QuestNet worked in the country without a legal license from any governmental Ministry of Administration. ·QuestNet activities has damaging effects on the people and the country including: 1. Huge economic loss of the country. 2. The outflow of foreign currency outside the country. 3. Economic loss of families joining the business.· General export/import licenses for individuals DO NOT authorize pyramid activities.

Rwanda
· Government believes Quest Net is illegal and fraud. ·Quest Net DOES NOT follow the companies and tax laws imposed by the country.

· The National Bank of Rwanda (BNR) believes that Quest is operating under a pyramid scheme and could be involved in money laundering.

· Quest IR representatives declare that they do not need an office because it’s an e-commerce business, which contradicts the Companies Act of Rwanda that it is COMPULSORY to register the in the Registrar General’s office. It only takes 7 days to register a business.

· Income tax by individuals is not reported.

· QuestNet use of illegal commercial transactions.

· Individuals joining QuestNet destabilized the status and welfare of their families.

· The outflow of the money is distributed outside the country in uncontrolled and unsupervised ways.

· Government accused QuestNet of sending $500,000 out of the country untaxed.

Iran
· Gold Quest is described as a pyramid scheme and a form of fraud and deception.

· Gold Quest was banned in 2005.

· Gold Quest agents has been arrested in Iran at the Imam Khomeini International Airport (IKA) in 2009.

· GoldQuest has led to the outflow of half a billion dollars outside of Iran.

· Anyone who participates on those companies is legally responsible and disturbs the economy of the country.

Sri Lanka
· Sri Lanka banned pyramid schemes and network marketing to encounter Gold Quest and Quest Net.

· Pyramid schemes in Sri Lanka has led to the outflow of $50 million.

· Since many investors borrow to invest, they resulted in great debt.

· The Central Bank of Sri Lanka warned for the damage it can hit the country for the outflow of the money without any corresponding return of goods or services of the same value.

· Pyramid schemes target poor countries because they are more attracted to the promised high returns and thus so hard to resist.

USA & Canada
· Canada regulators declare that Gold Quest is both a classic Ponzi scheme and Pyramid scheme.

· Gold Quest raised US$29 million from 2940 investors.

· The Securities and Exchange Commission accused Gold-Quest of cheating US and Canadian citizens.

Syria
· QuestNet in Syria collected millions of Syrian pounds, shutdown their offices and disappeared from the country without any prior warning.

India
· The Central bureau of Crime Investigation Department (CB-CID) has filed a charge against Gold Quest.

·265,757 IRs has been cheated from all over India.

Some people will argue that Gold Quest is not the same as QuestNet and therefore I invite you to check this: Proof for “QuestNet” and “Gold Quest” belongs to same group of company…[13]

Haven’t you wondered why QNet changed its previous name Quest and its domain fromhttp://www.quest.nettohttp://www.qnet.net?

According to the above information, it might be concluded that the domain name has been changed for the following reasons:

1. It was banned under the name Quest.

2. Potential victims will search for QNet not Quest on the Internet and government directories for further information and therefore will not find complains under the name of QNet.

Case Study: Effect of Pyramid Schemes on Albania

· 2/3 of the population participated in pyramid schemes.

· The country was bankrupted.

· When the scheme collapsed, the government fell and a near civil war resulted in the death of 2,000 people.

Reasons Pyramid Schemes grew in Albania:
· People’s unfamiliarity with financial markets.

· Deficiencies of the Albania’s formal financial system.

· The government’s unclear supervision of the responsibility of handling informal markets.

We should be able to learn from the mistakes of other countries in order to avoid falling in the same pitfalls and result in similar misfortunes.

Qnet or QuestNet has badly affected the above countries.

The network is still spreading in Tanzania very fast.

My question to you is: Do you still want to join remain in Qnet or join the group?
Vipi na wale forever living product!!? Huwa nahisi nao Ni sawa na hawa QNet
 
Nilichogundua kwamba wajinga duniani hawaishi na hawatokuja kuisha ,watu wanaingizwa mkenge sana hiyo qnet,,,Oriflame nao wanafunga virago , Forever nao wanapumulia mashine now wanauza hadi dawa za nguvu za kiume,ma tycoon wa forever wanapiga mishe nyingine za kuwatapeli wajinga(KEKUNDU KEKUNDU).
 
Kuna mfanyakazi mwenzangu alikopa 5m kujiunga jamani tumejuta aseehh!usumbufu kila kona anatushawishi na hakupata hata supporters mwisho kaja kuishia kua tapeli maana anakatwa pesa nyingi hela hana qnet wamekula mkopo wote
Kuna wanafunzi fulani pale UDSM juzi tu nikaona kuna mjinga mmoja anawaingiza mjini kuhusu QNET, nilimpa vidonge vyake! Aisee wale mabinti walinishukuru sana. Nikawaambia akija tena wamwambie akasombe wazazi wake na ndugu zake wachangamkie hiyo fursa ya utajiri wa rahisi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Daah, wapenda shortcut lazima walie tu

House girl(dada wa kazi) Ni binadamu aheshimiwe, apumzike, apewe Uhuru wa kuabudu pia
 
Hao Qnets nadhani wana watogaga..mana kuna jamaa alikua chuo..kapigwa upofu wa hilo kampuni..kamdanganya mzazi wake..6m kawapatia Qnet..sahv hana mbele wala nyuma.
Hivi watanzania tunakwama wapi?
Yaani mtu hajawahi kufanya hata biashara ya mtaji wa laki moja, anaenda QNET anaimbishwa maneno kibao halafu anakwenda kuzisaka popote zaidi ya 4milioni halafu anawapa QNET.
Tumerogwa na nani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari wadau, niliwahi kuja na uzi hapa kuhusu D09 CLUB Miezi michache kabla haijapotelea kusikojulikana na nilishambuliwa sana na waliliwa pesa zao na bila kujua hatma yao wanarudishiwa vipi na nani. Leo naomba nije na mambo 30 usiyoyajua kuhusu Qnet.

Qnet ni network marketing ambayo imevuta member wengi waliokua d09 Club kuingia huko haina tofauti kubwa na network marketing zingine unazozijua wewe mfano lugha wanayotumia kukushawishi zinafanana na wale wengine.

Kiuhalisia wanakuekea mazingira mazuri ya kuona unapata pesa kirahisi sana lakini kiukweli hakuna pesa rahisi unawafanyia kazi na wanakulipa kama kazi zingine lakini mfumo wao wa ulipaji na uendeshaji wa biashara yao ndio uko tofauti na wengine.

1. QNET ILIANZISHWA LINI?

Mwaka 1998 kampuni hii ilianzishwa huko Hong Kong mwaka ambao:

-Kampuni ya kutengeneza magari ya Benz iliinunua kampuni ya Chrysler kwa gharama za $36 billion ambayo ilivunja rekodi ya Dunia na kua biashara kubwa zaidi kihistoria kufanyika mpaka mwaka huo.

-Elton John anakua shoga wa kwanza kutunukiwa heshima ya "Sir" na malkia wa Uingereza
-Mwaka huo huo mwanzilishi mwenza wa google Larry Page na mwenzie Sergey Brin, waliokutana Stanford University, wanaisajili rasmi kampuni ya google California
kwa ajili ya kutoa huduma mtandao
-Mwaka huo pia mmiliki na mwanzilishi wa kampuni ya Microsoft anatupiwa ice cream usoni akiwa Belgium

Ni mwaka uliokua na mapinduzi makubwa kiuchumi pamoja na vituko vingi vya kushangaza Dunia.

2. NANI MWANZILISHI WA QNET?
-Vijay Aswaran akiwa kama mwenyekiti wa QI Group na mwenzie Joseph Bismark akiwa kama Director wa QI Limited

3. Majina mengine ya QNET usiyoyajua:

  • Questnet
  • Goldquest
  • and QI Limited
4. Makao makuu yake na Office zao:
Makao makuu ya QNET yapo Hong Kong lakini wana Ofisi katika miji ifuatayo:

  • Malaysia
  • United Arab Emirates
  • Indonesia
  • Ireland
  • Singapore
  • Rwanda
  • Philippines
  • Turkey
  • India
  • Algeria
  • Azerbaijan
  • Cote D’Ivoire
  • Burkina Faso
  • Georgia
  • Guinea
  • Moldova
  • Kazakhstan
  • Myanmar
  • Niger
  • Mandalay
  • Ukraine
  • and Russia
5. WALIANZA NA BIASHARA GANI?
QNET walianza kwa kuuza "Custom Coins" mfano zile zinazotumika kutunuku washindi wa michezo mbalimbali katika mashindano ya michezo n.k na ilikua inaitwa Goldquest

6. QNET At The Olympics
Kampuni ya QNET ndio ilipata deal ya kutengeneza na kusambaza Olympic coins mwaka 2000 zilizofanyika Sydney,pia 2004 Athens Games na 2008 Beijing Games.

7. QNET At The World Cup
QNET tena wakalamba bingo la kombe la Dunia mwaka 2002 kama official coin distributor for the 2002 FIFA World Cup soccer championships.

8. QNET na QVI Club
Ili kujitanua zaidi na kuongeza kipato QNET iliingia ubia na kua mwekezaji mwenza na QVI Club kampuni inayohusika sana na Vacations and Travell.

9.QI Comm
Mwaka 2005 QNET ikaingia kwenye uwekezaji wa kampuni ya mawasiliano wakainunua British communications company na kuibadilisha kua QI Comm.

10. Prana
Mwaka 2005,QNET ikaingia kuwekeza Thailand na kuinunua Prana Resorts and Spa

11. Cimier
Mwaka huo huo 2005 wakakinunua kiwanda kikubwa cha kutengeneza saa huko Uswisi Swiss watch manufacturer Cimier.

12.Down To Earth
Mwaka 2007, kampuni ikapiga hatua zaidi na kununua kiwanda cha vyakula na afya huko Hawaii kinachoitwa Down To Earth.

13. Meritus
Kampuni ya QNET inaanza kusponsor the Meritus Malaysian Motor timu ya mashindano ya magari.Timu hiyo ilibadilishwa jina na kua MY QI Meritus.

14. Virgin Racing
Mwaka 2010, wakaingia ubia na Virgin racing ambao walikua wanashiriki pia the Grand Prix series mashindano makubwa ya mbio za magari Duniani.Haikufanya vizuri na waliacha nayo 2011.

15. Bidhaa ambazo QNET imewekeza tangu 1998 mpaka 2010
Mpaka mwaka 2010 QNET ilikua na bidhaa tofauti tofauti sokoni na zingine zikiwa ni zile mahitaji mhimu kwa binadamu kama afya na chakula.Kampuni ikaanz kujikita zaidi katika kutafuta wasambazaji katika category tofauti tofauti;

  • Health and wellness
  • Vehicle motor care
  • Personal Care
  • Beauty
  • Technology
  • Jewelry and watches
  • Holiday and recreational travel
  • and Education
Post ijayo ntakuja kuelezea namna QNET inavyolipa na nchi kadhaa ilikofungiwa na mmiliki wake kukamatwa mara kadhaa kwa mashtaka ya kutakatisha fedha (baadhi ya nchi).........

======


Naomba tuendelee sehemu ya pili kisha ntatoa hitimisho kwa mtazamo wangu.......karibuni

16. Namna wawakilishi/waliojiunga na QNET wanavyopata mgao
Haina tofauti sana na networking market zingine ama ile d09,lakini huku yule TOP (ambae ni QNET) ndio ananyonya member na member aliejuu yako hali jasho lako bali kwa juhudi zake ndivyo anapata commission zaidi na namna anavyoingiza member wapya ama kuuza bidhaa za QNET. kuna njia 10 za kupata pesa ya mgao wako baada ya kufanya kazi ya maana;

  1. Retail Profits
  2. Early Payout
  3. Step Commissions
  4. Repeat Sales Points
  5. Year-Round Incentives
  6. New Program Bonus
  7. Main Plan Rank Advance
  8. RSP Plan Rank Advance
  9. RSP Rank Advance Bonus
  10. and RSP Rank Maintenance Bonus
Sitazielezea hizi kwa undani kwa sababu si nia ya huu uzi labda tukijaliwa nafasi siku nyingine,nia ya huu uzi ni kukujulisha usalama wa uwekezaji wako juu ya QNET kisha uamue kujitundika mwenyewe....tuendeleee

17.Quest University
Hiki ni chuoa cha QNET kipo Malysia (Perak) na wanatoa kozi za Afya na Uuguzi na zingine nyingi so far hakuna review mbaya kuhusu hiki chuo.

18. Australia
The Australian Office of Consumer and Business Affairs waliitaja QNET kama pyramid scheme 2002.

19. Nepal
Mwaka 2003, the Nepalese Home Ministry walifunga kazi na biashara zote zinazoihusu QNET nchini humo.

20.Sri Lanka
Mwaka 2005, waliishutumu QNET imeisababishia nchi hasara ya $15,000,000 kwa kuikosesha kodi na kufanya biashara zinazofanana na utakatishaji wa pesa, serikali ya Sri Lanka ikaipiga banned QNET nchini humo.

21.Iran
Mwaka huo huo 2005,Serikali ya Iran waliishtumu shutma zile zile QNET ilizokutana nazo Sri Lanka kua imesababisha hasara kwa nchi ya takribani $500,000,000 wakaipiga banned QNET pia nchini Iran.

22.kukamatwa kwa Vijay nchini
Mwaka 2007, Direct Selling Association huko Indonesia waliishtaki QNET kwa serikali ya nchini humo, kua ni pyramid scheme. Interpol walimkamata Vijay Eswaran na wahusika wengine na kuwafungulia mashataka ya fraud. Wiki chache baadae washtakiwa wote waliachiwa huru na mashtaka yalifutwa na QNET ikaendelea kuoperate nchini Indonesia.

23.Maandamano ya kuipinga QNET nchini Afghanistan
QNET ilianza shughuli zake Afghanistan mwaka 2006.Na ilishika kasi kwa speed na kupata washirika wengi ndani ya mda mfupi na mwaka 2008 ikasajiliwa rasmi nchini humo.Ghafla siku moja kukazuka maandamano makubwa takribani watu 3,000 wakipinga namna QNET inavyofanya biashara zake nchini humo na mamlaka zikaibana QNET na kuipa masharti ya namna ya kujiendesha ikiwa nchini humo.

24.Sudan
Serikali ya Sudan government ika bann shughuli zote za QNET nchini humo kwa sababu ya malalamiko kutoka kwa watu walifanya nao biashara kutokupokea vitu walivyonunua na hata kama wakiletewa hivyo vitu quality yao ni mbovu Duniani hakuna hapo ilikua mwaka 2009.

25. Syria
Mwaka huo huo 2009, the Syrian Ministry of Economics wakaishtaki QNET kwa kufanya biashara kubwa nchini humo na bila kulipa kodi lakini pia kampuni inaendesha shughuli zake kwa mtindo wa pyramid scheme ambao ni kinyume na sheria za nchi hiyo QNET was not allowed to operate in Syria anymore.

26. Turkey
Mwaka 2010 huku ikijulikana kama Questnet, watu wanaojihusisha na Questnet wapatao 80 walikamatwa na 40+ walifunguliwa mashtaka ya "gaining an unfair advantage".Wakabadili jina la kampuni na kuanza kuitwa QNET, serkali ikaanzisha uchunguzi wa kina kuhusu QNET wizara ya biashara ya Uturuki. Mwaka 2011, QI Group wakanunua Dögan Hotel iliyopo Antalya, Turkey.

27.Egypt
Kampuni ilipelekwa katika chombo kinaitwa Dar al-Ifta al-Misriyyah ambacho kinasimamia maswala ya elimu na maadili ya kiislam. Dar al-Ifta al-Misriyyah wakasema QNET ni kinyume na hairuhusiwi pia italeta madhara kwa uchumi wa Egyptian hapo ilikua 2012.

28.Saudi Arabia
Mwaka 2010, the Saudi Arabia Ministry of Commerce and Industry walitoa onyo kali kwa wananchi wake kujihusisha na kampuni kama QNET. Na ilifungiwa mara moja kufanya shughuli zake nchini humo.

29.Kamata kamata nchini India
Mwaka 2008, the Central Bureau of Investigation huko India walianza uchunguzi na kupeleleza shughuli zote zinazofanywa na viongozi wa QNET.Walipitia historia ya mashtaka yote aliyoshtakiwa Vijay Eswaran and QNET ikiwa ni pamoja na yale ya kujihusisha na utakatishaji wa pesa. Walifreeze account za QNET na mwaka 2013 walianza kukamata wahusika wote

Serikali ya India haikua na sheria inayozungumzia kuhusu direct selling and multilevel marketing,hivyo hakuna mahakama ya India iliyoweza kuwatia hatiani wahusika wa QNET wakawa huru.

30. Sura nyingine ya QNET

Tutizame positive side ya QNET na Vijay kwa kiasi;

  • Forbes listed Vijay Eswaran as one of the biggest philanthropy heroes. You can read about that here: 48 Heroes Of Philanthropy
  • It is listed on the World Economic Forum
  • QI Comm is one of the fastest growing tech companies in the United Kingdom.
QNET inaendesha biashara zake kwa mfumo wa Multi-level marketing ambao unatumika sana na pyramid scheme nyingi kama d09 iliyokufa hivi karibuni na zingine.
View attachment 616923

Kinachofanya usione kama ni pyramid scheme wanatumia kivuli cha bidhaa na vitu wanavyomiliki ili kuficha uhalisia wa pyramid scheme (ntaielezea siku nyingine hii).

Utajiuliza kwa nini haifungiwi sehemu nyingi duniani mpaka kutokee majanga ???
Ni kwa sababu sehemu nyingi duniani nchi nyingi hazina sheria inayosimamia multi level marketing na operations zake pamoja na direct selling kama ilivyotokea nchini India kweli mnaona kuna uovu unatokea watu wanarun business kinyume kabisa na mipango ya nchi lakini mnawatia nguvuni na kuwashtaki kwa sheria ipi ? Hii imefanya hawa jamaa kuendelea kupeta nchi nyingi ikiwemo na hapa kwetu na ndio maana hujasikia mtu kakamatwa kwa kupotea na pesa za d09 hata hii QNET itakuja kuishia hewani tu kama mvuke........(haya ni maoni yangu)

Mfumo wa Forever Living au Oriflame ni tofauti sana na mfumo wanaotumia hawa QNET as network market na hicho ndio kinachofanya kue na doubt nchi nyingi inakoingia na kuanza ku operate.

Niwakumbushe wanaotamani kuingia huku usiwekeze kiasi kikubwa cha pesa ambacho hutamudu kukipoteza namaanisha don't invest amount of money that you couldnt afford to loose it,that is risk management.....hata siku unaambiwa ime collapse au imefungiwa nchini kwetu hutaumia kwa ile pesa ulikua umeweka kule utaumia kwa mda ulio poteza ungeweza kufanya uwekezaji mwingine wenye tija.

Kwa wafanya biashara nafikiri ukiweza ku adopt hii system ya mult level marketing (kumfanya mtu awe part ya uwekezaji wako au part ya biashara yako na si kumuajiri) ni mfumo mzuri sana.

Kwa TRA kuna mirija ya upotevu wa pesa hasa kwa shughuli kama hizi niliwahi hata kuuliza hivi google,facebook si wanarusha matangazo yao online wanalipa kodi ? sheria zinasemaje ?

Ntaishia hapa kwa leo ntaendelea kukuletea zaidi na zaidi kwa kadri ntavyoibua haya mambo
Umeeleza kwa ufasaha sana hongèra sana
 
Qnet Ni utapeli
Kwamba huo ushahidi wa kimahakama unaelezea hukumu ipi kwa hatia ipi?
Hivi unadhania wenye akili timamu wakisoma unachoandika wewe na mimi yupi anayeonekana mwenye shida kichwani?
Unazungumzia kulizwa kulizwa vipi labda? kwamba wa kutumia ecommerce sytem ya qnet nitalizwa pesa zangu kwa maana sitopewa nilichonunua au?
Lete vitu kama hivi.. baki kwenye mada.

Mimi ni mtalii tuseme, unataka kusema kama nahitaji kununua tripsavr pacage ili nitumie Zanzibar kwenye holiday yangu nisinunue kwa vile sitopewa huduma au naibiwaje labda?

Embu niambie napigwa vipi kwa kutumia Ecommerce platform ya Qnet kununua bidhaa nipendayo? Au twambie wewe uliibiwa vipi hukupewa bidhaa? Ulipewa bidha fake au? Kwamba cheni zao wanazouza ni feki au?
Embu nipe fact kwa mujibu wa mada. Achana na habari za Fulsa za kibishara. Sijazizungumzia kw enye mada.
Subiri ijumaa nitakuja pande hizo. But leo kaa kwenye mada.


Hata wewe waweza tuhumiwa umebaka na kumbe sio.. wangapi wametuhumiwa wameua kumbe sio.. embu tuambie ushahidi wa mahakama umesemaje juu ya jiyo kesi ya kihindi? Hahhaha

Au hujui kusoma wewe umekop tu ukapest.. hujaona kuwa huo ushahidi uliouleta unakuonesha kuwa mahakama haikuishika kampuni kwa hatia yeyote. Na mwisho unaambiwa kuwa upande wa mashtaka wanajipanga kukata rufaa.. si ndio bandiko lako ulilolileta. Kw taarifa yako mabandiko kama hayo yapo lukuki na niliyasoma tangu 2016 We unaleta leo.. hhhaaha
Baki kwenye mada sipo kushawishi mtu hapa.
Kuna watu wanachambua pumba mchele na hawacomment kitu.
Relax.
 
Hawa majamaa wameniita wamenipiga msasa wa hatari et Nina Bahat sana, Mara good morning hata jioni....nimewauliza kiingilio sh ngap...wakanificha wanadai kesho nirud ndo watanijuza...alaf hawatak nimwambie mtu.... Kesho hawanioni....
Jamiiforums is a school of aweareness.!
Bear it in your mind

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nafaidi matunda ya Qnet kupitia mteja wangu aliyejaribu kunirubuni akashindwa, huwa akija kwangu nikitaja bei wala haliilii kupunguziwa sijui ndo ananiringishia utajiri.... huwa nafurahi sana anavyonikomoa kwa kuniachia vichenji ili nimwone maisha bora.

Good morning.
 
Hahahaha dah, sawa mkuu
Naomba kujuzwa sawia kuhusu hii kampuni (networking bussiness company) ijulikanayo lwa jina la Qnet.

Nimefuatilia kiingilio chao ni kuanzia milioni 4. Kisha ili upate commission inabidi uingize watu wawili wenye uwezo wa kutoa hizo 4m kila mmoja. Na wao wakiingia wawaingize watu wawili kila mmoja kwa gharama hiyo au zaidi. Kila watu wanavyoingia ndivyo waliotangulia wanavyopata commission.

Hiyo 4milion ni kiwango cha chini na hutolewa kununua moja ya product za kampuni hiyo kama saaa, mikufu, na hereni.

Inasemekana ukijiunga, unaweza kuwa bilionea ndani ya mwaka mmoja. Naomba ufafanuzi ama ushuhuda juu ya hili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom