Maoni: Ili kujenga uzalendo, Serikali ifute shule zote binafsi hapa nchini tubaki na shule za kata tu!

Maoni: Ili kujenga uzalendo, Serikali ifute shule zote binafsi hapa nchini tubaki na shule za kata tu!

Kama serikali imeshindwa kuboresha shule zake itawezaje kuboresha shule binafsi???
Kwa kuwa baadhi ya shule binafsi ni bora, hii itakuwa chachu kwa serikali kuboresha shule zote kwa pamoja.
 
Unahitaji kuboresha Elimu au kuleta uzalendo?
Nahitaji kuboresha elimu kupitia uzalendo ulio bora. Huwezi kuboresha elimu ikiwa uzalendo wa raia upo chini. Na uzalendo ukiwa chini, sio rahisi kuboresha elimu. Vitu hivi wiwili vinategemeana.....ni kama kuku na yai.
 
Kwa kuwa baadhi ya shule binafsi ni bora, hii itakuwa chachu kwa serikali kuboresha shule zote kwa pamoja.
Yani umeshindwa kubeba kilo 10 alafu unaomba uongezewe ubebe kilo 100 ???

Hii reasoning ni ya kiwango duni sana.
Its too low to he here.
 
Hapo utakuwa umekosa uzalendo mkuu. Na ikiwa utawapeleka watoto wako Kenya basi uhamie huko huko. Hatutakutaka kurejea hapa nchini tena.
Kuna haja serikali/jamii ifanye utafiti wa kina, kujua ni kwanini idadi ya raia wajinga inazidi kuongezeka badala ya kupungua.
 
Nahitaji kuboresha elimu kupitia uzalendo ulio bora. Huwezi kuboresha elimu ikiwa uzalendo wa raia upo chini. Na uzalendo ukiwa chini, sio rahisi kuboresha elimu. Vitu hivi wiwili vinategemeana.....ni kama kuku na yai.

Kwa hiyo kuboresha Elimu ndio kufuta shule Binafsi?
Kumaanisha shule Binafsi ndio Sababu kuu ya Elimu yetu kuwa hovyo?

Kuwa Serious Mkuu
 
Kabla kuna wazazi walikuwa wanapeleka watoto wao Kenya na Uganda. Na wengine UK.
 
Kwa hiyo kuboresha Elimu ndio kufuta shule Binafsi?
Kumaanisha shule Binafsi ndio Sababu kuu ya Elimu yetu kuwa hovyo?

Kuwa Serious Mkuu
Mkuu naona bado hujanielewa. Simaanishi kufuta kama kufuta bali namaanisha kutaifisha au kuhamisha umiliki kutoka binafsi kwenda serikalini (umma). Ina maana hizi shule bado zitaendelea kutoa huduma zikiwa chini ya serikali. Na walimu wanaofundisha kwenye shule hizi pia watapewa ajira serikalini. Nadhani sasa nimeeleweka.
 
Kabla kuna wazazi walikuwa wanapeleka watoto wao Kenya na Uganda. Na wengine UK.
Haya mambo sasa ndio hatutaki. Tunataka tubanane humu humu ndani.......hakuna kutoka nje.
 
Mkuu naona bado hujanielewa. Simaanishi kufuta kama kufuta bali namaanisha kutaifisha au kuhamisha umiliki kutoka binafsi kwenda serikalini (umma). Ina maana hizi shule bado zitaendelea kutoa huduma zikiwa chini ya serikali. Na walimu wanaofundisha kwenye shule hizi pia watapewa ajira serikalini. Nadhani sasa nimeeleweka.
Serikali ijenge za kwake.
 
Habari wakuu? Naingia kwenye mada moja kwa moja bila kuwachosha. Baada ya Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) kutangaza matokeo ya mitihani ya Kidato cha Nne (CSE), nimetafakari sana na kugundua njia nzuri ya kuboresha elimu hapa nchini ni ama kufuta au kutaifisha shule zote za binafsi ili wanafunzi wote wakasome kwenye shule za umma (shule za kata).

Mfumo huu sio mgeni hapa duniani. Nchi nyingi za Ulaya, Asia na Marekani hawa-entertain uwepo wa shule binafsi kwani waligundua zinachangia sana kudhoofisha kiwango cha elimu katika nchi zao. Ndio maana Mwalimu Nyerere aliona hili tatizo mara baada ya nchi kupata uhuru akaamua kutaifisha shule za wamisionari na kuzirudisha serikalini. Sasa wakati umefika Rais Samia afuate nyayo za Nyerere ili kulikomboa taifa hili kielimu. Kuna sababu kadhaa zilizonifanya nitafakari jambo hili kwa kina:

Mosi, ikiwa shule binafsi zitataifishwa, kutakuwa hakuna mashindano ya ubora wa shule kwa kuangalia ufaulu. Kwa hiyo, suala la ku-promote shule kwa kuzichuanisha kiubora litakuwa limekufa kifo cha mende. Na serikali haitapata tena wakati mgumu kutangaza shule bora kwani shule zote zitakuwa na viwango sawa au vinavyokaribiana.

Pili, kwa kuwa hakutakuwa na sehemu mbadala ya kuwasomesha wanafunzi zaidi ya shule za kata, itawalazimu wananchi wote kuthamini shule hizi na kuhakikisha kuwa wanaziboresha kwa udi na uvumba. Kwa sasa sio watu wote wanaopenda kuona shule za kata zinakuwa bora kwani hata zikiendelea kuwa duni, wazazi wanazo shule mbadala ambako wanaweza kuwapeleka watoto wao kupata elimu bora. Wakikosa mbadala lazima tu wataboresha shule hizi ili watoto wao wapate elimu bora.

Tatu, kwa kuwa shule hizi zitakuwa zimewashikanisha watanzania wote kwa pamoja (kama ilivyokuwa kipindi cha Ujamaa na Kujitegemea), hii itasaidia kurudisha uzalendo wa kitaifa kwa wananchi ambao umeshuka kwa kiwango cha kutisha. Kwa mfano, imefika wakati sasa wazazi wenye uwezo wa kusomesha watoto wao kwenye shule binafsi hawaoni uchungu pale elimu kwenye shule za kata inaposhuka kwani wanaona hilo haliwahusu. Lakini wazazi wakishabanwa kusomesha watoto wao kwenye shule za kata (watake wasitake) lazima tu watakuwa na uchungu na maendeleo ya shule hizi.

Kwa mantiki hii, ipo haja ya serikali sikivu ya mama yetu mpendwa Rais Samia Suluhu Hassan kufuta shule zote za binafsi hapa nchini ili kila mtanzania mzalendo akamsomeshe mwanaye kwenye shule za kata. Hakuna namna nzuri ya kukuza uzalendo zaidi ya kuchukua maamuzi haya magumu. Najua wapo watakaonuna lakini hatimaye tutaelewana tu.

Nawasilisha
Teh! Bange + ugoro ni hatari kuliko cocaine na heroine
 
Kweli mleta mada, shule kama st Mary's, kemebos, st Francis, uwata girls, uwata boys na zingine za namna hiyo, futilia mbali majengo tuweke Kambi za jeshi na vituo vya afya... Elimu ni huduma not a means of gain, hatuwezi kuendelea na utaratibu wa kufanya elimu kama njia ya kuwaibia watu fedha.
 
Mkuu naona bado hujanielewa. Simaanishi kufuta kama kufuta bali namaanisha kutaifisha au kuhamisha umiliki kutoka binafsi kwenda serikalini (umma). Ina maana hizi shule bado zitaendelea kutoa huduma zikiwa chini ya serikali. Na walimu wanaofundisha kwenye shule hizi pia watapewa ajira serikalini. Nadhani sasa nimeeleweka.

😀😀😀
Mkuu hivi unaelewa mishahara wanayolipwa waalimu wanaofundisha hizo shule au unaandika humu?

Badala uishauri serikali ijenge mazingira mazuri ya utoaji Elimu, mishahara ya waalimu, zana za kufundishia na kujifunzia, n.k.

Mwalimu analipwa milioni 2 mpaka nne wa Private unataka akafundishe shule za government wanazolipwa laki 7?
 
Serikali ianzishe English medium zake za kulipia
 
Akili yako ndogo sana!

Halafu mtu kama huyu akiambiwa atoe mchango wa elimu katika Shule zake hizo za kata,povu kama lote!
Uzalendo haujengwi kwa kusomea ktk Shule za kata!

Mwigulu Nchemba analala na tai ya bendera ya Taifa lakini watoto wake nadhani wote wanasoma Feza!

Analipa karibia Milioni 40 kwa mwaka kama school fees.
UONGO Feza Primary Ada haifiki 10mil kwa Mwaka, hata A level haifiki hiyo ADA
 
Mkuu shule hizi hazifutwi bali umiliki wake unahamishiwa serikalini ili kuziboresha zaidi.
Unataka kuboresha shule ambazo tayari ni bora? Yani uichukue St.Francis uipeleke Serikalini ukaiboreshe?
 
No. Dhamira ni kujenga taifa lenye usawa wa kielimu na kimaendeleo kupitia kuboresha elimu ya umma kwa manufaa ya wananchi wote.
Chukua mfano kidato cha nne,darasa darasa lina watoto 800+ mikondo pengine hadi C au D,je darasa za kutosha walimu,wakutosha,je wanaweza kuhudumiwa vipi kwa idadi hiyo,wimbo wa ujenzi,unakwamia makooni mwetu,njoo kwenye namna ya ufikaji shule kwa idadi hiyo ya wanafunzi,hadi huruma,hili linachangia pakubwa utoro mashuleni na kulea tabia mbovu za kihuni,na ufaulu hafifu,kujaribu kuudhoofisha kwa namna yeyote watoa elimu,binafsi itakuwa ni kosa kubwa,sawa na kujikimu wenyewe 🤔
 
Nahitaji kuboresha elimu kupitia uzalendo ulio bora. Huwezi kuboresha elimu ikiwa uzalendo wa raia upo chini. Na uzalendo ukiwa chini, sio rahisi kuboresha elimu. Vitu hivi wiwili vinategemeana.....ni kama kuku na yai.
Naanza kukusoma kati kati ya mistari,naona umeamua kuwachokonoa na kuwadhihaki NECTA na zile sababu zao walizotaja za kutotaka kutangaza Shule 10 bora.
 
Back
Top Bottom