Maoni: Ili kujenga uzalendo, Serikali ifute shule zote binafsi hapa nchini tubaki na shule za kata tu!

Maoni: Ili kujenga uzalendo, Serikali ifute shule zote binafsi hapa nchini tubaki na shule za kata tu!

Habari wakuu?

Naingia kwenye mada moja kwa moja bila kuwachosha. Baada ya Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) kutangaza matokeo ya mitihani ya Kidato cha Nne (CSE), nimetafakari sana na kugundua njia nzuri ya kuboresha elimu hapa nchini ni ama kufuta au kutaifisha shule zote za binafsi ili wanafunzi wote wakasome kwenye shule za umma (shule za kata).​

Mfumo huu sio mgeni hapa duniani. Nchi nyingi za Ulaya, Asia na Marekani hawa-entertain uwepo wa shule binafsi kwani waligundua zinachangia sana kudhoofisha kiwango cha elimu katika nchi zao. Ndio maana Mwalimu Nyerere aliona hili tatizo mara baada ya nchi kupata uhuru akaamua kutaifisha shule za wamisionari na kuzirudisha serikalini. Sasa wakati umefika Rais Samia afuate nyayo za Nyerere ili kulikomboa taifa hili kielimu. Kuna sababu kadhaa zilizonifanya nitafakari jambo hili kwa kina:

Mosi, ikiwa shule binafsi zitataifishwa, kutakuwa hakuna mashindano ya ubora wa shule kwa kuangalia ufaulu. Kwa hiyo, suala la ku-promote shule kwa kuzichuanisha kiubora litakuwa limekufa kifo cha mende. Na serikali haitapata tena wakati mgumu kutangaza shule bora kwani shule zote zitakuwa na viwango sawa au vinavyokaribiana.

Pili, kwa kuwa hakutakuwa na sehemu mbadala ya kuwasomesha wanafunzi zaidi ya shule za kata, itawalazimu wananchi wote kuthamini shule hizi na kuhakikisha kuwa wanaziboresha kwa udi na uvumba. Kwa sasa sio watu wote wanaopenda kuona shule za kata zinakuwa bora kwani hata zikiendelea kuwa duni, wazazi wanazo shule mbadala ambako wanaweza kuwapeleka watoto wao kupata elimu bora. Wakikosa mbadala lazima tu wataboresha shule hizi ili watoto wao wapate elimu bora.

Tatu, kwa kuwa shule hizi zitakuwa zimewashikanisha watanzania wote kwa pamoja (kama ilivyokuwa kipindi cha Ujamaa na Kujitegemea), hii itasaidia kurudisha uzalendo wa kitaifa kwa wananchi ambao umeshuka kwa kiwango cha kutisha. Kwa mfano, imefika wakati sasa wazazi wenye uwezo wa kusomesha watoto wao kwenye shule binafsi hawaoni uchungu pale elimu kwenye shule za kata inaposhuka kwani wanaona hilo haliwahusu. Lakini wazazi wakishabanwa kusomesha watoto wao kwenye shule za kata (watake wasitake) lazima tu watakuwa na uchungu na maendeleo ya shule hizi.

Kwa mantiki hii, ipo haja ya serikali sikivu ya mama yetu mpendwa Rais Samia Suluhu Hassan kufuta shule zote za binafsi hapa nchini ili kila mtanzania mzalendo akamsomeshe mwanaye kwenye shule za kata. Hakuna namna nzuri ya kukuza uzalendo zaidi ya kuchukua maamuzi haya magumu. Najua wapo watakaonuna lakini hatimaye tutaelewana tu.

Nawasilisha​
Ulishafikiria kuwa kuna kodi ambazo serikali ya samia inazichukua toka kwenye haya mashule ili kuendeshea mambo yake.

Kama kuna point ya msingi ya kukupuuza basi ni ikifika kwenye swala la kodi.

Kumbuka shule za serikali zinatumia gharama toka serikalini tu. Hazizalishi sababu zinagharamiwa zaidi. Ila shule za private zinajiendesha kwa ada.
 
Habari wakuu?

Naingia kwenye mada moja kwa moja bila kuwachosha. Baada ya Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) kutangaza matokeo ya mitihani ya Kidato cha Nne (CSE), nimetafakari sana na kugundua njia nzuri ya kuboresha elimu hapa nchini ni ama kufuta au kutaifisha shule zote za binafsi ili wanafunzi wote wakasome kwenye shule za umma (shule za kata).​

Mfumo huu sio mgeni hapa duniani. Nchi nyingi za Ulaya, Asia na Marekani hawa-entertain uwepo wa shule binafsi kwani waligundua zinachangia sana kudhoofisha kiwango cha elimu katika nchi zao. Ndio maana Mwalimu Nyerere aliona hili tatizo mara baada ya nchi kupata uhuru akaamua kutaifisha shule za wamisionari na kuzirudisha serikalini. Sasa wakati umefika Rais Samia afuate nyayo za Nyerere ili kulikomboa taifa hili kielimu. Kuna sababu kadhaa zilizonifanya nitafakari jambo hili kwa kina:

Mosi, ikiwa shule binafsi zitataifishwa, kutakuwa hakuna mashindano ya ubora wa shule kwa kuangalia ufaulu. Kwa hiyo, suala la ku-promote shule kwa kuzichuanisha kiubora litakuwa limekufa kifo cha mende. Na serikali haitapata tena wakati mgumu kutangaza shule bora kwani shule zote zitakuwa na viwango sawa au vinavyokaribiana.

Pili, kwa kuwa hakutakuwa na sehemu mbadala ya kuwasomesha wanafunzi zaidi ya shule za kata, itawalazimu wananchi wote kuthamini shule hizi na kuhakikisha kuwa wanaziboresha kwa udi na uvumba. Kwa sasa sio watu wote wanaopenda kuona shule za kata zinakuwa bora kwani hata zikiendelea kuwa duni, wazazi wanazo shule mbadala ambako wanaweza kuwapeleka watoto wao kupata elimu bora. Wakikosa mbadala lazima tu wataboresha shule hizi ili watoto wao wapate elimu bora.

Tatu, kwa kuwa shule hizi zitakuwa zimewashikanisha watanzania wote kwa pamoja (kama ilivyokuwa kipindi cha Ujamaa na Kujitegemea), hii itasaidia kurudisha uzalendo wa kitaifa kwa wananchi ambao umeshuka kwa kiwango cha kutisha. Kwa mfano, imefika wakati sasa wazazi wenye uwezo wa kusomesha watoto wao kwenye shule binafsi hawaoni uchungu pale elimu kwenye shule za kata inaposhuka kwani wanaona hilo haliwahusu. Lakini wazazi wakishabanwa kusomesha watoto wao kwenye shule za kata (watake wasitake) lazima tu watakuwa na uchungu na maendeleo ya shule hizi.

Kwa mantiki hii, ipo haja ya serikali sikivu ya mama yetu mpendwa Rais Samia Suluhu Hassan kufuta shule zote za binafsi hapa nchini ili kila mtanzania mzalendo akamsomeshe mwanaye kwenye shule za kata. Hakuna namna nzuri ya kukuza uzalendo zaidi ya kuchukua maamuzi haya magumu. Najua wapo watakaonuna lakini hatimaye tutaelewana tu.

Nawasilisha​
Mzee baba, umefuka moshi wa kuni mbichi..!! Unakoelekea utataka;
1. Wanaosoma nje wote warudi wakasome UDOM etc
2. Wanaoishi nje nao warudi nyumbani wakaishi kishumundu
3. Wanaotibiwa nje wasiende kutibiwa huko, bali waende Mkuranga wakakutane na yule nesi aliyemnyima mjamzito vifaa vya kujifungulia
4. Wenye magari wote wayarudishe huko nje, wote tumiliki nyumbu
5. Computer zote zirudishwe kwao Japan na kwingineko, tubaki na BLACKBOARD zetu

If you think outside the box, hutawaza huo upuuzi unaouwaza in the name of UZALENDO
 
sasa utajue ubora wako kama hauna mshindani? kama hizi mlizonazo tu zimewashinda sasa mkitaifisha na hizo za private mtaziweza?
 
😀😀😀
Mkuu hivi unaelewa mishahara wanayolipwa waalimu wanaofundisha hizo shule au unaandika humu?

Badala uishauri serikali ijenge mazingira mazuri ya utoaji Elimu, mishahara ya waalimu, zana za kufundishia na kujifunzia, n.k.

Mwalimu analipwa milioni 2 mpaka nne wa Private unataka akafundishe shule za government wanazolipwa laki 7?
Mkuu unatakiwa kuwa mzalendo hata kama unalipwa mshahara kidogo unatakiwa upige kazi kwa uhakika.
 
Serikali inabid iboreshe hizo shule na sio kufuta shule binafsi,utakuta shule binafsi walimu wa hesabu wapo 3 tena wanafunzi sio wengi,sasa nenda serikalini mwalim wa hesabu mmoja tena huyo huyo kwa form one hadi 4 afu ukute darasa1 lina wanafunzi wengi,,Yan usiposoma tuition kuchomoka ngumu!
 
sasa utajue ubora wako kama hauna mshindani? kama hizi mlizonazo tu zimewashinda sasa mkitaifisha na hizo za private mtaziweza?
Sasa utashindanaje na mtu ambaye mazingira yenu hayafanani?
 
Sasa utashindanaje na mtu ambaye mazingira yenu hayafanani?
kwan wamezuiliwa kuziboresha? ndio waboreshe na wao kuanzia mazingira ya watumishi woa, mazingira ya shule zao nk ili waendane na washindani wao
 
Back
Top Bottom