Mara yangu ya kwanza kukutana na malaika(1987)

Mara yangu ya kwanza kukutana na malaika(1987)

Ulijuaje Kama alie kutokea Ni Malaika isije kua umetokewa na majini mzee
 
Acha kulipua hio sigara ya Urusi Braza [emoji2][emoji2] unaturushia sana...


Hivi unakumbukaje mambo yaliyotokea mwaka 1989 kwa usahihi hivyo???

Halafu malaika na vitu vya kufanana na malaika vyote vipo kwenye ulimwengu wa roho. Watu waache kuchanganya ulimwengu wa Roho na mwili kama wanavyichanganya UNIVERSE na COSMOS .
Hayo unayoona kama uko timamu ni Hallucination tu, labda kama unaona ukilala maana ulimwengu wa roho huwasiliana kwa ndoto pia.
Ila kimwili Malaika na Shetani ni matendo ya watu ikitegemeana na roho ipi iko ndani ya mtu husika (Mungu/Shetani anamtumia nani na kwa wakati gani)
Mfano;
Kuna vitu hutokea kwenye maisha unajikuta hii hio kawaida huyu mtu kama Mungu vile!

Ulimwengu wa roho kwenye mwili hauna nafasi bila mwili unao exist.
Punguza ujuaji brother.
 
Mzee mbona mmengangana bangi bangi..wew unakiamin ulichofundishwa kanisan au msikitini..what if si kwel...so watu wakija na bahar nyingne why usisome na kutulia uka judge mwenyew..unabak kusema bang bang...hii dunia ina watu 8bil...wakristu ni 20 % waisilamu sijui ..inamana hao wengne woote ni wajinga na iman wanazoamin...so ikiletwa hoja usikimbilie tu kusema bangi bangi....

Sent using Jamii Forums mobile app
Wajuaji ni wengi humu halafu wajinga wajinga tu hawana lolote wanalolijua.

Tuvumiliane tu.
 
Unaisoma biblia yote au unanukuu vifungu tu!?

Nipatie maelezo kuhusu mistari hii

1 Sina budi kujisifu, ijapokuwa haipendezi; lakini nitafikilia maono na mafunuo ya Bwana.
2 Wakorintho 12:1

2 Namjua mtu mmoja katika Kristo, yapata sasa miaka kumi na minne, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua). Mtu huyo alinyakuliwa juu mpaka mbingu ya tatu.
2 Wakorintho 12:2

3 Nami namjua mtu huyo, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua);
2 Wakorintho 12:3

4 ya kuwa alinyakuliwa mpaka Peponi, akasikia maneno yasiyotamkika, ambayo haijuzu mwanadamu ayanene.
2 Wakorintho 12:4
Samahn kwa kuingilia... Naomba nijuze siri ya number 3 na nguvu ya mfungo wa Tatu kavu
 
jamaa smart sana asante kwa ujumbe nimejifuna kitu akija tena ukipost ni tag...
 
kila anachoongea nikweli jinsi duniani tunavyozidi kuungana tunaidi kua na Amani tunazidi kujua vitu vingi furaha uleta aman na upendo na hapo ndipo tunapo mtukuza MUNGU achana na dini japo akuna dini duniani inayo ubiri chuki nyingi zazo zinatangaza Amani na upendo na Umoja sema tu vitabu na maandishi ndo yapo tofauti ila vyote vinakauli mbiu moja kutangaza Amani furaha na upendo tu
 
Aliendelea kuniambia,

Imani ni hisia, imani ipo moyoni. Basi sasa imani pasipo matakwa, imani pasipo akili haiwezi kufanya chochote.

Vivyo hivyo matakwa, akili pasipo imani haiviwezi kufanya chochote. Basi sasa mwenye imani lazima awe na akili. Na mwenye akili lazima awe na imani.

Kisha malaika akanichukua na kunipeleka sehemu nyingine. Akanionesha eneo kubwa lililojaa viumbe waliofanana na wanadamu. Miiliyao siyo ngozi kama za kwetu, ngozi zao mithili ya chuma. Malaika akaniambia, umeona wale!? Nikasema ndio nimewaona. Hao ni watu kama wewe wapo katika ulimwengu wa mwili mwingine. Wamevaa miili ya chuma maana ulimwengu unaoishi wewe ni tofauti na huu. Hapo wapo katika makutano makuu kwa imani yao wanamwabudu Mungu wao.

Kisha nikamuuliza je, hapo ni wapi!? Sisi tunaweza kufika hapo!?
Akanijibu na kusema hapo ni ulimwengu wa mwili mwingine ili uweze kwenda katika ulimwengu huo wa mwili ni lazima uondoke katika ulimwengu huu wa mwili wako na utaweza kwenda huko. Akaniambia katika ulimwengu wenu wa mwili mnaweza kusafiri kwenda sehemu yoyote ya ulimwengu wenu. Pale mtakapopata na maarifa na kuwa kitu kimoja mtaweza kusafiri katika ulimwengu wote wa mwili. Umesoma kuhusu sayari, umesoma kuhusu nyota ndivyo hivyo mtakuwa na uwezo wa kusafiri kutoka sayari nyingine na kwenda nyingine. Lakini hao unaowaona hawapo katika sehemu ya ulimwengu wenu wa mwili.

Hekima hii mwenye ufahamu aifahamu na mwenye kujua aijue. Ulimwengu wenu upo kwaajili yenu. Ndio maana mnaweza kuuona kwa macho yenu na vifaa vyenu. Lakini ulimwengu mwingine wa mwili hauwezi kuuona kwa macho yenu na vifaa vyenu. Hisia na matakwa yako yatakufanya uweze kuuona ulimwengu mwingine na siyo kuishi ukiwa kwenye mwili huu wa sasa.

Ulimwengu wa mwili upo mwingi tu, kila sehemu yao wanaishi kwa namna yao. Ukiwa katika ulimwengu wa roho utaweza kuuona bali hutaweza kuishi mpaka utakapovishwa mwili wa ulimwengu huo.

Mwenye ufahamu atambue haya....
Daaàh Mzee huyo malaika ni muongo sijapata kuona!! Hahaha [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mwenye ufahamu afahamu haaya....

Kisha malaika akaniambia. Malaika akaniambia, kwa habari ya imani, ni jambo la moyo. Unataka ujue imani yako iendane na akili yako.

Ulimwengu wenu wa mwili mpo na imani zenu, zitumieni hizo imani zenu kujenga umoja ili muweze kuangaziwa. Mkiacha kushindana na kuanza kuaminiana ndipo imani zenu zitakapo zaa matunda.

Mwingine anaamini katika Mungu, mwingine anaamini katika jua, na mwingine anamini katika Miungu wengi. Hakika nakuambia imani ni hisia ni mlango wa kuunganisha mwili na ulimwengu wa roho ili uangaziwe.

Utakapojua kuwa imani ni hisia, utakuwa umeangaziwa. Mwingine imani yake ipo katika majira, mwingine katika mimea na mwingine sehemu tofauti tofuati. Nakusihi uelewe kuwa hayo yote yapo katika moyo ili kujenga hisia na kuzalisha nguvu ya kiroho. Nakuambia hivi leo usingejua kama kuna giza kama mwanga usingekuwepo. Vivyo hivyo mwanga usingekuwa na maana yoyote kama giza halipo. Yapo yanatakiwa kufanyika gizani na mengine yapo yanatakiwa kufanyika kwenye mwanga.

Mwenye ufahamu afahamu haya. Imani yako iunganishe na matakwa. Koleza moto wa imani huku akili yako ikiwa sawa.
Yaani Mkuu ungemshitukia mapema huyo jamaa kwamba anakupiga na kitu kizito ungemwacha amtafute mtu mwingine aizee!!
 
Mwenye ufahamu afahamu haaya....

Kisha malaika akaniambia. Malaika akaniambia, kwa habari ya imani, ni jambo la moyo. Unataka ujue imani yako iendane na akili yako.

Ulimwengu wenu wa mwili mpo na imani zenu, zitumieni hizo imani zenu kujenga umoja ili muweze kuangaziwa. Mkiacha kushindana na kuanza kuaminiana ndipo imani zenu zitakapo zaa matunda.

Mwingine anaamini katika Mungu, mwingine anaamini katika jua, na mwingine anamini katika Miungu wengi. Hakika nakuambia imani ni hisia ni mlango wa kuunganisha mwili na ulimwengu wa roho ili uangaziwe.

Utakapojua kuwa imani ni hisia, utakuwa umeangaziwa. Mwingine imani yake ipo katika majira, mwingine katika mimea na mwingine sehemu tofauti tofuati. Nakusihi uelewe kuwa hayo yote yapo katika moyo ili kujenga hisia na kuzalisha nguvu ya kiroho. Nakuambia hivi leo usingejua kama kuna giza kama mwanga usingekuwepo. Vivyo hivyo mwanga usingekuwa na maana yoyote kama giza halipo. Yapo yanatakiwa kufanyika gizani na mengine yapo yanatakiwa kufanyika kwenye mwanga.

Mwenye ufahamu afahamu haya. Imani yako iunganishe na matakwa. Koleza moto wa imani huku akili yako ikiwa sawa.
Mi naona Mzee unachojaribu hapa ni kutulazimishia tu fikra na na Mitazamo yako to kwa kisingizio cha malaika!! [emoji23] [emoji23] Binafsi nimekushitukia!!
 
Za masaa wana JF.

Leo nimeona ni vyema kuwaletea kisa kilichonitokea mwaka 1987 nikiwa kidato cha tano huko Ilboru secondary school. Nilikuwa nikisikia tu habari za malaika kwenye ibada za kidini.

Siku hiyo niliamka usiku kwenda kusoma darasani kama kawaida yangu, yapata saa nane za usiku. Hakukuwa na mtu yeyote darasani bali mimi tu. Wakati naendelea na kubukua ghafla ukatokea mwanga mkali mbele yangu. Ukaniangazia, niliingiwa na hofu na kuanza kutetemeka. Mara nikasikia sauti ya binadamu ikitoka kwenye mwanga ule. Ikiinita jina langu David, David usiogope tazama hapa.

Nilijawa na nguvu na kukaza macho yangu kuutanzama ule mwanga. Ghafla nimuona kiumbe afananae na mwanadamu rangi yake ya silver inayong'aa sana. Mdomo wangu ulikuwa mzito nilishindwa kuongea. Yule kiumbe alinisogelea na kuniambia "Nimekuja kukupa siri ya ulimwengu" Ndipo kiumve hicho kilinigusa kidevu changu, nilihisi kupigwa shot ya umeme. Akaendelea kusema mimi ni malaika, nimekuja kujidhilisha kwako. Ndipo mwili wangu wote ulianza kutetemeka. Alinishika na nikajikuta nipo katika eneo ambalo sijawahi kuliona ni zuri sana.

Akaniambia hapa ndipo huja watu wanapokufa duniani. Alinionesha watu mbalimbali waliokufa, walikuwa pale wakiwa na furaha. Nilimuona mwalimu wangu wa Hisabati kidato cha pili aliyekufa kwa ajali ya gari. Nilimuona akiwa na furaha.

Malaika huyo aliniambia usiogope kuhusu kifo maana ni sehemu ya ukamilisho.

Ni mambo mengi mno niliyapata siku hiyo. Kwa leo naongelea haya tu. Mpaka sasa malaika mbalimbali huwa wanakuja. Nimeshawazoea na tunaongea nao mambo mengi tu.

Nitakuja kuwaeleza namna yetu sisi tulivyofungwa kwenye kifungo cha hapa duniani. Na namna gani ya kuuona ulimwengu wote.

Asante kwa sasa.
Wenu mtiifu D.
Utakua na roho safi sana, na utakua unaomba sana sio rahisi hivyo malaika kumtokea mtu
 
[emoji22][emoji22] Kaka.... mbona unatulisha matango pori...??
74cb0d1c4a4039971641b5e878b8753d%20(1).jpg
 
Back
Top Bottom