Marekani: Ndani ya siku 100 tu deni la taifa la Marekani lafikia $35 trillion kutoka $34 trillion

Marekani: Ndani ya siku 100 tu deni la taifa la Marekani lafikia $35 trillion kutoka $34 trillion

Xi Jinping

JF-Expert Member
Joined
Jun 14, 2023
Posts
3,651
Reaction score
11,548
Deni la taifa la Marekani au kama wao wanavyoliita Federal Debt, Government Debt, National Debt, U.S Public Debt linapaa kwa kasi sana limefikia $35 trillion ambalo ni sawa na $104,082 kwa kila mtu anayeishi Marekani.​

20240617_002531.jpg

Deni la taifa la Marekani linakua kwa kasi zaidi kuliko uchumi.

Kuna sababu kadhaa zinazotajwa kuifanya serikali ya Marekani au unaweza kuiita the Federal Government ifikie hatua ya kukopa kutoka kwa wakopeshaji (creditors) wa ndani au wa nje ni kuongezeka matumizi ya serikali kuliko mapato yanayokusanywa.

Hii imepelekea Marekani iwe na ufinyu wa bajeti (deficit budget), bajeti ya serikali inapokuwa kubwa kuzidi mapato yake. Kwa mfano:

Mwaka wa fedha wa 2023 serikali ya Marekani ilitumia $6.13 trillion na kukusanya $4.44 trillion tu.
–The Fed


Mara ya mwisho Marekani kuwa na ziada ya bajeti (surplus budget) yaani matumizi ya serikali yanapokuwa chini ya mapato yanayokusanywa kupitia kodi, ilikuwa ni 2001.

Sehemu kubwa ya pesa ambazo Marekani inakusanya ili kufidia ufinyu wa gharama ni kwa kuuza bonds.

Kwa sasa kwa wastani Marekani inatengeneza deni la $1 trillion kila baada ya siku 100 au $10 billion kwa siku.
 
Ndio maana The Federal Reserve na The US Treasury wanapambana sana kuuza bonds za serikali kuraise pato la serikali
Na hapo kwenye kuuza bonds The Fed (benki kuu) na Treasury (hazina) wanalenga sana kuwauzia investors wa ndani na wa nje kama foreign central banks na foreign private investors
 
Deni la taifa la Marekani au kama wao wanavyoliita Federal Debt, Government Debt, National Debt, U.S Public Debt linapaa kwa kasi sana limefikia $35 trillion ambalo ni sawa na $104,082 kwa kila mtu anayeishi Marekani.​

View attachment 3067380
Deni la taifa la Marekani linakua kwa kasi zaidi kuliko uchumi.

Kuna sababu kadhaa zinazotajwa kuifanya serikali ya Marekani au unaweza kuiita the Federal Government ifikie hatua ya kukopa kutoka kwa wakopeshaji (creditors) wa ndani au wa nje ni kuongezeka matumizi ya serikali kuliko mapato yanayokusanywa.

Hii imepelekea Marekani iwe na ufinyu wa bajeti (deficit budget), bajeti ya serikali inapokuwa kubwa kuzidi mapato yake. Kwa mfano:

Mwaka wa fedha wa 2023 serikali ya Marekani ilitumia $6.13 trillion na kukusanya $4.44 trillion tu.
–The Fed


Mara ya mwisho Marekani kuwa na ziada ya bajeti (surplus budget) yaani matumizi ya serikali yanapokuwa chini ya mapato yanayokusanywa kupitia kodi, ilikuwa ni 2001.

Kwa sasa kwa wastani Marekani inatengeneza deni la $1 trillion kila baada ya siku 100 au $10 billion kwa siku.
Watakuja kumlalamikia mama…

Hawana Jema
 
Deni la taifa la Marekani, lililo katika dola za Kimarekani, wanazozi control na kuzichapisha Wamarekani, halina usawa na deni la taifa la nchi nyingine.

Kwa sababu wao ndio wana control na kuchapisha dola za Kimarekani.

Ni sawa na serikali ya Tanzania idaiwe katika shilingi za Kitanzania, hela ambazo ina uwezo wa kuzichapisha.

Kitu muhimu ni ku control inflation tu.
 
Deni la taifa la Marekani, lililo katika dola za Kimarekani, wanazozi control na kuzichapisha Wamarekani, halina usawa na deni la taifa la nchi nyingine.

Kwa sababu wao ndio wana control na kuchapisha dola za Kimarekani.

Ni sawa na serikali ya Tanzania idaiwe katika shilingi za Kitanzania, hela ambazo ina uwezo wa kuzichapisha.

Kitu muhimu ni ku control inflation tu.
Unamaanisha watachapisha Dola nyingi ili kulipa hilo deni?
 
Deni la taifa la Marekani, lililo katika dola za Kimarekani, wanazozi control na kuzichapisha Wamarekani, halina usawa na deni la taifa la nchi nyingine.

Kwa sababu wao ndio wana control na kuchapisha dola za Kimarekani.

Ni sawa na serikali ya Tanzania idaiwe katika shilingi za Kitanzania, hela ambazo ina uwezo wa kuzichapisha.

Kitu muhimu ni ku control inflation tu.
Msisahau kuwa hata Tz deni limeongezeka kwa siku miamoja kwa kiasi cha trillion 37.0
 
Doesn’t add up $35 trillion ni national debt (not public debt).

National debt ina public debt (deni la serikali) na private debt (madeni ya wananchi).

Deni la serikali kwa marekani lipo kwenye (bonds).

Private debt lipo kwenye amana za banks na Skiba za wananchi.

Unapoangalia mikopo ya taifa kama la marekani kwenye deni la taifa (private debt Ndio shida zaidi). Why? Sehemu kubwa ya hiyo mikopo ipo kwenye secured loans (mortgages) na sehemu ya pili credit (mikopo ya Visa cards, car loans and other credits madukani).

Sustainability ya private loans depends on macro economy activities mainly employment figure (high employments) equates high taxes and maintanance of public and private debt.

Then there is also the equation of inflation in macro economy,

Nimechangia tu juu kwa juu; point ya msingi kuongelea maswala ya madeni ya nchi ziliziendelea unahitaji wa uelewa namna gani mwenendo wa economic data una impact kwenye deni.

The world don’t take lightly US debt bila ya kusoma data muhimu za uchumi wake. Kama ni hatari banks na international investors zikianza kutoa hela zake na credit ratings kushuka the.n it becomes.

You need to understand economics to see the value of the post.
 
Deni la taifa la Marekani, lililo katika dola za Kimarekani, wanazozi control na kuzichapisha Wamarekani, halina usawa na deni la taifa la nchi nyingine.

Kwa sababu wao ndio wana control na kuchapisha dola za Kimarekani.

Ni sawa na serikali ya Tanzania idaiwe katika shilingi za Kitanzania, hela ambazo ina uwezo wa kuzichapisha.

Kitu muhimu ni ku control inflation tu.
Kwa hiyo dawa ni kuchapisha dollars sio?

Kwa hiyo the U.S Treasury na Federal Reserve waiamuru the Bureau of Engraving and Printing iprint notes walipe madeni?
 
Back
Top Bottom