Masikini kuwaza kujenga nyumba ya kuishi ni umasikini pia

Masikini kuwaza kujenga nyumba ya kuishi ni umasikini pia

Mtu unajibana wee Ili ujenge nyumba ya kuishi, ukimaliza unaanza kuishi kwenye hiyo nyumba kwa tabu nyingi. Ingekuwa na maana kama kungekuwa na maisha bila kifo, umasikini uliouchochea kwa kujenga ungepambana nao kwa kuwa muda upo tu. Kama we masikini pambana uweze kipato cha uhakika ambacho ndio kitawezesha mengine ikiwamo ujenzi.
Naishi kwangu sipanga, lakini nauli ya kuwapa watoto kwenda shule shida watoto wangu sale za shule zimechanika wanavaa yebo wali nyama wanausikia kwa jirani kutwa ugali vamia,lakini niko kwangu sipanga[emoji14][emoji14][emoji14]
 
Ukitaka kuona Umuhimu wa Kujenga, Kufa alafu uache watoto wako 3 ama 4 kwenye nyumba ya Kupanga.

Hata kama unadhani ni umasikini kuanza kujenga lakini ni muhimu sana Kaka. Tafakari kwenye hilo

Hakuna Baba mwenye gari ila kuna Baba mwenye nyumba.
Ukumuelewa nilivyo muelewa nikwamba bora kuimalisha uchumi kwanza kisha mengine yatafuata tena kwa wepesi,mfano mama rishi au muuza nyaya au mbeba mizigo anajibana kwa ajili ya kujenga nyumba badala ajibane kupanua wigo wa kazi yake mfano mama rishe kutwa anaungua moto bora ajibane abadilishe kazi kisha atajenga kuliko kujenga na kuhamia huku ukiendela kubeba mizigo mabibo
 
Nimezunguka sana nyumba za kupanga faida niliyoipata ni kukosa furaha na amani ndani ya nyumba hizo..

Sasa nipo kwangu wanangu wanazunguka ndani ya fensi Kwa furaha mtambuka...

Kupanga ni kuchagua. Over
Ukishindwa kupanga uwezi kujenge kuna upangaji wa aina 2 kupanga nyumba yenye familia zaidi ya 10 kuoga kujisaidia kwa foleni pia kuna upangaji wa nyumba ya pekee yako wewe ulikuwa unapanga nyumba gani kati ya hizo?
 
Ukitaka kuona Umuhimu wa Kujenga, Kufa alafu uache watoto wako 3 ama 4 kwenye nyumba ya Kupanga.

Hata kama unadhani ni umasikini kuanza kujenga lakini ni muhimu sana Kaka. Tafakari kwenye hilo

Hakuna Baba mwenye gari ila kuna Baba mwenye nyumba.

Kweli,Ila utaonaje wakati umekufa
 
Kujenga ni muhimu hata Kama hauna Familia.

Then MAZINGIRA ya Biashara kwa nchi Kama TANZANIA sio consistentlce so unaweza kufanyiwa sabotage na serikali ukajikuta unabaki 0-0

Binafsi Napenda kujenga jumba kubwa kibaha kufika 2025 liwe limekamilika .
Tatizo wabongo ufahamu wao mdogo jamaa akupinga kujenga mueleweni kwanza
 
Ata na Mim ninA mawazo hayo ya kimaskin [emoji16][emoji112]
 
Ukitaka kuona Umuhimu wa Kujenga, Kufa alafu uache watoto wako 3 ama 4 kwenye nyumba ya Kupanga.

Hata kama unadhani ni umasikini kuanza kujenga lakini ni muhimu sana Kaka. Tafakari kwenye hilo

Hakuna Baba mwenye gari ila kuna Baba mwenye nyumba.
Mawazo ya kimaskini kabisa haya, hizo nyumba zinapigwa bei ili watoto wapate mitaji wafanye mambo yao.
 
Nimezunguka sana nyumba za kupanga faida niliyoipata ni kukosa furaha na amani ndani ya nyumba hizo..

Sasa nipo kwangu wanangu wanazunguka ndani ya fensi Kwa furaha mtambuka...

Kupanga ni kuchagua. Over
Hujakatazwa kujenga,ila jenga uchumi imara kwanza.
 
Mawazo ya kimaskini kabisa haya, hizo nyumba zinapigwa bei ili watoto wapate mitaji wafanye mambo yao.
Wanauza sio wapate mitaji, wanauza wasovu maisha ya kugombania gombana kila siku kwa kukaa pamoja.

Familia zinazouza nyumba wagawane hela sio kwa kupenda
 
Katika maisha ya mwanada Nyumba ni hitaji la muhimu sana.
Waliosoma Manslow Theory of Human Needs wanafanamu vizuri.

Mtu unaenda kufanya kazi mbali na Nyumbani kwako. Manyanyaso ya nyumba za kupanga yanafahamika.

Ni bora ujenge hata chumba kimoja chako uanzie maisha, huku ukiendelea kujenga kidogo kidogo.

Tulioanzia nyumba za kupanga tunazifahamu kadhia zake.
Manyanyaso ya nyumba ya kupanga ni kwa kapuku,siyo kwa mwenye hela,wewe unaye bangaiza kulipa kodi ya afu 50 kwa mwezi ni tofaut na yule anaye lipa laki 3 kwa mwezi. Pia tambua kuwa siyo kila aliye panga hana uwezo wa kujenga..ni malengo na vipaumbele
 
Wanaoponda kujenga mbona hatuwaoni kuishi chini ya miti au mapangoni, tunaona wamepanga au wapo home na hizo nyumba nawao wasingeJenga Kama wao wanaosema kujenga ni uoga wa maisha wangekaa mapangoni labda.
Jengeni,sisi tutapanga.
 
Ukumuelewa nilivyo muelewa nikwamba bora kuimalisha uchumi kwanza kisha mengine yatafuata tena kwa wepesi,mfano mama rishi au muuza nyaya au mbeba mizigo anajibana kwa ajili ya kujenga nyumba badala ajibane kupanua wigo wa kazi yake mfano mama rishe kutwa anaungua moto bora ajibane abadilishe kazi kisha atajenga kuliko kujenga na kuhamia huku ukiendela kubeba mizigo mabibo
Umenisoma
 
Wabongo aka waturutumbi wao wanachojua uwa ni kujenga nyumba tu ndio investment, kumbe ni akili za kimaskini walizonazo. Kujenga nyumba ni investment ikiwa tu hio nyumba ni ya kupangisha sio kuishi otherwise ni liability, utumie milioni 100 uisimike tu hapo ardhini huku unapiga miayo kila siku mwishowe ufe kwa diabetes shauri ya kufakamia vyakula vya ng'ombe i.e ugali wa mahindi na maharage 😂 😂 😂 . waturutumbi aka wabongo uwa hawawazi kua hio pesa ya kujenga wangeweka fixed deposits au wangenunua bonds BOT ni investment nzuri kuliko kujenga kibanda huko kigamboni. US baby. 😂 😂 😂 😂
Hata akiweka UTT ndani ya miaka mitano hyo pesa inakuwa nyingi. Tatizo wabongo ni wavivu wa kutafuta maarifa. Kila mtu anawaza kujenga tu. Hakuna anaye waza hata kuwekeza,ni nyumba tu.
 
Mtu unajibana wee Ili ujenge nyumba ya kuishi, ukimaliza unaanza kuishi kwenye hiyo nyumba kwa tabu nyingi. Ingekuwa na maana kama kungekuwa na maisha bila kifo, umasikini uliouchochea kwa kujenga ungepambana nao kwa kuwa muda upo tu. Kama we masikini pambana uweze kipato cha uhakika ambacho ndio kitawezesha mengine ikiwamo ujenzi.
Watu Hawa ndio wakudai katiba Mpya Aisee
 
Back
Top Bottom