Masikini kuwaza kujenga nyumba ya kuishi ni umasikini pia

Masikini kuwaza kujenga nyumba ya kuishi ni umasikini pia

Nachomaanisha masikini kama unaona kabisa huna kipato cha kuanzisha ujenzi basi hicho kidogo peleka kwenye msosi, mavazi na mengine huku ukiendelea kuimarisha vyanzo vya pesa. Vyanzo vikiruhusu Jenga.
Tatizo la watu hawajakuelewa wako wanajua hutaki kabisa kujenga!
Ukiwa na kipato cha uhakika utajenga bila kuyumbisha mfumo wako wa maisha!
Ndo maana maisha ukae kwenu,upange au ujenge gharama za maisha ziko pale pale!
Kwa wale wenye kipato cha uhakika wajenge tu hakuna shida!
Ila kama unajitafuta unapata 20,000 kwa siku unataka ujenge familia ile hapo lazima uchemke!
Kwa nini usiwekeze kwenye kitu uanchofanya huku ukifanya saving na kuwekeza kidogo kidogo na baadae itapanda na kufikia hata 50,000 kwa siku na hapo unaweza kuanza kujenga pole pole bila kuvuruga mtaji!
Ila kuanza kujenga tu bila kutazama uchumi wako vizuri lazima kwa mbeleni uje uteteleke na waliopanga watakuzidi ubora wa maisha!
 
Wewe hujamwelewa mtoa mada! Anamaanisha kujenga bila kuwa na uchumi wa uhakika ni Umasikini!
Mfano unajenga nyumba ya million 100 kwa kijibana unakaa humo lakini mifumo yako ya fedha ishaharibika utakomea kuishi maisha duni tu!
Lakini mtu akiwekeza hiyo hela na akaanza kujenga taratibu bila kuharibu capital yake ina maana atajenga na atamaliza nyumba yake akiwa na uchumi wake imara!
Sasa mtu kama ameweza kupata hiyo milion 100 akajenga nyumba atashindwaje kupata hela ndogo ya kujikimu kwenye maisha yake.
 
Mtu unajibana wee Ili ujenge nyumba ya kuishi, ukimaliza unaanza kuishi kwenye hiyo nyumba kwa tabu nyingi. Ingekuwa na maana kama kungekuwa na maisha bila kifo, umasikini uliouchochea kwa kujenga ungepambana nao kwa kuwa muda upo tu. Kama we masikini pambana uweze kipato cha uhakika ambacho ndio kitawezesha mengine ikiwamo ujenzi.
Hesabu ya kipato chako ndiyo itakayo amua,, ujenge au upange
 
Sasa mtu kama ameweza kupata hiyo milion 100 akajenga nyumba atashindwaje kupata hela ndogo ya kujikimu kwenye maisha yake.
Mimi nina mifano mingi sana!
Bila kuwa na biashara au shughuli ya kukufanya uwe na mzunguko wa pesa haijarishi umejenga lazima maisha yakupige!
Kikubwa kuliko vyote tufanye mambo kwa uwiano!
Tusijenge kuonekana tunajenga tu mda mwingine hata ubora wa nyumba ni mdogo!
Tujenge kwa kujua kesho kuna maisha pia na nyumba haitaingiza fedha ni Liability kwa hiyo lazima tujue gharama ziko pale pale na haziepukiki!
Hata watu wanaostaafu na kupata changamoto ya kiafya baada ya uchumi kupungua sio kwamba huwa hawana nyumba ila huwa hawana fedha ndo maana yanawatokea madhira ya kiafya na kufa mapema!
 
Kujenga ni sahihi katika hali yoyote ile. Ukikosa yote utarudi kula hayo matembere uliyopanda nje kwako. Sasa huna kodi hizo tembere utachuma wapi? Stand za mabasi?

BINAFSI NAONA NI SAHIHI SANA, KAMA UNA KAENEO KAKO NA UNA KAAKIBA KANAKOTOSHA KUSIMAMISHA HATA CHUMBA, SIMAMISHA KWANZA HALAFU NDO TAFUTA PESA NYINGINE ZA BIASHARA. KAMA UNAPENDA SANA BIASHARA KULIKO NYUMBA BASI FANYA KAMA HIYO PESA ULIIPELEKA KWENYE BIASHARA MTAJI UKAKATA HIVYO UNAANZA UPYA ILA ULIIJENGEA.
Sasa kachumba ndio nyumba!


Elimu ya fedha ni shida sana Kwa mapumbavu kama wewe.



Endeleeni kupigwa shwain wewe maana mnaelimishwa ila vichwa ni kama mmekodisha ubongo

Sent from my Pixel 5 using JamiiForums mobile app
 
Mimi nina mifano mingi sana!
Bila kuwa na biashara au shughuli ya kukufanya uwe na mzunguko wa pesa haijarishi umejenga lazima maisha yakupige!
Kikubwa kuliko vyote tufanye mambo kwa uwiano!
Tusijenge kuonekana tunajenga tu mda mwingine hata ubora wa nyumba ni mdogo!
Tujenge kwa kujua kesho kuna maisha pia na nyumba haitaingiza fedha ni Liability kwa hiyo lazima tujue gharama ziko pale pale na haziepukiki!
Hata watu wanaostaafu na kupata changamoto ya kiafya baada ya uchumi kupungua sio kwamba huwa hawana nyumba ila huwa hawana fedha ndo maana yanawatokea madhira ya kiafya na kufa mapema!
Mkuu umenikumbusha point ya kujenga Ili kuonekana unajenga. Hii imetuharibu akili, mtu anaona akijenga basi maisha kayapatia jambo ambalo si kweli. Umejenga sawa halafu mahitaji mengine unashindwa kumudu hapo ni bilabila.
 
Mkuu umenikumbusha point ya kujenga Ili kuonekana unajenga. Hii imetuharibu akili, mtu anaona akijenga basi maisha kayapatia jambo ambalo si kweli. Umejenga sawa halafu mahitaji mengine unashindwa kumudu hapo ni bilabila.
Kikubwa ni kubalance mambo!🙏
 
Nachomaanisha masikini kama unaona kabisa huna kipato cha kuanzisha ujenzi basi hicho kidogo peleka kwenye msosi, mavazi na mengine huku ukiendelea kuimarisha vyanzo vya pesa. Vyanzo vikiruhusu Jenga.
Unajua mkuu, Binafsi huwa naamini zipo nyakati unaweza kosa nguvu za kutafuta pesa ya kodi ila ukawa na nguvu kiasi ya kutafuta chochote cha kujaza tumbo. Hii inaweza sababishwa na lolote. Maradhi, uzee, mkosi, mtaji kupotea, kukosa kazi n.k

Sasa ukishakula ukishashiba utalala kwa nani? Bora udundulize tu ikiisha hata chumba kimoja utalala hapo iwapo lolote limekupata ukashindwa kuitafuta kodi.
 
Unajua mkuu, Binafsi huwa naamini zipo nyakati unaweza kosa nguvu za kutafuta pesa ya kodi ila ukawa na nguvu kiasi ya kutafuta chochote cha kujaza tumbo. Hii inaweza sababishwa na lolote. Maradhi, uzee, mkosi, mtaji kupotea, kukosa kazi n.k

Sasa ukishakula ukishashiba utalala kwa nani? Bora udundulize tu ikiisha hata chumba kimoja utalala hapo.
Wewe nasema bado hujaelewa!
Mtoa mada hajasema usijenge kasema imarisha kwanza uchumi wako then jenga!
Sema Masikini wengi hata akiwa kijana mdogo kwenye 20 atalazimisha kujenga lakini hawazi kabisa kuimarisha uchumi wake kwanza then ujenge!
 
Sasa kachumba ndio nyumba!


Elimu ya fedha ni shida sana Kwa mapumbavu kama wewe.



Endeleeni kupigwa shwain wewe maana mnaelimishwa ila vichwa ni kama mmekodisha ubongo

Sent from my Pixel 5 using JamiiForums mobile app
Mwenye jumba la vyumba nane na mwenye chuma kimoja wote wanalala kwenye chumba kimoja na wote hawalipi kodi.

Haya mengine ya elimu sijui fedha ni mfumo wako wa maisha si lazima kila mtu awe tajiri kama wewe mwenye elimu kubwa ya fedha.
 
Wewe nasema bado hujaelewa!
Mtoa mada hajasema usijenge kasema imarisha kwanza uchumi wako then jenga!
Sema Masikini wengi hata akiwa kijana mdogo kwenye 20 atalazimisha kujenga lakini hawazi kabisa kuimarisha uchumi wake kwanza then ujenge!
Mm nimesema ukiweza dunduliza ukajenga ni sahihi sababu naamini uchumi haujaagi.
 
Kijana akiwa na miaka 25 Kama hakuweza kujenga mjini ila akawa na kabalance kake akaamua aende kerege pwani au bunju mwisho kule akachukua plot taratibu na kwa tabu akajenga chumba na sebule akamwacha mtu akae kwa makubaliano yeye akaendelea kubaki kariakoo akipambana na sasa ana 50 hawezi tena mikiki ya kupambana na kifua kinamsumbua sababu ya kubeba magunia akienda hapo bunju kulivyoendelea na thamani yake ya sasa ataona alifanya maamuzi sahihi miaka 25 iliyopita.
 
Unaponda walio jenga wakati huo unaishi kwenye nyumba iliyo jengwa na wanaume wenzio hivi una akili kweli?

Kama kujenga hakuna maana mbona hujaenda kuishi juu ya mti?
mwambie
 
Siku ukitafuniwa mkeo na baba mwenye nyumba wako ndy akili itakukaa sawa,,


Jiulize kwann hata ndege wanahangaika kujenga viota vyao?
Sembuse wewe mwanadamu uendelee kuishi kwenye nyumba ya mwanaume mwenzio.
kweli
 
Katika maisha ya mwanada Nyumba ni hitaji la muhimu sana.
Waliosoma Manslow Theory of Human Needs wanafanamu vizuri.

Mtu unaenda kufanya kazi mbali na Nyumbani kwako. Manyanyaso ya nyumba za kupanga yanafahamika.

Ni bora ujenge hata chumba kimoja chako uanzie maisha, huku ukiendelea kujenga kidogo kidogo.

Tulioanzia nyumba za kupanga tunazifahamu kadhia zake.
embu tuma hapa
 
Kijana akiwa na miaka 25 Kama hakuweza kujenga mjini ila akawa na kabalance kake akaamua aende kerege pwani au bunju mwisho kule akachukua plot taratibu na kwa tabu akajenga chumba na sebule akamwacha mtu akae kwa makubaliano yeye akaendelea kubaki kariakoo akipambana na sasa ana 50 hawezi tena mikiki ya kupambana na kifua kinamsumbua sababu ya kubeba magunia akienda hapo bunju kulivyoendelea na thamani yake ya sasa ataona alifanya maamuzi sahihi miaka 25 iliyopita.
gud
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Unafukia millions chini halafu unamadeni kibao...mwisho hata na nyumba yenyewe ukiiangalia ham huna na ukute umejenga nje ya mji mbali na kazini hapo zinakuja gharama za usafiri.
 
Back
Top Bottom