Biashara ya cm haitofautiani sana na games za pes/pro evolution soccer so kila mwaka ni bandika bandua!
Hao jamaa wenye hizo kuzitengeneza hawalali kuzi promote na kuonyesha zilivyo na uzuri ama utamu utadhani is our basic needs.
Yaani lazima matangazo yatangazwe kwa nguvu Mana watu wavune hela wapeleke watt wao private schools huku wa wanunua bidhaa zao wakienda public.
Kuna shule like Hopac unajua watanzania wangapi wanaosomesha watt wao huko?
Kamari saivi zinatangazwa kwa nguvu zote yaani kila kona.
Ni rahisi mno kuwa tajiri katika dunia ya watu masikini wa kipato na kielimu Kuna jamaa mmoja alitoa humu bandiko.
Mana masikini nayeye ananunua ghali ili apate validation kuwa sio masikini. Nayeye ana belong to high status classes of riches peopyna huku ukweli utabakia pale pale.
Kuna mtu ananunua simu ya laki 5+ bado akapanga na huku iyo hela angeozea ziwe 2m anapata kiwanja baadhi ya mikoa Tanzania ajenge kanyumba hata apangishe.
Yaani we're poor not because we lack something but our mindset na dunia ya saivi Ni ya ushindani mno na hii mitandao inatuvuruga within 24/7 days.
Yaani Ni mwendo wa kukutamanisha ili na wewe utuate mkumbo.
Umemuona Kim kardishian akavaa Gucci clothes Basi na wewe unawaza uvae Kama yeye ili upande value.
Iyo laki tano unao uwezo wa kulima hata alizeti ama kitunguu mkoa fulani ukapata kipato ama ukapata kaeneo ukafuga kuku wako hata 20 zitaziliana.
Mambo ya msingi hayapigiwi chapuo Mana hakuna anayefaidika naye.
Umeshawahi ona tangawizi kitunguu swaumu ama maji ya limao yamechanganywa na asali uyanywe asubuhi kuwa Ni Tiba ya magonjwa mengi mno. Sasa huyo anayekutangazia anafaidikaje.
Lazima watu wajue kuwa people eats people Sasa wewe waza kuwa unapendwa sijui na mwanasiasa ama mfanyabiashara.
Ila dawa utatangaziwa mpaka sigara na pombe ununue wanaokula hapo kwa ha yako Ni wengi na serikali inapata Kodi.
Sasa bangi kila mtu anaweza akalima so watapataje Kodi.
Yaani ishu kubwa Ni kuifanya dunia iwe watumwa wa kitu fulani.
Saivi watu wanashindana kwa brain muscles and not chest or hand muscles Basi.
Mwanao anaangalia tv muda ambao ungemuandikia hata awe anajifunza sport fulani ama anakaa kwa biashara fulani ili umuandae akiwa mdogo unabakia mtumwa wa kinga'muzi na series zinazofanya bongo yako ipate pleasure ambayo Ni limitless na haina faida kwako.
Jaribu kuumiza akili mwanao anapendelea Nini ili umuandae akiwa mdogo Basi na umuonyeshe various fields so anaweza aka develop interest fulani ama ipo itakayomchagua.
Nenda naye hospital kazi za watabibu,nenda naye banks aone huko bankers,nenda naye kwa meli aone captain,omba site visit ya kiwanda fulani,nenda naye airport,nenda naye kwenye michezo like 🎾 utashangaa yeye anaanza kukuambia ili uwe Kama yule baba ivi unafanyeje ama unasoma Nini.
Samahani siwapangii maisha ama namna ya kuishi.
Ngoja nicheki hapa Simba na yanga ,nicheze pes5 , baadaye pool table kwa bar fulani, baadaye nikakae kijiwe fulani Cha kahawa nibishane Simba na yanga baadaye niilamu serikali kwa maisha magumu Sina Ajira na huku Nina bachelor ya uhandisi katika ujenzi tokea CoET Mana Sina network ama wa kunishika mkono jamani watt wa vigogogo wenyewe wanapata kazi.
Mana kujisomea na ku upgrade my skills hakuna Mana yyte,nikirudi home nacheki series za Filipino na Koreans kwa Netflix na ninavyo visimbuzi vyote vya Azam,DStv supersport,nawaza nitaipataje iPhone 14 ViP pro Maxim sio iPhone sie Ni w high class bana lazima niwe na vip, baadaye nakuja kulia hapa mwanangu anaombwa 200 ya mtihani sijui twisheni na huku majuzi nimechangia kadi Kama sita za harusi za washkaji kadi ya chini Ni 50k.
Si unajua Tena nikiwa naitoa my pro Maxim kwa mwendo Kasi napata status kubwa mie sio wa Android,Wala ma infinix,Tecno ama mobitel.
Yaani Bora tushindie sembe na dagaa Ila pro maxim ndio ujanja jamani.
Hata Ni rahisi kupata demu kisa my pro na ka ist kidogo yaani situmii nguvu mno. Yaani nikipaki pale samaki samaki wanachuo nakula mpaka nasaza mwenyewe