Mbinu ya Maisha kwa vijana: Kataa Mwanamke Masikini

Mbinu ya Maisha kwa vijana: Kataa Mwanamke Masikini

hii ni kali ya mwaka
jaribu uone atakunyanyasa hadi ukome. chezea watu waliopiga stori na nyoka utajuta
Mwache ajitoe akili, na mnavyojifanyaga mnataka kuheshimiwa, yaani upo tu ndani ya nyumba nakulisha, nakuvisha, mashavu yamekuvimba kama mimba ya panya utegemee nikuheshimu kwa lipi la maana hasa!
Heshima ya mwanaume ni kubeba majukumu yake kama mwanaume.
Vinginevyo utadharauliwa hadi na sisimizi waliopo ndani kwako.
 
Bora huyo taarabu mimi nakukodia tarumbeta.
Mwanaume mzima na kikojoleo chake ahudumiwe na mwanamke aibu gani hii.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Ikitokea hiyo tuite na uduguu wangu cocastic tukusaidie kukiwasha
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] Tena kivumbi kitatokea

Tunamkatia na sare ya kijora mbona atafurahi yeye bila kusahau na Gea tutamualika [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mwanamke TAJIRI akupende mwenyewe kaka,ila ukitaka mwanamke Tajiri lazima na wewe uwe stable

huwezi kwenda kula chipsi SINZA useme utakutana na mwanamke TAJIRI kuna sehemu ambazo zinatakiwa

ziwe katika circle yako ya maisha,mwanamke Tajiri hupatikana sehemu za matajiri ishu ni kuweza afford ingia

hizo mahala,maana kununua soda/juice/soft drink (ya kawaida) kwa 50k mkuu yakupasa ujitoe sadaka haswa

ila Yote kwa Yote Mapenzi ya kutafuta SIO mapenzi,ukiweza Afford ingia 5 star hotel kila siku kwa lengo eti upate

mwanamke TAJIRI nadhani si sawa,Mapenzi ni zaidi ya status zenu Financialy,Sawa una pesa Utapata Mke ana Pesa

haya sasa mko kwenye NDOA mna watoto, mke hajui malezi,mke hajui kitu,Yani huelewi hata ni imekuaje akawa MKE wako.

Fungua akili yako Omba Mungu akupe mke mwenye Hekima zake asie Mbinafsi mtakae ongea Lugha 1,Kaka amini nakwambia

Unaweza kuwa na mwanamke Kapuku Masikini na asikuombe hata senti yako na daily anapendeza kwa pesa za wazazi/kaka/ndugu zake,nk ni pure Maskini ambae si mzigo.

Tabia ya kuomba omba,ipo ndani ya Mtu na si katika uhalisia wa kipato chake,Nimeshawahi date mwanamke hana shida kabisa kuanzia familia yake mpka pale alipo sasa Lakini ni omba omba yule mwanamke Matonya akasome.

Uzungu mwingiiii kumbe ni ili tu atumie zangu zake zitulie bank so ishu sio Mtu mwenye PESA ishu ni MOYO brother, Ukipata mwanamke mwenye Moyo/utu/upendo,nk umemaliza

Hii ya kutafuta Mahusiano na stable woman kipesa au stable Man Kipesa itatokea watu puani na wapo ambao wanakula matunda ya walichokipanda.

Omba Mungua akukutanishe na Ubavu wako,Kwisha.
 
Jomba kama wewe ni maskini basi uwezekano mkubwa ni kuoa maskini mwenzako. Hii inasababishwa na kwamba hata maeneo unayokuwepo mara nyingi ni yà kimaskini hivyo kukutana na wanawake wenye hela zao ni ngumu. Nakushauri endelea kupambana upate hela... ukishaanza safari za TRA, Benki, Airport na kwenye maofisi makubwa basi utapata mwanamke mwenye nazo. Kinyume na hapo tafuta maskini mwenzako ambaye ni mwelewa na sio mbinafsi kama alivyotangulia kusema mjumbe Gentlemen_
 
Back
Top Bottom