Mbowe: Hatutakubali Bunge lililopo litengeneze Katiba Mpya

Mbowe: Hatutakubali Bunge lililopo litengeneze Katiba Mpya

..Naomba mjizuie kuhamasisha violence dhidi ya wapinzani.

..Tutajenga utamaduni mbaya wa ukatili ktk siasa zetu.

..MUNGU ametupa nafasi ya kujirekebisha kwani tulifika pabaya. Tusipoteze nafasi hii adhimu.
Mwambie mwenyekiti wa kudumu aache matamko tatanishi, mbona aliufyata iweje leo ndio aongee utafikiri katoka kwenye handaki?
 
Samia’s ‘tensile strength’ is being tested.
CCM wameshindwa Kubadilisha Katiba Kongwe ya 1977, Hivohivo Wameshindwa Kubadilisha Mifumo ya Kiuchumi,Kimaendeleo,Kiutawala nk.
Watanzania Tuelewe kuwa CCM ni Mabingwa wa Kushindwa kufanya Mabadiliko ya msingi nchini kwetu.
 
..Naomba mjizuie kuhamasisha violence dhidi ya wapinzani.

..Tutajenga utamaduni mbaya wa ukatili ktk siasa zetu.

..MUNGU ametupa nafasi ya kujirekebisha kwani tulifika pabaya. Tusipoteze nafasi hii adhimu.
Wapinzani wa Tanzania ni zaidi ya corona ukiwachekea
 
Kwa kauli hii ya Mbowe mama hana option zaidi ya kuwa dikteta.....
otherwise watampelekesha sana hawa....
mama inaonekana ni mpenda haki na utu
lkn naona wanamforce awe dikteta.....
wanasema hakuna mchawi mbaya kama mwanamke....
Hakuna mtu anaweza kulazimishwa kuwa dikteta kama sio hulka yake. Mtu akiwa dikteta ni kwa sababu ana udikteta ndani yake. Msitafute visingizio.

Amandla...
 
Mwambie mwenyekiti wa kudumu aache matamko tatanishi, mbona aliufyata iweje leo ndio aongee utafikiri katoka kwenye handaki?

..amesahau kwamba Mbowe alikoswa-koswa na masasi na kupelekea Akwilina kuuwawa?

..sasa mnataka Rais Samia naye apatikane na kashfa mbaya za ukatili?

..siasa zinapendeza kama wanaohusika watashindana kwa HOJA?
 
..Na mimi naheshimu sana maoni yako.

..Ningependa sana wanaomuunga mkono Rais Samia wawe na lugha nzuri tofauti na awamu iliyopita...
Watanzania hawali mikutano ya kisiasa
 
..Na mimi naheshimu sana maoni yako.

..Ningependa sana wanaomuunga mkono Rais Samia wawe na lugha nzuri tofauti na awamu iliyopita.

..Rais ametoa agizo ambalo linakiuka katiba. Pia agizo hilo linakipendelea chama chake na kuvionea vyama vya upinzani.

..Mbowe ameonyesha kutokukubaliana na msimamo wa Raisi. Sijaona mahali alipotumia lugha ya matusi au kumvunjia heshima Raisi.

..Mwisho, ningekuwa mshauri wa Raisi ningemshauri amtume msemaji wake aliweke suala hili vizuri, ili lifuate sheria na katiba.

..Suala kama hili lilitokea wakati wa Rais Magufuli. Lilituletea shida kubwa. Why is president Samia repeating the same mistake.? Kwanini washauri na wapambe wanamshangilia na kumhimiza Rais ktk jambo baya badala ya kumsaidia kurekebisha?
Ok mkuu
 
..amesahau kwamba Mbowe alikoswa-koswa na masasi na kupelekea Akwilina kuuwawa?

..sasa mnataka Rais Samia naye apatikane na kashfa mbaya za ukatili?

..siasa zinapendeza kama wanaohusika watashindana kwa HOJA?
Mwenyekiti wa kudumu aache siasa za kiuanaharakati ukombozi wa Africa ulishaisha kwasasa tunapambana kufanya wananchi wawe na uchumi imara.

Katiba inayodaiwa na mwenyekiti wa kudumu sio ajabu ikamtaka rais naye awe wa kudumu kama yeye, hebu aoneshe kwa mfano kumuachia nafasi mwingine kuongoza.
 
..Raisi amekataza mikutano ya hadhara, isipokuwa kwa wabunge.

..agizo hilo ni kinyume na sheria na katiba.

..vilevile agizo hilo linaipendelea ccm na kuviumiza vyama vya upinzani.

..Chama kama chadema kina mbunge mmoja tu ktk bunge la muungano, na vyama vingine vya upinzani havina wabunge kabisa.

..Raisi angeruhusu tu mikutano ya vyama vya siasa. Mikutano hiyo haimzuii yeye au serikali yake kurekebisha uchumi, au kuvutia wawekezaji.

..Kuna shughuli za michezo zinaendelea nchi nzima. Kuna mihadhara ya kidini inafanyika maeneo mbalimbali. Mikutano ya kisiasa haina madhara yoyote ile kwa ustawi wa nchi na ni halali kisheria.
Wafuasi wa chadema ni wapenda chuki,walipandikiza chuki kule Mtwara hadi vurugu za gesi zikatokea hadi watu wakauliwa.

Wakawahadaa wana arusha hadi wakapigwa na kuuwawa. Chadema hawahawa ndio waliomponza dk ULIMBOKA.

Lakini ni chadema ndio walisabisha hadi binti yetu AQUILINA akapigwa risasi na polisi
HALAFU NDO UNADAI MIKUTANO haina madhara?
 
Wafuasi wa chadema ni wapenda chuki,walipandikiza chuki kule Mtwara hadi vurugu za gesi zikatokea hadi watu wakauliwa.
Wakawahadaa wana arusha hadi wakapigwa na kuuwawa...
..ungeeleweka kama chadema ndio wangekuwa wamechukua silaha na kuuwa wananchi mtwara, arusha, na kwingineko.

..ungekuwa sahihi kama aquilina angekuwa ameuwawa na watu wa chadema, au walioamrishwa na chadema.

..mikutano haina madhara. Wenye madhara ni wahusika wanaoamrisha mauaji na dhuluma dhidi ya Watz wenzetu.
 
Moja ya sababu kubwa ya kushindwa kukamilika kwa mchakato wa katiba mpya ni wingi wa wabunge walio kuwemo. Muda mwingi ilitumika kulumbana, kweli mapanya wengi hawachimbi shimo likaenda.
Kwenye nia njema ya uwakilishi sawia, huwezi kutumia bunge la jamhuri kuwa bunge la katiba kwa sababu halina uwiano wowote. Linakuwa ni bunge la siasa lenye kundi moja kubwa lililo na mrengo, itikadi na kauli moja na hivyo ni rahisi sana ku compromise hata masuala ya msingi kitaifa, ili kulinda maslahi ya kundi hilo lililokubwa kwenye bunge.

Bunge la katiba linapashw a kuwa na uwakilishi usio na asili ya ititkadi za kisiasa. Ni chombo kinachopashwa kuundwa na makundi yote muhimu katika taifa vikiwemo vyama vya siasa, vyama vya wafanyakazi, taasisi za umma na zile za binafsi, vyama vya kijamii, makundi mbali mblai ya watu kama wazee, vijana, wakulima, wafugaji, n.k.

Kugeuza bunge la wanasiasa ndilo liwe bunge la katiba, na kutupia tupia watu wengine wachache humo, ni kutaka kuhalalisha maslahi ya chama chenye wabunge wengi kuwa katiba ya nchi, wakati vyama vya siasa vina katiba zake.

Naunga mkono hoja ya Mbowe kwamba bunge la siasa halipashwi kubadilishwa na kuitwa bunge la katiba kwa kuwa tayari lina kundi kubwa la watu aina moja na hivyo kufanya uwiano wa uwaklishi kukosa mashiko kitu ambacho kama hakitakuwepo, basi itakuwa ni katiba inayolind amaslahi ya kundi lenye watu wengi ambacho ni chama cha siasa.
 
Back
Top Bottom