Mbowe na siasa zake za "I am the only negro incharge in here"

Mbowe na siasa zake za "I am the only negro incharge in here"

Mbowe hakwamishi jitihada za watanzania kujikomboa. Watanzania wenyewe ndio wanajichelewesha.
Mnataka ajipeleke kichwa kichwa ili aliwe kichwa huku nyie mkichekelea nyuma ya keyboard sio? Mlikuwa wapi wakati anasota rumande? Mlikuwa wapi wakati biashara zake zikifungiwa? Mlikuwa wapi wakati mashamba yake yakifyekwa? Mlikuwa wapi wakati majengo yake yakivunjwa? Mlikuwa wapi wakati accounts zake zikiwa freezed kwa amri ya Magufuli?
Nimshangaa anavyojitapa kukwamisha jitihada za wananchi kuitia kibano serikali ya CCM kwenye ishu ya katiba mpya na bandari.

Badala awaone Sauti ya watanzania kama natural allies, yeye anaweka mbele ego yake tu ya uwenyekiti mbele.

OK sawa, wewe ni mwenyekiti so what?
 
Huu uzi umeletwa kwa hisani ya Lumumba FC na kufadhiliwa na chawa ambao wamejipanga kuleta mashambulizi hatari kweli kweli
 
Nilidhani wanaharakati na chadema wote wana akili timamu na aliyemkuu ni mwananchi.

Kulikoni kutojielekeza kwenye amani badala ya kuwa sehemu kwenye kuipigana hii stupid war kwa faida ya CCM no matter ilikoanzia?

View attachment 2772738

Unadhani ni wanaharakati ndiyo wanaona wameleta hii vita?

Ukombozi gani tunaopigania kwa mawazo yenu haya?

Kwamba mboga imemwagwa sasa ugali na umwagwe tu?

Kabila gani nyie?

Kenya hawako hivi. No wonder wanatembea.

..Kinachoendelea ni juhudi za kuidhoofisha Chadema.

..Kuna watu hawajafurahishwa na taarifa kwamba Chadema inaelekea kanda ya Nyasa kufanya mikutano na wananchi.
 
..Kinachoendelea ni juhudi za kuidhoofisha Chadema.

..Kuna watu hawajafurahishwa na taarifa kwamba Chadema inaelekea kanda ya Nyasa kufanya mikutano na wananchi.

Chadema imepinga hadharani jitihada za wananchi zilizokuwa zinashika kasi kupinga biashara ya bandari na kudai katiba mpya.

Tatizo ni hilo tu.

Mbaya zaidi ni kuwa kwa kujua au kutokujua, imefanya hivyo kwa niaba ya CCM.
 
Huu uzi umeletwa kwa hisani ya Lumumba FC na kufadhiliwa na chawa ambao wamejipanga kuleta mashambulizi hatari kweli kweli

Mtaitana majina hadi mmalize misamiati yote.

"Mwingine naye akisema huu uzi unapingwa kwa hisani ya Lumumba FC na kufadhiliwa na chawa ambao wamejipanga kuleta mashambulizi hatari kweli kweli."

Hapo napo utasema je?
 
Chadema imepinga hadharani jitihada za wananchi zilizokuwa zinashika kasi kupinga biashara ya bandari na kudai katiba mpya.

Tatizo ni hilo tu.

Mbaya zaidi ni kuwa kwa kujua au kutokujua, imefanya hivyo kwa niaba ya CCM.

..Hapana.

..Hakuna kiongozi wa Chadema aliyeunga mkono bandari kuuzwa, au mchakato wa katiba kusitishwa au kucheleweshwa.

..Na kwa uelewa wangu Chadema wamefanya mikutano mingi na maeneo mengi kuzungumza na wananchi kuhusu hoja hizo.

..Kwanini tunawakatisha tamaa? Kwanini tunawalaumu? Kwanini tunawazodoa? Tunafanya hivyo kwa faida ya nani?
 
..Hapana.

..Hakuna kiongozi wa Chadema aliyeunga mkono bandari kuuzwa, au mchakato wa katiba kusitishwa au kucheleweshwa.

..Na kwa uelewa wangu Chadema wamefanya mikutano mingi na maeneo mengi kuzungumza na wananchi kuhusu hoja hizo.

..Kwanini tunawakatisha tamaa? Kwanini tunawalaumu? Kwanini tunawazodoa? Tunafanya hivyo kwa faida ya nani?
Mbowe is just talking, talking, talking. Na kuongea anajua sana, kipaji cha kupiga tantalalia anajua.

Sasa tunataka kwenda beyond sweet talk. Tunataka action. Na ufortunately Mbowe kasukuma kete ya utengano , ambayo inakwaza azma ya wananchi eventually kuraise up na kulisongesha kitaa.

Mbowe anataka siasa za kishostishisti, na CCM hizo ndo siasa wanazozitaka!
 
Hebu fikirieni hili suala:

Umma wa Tanzania umeanza kuamka, unakataa udalali wa rasilimali zao, unaanza polepole kukataa chapa waliyopigwa kwa muda mrefu kimkakati ya uoga, unaanza kuchukua hatua ya kupeleka Struggle katika hatua ya pili ya matendo badala ya maneno.
Mkuu Missile of the Nation , hili nililizungumza hapa Watanzania ni maneno maneno na kulialia, Vitendo 0. Katiba ni maneno tu! Je, 2023 tuendeleze maneno matupu na kulialia au tubadilike tufanye kitu? nilisema
Wanabodi,

Nimegundua sisi Watanzania, kwa jina letu maarufu la Wabongo ni watu wa maneno maneno mengi, kulalamika sana na kulialia lia mwingi!, lakini tukija kwenye matendo, actions na kuchukua hatua, kusema ukweli kabisa, vitendo ni sifuri, zero, 0 nil!.

Kwenye hili la Katiba, Watanzania ni maneno maneno tuu meengii, na kulia lia kwingi!, lakini ukiangalia kwenye matendo, kuchukua hatua, to take actions ni hakuna kitu zaidi ya kelele!. Makala ya leo ni ya swali, huko nyuma tumekuwa tukipiga sana kelele miaka nenda, miaka rudi!, je na mwaka huu wa 2023, tuendeleze kulia lia kwa kupiga kelele kwa maneno maneno matupu au tubadilike tufanye vitendo, tuchukue hatua, tufanye kitu?. Yaani we have to do something!, au tuendelee tuu na maneno maneno, kulia lia na kupiga tuu kelele?.
Kisha nikashauri
Mwaka huu wa 2023, tupunguze maneno maneno, na kuongea ongea sana, tupunguze maandishi kuandika andika sana, hayo maneno maneno tunayoongea ongea sana, badaya ya kuishia kuongea ongea tuu, na kuandika andika tuu, tufanye jambo, tufanye na vitendo, tutende,!. Hivyo jambo langu kuu la kwanza kwa mwaka huu 2023 ni Katiba!. Japo kuna mambo mengi muhimu ya kuyashughulikia, lakini kwangu mimi kwa mwaka huu, naona muhimu kuliko yote ni hili la Katiba!, kwenye hili la Katiba, sasa tufanye kitu, tusiishie kuongea tuu na kuandika tuu, tufanye kitu cha ziada!, jee tufanye nini?, ungana nami wiki ijayo, nikiianzisha safari ya Katiba!, “it can be done, play your part” .

Paskali.
Cha kusikitisha anatokea kiongozi mmoja wa Taasisi muhimu ya wananchi, ambaye kwa nafasi yake, na mizizi ya taasisi yake angeweza kusaidia pakubwa kuwatoa wananchi kutoka katika kongwa hili la kutochukua hatua yoyote ya kuiadabisha serikali yao kutokana na madudu makubwa inayofanya yeye anarudi nyuma, na matokeo yake kuisaidia CCM kuzima cheche ambazo zingesaidia kutengeneza moto mkubwa wa mabadiliko huko mbele. Ni ajabu sana!
Kwa sisi waelewa hakuna ajabu yoyote!, huwezi kuukata mkono unaokulisha au kulikata tawi la mti ulioukalia!.
Mwisho.
Hapa nataka nitoe tahadhari kwa viongozi wa Chadema ambao wameanza kuwa arrogant kwa kudhani Chadema is too big, na hawahitaji kuchangamana na watanzania wengine hasa wa mitandaoni.)

Iko hivi, ni sisi wananchi wa Mitandaoni tuliopiga presha mpaka Mbowe akaachiwa. Ni sisi wananchi wengine wengi tu tusio na vyama lakini tuliokuwa tukiichangia Chadema katika operesheni zake. Ni sisi ambao tumeipa moral support, kwa kauli na matendo Na infact ni sisi ndiyo tunaolipa kodi ambayo leo hii Chadema wanapata ruzuku. Hii arrogance ya kijinga ambayo kwa bahati mbaya naona mnayo kuwa Walioko mitandaoni hawana dili, itakuja kuwatokea puani pale sentiment zitakapoanza kuwa negative kwenu na chama chenu. Kama mnabisha kaiulizeni ACT kwa nini haitoboi Tanganyika. Kawaulizeni negative content inawaathiri vipi!. Sasa msitufikishe huko.
Kama kweli Chadema ni chama cha wananchi, basi hiyo Taasisi ifanye kazi ya wananchi. Tungeshukuru sana kama Ingeshirikiana na Sauti ya Watanzani kuibana CCM zaidi, Kuitia kibado zaidi CCM kwenye suala la bandari na katiba. Kinyume cha hapo ni kuipa life support CCM na huo ni usaliti.

Nawasilisha!
Huu ni ushauri mzuri, akina sisi tumeisha ishauri Chadema, ushauri na ushauri. Kwenye CCM Imechokwa, CHADEMA Haijajipanga! niliishauri Chadema ijipange vipi, wapi na nilitoa ushauri kumhusu Mwenyekiti Mbowe
Wanabodi,
Hakuna ubishi, Chadema imenyanyuka, toka wabunge 5 mpaka 22 wa kuchaguliwa tena majimbo ya haja yenye impact ikiwemo kuyashika majiji makubwa katika mikoa the big five!, huku sio kukua bali ni kupaa, tatizo kubwa la Chadema, bado hawajipanga mkao wa kichama tawala, ili kikabidhiwe nchi, kitawale, Chadema bado kimekaa kichama harakati, hivyo kuna wengi wanakiona kama bado hakijakomaa kiasi cha kukabidhiwa ikulu yetu!.

Kichama, wanachadema mkubali msikubali, chama chenu kwa sasa japo kipo juu, lakini bado hamjakomaa kufikia kiwango cha kukabidhiwa nchi, bado mko kiuana harakati zaidi kuliko ki chama tawala, na hamjajipanga kwa sura ya kitaifa na utayari wa kutawala nchi.

Kwa vile CCM imechokwa na imekaa mkao wa kifo, hii ndio opportunity yenu Chadema kuongeza offensive ili kuisindikiza CCM kaburini, kwa kujipanga kimkakati ili muwe na sura ya kitaifa, kwa kuonyesha Watanzania kuwa mmekomaa na mko tayari kutawala, hivyo Watanzania watawamini watawakabidhi nchi mwaka 2015.

Sehemu muhimu kabisa kwa Chadema to keep watch kuhakikisha hamuiachii ni hiyo Kanda ya Ziwa ambayo imeipokonya CCM na kuishika, hii ndio Kanda determinant ya nani anakuwa rais wa nchi hii. Aliyeishika Kanda ya Ziwa ndio rais wa Tanzania. Hivyo CCM imeumia sana kupoteza Kanda ya Ziwa na wataelekeza all it might powers to reclaim what it has lost, hivyo Chadema itumie uwezo wake wote kulinda what it has!.

Kwa upande wa Chadema, lazima kibadilike, first and foremost, anzeni na Mwenyekiti wenu Freeman Mbowe, he should go!. Ajiuzulu uenyekiti, ampishe more able person kama Dr. Slaa kwenye usukani wa chama, Katibu Mkuu mpeni Zitto strategically, hii itaifuta ile dhana ya nepotisim kwenye chama chenu, na kulivua lile koti la ukanda na ukabila ili walioichoka CCM wawafungulie mikono kwa kujitokeza kwa wingi kuwapigia kura 2015 kwa kujionyesha Chadema ni chama cha wote, dini zote na kanda zote.

Kupumzishwa kwa Freeman Mbowe sio kuwa hafai no, anafaa sana lakini kwa background yake na nature ya kazi zake, as a businessman, hapo alipoifikisha Chadema amaishafanya kazi kubwa na kufikia mwisho wa uwezo wake. Kwa background yake ya a former DJ na sasa ni mfanyabiashara, focus ya wafanyabiashara kote dunia nzima ni maximisation of profits, hivyo Mbowe atahitaji ruzuku ya Chadema itumike kuivest kwenye assets, kwenye vitu vya kuonekanika yaani assets kama magari, mavazi, etc

Ili Chadema kiweze kushika nchi 2015, it has to invest on people na sio ku invest kwenye vitu. Chadema must invest kwenye mass mobilisation na sio kutegemea mikutano ya hadhara na maandamano. Chadema needs to have able people kuiwezesha kushika dola five years to come kwa kutumia reaching out mechanism kuwafikia the mases kwa kumiliki media yake yenyewe. Chadema lazima ifanye recruitment ya loyal able people, watakaokuja kuendesha serikali ya Chadema. Mbowe hawezi kukubali ruzuku ya Chadema itumike to invest on people, kwasabu it's a loss making venture kwa mfanyabiashara na kuivest kwenye mass media sio profitable investment kwa business man ambaye ni in for profits making!. Dr.Slaa na Zitto sio wafanyabiashara hawa ni ma technocrats. Chama kishikwe na wanasiasa watendaji ma technocrats na sio wanasiasa wafanyabiashara!. Chadema iwekeze kwenye watu na kupanua mtandao wake hadi vijijini, ili kwenda kuiongoa CCM kuanzia kule chini kabisa kwenye mizizi yake ambako ni kule kwenye mashina. Chadema imiliki media yake yenyeshe for mass mobilization na sio kutegemea mikutano na maandamano, huko ni kuendeleza uanaharakati, Chadema inatakiwa kukaa mkao wa kutawala, ikitangaza kitu, kinafika Tanzania nzima!

Chadema ina tatizo la umimi. Kitendo cha Chadema kuihodhi kambi rasmi ya upinzani Bungeni, huu ni udhaifu mkubwa ambao hautawafikisha mbali. Pamoja na kanuni za Bunge kuruhusu Chadema kuunda kambi rasmi ya upinzani peke yake, Chadema peke yenu hamuwezi!. Lazima muwashirikishe wapinzani wengine wote hata kama hawastahili. You have to unite and work as one against a common enemy. Umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu.

Paskali
Nikaja kutoa ushauri muhimu sana kwa Chadema Elections 2015 - Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni ...

Ndipo nikagundua CHADEMA ni sikio la kufa? Iambiwe vipi ili isikie? Masha ana hoja za msingi, zisikilizwe, zizingatiwe, zisipuuzwe! na kujiridhisha CHADEMA Hamkujipanga, hamjajipanga, hamjipangi na hamtajipanga!-2015 ni CCM tena! hivyo 2015 ilikula za uso!.

Tulipokuja 2020 hapa naomba nisizungumze kuepuka kitu kinachoitwa stigmata!.

Kuelekea 2025 pia nimeshauri Iwapo Watanzania wataamua 2025 twende na Mwanamke, mnaonaje tukiwashauri CHADEMA wasimamishe Mwanamke? Maana Mwanaume kushindwa na Mwanamke ni aibu!

Nimeshauri Wapinzani to concentrate on serikali za mitaa, udiwani na ubunge, urais wa 2025 bado ni CCM!, Uchaguzi mkuu wa mwaka 2030, ndio mwanzo wa mwisho wa CCM! Wajinga karibu wote watakuwa wamemalizika!

P
 
..Hapana.
Tuwe tunapiga hatua basi ndugu, bila kusahau Chadema si mtu na huko hamko peke yenu?

Kwamba hujui kuwa Chadema ilipinga hadharani jitihada za kina Mwabukusi kuhusiana na katiba mpya na mauzo ya bandari? Ni mwanzo kuyasikia haya hapa leo?

..Hakuna kiongozi wa Chadema aliyeunga mkono bandari kuuzwa, au mchakato wa katiba kusitishwa au kucheleweshwa.

Sasa Chadema si ingechagua hata kunyamaza tu badala ya kutokea hadharani kupinga harakati za wengine wale? Kulikoni kujitokeza hadharani kufanya ambacho angefanya CCM?

..Na kwa uelewa wangu Chadema wamefanya mikutano mingi na maeneo mengi kuzungumza na wananchi kuhusu hoja hizo.

Tatizo si kuwa Chadema Imefanya mikutano au kuzungumzia haya mambo.

Labda kama unasema mikutano ilikuwa imeshatosha na mwingine iikuwa asifanye tena?

..Kwanini tunawakatisha tamaa? Kwanini tunawalaumu? Kwanini tunawazodoa? Tunafanya hivyo kwa faida ya nani?

Huoni kuwa tunaitisha reconciliation? Tumemtaja hata mediator tokea Chadema. Au labda nyie mnataka nini?

Kwanini suluhu kwenu ni kuwakatisha tamaa, kuzodoa au kulaumu.
 
Ngoja chawa wake waje wakupopowe na mawe. Miongoni mwa viumbe vya ajabu duniani basi ni Wafuasi wa Mbowe au Chadema kwa ujumla. Wao wanaamini wako sahihi muda wote na wengine hawako sahihi. Wao wanaamini kila anayewakosoa ni CCM au ACT.Hii nchi kungekua na upinzani wa maana swala la Bandari na saizi umeme yalitosha kuitoa ccm madarakani au hata kuipa adabu tu CCM.Mbowe na genge lake wanawaza ubunge tu na sio kuleta mabadiliko yoyote Tanzania. Siasa zao ni za kujipendekeza kwa watawala angalau 2025 wawalegezee kwenye Ubunge. Wanafanya SIASA za kuogopa kuikwaza CCM wasije wapiga pini huko mbele.Hiki sio chama cha siasa bali genge la wahuni.
Ngombe wewe Mbowe anafungwa magereza miezi 8 kuna kima aliandamana ili Mbowe achiwe?
 
Tuwe tunapiga hatua basi ndugu, bila kusahau Chadema si mtu na huko hamko peke yenu?

Kwamba hujui kuwa Chadema ilipinga hadharani jitihada za kina Mwabukusi kuhusiana na katiba mpya na mauzo ya bandari? Ni mwanzo kuyasikia haya hapa leo?



Sasa Chadema si ingechagua hata kunyamaza tu badala ya kutokea hadharani kupinga harakati za wengine wale? Kulikoni kujitokeza hadharani kufanya ambacho angefanya CCM?



Tatizo si kuwa Chadema Imefanya mikutano au kuzungumzia haya mambo.

Labda kama unasema mikutano ilikuwa imeshatosha na mwingine iikuwa asifanye tena?



Huoni kuwa tunaitisha reconciliation? Tumemtaja hata mediator tokea Chadema. Au labda nyie mnataka nini?

Kwanini suluhu kwenu ni kuwakatisha tamaa, kuzodoa au kulaumu.

..Ndugu Chadema hawajawapinga kina Mwabukusi.

..Nionyeshe ni wapi Chadema wamesema Mwabukusi asidai Katiba, au asipinge bandari kuuzwa.

..Naona kama mnaibua ugomvi ambao haupo, halafu mnapendekeza msuluhishi.

..Sasa huo usuluhishi sio kupoteza muda wa kwenda kwa wananchi na kuwatia hamasa?

..Kwanini unataka Mwabukusi na wanaharakati wapoteze muda kuzungumza na Chadema, badala ya kukutana na wananchi na kupanga nao mikakati ya ku'deal na Ccm?
 
Kuwategemea Wanasiasa kuleta mabadiliko, ni kupoteza wakati tu, wanapigana vijembe majukwaani, jioni wanakuwa wote wakigonga cheers!
 
Mbowe kwenye mkutano wa Juzi na wazee alishindwa kujenga HOJA zenye mashiko.

Akumbushwe CDM inapata support na wananchi pia wasio na vyama vya siasa.
Njia halali ya kisheria ya kuwania madaraka ya uongozi wa nchi, ni kuanzisha na kuendesha chama cha siasa! Hiyo ya akina Mbambukusi ni uhuni na vurugu! Kama kweli wanania ya kuikomboa nchi, hakuna short cut, wajiunge na vyama vya siasa!
 
..Ndugu Chadema hawajawapinga kina Mwabukusi.

..Nionyeshe ni wapi Chadema wamesema Mwabukusi asidai Katiba, au asipinge bandari kuuzwa.

..Naona kama mnaibua ugomvi ambao haupo, halafu mnapendekeza msuluhishi.

..Sasa huo usuluhishi sio kupoteza muda wa kwenda kwa wananchi na kuwatia hamasa?

..Kwanini unataka Mwabukusi na wanaharakati wapoteze muda kuzungumza na Chadema, badala ya kukutana na wananchi na kupanga nao mikakati ya ku'deal na Ccm?

Nililazimika kukwambia tuwe tunapiga hatua. Andiko lako ni kama umefika duniani sasa tokea sayari nyingine.

Kwa andiko lako hujui kuna mtafaruku, kuwa hakuna hata usuluhishi unaohitajika.

"Kwamba unadhani kumbe wanaoandika hawa ni wendawazimu."

Sawa endeleeni kukaza shingo ila hoja haipigwi rungu.

Wapi umeona Mwabukusi na wanaharakati wanataka kuongea na chadema ambayo hata tumekubaliana si mtu, ya mtu na hayupo mwenye hati miliki peke yake humo?

Haya si ni maajabu yenyewe ya Mussa?
 
Njia halali ya kisheria ya kuwania madaraka ya uongozi wa nchi, ni kuanzisha na kuendesha chama cha siasa! Hiyo ya akina Mbambukusi ni uhuni na vurugu! Kama kweli wanania ya kuikomboa nchi, hakuna short cut, wajiunge na vyama vya siasa!

Ushauri kama wako unatolewa na CCM, kina bi tozo na kina Tulia huko.

Wewe ni mwenzao?
 
Opportunity....

Fursa....

Dunia ya fursa....

Tutadanganyana hadi lini ?!!![emoji1787][emoji1787]

Komredi Mbowe ni yuleyule....

Dr.Slaa ni yuleyule....

Uchizi wa Mdude ni uleule [emoji23][emoji23]

#Siempre SSH[emoji7][emoji7][emoji2956]
 
Mleta mada ungekuwa mkweli kwako mwenyewe (honest to yourself) usingeandika bandiko hili. Umeibua mambo kadhaa kuthibitisha kuwa Mbowe na CHADEMA “yake” hawana nia ya dhati ya kupambania katiba na ajenda zingine muhimu za wananchi; kwamba hawataki kumuudhi Rais na serikali yake kwa matarajio ya kutobanwa uchaguzi mkuu wa 2025 na hivyo kuambulia viti kadhaa vya ubunge. Kwamba wanapuuza vyama vingine vya upinzani na wanaharakati. Kwamba wanakwamisha juhudi za wananchi kuibana CCM; n.k.

Umeunga mkono wanaodai CHADEMA ni mali binafsi ya Mbowe na kwamba yeye na chama chake si wapinzani wa kweli bali wasaka fursa, vyeo na ruzuku; n.k.!

Honestly speaking, kwa fikra za aina hiyo, unapomlalamikia Mbowe kwa kutounganisha nguvu na wengine kuibana serikali kwenye suala katiba, bandari, n.k. inakuwa vigumu sana ukaeleweka. Huwezi kumtoa thamani mtu na chama chake kiasi hicho halafu ukategemea afanye mambo ya maana kama hayo unayolalamikia. HALAFU, si Mbowe wala CHADEMA wenye MONOPOLY ya upinzani Tanzania. Ni nani basi huyo anayewazuia nyinyi wapinzani na wanaharakati makini kuongoza hayo mapambano dhidi ya CCM na serikali yake? Ni Mbowe? Ni CHADEMA?

Hili bandiko haliko honest kabisa. Neither is it just and fair to Mbowe and CHADEMA.
 
Njia halali ya kisheria ya kuwania madaraka ya uongozi wa nchi, ni kuanzisha na kuendesha chama cha siasa! Hiyo ya akina Mbambukusi ni uhuni na vurugu! Kama kweli wanania ya kuikomboa nchi, hakuna short cut, wajiunge na vyama vya siasa!
Usichokijua ni kuwa watu hao wanaomsaport Mdude, Mwabukusi na Slaa ndo wanaisapot CDM.

Suluhu ni kuungana, Si kuanzisha chama kipya.

Chama kipya kitapunguza nguvu ya UMOJA wa watz na nguvu ya CDM kama main opposition party.

Kila kundi likianziaha chama chake Bado adui hatowezekanika ndo sababu ya Slaa kuomba support ya CDM.

Narudia HOJA za Mbowe hazikuwa na mashiko.
 
Usichokijua ni kuwa watu hao wanaomsaport Mdude, Mwabukusi na Slaa ndo wanaisapot CDM.

Suluhu ni kuungana, Si kuanzisha chama kipya.

Chama kipya kitapunguza nguvu ya UMOJA wa watz na nguvu ya CDM kama main opposition party.

Kila kundi likianziaha chama chake Bado adui hatowezekanika ndo sababu ya Slaa kuomba support ya CDM.

Narudia HOJA za Mbowe hazikuwa na mashiko.

Wakikuelewa usiache kutuletea mrejesho. Haijulikani wanataka au hawataki nini na wala kuwa wanamsemea nani.
 
Hebu fikirieni hili suala:
Umma wa Tanzania umeanza kuamka, unakataa udalali wa rasilimali zao, unaanza polepole kukataa chapa waliyopigwa kwa muda mrefu kimkakati ya uoga, unaanza kuchukua hatua ya kupeleka Struggle katika hatua ya pili ya matendo badala ya maneno. Cha kusikitisha anatokea kiongozi mmoja wa Taasisi muhimu ya wananchi, ambaye kwa nafasi yake, na mizizi ya taasisi yake angeweza kusaidia pakubwa kuwatoa wananchi kutoka katika kongwa hili la kutochukua hatua yoyote ya kuiadabisha serikali yao kutokana na madudu makubwa inayofanya yeye anarudi nyuma, na matokeo yake kuisaidia CCM kuzima cheche ambazo zingesaidia kutengeneza moto mkubwa wa mabadiliko huko mbele. Ni ajabu sana!

1. Mbowe na siasa zake za ki "Uncle Tom"
Kipindi cha utumwa huko Marekani na Jim Crow, walikuwepo wamarekani weusi ambao kwa kuwa wao walikuwa na vijinafasinafasi katika mfumo wa Marekani, walikuwa wakipenda kujitapa kwa kauli za "I am the only negro working as an engineer here", "I am the first black clerk in here". Leo hii Huwezi kushangaa kumsikia Mbowe akijitapa na kauli yake maarufu ya siasa za nchi hii ni ya Farasi wawili, CCM na Chadema. Na hii Mentality ndiyo inayomsukuma kutaka alambwe miguu pale wananchi wanapotaka kusogeza struggle kwenda next level, Ili kuitia kibano serikali ya CCM katika suala la bandari na katiba mpya. Ndiyo maana Juzi huko Zanzibar, huku akisimama kwa kujitapa mbele ya wazee wa chama anahoji eti Chadema haikushirikishwa katika maandalizi ya mikutano na maandamano ya kuibana serikali ya CCM katika suala la katiba mpya na Bandari. Yaani anataka apigiwe magoti na wananchi kwenye struggle za kuitia kibano serikali, yeye nani, na kwa nini?!.

2. Mbowe amesaliti struggle za Watanzania kupeleka struggle next level
Sijui kama Mbowe na chawa wake ndani ya Chadema wanatambua athari za walichokifanya dhidi ya struggle za Watanzania katika kujikomboa kutoka katika minyororo ya Siasa chafu na uongozi mbovu wa CCM. Badala ya kuweka ego ya Kiuenyekiti, na ego ya uchama mbele, Mbowe alipaswa aangalie picha pana ya movement ya wananchi ya kutaka kuitia kibano Serikali ya CCM zaidi katika suala la bandari. Infact struggle hii inacompliment kabisa jitihada za chama cha Chadema za kudai katiba mpya. Badala ya Mbowe kuwapiga Rungu Sauti ya Watanzania, kama kweli angekuwa anahitaji mabadiliko ya kweli nchini, alipaswa aweke ego yake pembeni na kuwasaidia kadri inavyowezekana. Hii ingesolidify movement ya mabadiliko kutoka pande zote za kijamii na kisiasa za kuleta mabadiliko nchini. Lakini cha ajabu at the critical hour, Mwenyekiti kama kawaida yake ANABADILI GIA angani.

3. Jeuri ya Nyomi mikutanoni na kudhani Chadema haihitaji Sauti za mitandaoni
Inavyoelekea, wingi wa watu katika mikutano ya Chadema umeanza kuwapa kiburi viongozi wa Chadema na kudhani kuwa nyomi hilo linamaanisha kushinda chaguzi na labda eti hiyo ndiyo force pekee inayoweza kuipeleka Chadema mbele. Nataka nimwambie Mwenyekiti Mbowe na Chawa wake ndani ya Chama kuwa kudhani hivyo ni very naive, Maana hata kama hilo nyomi lote litaichagua Chadema, kama hakuna katiba mpya, tume huru ya uchaguzi ni kazi bure. Ndiyo maana ni ujinga mtupu kubeza cheche za struggle ambazo zitazaa moto wa mabadiliko ya kisiasa na kijamii nchini yatakayoisaidia hata Chadema yenyewe. Na mtu yeyote anayedharau kundi la wananchi ambalo liko "Enlightened" basi huyo hajielewi.

Na labda tu nimwambie Mbowe, kuwa pengine Nyomi la mikutano linamtia kiburi na kuamini kuwa Hakuna haja ya kuwaengage Watanzania wa mitandaoni. Asubiri aone kama CCM nao watapita katika kata hizohizo anazopita leo watu walewale waliojitokeza kumsikiliza kama hawatakwenda kuwasikiliza CCM pia. Ni Ujinga kudharau movement ya kundi dogo wenye uelewa ktk society

4. Akili za kuwaza ubunge, wingi wa ruzuku na kuendelea kuwa Mwenyekiti
Siyo siri, viongozi wengi ndani ya Chadema ya leo wanawaza ubunge tu mwaka 2025. Ni wachache sana miongoni mwao wanaowaza beyond ubunge. Na hii sauti ya waota ubunge ndani ya chama ni kubwa zaidi kuliko wale ambao Genuinely kabisa wanawaza mabadiliko ya kweli ya kimfumo nchini. Ukisikiliza kauli za viongozi wengi wa Chadema wako more worried na uchaguzi mkuu ujao, na ndiyo maana sasa wanazungumza habari za mabadiliko ya katiba kuelekea uchaguzi. Hoja zilezile ambazo miaka mitatu iliyopita walikuwa wakiwatukana ACT kwazo, ndiyo hizohizo leo wanazileta kwetu kama eti ni maono ya hekima ya chama. Kama hekima zinapatika ndani ya miaka mitatu, basi maana yake huko nyuma hakuwa na hekima anyway.

5. Mbowe kama Gatekeeper
It seems Mbowe, hayuko tayari kwa massive action nchini. Yaani anadhani kuwa CCM itatuleta mabadiliko kwa kuombwa, kwa kujitungia sheria za kujidhibiti yenyewe, kwa kuombwa kuleta katiba ya kujimaliza yenyewe. Na CCM kwa kutambua udhaifu wa Mwenyekiti katika mambo makuu matatu, Mosi anautaka uenyekiti tena, Pili ni muoga wa kupush hard na Tatu ana maslahi nchini ambayo wanaweza kumblackmail nayo basi wako Comfortable kuwa Mwamba ataruka na chopa, ataongea rousy speeches lakini itakapokuja muda ambao Watu wanataka kuraise up, basi Mwenyekiti atatumia machinery ya chama chake kujiweka pembeni na kuwaacha wanaotaka kuraise wakiwa marginalized. Ni jukumu la Wanachadema kukifanyia review chama chao waone kuwa The same Old Mwenyekiti ana kipya au sasa ni time ya Change ili kupush mabadiliko ya kweli nchini.

6. Mwisho
Hapa nataka nitoe tahadhari kwa viongozi wa Chadema ambao wameanza kuwa arrogant kwa kudhani Chadema is too big, na hawahitaji kuchangamana na watanzania wengine hasa wa mitandaoni.

Iko hivi, ni sisi wananchi wa Mitandaoni tuliopiga presha mpaka Mbowe akaachiwa. Ni sisi wananchi wengine wengi tu tusio na vyama lakini tuliokuwa tukiichangia Chadema katika operesheni zake. Ni sisi ambao tumeipa moral support, kwa kauli na matendo Na infact ni sisi ndiyo tunaolipa kodi ambayo leo hii Chadema wanapata ruzuku. Hii arrogance ya kijinga ambayo kwa bahati mbaya naona mnayo kuwa Walioko mitandaoni hawana dili, itakuja kuwatokea puani pale sentiment zitakapoanza kuwa negative kwenu na chama chenu. Kama mnabisha kaiulizeni ACT kwa nini haitoboi Tanganyika. Kawaulizeni negative content inawaathiri vipi!. Sasa msitufikishe huko.

Kama kweli Chadema ni chama cha wananchi, basi hiyo Taasisi ifanye kazi ya wananchi. Tungeshukuru sana kama Ingeshirikiana na Sauti ya Watanzani kuibana CCM zaidi, Kuitia kibado zaidi CCM kwenye suala la bandari na katiba. Kinyume cha hapo ni kuipa life support CCM na huo ni usaliti.

Nawasilisha!
Ni maoni na mawazo yako, binafsi nayaheshimu...

Lakini bado, hii siyo hoja ya kuitumia kuilaumu CHADEMA na Freeman Mbowe kama ndiyo kikwazo cha wengine kuliamsha kwa namna yao na kwa njia zozote zile halali...

Mtu kama Dr Wlbroad Slaa anatoa wapi political moral authority ya kutoa maagizo kwa taasisi kubwa kama CHADEMA huku historia ya siasa za usaliti dhidi ya wenzake haohao ikimsuta?

Na wakati huohuo ukumbuke kuwa, siasa za ki - Afrika zikiwemo za kwetu Tanzania ni za utata sana na kubebwa na watu watata sana kama huyu Dr Wlbroad Slaa..

Anaweza kujitokeza mtu na kujifanya ni mwanaharakati na mpambanaji mpigania haki mwenzenu na akaonekana hivyo kwa macho ya damu na nyama, lakini kumbe ni kibaraka na ni mkono wa walewale mnaopambana ulingoni...!

Nina maana kuwa, ktk kila hatua ya maamuzi ya kisiasa ndani ya taasisi makini kama CHADEMA, umakini ni wa lazima sana kuepuka kujikuta mmejitia kitanzi wenyewe kwa uamuzi wa kipupa...

Ilisemwa zamani kuwa si vyote ving'aavyo ni dhahabu na wahenga wengine walisema; it's better late than never..."

Freeman Mbowe na CHADEMA wako sahihi na kwa kweli ni mjinga pekee anayeweza kuwalaumu CHADEMA kwa kukataa kupewa maagizo na amri na watu kama kina Dr Slaa ambaye moral authority yake kisiasa ina mashaka makubwa..!

However, bado hakuna kilichoharibika. Muda bado upo. Warudi kwenye drawing board na waweke mikakati ya pamoja...

By the way, mtu kama Wakili Boniface Mwambukusi na Mdude Nyangali mbona ni wanachama active wa CHADEMA!
..!!

Inakuwaje wanatumia jukwaa jingine kusukuma ajenda zao hizo nje ya utaratibu wa kichama na mwisho wa siku wanarudi tena chamani na kuanza kukilaumu kuwa hawaungi mkono mambo yao? Mbona kama haiingii akilini vile?
 
Back
Top Bottom