Uchaguzi 2020 Mbowe: Ndani ya saa 72 nitakuwa Waziri Mkuu

Uchaguzi 2020 Mbowe: Ndani ya saa 72 nitakuwa Waziri Mkuu

Mgombea ubunge wa jimbo la Hai ambaye ni mwenyekiti wa Chadema mh Freeman Mbowe amesema Tundu Lisu atakuwa Rais wa Tanzania na Mungu akipenda yeye ( Mbowe ) atakuwa Waziri mkuu.

Source Jamii Forums

My take; Zitto Kabwe mbona mnamsahau mapema hivi!

Maendeleo hayana vyama!
 
Mgombea ubunge wa jimbo la Hai ambaye ni mwenyekiti wa Chadema mh Freeman Mbowe amesema Tundu Lisu atakuwa Rais wa Tanzania na Mungu akipenda yeye ( Mbowe ) atakuwa Waziri mkuu.

Source Jamii Forums

My take; Zitto Kabwe mbona mnamsahau mapema hivi!

Maendeleo hayana vyama!
Acha kufarakanisha
 
Habari ya Tundu kuapishwa kuwa raisi ubalozini huko nga'mbo ni za kweli au ni maluelue ya vijana wake?!!
 
Watanzania Leo Kuna jamaa yangu kaniambia yupo kwenye usimamizi wa uchaguzi

Sasa semina Yao ya siku mbili iliyoanza leo wamepewa 80000/=

Chakushanga maneno waliyoambiwa kwamba presha huku nje ipo kubwa sana kwaiyo ikiwezekana kuua wakala waue tu ili mradi Maghufuri ashinde.

Kwanza walitolewa wote ambao walifatiliwa habari zai zikaonekana zinavinasaba vya upinzani.

Jaman tuweni makini uchaguzi huu ni hatari sana Kuna watu wapo tayari kuwa ili Meko ashinde usimwamini mtu.

Haki huinua TAIFA

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
Hata mimi kuna jamaa yangu alikuwepo kwenye semina na walielekezwa wafuate sheria na taratibu za uchaguzi. Hivyo ndivyo walivyoambiwa na kila mtu amuamini jamaa yake.
 
Ulibadili hadi gear angani na vyama vikaungana ila haukuwa waziri,kwahiyo utaka kuniambia kula hazikutosha wakati huo?
 
Mbowe amesema katika saa 72 zijazo Tundu Lissu atakuwa Rais wa Tanzania na Mimi nitakuwa Rais

Chanzo:
Mwananchi online

====

Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe, amesema ndani ya saa 72 zijazo, mgombea wao wa Urais, Tundu Lissu anakwenda kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mbowe ametoa kauli hiyo leo Jumapili Oktoba 25 katika mji mdogo wa Bomang'ombe wilaya ya Hai wakati akihutubia mkutano wa hadhara wa kampeni huku akisema Mungu akipenda, yeye anakwenda kuwa Waziri mkuu.

Hata hivyo, Mbowe ambaye pia anagombea ubunge jimbo la Hai, alitahadharisha kuwa kitendo chochote cha kuwazuia mawakala wao 80,160 nchi nzima wasiingie kwenye vituo vya kupigia kura Oktoba 28, kunaweza kubadili historia ya Tanzania.

Hivyo, aliisihi Tume ya Taifa ya Uchaguzi na vyombo vya Usalama, kuhakikisha hakuna jaribio lolote la kuwazuia mawakala wao kuingia kwenye vituo kusimamia upigaji kura na wao watakuwa tayari kukubali matokeo kama uchaguzi utakuwa wa huru na haki.

"Uchaguzi huu sio kati ya Chadema na CCM wala uchaguzi huu sio kati ya Lissu na Magufuli (mgombea urais wa CCM) bali ni kati ya wanaopenda uhuru na haki na waliokandamiza uhuru na demokrasia," alisema Mbowe.

Mbowe amesema wamezunguka mikoa yote ya Tanzania na wananchi wapo tayari kufanya mabadiliko ya uongozi na kusisitiza kuwa kwa mwonekano na hamasa waliyoionyesha Watanzania, Lissu anakwenda kuwa Rais ndani ya saa 72 zijazo.

Hivyo, ameitaka NEC kuhakikisha uchaguzi huu hauvurugwi kwa namna yoyote kwa sababu gharama yake itakuwa kubwa na kusisitiza kuwa wako tayari kukubali kushindwa kama NEC na vyombo vingine vitahakikisha uchaguzi umekuwa wa wazi, huru na haki.
Pesa kidogo tu anajitangaza kuwa PM.
 
Nashangaa moderator anakubali kurusha uzi wa uchochezi wa aina hii. JF tunajua mwelekeo wenu wa siasa ukoje lakini achaeni upendeleo wa wazi mnaoonesha hivi sasa na kuruhusu nyuzi kama hizi tu kwa sababu zinaegemea kuchafua CCM. Kuweni fair japo najua ni ngumu kwenu
Usipanic ndugu yangu wajinga Kama hao unawaangalia walivyochanga yikiwa unawaacha
Acha magu achukue nchi aendelww kuwanyoosha
Wameshaona wameshindwa wanaanza kutunga uongo wakifikiri uongo utawaokoa
 
Yani nasikia kwenye mafunzo ya wasimamizi huko,wasimamizi wakuu wanafundishwa namna ya kuukandamiza upinzani na kuhakikisha jiwe anapita kwa kura nyingiiii
Ulitaka lisu ashinde!!?
Mmefele mbaya
List mwenyewe anajua hashindu ndio maana anaticket ya ndege mfukon
Tar 29 anatimka
 
Duh huyu mwamba sijui huwa anarukwa akili? Inamaana hajui hata mchakato wa kumpitisha waziri mkuu ukoje? Achilia mbali kibaraka wa wazungu lissu kushinda urais,elimu ni muhimu sana kwa viongozi wa CHADEMA maana kama mwenyekiti anaongea upuuzi huu si ni hatari sana
 
Mbowe ametoa kauli hiyo leo Jumapili Oktoba 25 katika mji mdogo wa Bomang'ombe wilaya ya Hai wakati akihutubia mkutano wa hadhara wa kampeni huku akisema Mungu akipenda, yeye anakwenda kuwa Waziri mkuu.
Hii kauli inazidi kumnyima kura Lissu! Hatuwezi kumchagua Rais anayepangiwa nini cha kufanya hasa kwenye majukumu mazito! Kumpata waziri Mkuu ni jukumu zito!

Na katika hili, imedhihirisha kuwa CHADEMA ni wabinafsi kama nilivyowahi kueleza. Wanawaza vyeo badala ya kuwaza ni namna gani Tanzania itaimarishwa kiuchumi na kijamii kwa uendelevu! CHADEMA wanaanza kugawana vyeo hata kabla ya uchaguzi kufanyika hii inaleta picha kuwa kuna uwezekano mkubwa hawa jamaa watatuuza watanzania ama kwa mafungu ama kwa jumla huko kwa wabaya wetu! Mwenyekiti wa chama ni kielelezo cha uimara na nia ya chama hicho kupitia taratibu za chama hicho! Mbowe ameonyesha nia ya chadema.

Shime watanzania! Tuwakate wawakilishi wa CHADEMA kuanzia udiwani mpaka urais kwa sababu chama hicho kimeonyesha nia ya ubinafsi uliopitiliza kupitia viongozi wao! Hawa hawatatujali sisi watanzania!

Nina imani na watanzania, kwa sababu tunaenda kuonyesha nia ya dhati ya kuilinda nchi yetu Tanzania kwa kutowapigia kura Chadema na vyama vingine vyenye mlengo wa Chadema.

Mungu ibariki Afrika na watu wake; Mungu ibariki Tanzania, Amina.
 
Back
Top Bottom