Mbunge Shabiby: Hata wewe Spika ukileta siasa zako tunaweza kukuazimia

Mbunge Shabiby: Hata wewe Spika ukileta siasa zako tunaweza kukuazimia

Kwahio wewe ukikosa pesa haujiamini ?

Hio ni distorted view ya maisha na being vain..... Inaonyesha ukipata Pesa au kama una Pesa utakuwa una-belittle wengine yaani unajiona upo juu sababu ya pesa, Sadly hii view ndio sababu kubwa ya uchawa (kuona wengine ni superior; character counts for nothing in such people'e eyes)
Unaongea ukweli mtupu. Muone level ya Diamond. We unamuonaje?? Kwanini sio Chege? Maana wote ni wasanii tena Chege mkali kuliko Mondi. Tofauti ni pesa.
 
Kuwa jasiri na mtu mwenye misimamo ni hulka/tabia ya mtu. Haihusiani na umasikini au utajiri
 
Hizi ni fikra za kizamani sana. Nani kakwambia huwezi kuwa na msimamo bila ya kuwa na fedha?? Watanzania wengi wamekuwa dhaifu kimisimamo kwa kuwa na fikra kama hizi kwamba ili uwe huru ni lazima uwe na fedha.

Huyo Shabiby inawezekana katoa maneno hayo kutokana na mtizamo wake binafsi na wala si kwa hela alizonazo.
Bwashee, njaa na misimamo wapi na wapi?

Muulize Mbowe kwa lowasa
 
Bwashee, njaa na misimamo wapi na wapi?

Muulize Mbowe kwa lowasa
Acha uzushi wewe. Nyie mnawaaminisha watu kwamba hawawezi kuwa na misimamo kama hawana hela ili muendelee kuwatawala. Yaani mnatumia umaskini wao kuwatawala kifikra.

Mwalimu Nyerere alipobishana na Margaret Thatcher juu ya Rhodesia, Wakati ule Tanzania tulikuwa matajiri kuliko Uingereza??
 
Ulikuwa unajiamini umeshachuma pesa ulizoenda kuanzisha biashara
Niliacha kila kitu.. nilikuwa naidai kampuni milioni kadhaa nilizisamehe. Nilianza kupanga chumba cha 25000/= kwa mwezi. Katika maisha yangu ule ndo uamuzi wa kishujaa zaidi niliowahi fanya kwa sababu baada ya huo uamuzi nilikaa miaka miwili ya kupigika haswa. Ilinijengea heshima mimi binafsi hadi familia yangu. SIMAMA KWENYE HAKI hutaonewa wala kumsujudia mtu.
 
Why walimu waajiriwe wizarani na kusambazwa?why kila Halmashauri iajiri yenyewe moja Kwa moja??kusiwepo na kuhama Hama
Naunga mkono hoja. Ajira kama za walimu, manesi, waganga, watu wa mifugo, nk zifanyike kwenye halmashauri za wilaya na miji.
 
Hii yote ni serikali kushindwa kuajiri waalimu zamani lawama zilikuwa kupangwa mjini vs vijijini lkn watu walipata ajira sasa hv hamtoi ajiri zikitolewa kiduchu hd wabunge wanaacha kujadili mambo ya msingi km report ya CAG mnaanza kudiscus ajira za upendeleo mshahara laki tatu mnaacha kujadili mabilioni yaliyoibwa
 
Tafuta Hansard kuna mtu alikuwa anaitwa Phares Kashemeza Kabuye aliyekuwa Mbunge wa Biharamulo. Huyu Mzee alipiga kampeni kwa Baiskeli na kushinda ubunge dhidi ya mpinzani wake aliyekuwa anatumia magari kufanya kampeni zake.

Alipokuwa bungeni michango yake iliheshimika na kukumbukwa mpaka leo. Kabuye alikufa kwenye ajali ya Basi wakati akielekea Dar es salaam. Hakuwa tajiri lakini alikuwa ni mtu mwenye misimamo thabiti.

Nyie msiojiamini kwa kusingizia kwamba hamjiamini kwa kuwa hamna hela, mnamkufuru Mungu ama mnamuonesha kwamba alikosea kuwaumba binadamu.
Hata mchungaji Msigwa ni maskini lakini alikuwa anamkomalia Shujaa Magufuli japokuwa ni Ndugu yake!
 
Umasikini wa nini ? Umasikini wa Fikra ? Ofcourse ukiwa na Umasikini wa Fikra unaweza ukatafuta legitimacy ya Pesa au jambo lolote lile... (According to Nyerere utatafuta legitimacy kwenye Udini, Ukanda au Ukabila)...,

Kama una msimamo au kama unajua unachokisimamia hautayumbishwa na mtu yoyote...., Ingawa point yako labda useme mtu unayemtegemea akulishe ni vigumu kumpinga (lakini hapa ndani ya hii nchi kudhani mwanasiasa mwenzako au mtu pale serikalini ndio anakuweka duniani ni fikra potofu) and hence emancipation of mental slavery is needed...,

'I'd rather die like a man, than live like a coward' Why you might ask ?!!! Because a Coward dies a thousand Deaths...
Hii uliongea hapa sio sawa
Nyerere alikua na msimano sana ila during 1980's yalimshinda akasema nangatuka unajua ni kwanin ilikua nchi icolapse au ufuate wale mabeberu kupitia sap ili waokoe jahazi ujasiri wa nyerere haukumsaidia tena ikabid amwachie mwinyi ambaye akakubali matakwa ya sap kwa mlango wa ruksa

Kwenye maisha ni kweli unaweza ukawa maskin na jasiri ila likija swala linalohusu hela lazima ukawapigie magoti wenye fedha ndo hapo udhaifu unapokuja mfano unafamilia huna hela lazima ukubali ukawapigie magoti wenye hela ili uiokoe familia yako ndo alichofanya nyerere

Pambana sana uwe na financial freedom ndo ujasiri wenyewe huo
 
Hii uliongea hapa sio sawa
Nyerere alikua na msimano sana ila during 1980's yalimshinda akasema nangatuka
unajua ni kwanin ilikua nchi icolapse au ufuate wale mabeberu kupitia sap ili waokoe jahazi ujasiri wa nyerere haukumsaidia tena
Kwamba Nyerere mambo yangeendelea kuwa sawa angekuwepo madarakani mpaka siku anakufa ? Wale ambao wapo Madarakani na nchi zao zimewekewa vikwazo unawaweka kundi gani ? Je Nyerere aliacha kuwapiga misumari IMF na Developed Countries kwa Marginalization of Undeveloped Countries
ikabid amwachie mwinyi ambaye akakubali matakwa ya sap kwa mlango wa ruksa
Nikuulize swali dogo tu.... Where does Power Lies...




Power resides where men believe it resides. It's a trick. A shadow on the wall. And a very small man can cast a very large shadow.

Kwahio mtu unaweza usiwe na Pesa ukawa na Power unaweza ukawa masikini ukapata nguvu ya UMMA na kuwatetemesha hata wafalme, unadhani Gandhi angekuwa anatembelea Royce Loyce na kuishi maisha ya Makabaila angefanikiwa kama alivyofanikiwa......... (In short kizazi hiki kimekuwa brainwashed na kudhani real power ipo kwenye Pesa) and that my friend is being shallow.....; When Push comes to Shove hawa millions of Have Nots target yao itakuwa hao ambao kwa sasa wanawaona ni makupe / walamba asali
Kwenye maisha ni kweli unaweza ukawa maskin na jasiri ila likija swala linalohusu hela lazima ukawapigie magoti wenye fedha ndo hapo udhaifu unapokuja mfano unafamilia huna hela lazima ukubali ukawapigie magoti wenye hela ili uiokoe familia yako ndo alichofanya nyerere

Pambana sana uwe na financial freedom ndo ujasiri wenyewe huo
Basic Human Needs ni zipi ? Na unawapigia magoti ili wakupe nini na kibaki / kidumu kwa muda gani? Kwamba shughuli iliyobaki ya kuweza kupata Mavazi , Malazi na Chakula ni kupiga magoti ?

Ungekuwepo enzi za Unganyanganyi vita na utumwa ungeendelea kupiga magoti to infinity au ungekuwa tayari kufa ili kubadilisha mfumo ambao unaona haupo sawa sababu kuishi katika huo mfumo kwako ni kifo kwa kila sekunde unayoishi

NB: With Money you Get Mercenaries..., to get loyal followers you need to have a vision which people believe in....
 
Back
Top Bottom