Mchungaji Msigwa agoma kupanda gari za CCM, alakiwa na wana-CHADEMA

Mchungaji Msigwa agoma kupanda gari za CCM, alakiwa na wana-CHADEMA

Mbunge wa Iringa mjini, Mchungaji Peter Msigwa amekataa kupanda gari la serikali lililopelekwa gerezani Segerea ili kumchukua baada ya kulipiwa faini.

Awali kulitokea mzozo kati ya wafuasi wa CCM wakiongozwa na Ndugu Humphrey Polepole ambao walitaka Msigwa apande gari ya serikali kwa madai kuwa amelipiwa faini yake na Rais JPM, lakini wafuasi wa Chadema wakamtaka apande gari aliloandaliwa na Chadema kwa kuwa chama hicho ndicho kimemlipia faini kupitia michango ya watanzania.

Wafuasi hao walidai kwamba wakati Rais JPM anapeleka fedha tayari Chadema ilikua imeshamlipia Msigwa na hivyo fedha hiyo irudishwe kwa Rais ili ikafanye shughuli nyingine za maendeleo.

Kufuatia mzozo huo wafuasi wa Chadema walizuiwa kuingia gerezani humo na wafuasi wa CCM wakiongozwa na Polepole waliingia wakiwa kwenye magari ya serikali tayari kumlaki Msigwa.

Lakini Msigwa alikataa kupanda gari ya serikali aliyoandaliwa na kutembea kwa mguu hadi nje ya gereza walikokuwa wafuasi wa Chadema ambao wamemlaki kwa shangwe na sasa anaelekea makao makuu ya Chadema, eneo la Kinondoni ili kufanya mkutano na wanahabari.!
mbio za uchaguzi October zinaanzia cinema hii! Hivi naomba kuuliza, kama wananchi wasingejitokeza kuchangia faini CCM ingejipeleka kimbelembele kulipa?
 
Mchango wa mh Rais umesaidia sana,
Chadema iliomba msaada wa michango Kwa wananchi wote Na Rais JPM kaitikia ombi lkn pia familia ya mchungaji msigwa imeomba msaada kutoka Kwa Rais Na Rais kakubali ombi, tatizo linatoka wapi?
Hongera sana Kwa Rais
Zitto ni kiongozi wa ACT alifuata utaratibu wa chama akawakirisha mchango wake kwenye chama, wanachama wa CHADEMA na wananchi waliowengi kushinda hata wafuasi wa CHADEMA wametoa michango yao kwa kupitia kwenye utaratibu uliowekwa na chama, kama mchango wa muheshimiwa hauna hila ndani yake kwanini na yeye asifuate utaratibu kama wananchi walivyofanya? Mashinji na Msigwa wote walihukumiwa katika mahakama moja na wote walikuwa gereza moja lakini aliyelipiwa faini na Polepole ni Mashinji,Msigwa aliendelea kusubiri wananchi waendelee kujipigapiga ili wa kamtoe,kama viongozi wa CCM wana nia njema na Msigwa kwanini hawakumtoa sambamba na Mashinji?.
 
Dah Tanzania ya sasa imekuwa na viongozi wa kipumbavu sana yaan sio ccm wala chadema yaan viongozi wote wana Parsons interest yaan hakuna mzalendo wa nani yaan wote niwapumbavu sana nachukia sana yaan nakasilishwa sana sana yaan aisee mpaka nashindwa kueleza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio tatizo kikubwa kalipiwa faini Na mh. Rais Na katoka.
Mchango wa Rais umesaidia sana kutoka kwa msigwa leo Na kujumuika Na familia yake.
kama wananchi wasingechanga Mh Rais angejitokeza kulipa? Na mbona anabagua?
 
Kwaiyo ametoka Msigwa pekeake au pamoja na wale wengine wawili chadema iliyosema imewalipia?
 
Mkuu zimelipwa ila hajatak kuongea na waandishi
Hii ni km unakutana na demu bar mnaahidiana kulala naye.demu anakunywa bia nyingi weee ukijua unaenda kula mzigo .demu anapitia chooni huyoooo😠😠😠😠..so hapa Rais wenu alijua atakula mzigo...! Tumbafu!

Bank haijalipwa, nyaraka zilizopo ni za kuwahi mlango wa nyuma mahakamani na kuchukua releasing order chap
 
Labda umewazidi ukilaza
Sometimes Tujaribu kutumia akili dada yangu hatakama ni Ngumu
.
.
.
.
[emoji23]Napenda kuona Taifa letu Likiwa na watu wanaojiolewa Sanaa
Hakukua na Haja Hata kidogo ya kuja kufungua Mauzi na kubishana


We vipi?? Nan kafungua uzi? Mie nimeona you tube nikapita km sioni..kwani kuwa kilaza ndo nakufa! Nitokee mie hapa😏😏😏
 
Msigwa nae ana deko sana [emoji28]
Anaringa sbb anajua Mh. Rais ni ndugu yake, basi anafanya atakalo deko tupu. Mh. Rais wetu ana roho nzuri sana ya kibinadamu, ingekuwa mm hiiiiiiiii silipi wala simletei gari tena namuacha jela akae kae nikiona hakuna wa kumtoa ndio natoa mchango..[emoji28][emoji28]
Tuliisha lipa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu zimelipwa ila hajatak kuongea na waandishi
Hii ni km unakutana na demu bar mnaahidiana kulala naye.demu anakunywa bia nyingi weee ukijua unaenda kula mzigo .demu anapitia chooni huyoooo[emoji34][emoji34][emoji34][emoji34]..so hapa Rais wenu alijua atakula mzigo...! Tumbafu!
Heri uwe na makubaliano ya kula mzigo[emoji23] ww unanunua tuu bia huelezi shida zako mwisho wa siku dem anasepa,utaacha kuona aibu na kumkandia [emoji15][emoji15][emoji15][emoji15]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Msigwa nae ana deko sana 😅
Anaringa sbb anajua Mh. Rais ni ndugu yake, basi anafanya atakalo deko tupu. Mh. Rais wetu ana roho nzuri sana ya kibinadamu, ingekuwa mm hiiiiiiiii silipi wala simletei gari tena namuacha jela akae kae nikiona hakuna wa kumtoa ndio natoa mchango..😅😅
Huo msaada hata mbele ya Mungu ni batili. Unampaje mtu msaada kisha unapeleka makamera ili kumsimamanga kwa msaada uliompa? Mambo kama haya yanafanywa na watu wenye IQ below 50 points
 
Back
Top Bottom