Pre GE2025 Mchungaji Msigwa atangaza kukata rufaa kupinga Ushindi wa Joseph Mbilinyi (Sugu) Kanda ya Nyasa

Pre GE2025 Mchungaji Msigwa atangaza kukata rufaa kupinga Ushindi wa Joseph Mbilinyi (Sugu) Kanda ya Nyasa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ni yeye anasema hivi, au wewe?
Si walienda mpaka kwenye mdahalo star tv kwa odemba

Maswali:
Angeshinda yeye angelalamika?

Ushindi wa ndani ya chama Ni kwa faida ya Nani?

Yeye kaongoza muda wake Ni vyema sasa Ni muda Sasa aachie akili mpya iongoze nyasa

NB.
Eg. Kikwete vs mkapa mwaka 1995 mbio za uraisi alitoa speech nzurii Nanukuu ""Tunatoka hapa TUKIWA wamoja zaidi""

Msigwa alitakiwa aseme TUMEMALIZA UCHAGUZI NA TUMETOKA HAPA TUKIWA WAMOJA ZAIDII
 
Kama asemayo mchungaji yana ukweli; hata chembe ndogo tu ya ukweli, basi huyo virusi ndani ya chama atakuwa ni hatari sana kwa uhai wa chama chenyewe. Huyo kirusi siyo wa kuchezewachezewa na kujifanya chama hakimuoni.
Ngoja twende kwenye kamati kuu
 
Msigwa alitakiwa aseme TUMEMALIZA UCHAGUZI NA TUMETOKA HAPA TUKIWA WAMOJA ZAIDII
Kwa hiyo hata kama aliona dosari, alitakiwa akubali au siyo?

Ni hivi, wewe na mimi hatujui kilichotokea katika uchaguzi huo. Haitoshi tu kusema kwa kuwa Mchungaji kishaongoza, basi asilalamike kama anaona kuna dosari hili halina maana yoyote. Kama anaona alichezewa rafu, ni haki yake kueleza hivyo na kuomba chama kiliangalie hilo analolalamikia.
 
Kura alihesabu nani? hakuwa na wakala? Au hakwenda mwenyewe kusimamia kura zake kwenye majumlisho?
Alitakiwa kuwepo hata kule wajumbe walipopewa laki tano hadi milioni; si ndivyo unavyosema wewe hapa?
 
Alitakiwa kuwepo hata kule wajumbe walipopewa laki tano hadi milioni; si ndivyo unavyosema wewe hapa?
Wewe unaamini Msigwa hajatowa pesa? au amezidiwa dau?

Kwahiyo waliompigia kura 52 wao hawakupewa pesa?

Kwanza anawadharirisha wajumbe.
 
Wewe unaamini Msigwa hajatowa pesa? au amezidiwa dau?

Kwahiyo waliompigia kura 52 wao hawakupewa pesa?

Kwanza anawadharirisha wajumbe.
Hapana, siamini hivyo hata mara moja.
Kama na yeye kata chochote na kazidiwa dau na mwenzie, sidhani kwamba hilo ndiyo iwe sababu ya kumzuia asilalamike.
Kwa upande wangu, kama ni hivyo unavyo eleza wewe, basi wote hawafai kuwa viongozi.
Kamati Kuu ya chama iwasikilize wote na kama itabainika wote wanahusika, basi chama kina jukumu la kusahihisha hali hiyo,, na siyo kuifumbia macho.

Kamati Kuu ikiruhusu upumbavu huo, basi hakunma matumaini yoyote kwenye chama hicho; kwa sababu hakitakuwa tofauti na CCM wanaowachezea mchezo huo sasa hivi.

Pesa ya waarabu itaitesa sana nchi hii sasa hivi.
 
Mbowe ndio mchawi wa hiki chama. hatuna chama cha upinzani nchini, hata Tundu Lisu atakuwa anapata shida sana, anashindwa tu afanyeje, ila angekuwa na mbadala, hakika angeshakikimbia chama hiki zamani sana, kwasababu kina rafu, umwinyi, kupokea asali na udanganyifu mwingi. kama msigwa alilalamika kabisa kwamba Mrema kule mbeya alionekana ananyweshwa pombe na sugu, na lawama kibao, what do you expect.
Hata ACT sio cha upinzani kwani😁😁😭
 
Ni AIBU kubwa kwa CHADEMA kumchagua Sugu badala ya Peter Msigwa. Hata mukiniambia kuwa Sugu alikuwa na fedha chafu na kagawa kwa wajumbe, fedha unapokea lakini kura unapiga kwa kutumia akili yako.

Naiombea hiyo rufaa ipite ili IWASAFISHE CHADEMA.

Unamuachaje mtu kama Msigwa ana madini, amenyooka, hanunuliki na ana VISION na kwenda kumpa kura mvuta bangi, mtu wa matusi, mvaa mlegezo??

Mimi SIYO CHADEMA ila you people ARE NOT SERIOUS!!

Kwa taarifa yenu, mukirudia makosa haya kwenye Ubunge wa Mbeya Mjini mkamismamisha SUGU 2025, JIMBO MNALIPOTEZA.

TULIA hakubaliki Mbeya ukiacha maeneo ya Uyole, Itezi, Igawilo na Iduda anakogawa hela na T-shirt. Lakini zile kata asilia za Mbeya Mjini yaani kuanzia Mwakibete hadi Iyunga, Sisimba, Mwansekwa Tulia Ackson si lolote.

Tafuteni mtu anayeuzika ila siyo SUGU
Ya chadema waachie chadema mkuu
 


Akiongea na Waandishi wa Habari leo, Peter Msigwa amesema kwamba Ushindi wa Sugu ulijaa makando kando na Mchezo Mchafu (Hakufafanua)

Ametangaza kukata rufaa kwenye Kamati Kuu ya Chama chake kupinga ushindi huo wa Sugu, bado haijajulikana kama Kamati Kuu ikiridhishwa na Madai yake nini kitatokea, Sugu atanyang'anywa Ushindi na kupewa Msigwa au Uchaguzi utarudiwa

Binafsi nampongeza Mchungaji huyu kwa uamuzi wake huu, maana hii ndio njia Sahihi iliyowekwa na Chama chake ya kudai haki.

Pia soma

Hiyo ndio demkrasia tuitakayo, si mambo ya fomu moja ya uchaguzi.
 
Sasa kwa nini wachezewe akili namna hiyo kama wao ni watoto wachanga.

Maana yake ni kwamba wote wanaonekana kutokuwa imara katika wanayoyasimamia.
Urafiki wa Msigwa na ASAS una historia ndefu tangu 1980s hivyo kumfadhili siyo kumnunua
 
Namuona Mchungaji Msigwa nje ya CHADEMA. Hizo rufaa ni mwanzo wa safari yake kutoka CHADEMA. Kote atasema hajatendewa haki. Usiku ule na hotuba ile aliyoitoa, alisifiwa kwa political maturity aliyoionyesha. Nini tena kimempata? Anatafuta sababu na cha kusema akijiondoa CHADEMA..
Naiona chadema ikisambaratika endapo itashindwa kushughulikia kwa weredi ukigeugeu huu wa Msigwa. Kuna mkono wa adui nyuma ya Msigwa.
 
Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyasa aliyemaliza muda wake na kushindwa katika Uchaguzi uliompa ushindwa Joseph Mbilinyi (Sugu), Mchungaji Peter Msigwa amekata rufaa kupinga Uchaguzi huo akidai ulivurugwa
-
Akizungumza na Waandishi wa Habari, Msigwa amesema Uchaguzi huo ulitawaliwa na Mbinu Chafu ikiwa ni pamoja na Wasimamizi wa Uchaguzi kuwazuia Makatibu Watatu wa Mabaraza kupiga Kura kinyume na Katiba ya Chama hicho

#JamiiForums #Democracy #JFDemocracy #CivilRights
 
Kabla kusikiliza hiyo rufaa kamati ya nidhamu ya Chadema imuite na imhoji mchungaji Msigwa Kwa Nini aliita vyombo vya habari kusema atakata rufaa?

Kwani taratibu kichama si angeweza kata rufaa moja Kwa moja bila kuita vyombo vya habari

Kwani ndivyo katiba ya Chadema ndivyo inavyosema kuwa mtu akitaka kukata rufaa ndani ya chama lazima apitie kwanza kwenye vyombo vya habari Kwa kuitisha press conference?
Ndiyo demokrasia yenyewe hiyo. Hajatenda kosa lolote kwa kuita vyombo vya habari.
 
Back
Top Bottom