Mfumo wa Jeshi la Polisi ubadilishwe, Unakandamiza na kunyanyasa Wananchi hasa wa daraja la chini

Mfumo wa Jeshi la Polisi ubadilishwe, Unakandamiza na kunyanyasa Wananchi hasa wa daraja la chini

Polisi anakukamata huna kosa au kwa kosa la kuhisiwa tu, ukianza kuhoji kunanini anakukamata bila sababu, unatandikwa haswaa,unafika kituoni unaambiwa saini hapa ukiuliza kwanini mbona sielewi na sign nini?

Unapigwa haswa, na baada ya hapo unawekwa ndani, kisha ndugu wakija wanaambiwa hawezi kutoka huyu akae kwanza siku 10 si anajifanya mjuaji anajua sheria tuone sasa, na mkija bila laki 4 hatoki milele, baada ya siku 4 ndugu wana lia kuomba msaada utoke anaambiwa atoe laki 6, ndugu wanajichanga wanatoa laki 6 mtu anatoka akiwa kaumizwa na majeraha mengi mwilini ambayo kapigwa bila kosa.

Jeshi hili ni la kinyang'anyi, la kionezi kwa raia libadilishiwe muundo wake wa utendaji kazi, kwa jinsi ilivyo sasa polisi yuko juu sheria na hasa kwa raia ambao hawana watetezi.

Wananchi hawa wakawaida wananumizwa na kuteswa sana hiki chombo yani polisi wakiwa na shida na pesa tu wanatafuta sababu ya kukamata raia na kuwatoza fedha nyingi bila kosa na hawataki kuhojiwa ukowahoji unapigwa haswa , hiki chombo si rafiki kwa raia si msaada kwa raia kabisa na raia akinyanyaswa hakuna mamlaka ya kukiwajibisha hiki chombo, polisi wabadilishiwe namna ya kutekeleza kazi zao na kama ilivyo hivi sasa.
Yasiyowakuta hawawezi kukuelewa
 
Polisi anakukamata huna kosa au kwa kosa la kuhisiwa tu, ukianza kuhoji kunanini anakukamata bila sababu, unatandikwa haswaa,unafika kituoni unaambiwa saini hapa ukiuliza kwanini mbona sielewi na sign nini?

Unapigwa haswa, na baada ya hapo unawekwa ndani, kisha ndugu wakija wanaambiwa hawezi kutoka huyu akae kwanza siku 10 si anajifanya mjuaji anajua sheria tuone sasa, na mkija bila laki 4 hatoki milele, baada ya siku 4 ndugu wana lia kuomba msaada utoke anaambiwa atoe laki 6, ndugu wanajichanga wanatoa laki 6 mtu anatoka akiwa kaumizwa na majeraha mengi mwilini ambayo kapigwa bila kosa.

Jeshi hili ni la kinyang'anyi, la kionezi kwa raia libadilishiwe muundo wake wa utendaji kazi, kwa jinsi ilivyo sasa polisi yuko juu sheria na hasa kwa raia ambao hawana watetezi.

Wananchi hawa wakawaida wananumizwa na kuteswa sana hiki chombo yani polisi wakiwa na shida na pesa tu wanatafuta sababu ya kukamata raia na kuwatoza fedha nyingi bila kosa na hawataki kuhojiwa ukowahoji unapigwa haswa , hiki chombo si rafiki kwa raia si msaada kwa raia kabisa na raia akinyanyaswa hakuna mamlaka ya kukiwajibisha hiki chombo, polisi wabadilishiwe namna ya kutekeleza kazi zao na kama ilivyo hivi sasa.
Hivi mtu kaenda kusomea upolisi kwa matokeo ya division IV:26-33 unategemea awe na intelligence sahihi ya maisha ya kawaida?.
Mpaka tubadili mfumo wa elimu ya jeshi la polisi pamoja na usimamizi na utendaji kazi wao. Wengi ni washenzi sana(Naweza kuthibitisha).
 
Inasikitisha sana mfumo wa haki jinai ni shida hata report yake haifanyiwi kazi.

Kuna mmoja mwenye ulemavu wa ngozi amewekwa ndani kisa tu mwanamke ameenda kuripoti ampepigwa na wamemuibia vitu vyake vyote vya ndani.
Haki jinai wale wazee wali divert issue,badala ya kueleza namna watu wanavyo kosa haki zao polisi na mahakani wakakimbilia kusema eti fire wakitwa jeshi wanatisha wananchi.
Hata kama wewe ni polisi unapoenda kumkamata mtu lazima uvae uniform au awepo mmoja mwenye uniform na pia lazima awe na arrest warrant iliyosainiwa na hakimu…
 
Mbona inaeleweka Polisi huzingatia Taratibu zilizowekwa kisheria katika Utekelezaji wa majukumu yao. Wewe ilkuwaje?
Imefika mahali ni afadhari ukutane na jambazi huenda anaweza akaingiwa roho ya huruma sio hawa polisi wetu wana unyanyasaji mkubwa sana aisee sina hamu na hawa watu hasa akisha jiona kabeba bunduki na kavaa jezi anajiona ni mungu.
 
Hivi mtu kaenda kusomea upolisi kwa matokeo ya division IV:26-33 unategemea awe na intelligence sahihi ya maisha ya kawaida?.
Mpaka tubadili mfumo wa elimu ya jeshi la polisi pamoja na usimamizi na utendaji kazi wao. Wengi ni washenzi sana(Naweza kuthibitisha).
Kuna siku wamekuja mtaani wanakusanya tu pikipiki yeyote wanayo iona wanazirushia kwenye gari lao bila hata maswali yani wanazibeba tu hovyo hovyo zinavunjika vioo hawajali wanakuja shuka shuka shuka, hao wanabeba kwenye gari kituoni, wakifika wanazimwaga tu nje taa zimepasuka, vioo vimepasuka yani fujo tu, halafu sasa unaenda kufuatilia kuitoa unakutana na milolongo hata kama unakila kitu na kipo sawa wanakwambia tuibebe tuilete hapa halafu uichukue bure bure tu, haya mnamalizana ukitoka hapo uanze kuhangaika kwa mafundi taa zimepasuka, vioo vimepasuka na huna wa kumdai na imemebwa haina kosa lolote yani hawa watu hawa.
 
Kuna siku wamekuja mtaani wanakusanya tu pikipiki yeyote wanayo iona wanazirushia kwenye gari lao bila hata maswali yani wanazibeba tu hovyo hovyo zinavunjika vioo hawajali wanakuja shuka shuka shuka, hao wanabeba kwenye gari kituoni, wakifika wanazimwaga tu nje taa zimepasuka, vioo vimepasuka yani fujo tu, halafu sasa unaenda kufuatilia kuitoa unakutana na milolongo hata kama unakila kitu na kipo sawa wanakwambia tuibebe tuilete hapa halafu uichukue bure bure tu, haya mnamalizana ukitoka hapo uanze kuhangaika kwa mafundi taa zimepasuka, vioo vimepasuka na huna wa kumdai na imemebwa haina kosa lolote yani hawa watu hawa.
malipo yao ni hapa hapa duniani...
 
Askari wanatofautina...Kuna wapo wachache wenye roho nzuri na kusaidia...ila Kuna haya majanbazi yamevaa joho la police aisee mpka huwa nasema kimoyomoyo...ningekuwa mchawi Mimi aisee Hawa police wanaoonea watu hovyo ..nilikuwa nauwa wote..
 
Ila kuna muda askari wapewe maua yao hasa wa kituo cha igogo - Nyamagana 🙌
Kukiwa na OCS asiye penda mambo ya hovyo huwa anawaonya vijana wake wafunge brake, ila OCS akiwa mpenda pesa za mkato hilo eneo kazi mnayo, hakuna haki hapo kituoni utakayo ipata na ukijifanya kuuliza uliza haki yako unakula kipigo heavy , kuna kipindi hata kituo cha pale buhongwa kulikuwa na mkuu wa kituo mcha mungu sana ukiwa na kosa utatendewa sawa na kosa lako na kama umeonewa na askari wake atawaita na kuwapatanisha ili chuki isiendelee baina yenu ila ni wachache sana viongoz wa aina hiyo ndani ya jeshi la polisi
 
Nchi hii ukiwahuna hela, huna connection na viongozi wakubwa wa kisiasa haswa chama tawala, huna connection na viongozi wakubwa serikalini, maaskari wakubwa, wanajeshi wenye vyeo vikubwa, aale wavaa suti nyeusi wenye kutembelea gari ya mwaka 2024 lakini number plateni A, ombea lisikukute jambo, ndio utajua hukuumbwa kuishi nchi hii, wewe umevamia nchi ya watu.

Inasikitisha ila ndio maisha yetu kiuhalisia
Dawa yao ni kuwafanya kama alivyofanya Hamza mwaka 2021. Hao mbwa walinidhalilisha sana mwaka 2014/2015..
 
Mtu anaambiwa uko chini ya ulinzi na anauliza ni kwa Tuhuma/Kosa gani ; anaambiwa utafahamishwa ukifika Kituoni. Hapo inakuwa shida.
Kwanini usimwambie mtu kosa lake ni nini zaidi ya kuendekeza ubabe wa kijinga?? Ulaya hakuna upuuzi kama huu..
 
sheria ni ziliwekwa kwa ajili ya sisi maskini ili zitunyooshe ,.., matajiri , sheria ziko flexible zinajibadilisha kutokana na mazingira sheria duniani haki mbinguni
Ulaya na Marekani hakuna huu upuuzi mkuu. Muulize R Kelly..
 
Ata police wao kwa wao wana nyanyasana ukiwa police bila cheo kufukuzwa kama mwizi ni kugusa tu
 
kutokae huyu akae kwanza siku 10 si anajifanya mjuaji anajua sheria tuone sasa, na mkija bila laki 4 hatoki milele
Ushahidi haujitoshelezi!
====
Jamani mnapoleta issues nzito kama hizi jitahidi kuwarahisishia wahusika wa kumaliza tatizo husika kwa kutoa ushahidi uliokamilika.

Maelezo uliyoleta mleta mada hayajitoshelezi kusaidia kuondoa tatizo kwa sababu Yana ufafanuzi wa kina wa nani, wapi, na lini jambo hili lilitendeka. Vinginevyo, maelezo haya wengine tutayaona kama kulipaka matope jeshi la Polisi kwa sababu ambazo zimetokana na weledi wao katika kufanya kazi.
 
Back
Top Bottom