Pre GE2025 Mgombea Urais wa CCM 2030 lazima awe kijana with zero corruption status. Je, ni nani kati ya hawa?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Bila kujali wengi wanavyotamani Uchaguzi ujao wa mwaka 2030 zaidi ya 50% ya wapigakura wote watakuwa ni vijana.

Chama kitakachotaka kushinda Uchaguzi huo kisayansi lazima kije na mgombea mwenye maarifa ya kutosha na umri usiozidi miaka 50...​
Asiwe ametumika kisiasa kwa zaidi ya miaka mitano ili awe na open mind. Mtu aliyekwisha tumika kisiasa kwa muda mrefu anakuwa na mawazo yaliyogandia kwenye siasa zilizomkuza badala ya kuangalia dunia kwa mapana yake.
 
Bila kujali wengi wanavyotamani Uchaguzi ujao wa mwaka 2030 zaidi ya 50% ya wapigakura wote watakuwa ni vijana...​
Kwa mtazamo wa wengi makonda Ana nafasi kubwa kutokana na ushawishi anaoanza kujijengea kwa wananchi pamoja na kuchafuliwa sana toka enzi za jemedari jpm
 
Tundu Lissu
Tundu kuwa rais chenga tu..hana utulivu.Nyie urais kile cheo si mchezo - kizito sana.Kinahitaji mtu mtulivu asiyeropoka sana..Lissu ni mwanaharaki aendelee kuwa mwanaharakati...ndo kipaji chake..anafit huko
 
Miaka mitano ijayo hawa...
1.Hussein Bashe
2.Innocent Bashungwa
3.Tulia Ackson
4.Suleiman Jaffo
5.Jerry Slaa
 
Rais atakua Jerry Slaa baada ya Makamba kuvurunda.
Kama unamuita Simbachawene kijana sijui ulichelewa wapi.
 
Kingwalangwala hata kwenye hao 17 Bora hayupo? Kweli mdomo unaumba.
 
Rais wa 2030 ni huyo namba 11. (January Makamba).
 

Huko 2030 ni mbali. Kijana huyo apatikane 2025 kuliko hiki kituko kinachoendelea kwa sasa TZ
 
Tanzania hakuna uchaguzi, bali Kuna maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura. Hao vijana mnotegemea wataendelea kupanga mistari kwenye chaguzi za kishenzi watatoka wapi?
 
Mbona hakuna Kijana hapo kati ya hao uliowataja, zaidi sana 2030 wote watakuwa wazee kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…