Mgomo mkubwa Soko la Kariakoo: Maduka yamefungwa, Mei 15, 2023

Mgomo mkubwa Soko la Kariakoo: Maduka yamefungwa, Mei 15, 2023

Wana bahati wangefanya huo mgomo kipindi cha mwenda zake, sasa hivi tungekua tuna hesabu maiti za viongozi wa hilo soko.
Ndo maana Mungu aliamua kuwatetea Watanzania. Aliua sana na yeye kwa sasa ni mifupa mitupu kaburini bila kujali kaburi lake limepambwa na kulindwa usiku na mchana.
 
Leo asubuhi nimefika kariakoo kwenye biashara zangu lakini nimekutana na mgomo wa maduka kutofunguliwa

Nilikuwa bungeni kwa wiki kadhaa hivyo sikufuatilia sana mambo ya biashara nikiwaachia vijana

Maduka yamefungwa ingawa baadhi ya wamachinga wanaouza matunda wanaendelea

Sijajua sababu ya msingi zaidi ya ile ya TRA kututaka tuorodheshe store zetu tunazohifadhia mali

Hakuna mfanyabiashara ambaye yupo tayari kwa jambo hilo ,Jambo lilihitaji mjadala mpana

Hakuna fujo ingawa polisi ni wengi wanatembea tembea bila uelekeo.

View attachment 2622352
Ni vizuri serikali ikatatua matatizo yanayosababishwa na watumishi wa mamlaka zilizopewa jukumu la kukusanya kodi, RUSHWA nchi imehalalishwa na viongozi ambao wameweka mbele tamaa zao binfsi.
 
Hakuna mjomba wa kuwajengea Nchi,sio lazima Kila mtu afanye biashara,Kodi ya mtumishi ni kubwa kuliko Mfanyabishara mkwepa Kodi..

Serikali ikisema isimamiwe Sheria wote mtakuwa jela Kwa uhujumu uchumi,Sasa ni ajabu hata hiyo ndogonataka msilipe.
Mtumishi yupi unayemuongelea ambaye analipa kodi kubwa kuliko mfanyabiashara mkwepa kodi?
 
Shida ya kodi Ni kwamba wananchi tunaona zinatumika vibaya

Huwa nashangaa sana viongozi wanaodharau wananchi wao Ndo wanawalisha na kuwavisha Mia Mia za machinga na watu wa hali ya chini Zinafanya wao wawe juu

Hatutaki kudharau hawa watu kabisa
 
Hiyo comment yangu ni jibu la comment nyingine. Na kuna kitu umekikwepa umechukua kipande chako wacha nikuulize hapa.

Muuza madawa yaliyotengenezwa Tanzania ambayo hayajapita bandarini na mipakani hastahili kulipa kodi? Ukikata kodi mpakani na bandarini analipaje yeye.

Ulishawahi vuka mipaka ukaona mianya ya kupita bila kukaguliwa. Kule Arusha, Kilimanjaro na Tanga kuna mamia ya kilomita za mpaka na Kenya ziko wazi watu wanavuka. Mpaka sio ile border post pekee. Sasa hawa watalipaje kodi mpakani.

Simaanishi nawapinga ila jenga hoja isiyo na mashaka msije onekana mnakwepa
Hii inatumika kama justification ya kuwasumbua wafanyabiashara K/Koo na sehemu zingine za biashara ktk nchi hii. But sababu kubwa ni kutaka rushwa tu, period!!!!!!!!!!!!
 
Habari wakuu nipo mtaa wa mchikichi huku kariakoo maduka hayajafunguliwa hadi muda huu kuna nini kwani?

Ngoja niangalie na mitaa mingine.

img-20230514-wa0007-jpg.2622352

View attachment 2622412
View attachment 2622413


UPDATES...
Muonekano wa maduka mbalimbali katika soko la Kariakoo hadi saa 8.23 asubuhi huku kufungwa kwa maduka hayo kukihusishwa na uwepo wa mgomo wa wafanyabiashara wa soko hilo kongwe na maarufu Afrika Mashariki.

Wafanyabiashara wa Kariakoo wanafanya mgomo wa kufunga maduka wakishinikiza kupungua kwa kodi wanazotozwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

WAFANYABIASHARA WAGOMA KUMFUATA WAZIRI MKUU DODOMA

Ni baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makala kuwataka kupeleka malalamiko yao kwa Kassim Majaliwa ambaye anatarajiwa kukutana na uongozi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mawaziri husika na Kamati ya Wafanyabiashara ili kutafuta suluhu ya mgomo huo

Makalla amefika katika Soko Kuu la Kariakoo baada ya Wafanyabiashara kugoma kufungua biashara huku wakitoa malalamiko kadhaa ikiwemo madai ya uwepo wa utitiri wa kodi.

Wakizungumza baada ya Mkuu wa Mkoa kuondoka eneo la Kariakoo, wafanyabiashara wamesisitiza kuwa wanahitaji kuonana na Rais Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya kutoa kero zao huku wakisisitiza kuendelea kufunga maduka yao
.............
Takwa la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla la wafanyabiashara kumfuata Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa mjini Dodoma limepingwa.

Wafanyabiashara hao walioitisha mkutano mwingine baada ya Makalla kuondoka wamesema wanalipa kodi hivyo Waziri Mkuu Kama anataka kuonana nao awafuate kariakoo na sio wafanyabiashara kumfuata.

Azimio la wafanyabiashara hao endapo mfanyabiashara atakayefungua duka leo ni halali yao.

"Mwenyekiti usiogope tupo nyuma yako usiogope chochote," ameeleza mmoja wa wafanyabiashara hao aliyepanda jukwaani na kutoa muongozo alioudai ni wa kisayansi.
Kwa mtazamo wangu Serikali inapata kodi ya kutosha lakini haina mpango madhubuti wa kusimamia vizuri matumizi. Kodi ya wafanyabiashara iwatengenezee mazingira mazuri ya biashara. Tuna nchi ambayo tunanunua magari ya gharama kuendana na wakati kwa ajili ya wakuu wa wilaya lakini bado hatuna miundo mbinu salama ya kukuza biashara. Mfano kuruhusu watu kuendelea kuagiza bidhaa nje badala ya kuwapa ruzuku kuruhusu uzalishaji wa ndani ni kitu kibaya sana. Pia nchi yetu mfanyabiashara anaonekana ni chanzo cha mapato, inabidi tuwekeze katika mazingira mazuri ya uwekezaji ili ajira nyingi zitengenezwe. Na cha kuongeza serikali itumie vizuri Kodi ili kila mtanzania ahamasike kulipa kodi. Kwangu mimi kuona kila Landcruiser mpya ikitoka serikali inanunua bado hamjanishawishi. Ninalipa kodi ninayoona serikali inastahili na si zaidi. Na kijijini kwetu maendeleo mengi tumefanya sisi wenyewe wanakijiji kwa kuchangishana. Kwa hio sijahamasika kabisa.
 
Kama umewahi kufanya biashara kipindi cha tech za efd , Vat and the likes kuna kipindi at your will unatamani kabisa ufunge biashara kwa hiyari. Ili upumzike na usumbufu wa Tra.
Halafu kariakoo kusimama kishughuli sio jambo dogo ati.
True kabisa, wanakadiria wanavyojisikia
 
Kwan mipakani ndio hazichajiwi kodi mkuu au ulitaka kusemaje sijakupata vema?!
Kunatofauti kubwa kati ya mpakini na Bandari mkuu pale bandari kuna mamlaka nyingi sana kuna rushwa inatembea wanajua ukichelewa storeji inangezeka kilasiku boda tualipa pesa za Custom tu

lakini bandari kuna utaambiwa TPA TBS SIPING kwajili ya Delivery Order utaambiwa lipa pesa ya ukaguzi wa Mizigo utaambia lipia Lent utaambilia lipa storage mala agency fee kuna uswahili mwingi pale ukishindwa wanapiga mnada umesikia boda kuna hizo hekaheka?
 
Back
Top Bottom