Miaka 22 ya TICTS nchini yafika mwisho, mamlaka ya bandari kutosaini mkataba mpya

Ni ajabu sana. Ni kama serikali haikujua kuwa mkataba unaisha kabla. Halafu mkataba ukikaribia kwisha si unatangaza tenda upya? Ku negotiate na current contractor ni sawasawa na kufanya sole source procurement.
 
Ahsante mkuu 'imhotep', kwa hizo taarifa ulizoniwekea kama ushahidi wa umahiri wa kampuni hiyo, ambao hata TICTS ukitafuta habari zao na wao watakuwa na wasifu wa namna hiyo.
Hivi unajua TCTS ni kitawi cha kampuni gani duniani?
Hutchson
 
Nimependa tu ulivyotoa Credits kwa Gazeti langu pendwa la Kiswahili nchini Tanzania la MWANANCHI.
 
Jambo jema? Hiyo culture kwetu ni neno la kichina.
Ubinafsi umetujaa sana
Ni kukosa uongozi tu unaoamini kwamba sisi tunaweza sana kusimamia mambo yetu wenyewe.

Tukipata uongozi wenye uamini huo, utaona jinsi tunavyoweza kufanya mambo yetu tofauti kabisa na sasa hivi.


Ubinafsi siyo kitu kibaya kama ubinafsi huo unalenga katika kufanya mambo kwa mafanikio ndani ya mipaka ya sheria zilizopo.
Kila mtu, au wengiwetu tukifanikiwa kufanya hivyo, bila shaka taifa litainuka zaidi kuliko ilivyo sasa hivi wakati ubinafsi unalenga kunufaisha wengine wasiokuwa na manufaa yoyote kwa nchi yetu.
 
Sijawahi labda ni gugo.
LOooh, umenifanya nicheke kwelikweli.
Mimi sipo kwenye mambo haya, lakini katika ufuatiliaji tu wa haya maswala, hasa baada ya kuona mizunguko hii ya TICTS miaka yote, ilinilazimu niwajue hao wakubwa, kama nilivyokuja kuwajua hao Duai Port.

Sasa wewe mwenzangu, sijui ulianzia wapi kuwajuwa wababe hao wa Dubai, na kutoweza kujua kabisa habari za washindani wao wakuu duniani. Hivi kweli hiyo inaingia akilini?
 
Mwisho wa TICS ni mwanzo wa TICS nyingine, kwa Tanzania tegemea yaleyale au zaidi ya yale, God father wa TICS hayupo sasa amelala Lupaso, shamba linawaniwa na wahuni wengine..
Waipe sido hiyo kazi,, 😂
 
Hao DPWorld kuna jamaa yangu anafanya nao anasema wanatoa mshahara mnono.
 
Nimeiona Wachina hao hawafai.
Naona "sahihi yako" hapo chini.
Nikiunganisha na haya unayoeleza naanza kuwa na wasiwasi, usijekuwa kama "mhanga wa madawa ya kulevya", anayepambana bila ya mafanikio yoyote kuachana na ulevi wake.
 
Ahsante mkuu 'imhotep', kwa hizo taarifa ulizoniwekea kama ushahidi wa umahiri wa kampuni hiyo, ambao hata TICTS ukitafuta habari zao na wao watakuwa na wasifu wa namna hiyo.
Hivi unajua TCTS ni kitawi cha kampuni gani duniani?

hajui kama TICTS ni familia ya Hutchikson Container ya Hongkong na iliitwa TICTS huku Tanzania ili watu wapate pakupigia na wahongkong wawe salama likiwaka...

Ni kama Barrick alivyomtanguliza ACACIA TZ ili likiwaka yeye awe salama duniani asichafuke kwenye clean business...where is fuckin ACACIA after the Saga..

Umafia ulianzia duniani huku tunajifunza tu mbaya zaidi tunatia umasikini mataifa yetu tunanufaisha watu Ulaya na Asia huku tukiishia kupata pet money pumbavu.... Yaani unaiba kwenu hela unakwenda kudeposit kwa Mzungu Swiss pale huku wenzio nanyamba, naliendele, kachumu, Kemakolele nk wakifa njaa shenzi taipu..
 
Wakiwapa wazawa tumeisha....rushwa. ifisadi na inefficiency itasababisha wadau wakimbilie kwingineko
 
Wakiwapa wazawa tumeisha....rushwa. ifisadi na inefficiency itasababisha wadau wakimbilie kwingineko

sio lazima wapewe wazawa, we want clean business itakayonufaisha watanzania wooote sio pumbavu chache na familia zao.
 
Maccm hayo!
 
Mkuu serikali ndio tatizo,wala si TPA,kwani TPA ni mali ya serikali.
Management na bodi ya TPA zinateuliwa na serikali.
Serikali kwa kujuwa au kwa kutojua wamekuwa wakifanya maamuzi yasiyokuwa na tija.
Aliyetia mkataba wa awali na TICS ni serikali hiyo hiyo.
Hata pale wananchi walipoilalamikia serikali kuhusu mkataba huo,serikali iliongeza mkataba kabla ya expire date ya awali.
Magu alinguruma lakini aliishia kuongeza kodi tu ya upangaji tu.
Yawezekana TICS kama kampuni sio tatizp,tatizp ni baadhi ya watawala waliojiwekea maslahi yao binafsi.
 
Mwisho wa TICS ni mwanzo wa TICS nyingine, kwa Tanzania tegemea yaleyale au zaidi ya yale, God father wa TICS hayupo sasa amelala Lupaso, shamba linawaniwa na wahuni wengine..
Safari hii lazima atapewa Mzanzibari
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…