Miaka 22 ya TICTS nchini yafika mwisho, mamlaka ya bandari kutosaini mkataba mpya

Miaka 22 ya TICTS nchini yafika mwisho, mamlaka ya bandari kutosaini mkataba mpya

Ohooooo, si walisema watafanya wenyewe.

Serikalini kuna kitu huwa kinafurahisha sana, huwa maamuzi yanaanza halafu ndio wanagundua kuwa hata hata plan ya kutekeleza haipo.

Kwa pale TPA manpower na miundombinu ya kuziba pengo la TICS haipo.

Yaani hadi TPA waombe vibali vya ajira, waajiri watu wapya, wafanyiwe mafunzo kazini ndipo mambo yakae sawa, sio leo wala kesho.

Ni lazima tuache maamuzi ya kukurupuka haya, awamu nyingine hii.
 
Mamlaka ya bandari nchini Tanzania (TPA) imesema baada ya kampuni ya wazawa TICTS kuondolewa kuhudumu kwenye bandari ya Dares salaam tayari wameshapata mbadala wake ambao ni kampuni ya kigeni kutoka India itakayoanza rasmi kuhudumu bandarini hapo.

[emoji38][emoji38][emoji38]
 
Kama wamemleta muhindi basi tena tukubali tumeshapigwa. Muhindi hajawahi kufanya uwekezaji kwa faida ya nchi hii hata siku 1 nina uhakika 100% kuanzia hapo TPA mpaka magogoni rushwa imetembea. Hivi kweli mkurugenzi TPA upo serious na hii kazi kweli? Unamleta muhindi? Hii nchi ina laana haki ya mungu
 
Ohooooo, si walisema watafanya wenyewe.

Serikalini kuna kitu huwa kinafurahisha sana, huwa maamuzi yanaanza alafu ndio wanagundua kuwa hata hata plan ya kutekeleza haipo.

Kwa pale TPA manpower na miundombinu ya kuziba pengo la TICS haipo.

Yaani hadi TPA waombe vibali vya ajira, waajiri watu wapya, wafanyiwe mafunzo kazini ndipo mambo yakae sawa, sio leo wala kesho.

Ni lazima tuache maamuzi ya kukurupuka haya, awamu nyingine hii.
Wafanyakazi wote wa zaman wa kampuni iliyokuwa inafanya Kazi wapo na wanaendelea na Kazi
 
-Serikali/TPA ilipaswa kuandaa vijana wetu wa kitanzania ambao wamehitimu kwenye vyuo vya mbalimbali na hawana ajira miaka 10 iliyopita,
-Vijana wangepewa mafunzo ya manejimenti na uongozi au utawala wa masuala ya bandari.
-Vijana hawa wangekuwa attached kwenye bandari mbalimbali kubwa huko duniani kupata uzoefu kuhusu masuala ya management na uhandisi wa mitambo ya bandari.
-Ninashauri, Serikali au TPA,ingechukua mkopo kutoka taasisi za fedha za nje au ndani kwa ajili ya uwekezaji/kununua vitendea kazi vya kisasa na kutoa mafunzo kwa watumishi,jinsi ya kuvitumia vifaa hivyo.
-Faida ya Uwekezaji huo,ni kuondoa au kupunguza changamoto ya ajira kwa wahitimu wetu, Serikali au TPA kuongeza ukusanyaji wa mapato ya kulipa mkopo, watumishi,na Pato kubwa kwa Serikali.
-Hiyo Kampuni ya India,italeta wahindi kwenye Management,wa kusimamia interest zao/ watanzania wenzetu kitwana,
- Ni nadra kampuni ya India kuwekeza kwenye miundo mbinu,kama watawekeza wataleta mitambo iliyotumika kwenye bandari zao za nje.
-Tanzania itakuwa dumping place,tuliona mkataba na kampuni ya India ya RITES na TRC walileta mabehewa yaliyotumika na mtaji waliupata hapahapa Tanzania,it was a shame and this is going to recur,if the Government is not going to be Keen.
-Kama Serikali/TPA itasisitiza kuendelea na mpango wa kukodisha and kwenye kampuni ya India,tahadhari zichukuliwe kwenye vipengere vya mkataba, suala la uwekezaji miundo mbinu iliyotumika lipigwe marufuku na masuala yote yatakayo ahidiwa kwenye mkataba yatekelezwe kwa muda mwafaka.
-Mwekezaji atatumia mkataba huo kama collateral kukopa fedha kwenye mabenki yetu au mabenki ya India.
-Mkataba wa ukodishaji wa Berths hizo 4-11 upitiwe na bunge letu kwa niaba ya wananchi,tumechoka kupigwa na watanzania wenzetu ambao hawana uzalendo na huruma kwa watanzania wenzao.
-Serikali inakwama wapi, hatuna watalaam au tamaa za watu binafsi.

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Usalama usiokidhi wa wafanyakazi kazini.
Mishahara midogo kwa wafanyakazi.
Mafunzo kwa wafanyakazi kutokuwepo.
Kujazana wahindi hapo bandarini.
Mizigo ya wahindi kupewa kipaumbele.
Unyanyasaji na mambo mengi ya hovyo.

Hizi kazi bado zinawahitaji sana Wazungu kutoka Ulaya, tungempa Messina, Maersky, Blue water, hata mfaransa Bollore.
 
Kama wamemleta muhindi basi tena tukubali tumeshapigwa. Muhindi hajawahi kufanya uwekezaji kwa faida ya nchi hii hata siku 1 nina uhakika 100% kuanzia hapo TPA mpaka magogoni rushwa imetembea. Hivi kweli mkurugenzi TPA upo serious na hii kazi kweli? Unamleta muhindi? Hii nchi ina laana haki ya mungu
Subiria migogoro na wafanyakazi wake kila uchwao itakuwa ni migomo, shenzi sana wale jamaa.
 
Back
Top Bottom