jana nilitaka kujilipua na laki2 kwa timu 2, 1860 Munchen ll na Lyon , odds jumla zilikuwa 4.2, gemu ya 1860 Munchen ll ilikuwa inaanza saa 10 jioni na Lyon saa moja usiku.
Nikafika betshop mwenge ilikuwa 10 kasoro, gemu ya 1860 Munchen ll ndio ilikua inakaribia kuanza, kukawa umeme umekatika na network zao zinazingua, nikasema mbona leo nitakosa pesa, wakarebisha mambo saa 10 na dk 20 gemu ya 1860 Munchen ll ilikuwa ishaanza. Nikawa naitafuta kwenye live in play ya meridian niicheze live sababu niliangalia matokeao bado walikuwa hawajafungana kwahiyo odds hazijabadilika na nimuweke pamoja na Lyon, nillitafuta wee sikuiona kabisaa.
Nikajiondokea nikasema basi nimekosa ela leo, nikaenda kutafuta timu nyingine kuiweka na Lyon nikaifikiria Juventus, kwahiyo nikarudi beshop nikiwa na timu 2 Lyon na Juventus, lakini nikakumbuka nilivyokuta umeme umekatika pale betshop nikasema labda was warning sign nisije lazimisha nikapigwa za uso. Baadaye naangalia matokeo Lyon kadrwa 0-0 japo 1860 Munchen ll alishinda1-2! Nikasema mama yangu saivi laki2 ingekuwa imeshakwenda na maji, sasa sijui kuna ukweli kweny hizi warning sign, ebu ngoja nimuulize
Pasco .