Mimi naona dunia iachane na mfumo dume na rasmi 50/50 ishike hatamu

Mimi naona dunia iachane na mfumo dume na rasmi 50/50 ishike hatamu

haina noma ila kwenye mali labda tulizochuma wote, kama alinikuta nazo BIG NOOOOOO
Sasa kitendo cha kuchuma wote mali maana yake amekusaidia majukumu yako, mfumo dume unataka mume umhudumie mkeo kwa mali ulizochuma mwenyewe, bila kutegemea akusaidie majukumu yako
 
Lakini kwa mfano kama wewe mkuu huwa unasema unakataa ndoa kwa sababu wanawake wanafuata pesa na mali kwenye ndoa, maana yake ni kwamba unataka wanawake nao wajitafutie pesa na mali zao wasitegemee za mwanaume si ndio, sasa nakuuliza je unaona ni sahihi wewe kutaka mfumo dume kumtawala mwanamke ikiwa hutaki kutekeleza majukumu yako juu ya mwanamke wako
Apana sio halali kuendelea na mfumo dume, kila mmoja apambane chakula kiwekwe mezani mkizinguana mkashindwana, kila mmoja apite kushoto .

Ndio maana tunaukataa mfumo dume kwa kuwapa mabinti zetu elimu na kuwafanya wajiamini na kujipambania kama tufanyavyo wanaume .


Humu watu wanataka mfumo dume kimaneno ila kimatendo wanapambana binti zao waende shule za maana wajitambue, na kuwa na maarifa ya kujipambania.
 
Toa mashoga hapo, ushoga hauhusiani na matatizo au kutokua na akili, sijuagi kwann huwa mnahusisha nalo hili.

Mbona mashoga ndo wanao ongoza ku run dunia kwa sasa, wakiwa wana deliver vitu mbali mbali vinavyorahisisha maisha ktk nyanja zote.
"Ushoga ni ukosefu wa akili" Wewe ni mjinga kama wajinga wengine .
Hapa sijazungumzia wale wanaofanya ushoga kama sexual identity yao bali wale wanaofanya ushoga ili kutafuta urahisi wa maisha na hao ndio wengi sasa mimi sijui kuwatofautisha kwa majina ndio maana nikawa address tu kama mashoga, mimi huwa siwalaani mashoga na at times huwa nawatetea lakini huwezi kuwaweka kundi moja watu kama kina Steve Jobs au Tim Cook na hawa vijana wa mitaani wanaofanya ushoga kama kazi ili wapunguze ukali wa maisha na si kwamba eti wanapenda, ndio maana nikawaweka kundi moja na machawa maana wao wanaona hizo ni kazi lakini ukweli ni kwamba hawana akili kiasi cha kuwalinganisha na baadhi ya wanawake
 
Apana sio halali kuendelea na mfumo dume, kila mmoja apambane chakula kiwekwe mezani mkizinguana mkashindwana, kila mmoja apite kushoto .

Ndio maana tunaukataa mfumo dume kwa kuwapa mabinti zetu elimu na kuwafanya wajiamini na kujipambania kama tufanyavyo wanaume .


Humu watu wanataka mfumo dume kimaneno ila kimatendo wanapambana binti zao waende shule za maana wajitambue, na kuwa na maarifa ya kujipambania.
Oohh kwa michango yako huwa nadhani na wewe ni muumini wa mfumo dume mkuu, kiukweli wanaume wengi ni wanafiki sana wanataka mfumo dume kwa wake zao ila kwa mabinti zao hawautaki, ukiwauliza vipi unataka binti yako naye amtendee mumewe kama vile unavyotaka mkeo akutendee wewe hawana majibu
 
vipi mfumo dume unatambulika kisheria? hapa na maan ya kwamba ikitokea tumeachana, mali tulizochuma wote tunagawana, ila mali zangu alizo nikuta nazo au zake nilizomkuta nazo hatugawani.
Sasa kitendo cha kuchuma wote mali maana yake amekusaidia majukumu yako, mfumo dume unataka mume umhudumie mkeo kwa mali ulizochuma mwenyewe, bila kutegemea akusaidie majukumu yako
 
Oohh kwa michango yako huwa nadhani na wewe ni muumini wa mfumo dume mkuu, kiukweli wanaume wengi ni wanafiki sana wanataka mfumo dume kwa wake zao ila kwa mabinti zao hawautaki, ukiwauliza vipi unataka binti yako naye amtendee mumewe kama vile unavyotaka mkeo akutendee wewe hawana majibu
Huo mfumo umepitwa na wakati ukiiendekeza kila siku utakua na makasiriko ,mwisho wa siku unakufa bila furaha, watu huwa wanabadilika.
 
Sawa hatujakataa hilo lakini huo utawala unakuja pamoja na majukumu juu ya hao wanawake, uzi wangu unasema kama unataka kumtawala mwanamke basi ni lazima umhudumie bila kutaka naye akufanyie hivyo, mkishaanza kutaka kusaidiwa majukumu yenu na wanawake hapo ndipo mfumo dume unapokosa maana na kuanza kupingwa
Kiongozi hata mimi pia sikubaliani na mfumo dume. Palipo na mfumo dume hakuna UPENDO. Na sisi wanaume tumeelekezwa kumpenda mwanamke. Kupenda ndani yake kuna kujali, kumlinda, kumuelekeza kwa staha, kumtekelezea mahitaji yake na vyote vinavyoendana na upendo. Mwanamke ameelezwa amtii mwanaume.

Naongezea hapo kama mwanaume ambaye hana upendo kwa mwanamke haina haja ya kumtii na
hili pia lipo automatic mtu ambaye hana upendo kwako huwezi kumtii kwa hiyari labda kwa kuogopa. Mwanaume asiye na upendo kwa mwanamke huyo ni sawa na muuaji.

Tunapo tekekeleza maagizo ya Mungu katika kuishi mwanaume na mwanamke inakuwa ni mzunguko (circle) mwanaume ampende mwanamke, mwanamke amtii mwanaume, watoto wawaheshimu wazazi na watu wote wapendane. Hakika kama tungefuata haya wote kwa pamoja usingesikia jambo baya katika jamii zetu. Hiyo kwa ufupi formula tuliyowekewa na Mungu, ni rahisi sana kuifuata kama binadamu akiamua.

Kuhusu 50/50 sikubaliani nayo kwa sababu ina muumiza mwanamke mwenyewe na kuharibu mfumo mzima tuliowekewa na Mungu. Niweke wazi hapa katika 50/50 simaanishi fursa ya jambo fulani kati ya mwanamke na mwanaume kama vile elimu, kazi, afya, umiliki wa mali, biashara, n.k. Mwanamke na mwanaume wote wanahitaji fursa sawa kama nilizo eleza hapo juu.

Ila sikubaliani na MFUMO DUME (Kumyanyasa mwanamke) ❌ na pia sikubaliani na kuweka mazingira ya kumfanya mwanamke awe kiburi na jeuri cross ❌, haya yanasababisha kutengeneza watoto wasio na heshima, adabu na baadaye kuja kuwa wezi, mafisadi, n.k.

50/50 inayoongelewa na wengi ni kumfanya mwanamke awe juu ya mwanaume hususa katika familia (yaani kuwa kichwa cha familia huku mwanaume akiwepo) jambo ambalo ni kosa ❌.
 
Mkuu hakuna jipya chini ya jua maovu yote yalianza tangu kipindi cha agano la kale, kipindi ambacho mfumo dume ulikuwa umeshika hatamu na feminism ilikuwa haina hata dalili, au wewe unaweza ukaniambia ni maovu gani ambayo hayakuwepo enzi hizo na je mfumo dume umefanya nini kuzuia maovu yaliyokuwepo
Mfumo dume ni jambo ovu pia.
 
Mkuu unaposema "mali mbona ni za mwanaume ila mkiachana zinakatwa 50/50" unamaanisha nini, je wakati wa ndoa yenu ulikuwa unamsaidia kufanya majukumu ya nyumbani ikiwemo kulea watoto tangu wakiwa wachanga, na je alikuwa hakupi ile heshima na utii kama mwanaume au hayo hayawi considered
Nina majibu manne kwenye hii paragraph yako.

1.

Majukumu ya nyumbani hayana uhusiano wowote kwenye kufanikisha maendeleo.

Na ndio maana hata tunapo waoa mnatukuta tayari tupo kwenye progress tushafanya achievements kadhaa na hivyo tunaamua kuoa kwa lengo moja tu la kupata familia.

Kwa maana hiyo tunaona jinsi mwanaume alivyoweza kufanya maendeleo hayo pasipo kuwa na mwanamke huyo wa kumsaidia kazi za nyumbani.

Hiyo inatupa tafsiri kwamba uwepo wa mke kufanya kazi za nyumbani haina mchango wowote kwa mume kuweza kufanya maendeleo ambayo baadaye huyo mwanamke naye ahesabike kuwa ni sehemu ya maendeleo.

Hata nyinyi mara nyingi tunawaona vipaumbele vyenu katika kuolewa huwa mnataka muolewe na mtu ambaye tayari amejipata eidha ana pesa au kazi ya uhakika.
 
Mkuu unaposema "mali mbona ni za mwanaume ila mkiachana zinakatwa 50/50" unamaanisha nini, je wakati wa ndoa yenu ulikuwa unamsaidia kufanya majukumu ya nyumbani ikiwemo kulea watoto tangu wakiwa wachanga, na je alikuwa hakupi ile heshima na utii kama mwanaume au hayo hayawi considered
Lakini hoja nyingine

2.
Kama kazi za nyumbani ndio kiwe kigezo cha kutaka ulipwe, vipi kama tukisema malipo yako yalifanyika kupitia mali?

Vipi nikisema ile mali ndio thamani yako wewe ambayo wazazi wako walikuthaminisha, na mimi baada ya kutoa hiyo mali ni lazima ufanye majukumu ya nyumbani ili kuifidia ile mali?
 
Mkuu unaposema "mali mbona ni za mwanaume ila mkiachana zinakatwa 50/50" unamaanisha nini, je wakati wa ndoa yenu ulikuwa unamsaidia kufanya majukumu ya nyumbani ikiwemo kulea watoto tangu wakiwa wachanga, na je alikuwa hakupi ile heshima na utii kama mwanaume au hayo hayawi considered
Lakini

3.

Vipi kama nilikuwa mtu wa huruma nisiyependa kukuona ukihangaika na hivyo kuamua kutafuta mfanyakazi wa kukusaidia?

Bado utaendelea kudai 50/50 ya mali kwenye kazi ambazo hufanyi wewe??
 
Mkuu unaposema "mali mbona ni za mwanaume ila mkiachana zinakatwa 50/50" unamaanisha nini, je wakati wa ndoa yenu ulikuwa unamsaidia kufanya majukumu ya nyumbani ikiwemo kulea watoto tangu wakiwa wachanga, na je alikuwa hakupi ile heshima na utii kama mwanaume au hayo hayawi considered
4.

Wapo wanawake wenye pesa na kazi zao nzuri waliolewa na wanaume choka mbaya.

Wanaume hao hawana kazi, mke ndio anaye hudumia familia kwa kila kitu.

Huyo mume anaweza akawa anafanya vikazi vidogovidogo pale nyumbani kipindi mke yupo kazini.

Kwa hiyo unavyoona wewe huyo jamaa siku wakiachana na mke wake, anayo hiyo haki ya kudai 50/50 kwa kigezo cha kazi za nyumbani kipindi wife yupo job?
 
Na hata hivyo mbona wapo wanawake wengi tu wanaopambana na wanaume katika mazingira tofauti tofauti na wanashinda, nilichogundua wanawake wengi bado wanasita kuitumia hiyo 50/50 kwa asilimia mia kwa sababu wanaume wengi bado mnataka mfumo dume, siku mkiachana kabisa na mfumo dume basi hata wanawake nao watakubali kufanya hayo mnayotaka wafanye bila hiyana
Sasa kama hilo lipo kwanini ukatae kutangulia mbele kwenda kupambana na jambazi kwa kigezo cha maumbile??

Ni kweli wanawake wanasita sita sana na hiyo kwasababu ya sisi kuwadekeza.

Kumbe udhaifu wa wanawake upo kwenye hesitation.

Hata kwenye mgawanyo wa mali tunapaswa kufanya kila linalowezekana msipate chochote ili tuwape ujasiri wa kutafuta vya kwenu.
 
Na ukizingatia siku hizi wanawake wengi tu wanafanya kazi ngumu mnazoziita za kiume kuna hadi makomandoo wanawake kwenye majeshi ya nchi mbalimbali, ila ninyi hadi leo bado mnakomaa kwamba majukumu ya nyumbani ni ya mwanamke na kwamba bado mwanaume anatakiwa amtawale mwanamke, sasa kwa mitazamo hiyo wanawake wanaona kama mnataka kuwatapeli yani eti wakubali majukumu sawa ndio muwape haki sawa
Kwanza nataka nijue, nawewe ni mmoja wapo wa hao wanaofanya kazi ngumu??

Halafu kuhusu makomandoo wa kike kuna kitu hukijui.

Hao makomandoo wa kike unafikiri wana hitimu kozi yenye mafunzo sawa na makomandoo wa kiume?

Unafikiri komandoo wa kike ni sawa na komandoo wa kiume?

Hao ni makomandoo wa kike dhidi ya wanawake wenzao ambao walishindwa kufuzu hayo mafunzo.

Unafikiri kwanini kwenye parade za majeshi yote huwaoni makomandoo wakike wakivunja mawe kwa kichwa??
 
Lakini kumbe shida yenu mnataka wafanye majukumu mengi zaidi huku hiyo haki sawa yenyewe mnasuasua kuwapa na mnaitafutia visingizio vingi, na kama nilivyosema hii haki sawa kwa asilimia kubwa ililenga zile day to day activities sasa mambo ya kupigana vita na kupambana na majambazi siyo day to day activities kwenye individual life, kuna wanaume wengi tangu wanazaliwa hadi wanakufa wazee hawajawahi kupigana vita au kupambana na majambazi kabisa
Inawezekana ukawa na majukumu mengi kakini yasiwe magumu.

Na mwingine akawa na jukumu moja likawa gumu kuliko hata yule mwenye majukumu mengi.

Mfano wewe upo nyumbani majukumu yako ya kila siku ni usafi wa ndani, kupika, kuosha vyombo, na baadaye kumuandalia mumeo maji ya kuoga.

Ukimaliza hapo kinachofuata ni kuangalia Sinema zetu na kuchati tu kwenye simu.

Hii haiwezi kufanana hata na mtu anayefanya kazi ya zege.

Ni kweli kupigana na jambazi haiwezi kuwa ni jambo la kila siku lakini lilipaswa kuwa katika sehemu ya sera zenu kwenye kunadi 50/50

Hiyo ni kuonesha kuwa 50/50 sio mkakati wa kimaslahi unaodiki kwenye vitu simple bali ni fairness katika kila aspects
 
Ndio, kuna msemo unasema "with great authority comes great responsibility" yani kila mamlaka makubwa huambatana na majukumu makubwa, lakini jambo la kushangaza ni kwamba wanaume wengi hasa wa kiafrika wanayataka hayo mamlaka tu ila majukumu hawayataki

Mimi naona ifike pahala dunia iachane rasmi na mfumo dume na haki sawa ishike hatamu, kwa sababu wanaume hawataki tena majukumu hivyo hata hayo mamlaka hayawafai, wanaume wengi hawataki haki sawa ila wanataka majukumu sawa tena ikibidi mwanamke ndio afanye zaidi ya mwanaume

MImi naona kusiwe tena na mgawanyo wa majukumu yani hata kazi za nyumbani zifanywe na wote kama ambavyo kutafuta pesa limekuwa ni jukumu la wote, majukumu ya mwanamke yabaki yale ya asili na ya kimaumbile tu ambayo ni kubeba ujauzito, kuzaa na kunyonyesha, hayo tu ndio ambayo mwanaume hawezi kuyafanya ila majukumu mengine yote ya nyumbani kama kupika, kuosha vyombo, kufua, kusafisha nyumba, kulea watoto tangu wakiwa wachanga mfano kuwasafisha, kuwauguza wakiumwa, nk yafanywe na wote kwa usawa kabisa

Na vile vile kwa mfano mume akiweka laki mezani na mke naye aweke laki mezani mahitaji yote ya nyumbani wanunue kwa usawa bills zote walipe kwa usawa, na watoto wao wawahudumie kwa usawa ikiwemo kuwalipia ada na mahitaji yao mengine yote kwa usawa, hiyo ndio maana halisi ya 50 50 siyo mmoja anamtegea mwenzie eti mtu anataka pesa mtafute wote na bills mlipe wote, ila kazi za nyumbani na kulea watoto afanye mmoja na bado huyo mmoja amtii mwenzie na amlee kama anavyowalea watoto wake, what kind of cockamamie logic is this

Na jambo jingine naona pia tuachane na suala la mwanaume kumtawala mwanamke kila mtu ajitawale mwenyewe kusiwe na habari za kichwa cha familia, yani hakuna tena kusema kwamba mwanamke anatakiwa amtii mumewe kila mtu awe na maamuzi juu ya maisha yake mwenyewe, kusiwe na wa kumuongoza mwenzake na pia kusiwe na habari za kuoa wala kuolewa tena bali iwe ni kuoana

Mnawalaumu wanawake kuwa wanadai haki sawa halafu hawataki majukumu lakini mnasahau kwamba sababu ya wao kukataa hayo majukumu ni kwa sababu mnataka wafanye yale ya kwenu tu, ila ya kwao bado mmewaachia wenyewe hamtaki kuyafanya yani huwezi kumuambia mwanamke ajitafutie pesa zake na akusaidie majukumu, halafu hapo hapo bado unataka huyo mwanamke akufanyie majukumu ya nyumbani na bado akupe heshima na utii

Kwanza hapo huyo mke anakuwa siyo msaidizi tena bali ni kama business partner tu hivyo ondoa kichwani suala la kumlazimisha akutii, hivi mnadhani mwanamke aliambiwa amtii mwanaume kwa misingi gani kama siyo kuhudumiwa maana huwezi kukitawala kiumbe usichokihudumia, hakuna binadamu mwenye akili timamu anayefurahia kutawaliwa na binadamu mwenzie asiyewajibika kwa lolote juu yake na kiuhalisia ukitoa huduma zinazohusisha pesa hakuna wajibu mwingine mwanaume alionao juu ya mwanamke

Kama ikiwa mtoto anamtii mzazi wake kwa sababu amemzaa na amemlea, watu wa dini wanaitii miungu yao kwa sababu wanaamini imewaumba na inawapa uhai, je mwanamke anapaswa amtii mumewe kwa sababu gani, tena hata mtoto mwenyewe akishatoka kwao akaanza kujitegemea kinachobaki kwa mzazi wake ni ile heshima tu kuwa amemzaa, lakini huyo mzazi anakuwa hana mamlaka tena ya kumpangia mtoto maisha yake mfano afanye kazi gani au arudi nyumbani muda gani kwa sababu hamhudumii tena

Sasa inashangaza pale mwanaume anapotaka mkewe atafute pesa wasaidiane maisha kwa kisingizio kwamba mke naye ana mikono miwili na miguu miwili, ila huyo huyo mwanaume haoni ajabu kumtawala huyo mke mwenye mikono miwili na miguu miwili kama yeye, yani imefikia hatua wanaume wanaona uchungu kugawana mali na wake zao na wengine ndio kabisa hawataki kuoa kwa kisingizio kwamba eti wakishafanikiwa wake zao watadai talaka ili wagawane mali

Yani hawaconsider tena yale majukumu yote ambayo wake zao wanawafanyia pamoja na utii ambao wake zao wanawapa, siku hizi wanadai kwamba kila mtu ajitafutie pesa zake na ikitokea wameachana kila mtu aondoke na chake, lakini cha kushangaza kwenye majukumu mengine hawasemi kila mtu afanye kwa usawa na kwenye suala la mamlaka hawasemi kila mtu ajitawale mwenyewe

Wale waumini wa ukristo hasa wanaume kama mmeamua kufuata maandiko basi fuateni yote, na kama mmeamua kuyapuuzia basi yapuuzieni yote msichague yale yanayowanufaisha ninyi tu halafu mengine mnajifanya hamyaoni, kwa sababu maandiko yanasema mume ndio atakula kwa jasho na si mke, halafu mbele ndio yanaendelea kwamba mwanaume atamtawala mwanamke, yule mke mnayemuota wa Mithali 31 yalikuwa mawazo binafsi ya mfalme Suleiman na si maagizo ya muumba

Hivo basi ifike pahala wanaume mchague moja kati ya mwanamke mfanyakazi/mfanyabiashara au mama wa nyumbani, na aina yoyote utakayochagua hapo lazima ukubaliane na sifa zinazoambatana na aina hiyo ya mwanamke siyo unachagua mfanyakazi/mfanyabiashara mnasaidiana majukumu, halafu hapo hapo unataka awe kama mama wa nyumbani au unachagua mama wa nyumbani halafu hutaki kumhudumia unaanza kumuona golikipa
Na mahali tulipe wote.
 
Ndio, kuna msemo unasema "with great authority comes great responsibility" yani kila mamlaka makubwa huambatana na majukumu makubwa, lakini jambo la kushangaza ni kwamba wanaume wengi hasa wa kiafrika wanayataka hayo mamlaka tu ila majukumu hawayataki

Mimi naona ifike pahala dunia iachane rasmi na mfumo dume na haki sawa ishike hatamu, kwa sababu wanaume hawataki tena majukumu hivyo hata hayo mamlaka hayawafai, wanaume wengi hawataki haki sawa ila wanataka majukumu sawa tena ikibidi mwanamke ndio afanye zaidi ya mwanaume

MImi naona kusiwe tena na mgawanyo wa majukumu yani hata kazi za nyumbani zifanywe na wote kama ambavyo kutafuta pesa limekuwa ni jukumu la wote, majukumu ya mwanamke yabaki yale ya asili na ya kimaumbile tu ambayo ni kubeba ujauzito, kuzaa na kunyonyesha, hayo tu ndio ambayo mwanaume hawezi kuyafanya ila majukumu mengine yote ya nyumbani kama kupika, kuosha vyombo, kufua, kusafisha nyumba, kulea watoto tangu wakiwa wachanga mfano kuwasafisha, kuwauguza wakiumwa, nk yafanywe na wote kwa usawa kabisa

Na vile vile kwa mfano mume akiweka laki mezani na mke naye aweke laki mezani mahitaji yote ya nyumbani wanunue kwa usawa bills zote walipe kwa usawa, na watoto wao wawahudumie kwa usawa ikiwemo kuwalipia ada na mahitaji yao mengine yote kwa usawa, hiyo ndio maana halisi ya 50 50 siyo mmoja anamtegea mwenzie eti mtu anataka pesa mtafute wote na bills mlipe wote, ila kazi za nyumbani na kulea watoto afanye mmoja na bado huyo mmoja amtii mwenzie na amlee kama anavyowalea watoto wake, what kind of cockamamie logic is this

Na jambo jingine naona pia tuachane na suala la mwanaume kumtawala mwanamke kila mtu ajitawale mwenyewe kusiwe na habari za kichwa cha familia, yani hakuna tena kusema kwamba mwanamke anatakiwa amtii mumewe kila mtu awe na maamuzi juu ya maisha yake mwenyewe, kusiwe na wa kumuongoza mwenzake na pia kusiwe na habari za kuoa wala kuolewa tena bali iwe ni kuoana

Mnawalaumu wanawake kuwa wanadai haki sawa halafu hawataki majukumu lakini mnasahau kwamba sababu ya wao kukataa hayo majukumu ni kwa sababu mnataka wafanye yale ya kwenu tu, ila ya kwao bado mmewaachia wenyewe hamtaki kuyafanya yani huwezi kumuambia mwanamke ajitafutie pesa zake na akusaidie majukumu, halafu hapo hapo bado unataka huyo mwanamke akufanyie majukumu ya nyumbani na bado akupe heshima na utii

Kwanza hapo huyo mke anakuwa siyo msaidizi tena bali ni kama business partner tu hivyo ondoa kichwani suala la kumlazimisha akutii, hivi mnadhani mwanamke aliambiwa amtii mwanaume kwa misingi gani kama siyo kuhudumiwa maana huwezi kukitawala kiumbe usichokihudumia, hakuna binadamu mwenye akili timamu anayefurahia kutawaliwa na binadamu mwenzie asiyewajibika kwa lolote juu yake na kiuhalisia ukitoa huduma zinazohusisha pesa hakuna wajibu mwingine mwanaume alionao juu ya mwanamke

Kama ikiwa mtoto anamtii mzazi wake kwa sababu amemzaa na amemlea, watu wa dini wanaitii miungu yao kwa sababu wanaamini imewaumba na inawapa uhai, je mwanamke anapaswa amtii mumewe kwa sababu gani, tena hata mtoto mwenyewe akishatoka kwao akaanza kujitegemea kinachobaki kwa mzazi wake ni ile heshima tu kuwa amemzaa, lakini huyo mzazi anakuwa hana mamlaka tena ya kumpangia mtoto maisha yake mfano afanye kazi gani au arudi nyumbani muda gani kwa sababu hamhudumii tena

Sasa inashangaza pale mwanaume anapotaka mkewe atafute pesa wasaidiane maisha kwa kisingizio kwamba mke naye ana mikono miwili na miguu miwili, ila huyo huyo mwanaume haoni ajabu kumtawala huyo mke mwenye mikono miwili na miguu miwili kama yeye, yani imefikia hatua wanaume wanaona uchungu kugawana mali na wake zao na wengine ndio kabisa hawataki kuoa kwa kisingizio kwamba eti wakishafanikiwa wake zao watadai talaka ili wagawane mali

Yani hawaconsider tena yale majukumu yote ambayo wake zao wanawafanyia pamoja na utii ambao wake zao wanawapa, siku hizi wanadai kwamba kila mtu ajitafutie pesa zake na ikitokea wameachana kila mtu aondoke na chake, lakini cha kushangaza kwenye majukumu mengine hawasemi kila mtu afanye kwa usawa na kwenye suala la mamlaka hawasemi kila mtu ajitawale mwenyewe

Wale waumini wa ukristo hasa wanaume kama mmeamua kufuata maandiko basi fuateni yote, na kama mmeamua kuyapuuzia basi yapuuzieni yote msichague yale yanayowanufaisha ninyi tu halafu mengine mnajifanya hamyaoni, kwa sababu maandiko yanasema mume ndio atakula kwa jasho na si mke, halafu mbele ndio yanaendelea kwamba mwanaume atamtawala mwanamke, yule mke mnayemuota wa Mithali 31 yalikuwa mawazo binafsi ya mfalme Suleiman na si maagizo ya muumba

Hivo basi ifike pahala wanaume mchague moja kati ya mwanamke mfanyakazi/mfanyabiashara au mama wa nyumbani, na aina yoyote utakayochagua hapo lazima ukubaliane na sifa zinazoambatana na aina hiyo ya mwanamke siyo unachagua mfanyakazi/mfanyabiashara mnasaidiana majukumu, halafu hapo hapo unataka awe kama mama wa nyumbani au unachagua mama wa nyumbani halafu hutaki kumhudumia unaanza kumuona golikipa
Hii 50/50, imekuwa strategy ya muda mrefu ya mabeberu kusambaza ushoga duniani.
Je, waweza furahi kuona kijana wako wa kiume akijihuaisha na ushoga?
Faida kuu ya mfumo dume ni kuandaa vijana madume kweli kweli.
Siyo kijana wa kiume ajionaye kuwa sawa na Binti Kwa namna yoyote.
 
Hii 50/50, imekuwa strategy ya muda mrefu ya mabeberu kusambaza ushoga duniani.
Je, waweza furahi kuona kijana wako wa kiume akijihuaisha na ushoga?
Faida kuu ya mfumo dume ni kuandaa vijana madume kweli kweli.
Siyo kijana wa kiume ajionaye kuwa sawa na Binti Kwa namna yoyote.
Ni kweli wamekuwa wakitumia 50/50 kama gia ya wema lakini imekuja kubadilika baada ya kuingiza masuala yasiyofaa katika jamii.

50/50 naikubali katika fursa kama vile mwanaume na mwanamke wote wanaweza kusoma, kupata kazi, kumiliki ardhi, biashara, n.k.

Lakini napo pia kama ni kazi lazima kuangalia uwezo maana kuna kazi ukimpa mwanamke ni kama unamnyanyasa alkadhalika na upande wa pili pia. Mfano kama kazi zinazohitaji nguvu zaidi au mazingira magumu, hizo zinawafaa wanaume zaidi kutokana na asili ya miili ilivyoumbwa.

Tunapokuja katika familia au ndoa mwanaume na mwanamke kila mmoja amepewa majukumu ambayo yanafaa kulingana na uumbaji wa Mungu ulinyofanyika na ametoa maelekezo namna tunavyopaswa kuishi.
 
vipi mfumo dume unatambulika kisheria? hapa na maan ya kwamba ikitokea tumeachana, mali tulizochuma wote tunagawana, ila mali zangu alizo nikuta nazo au zake nilizomkuta nazo hatugawani.
Mkuu sijui kama umeelewa hoja yangu, mfumo dume hauangalii mali mmechuma wote au la mfumo dume unataka umhudumie mkeo, and yes mkiachana mnagawana mali bila kujali mmechuma wote au umechuma peke yako
 
Back
Top Bottom