Mimi naona dunia iachane na mfumo dume na rasmi 50/50 ishike hatamu

Mimi naona dunia iachane na mfumo dume na rasmi 50/50 ishike hatamu

Kiongozi hata mimi pia sikubaliani na mfumo dume. Palipo na mfumo dume hakuna UPENDO. Na sisi wanaume tumeelekezwa kumpenda mwanamke. Kupenda ndani yake kuna kujali, kumlinda, kumuelekeza kwa staha, kumtekelezea mahitaji yake na vyote vinavyoendana na upendo. Mwanamke ameelezwa amtii mwanaume.

Naongezea hapo kama mwanaume ambaye hana upendo kwa mwanamke haina haja ya kumtii na
hili pia lipo automatic mtu ambaye hana upendo kwako huwezi kumtii kwa hiyari labda kwa kuogopa. Mwanaume asiye na upendo kwa mwanamke huyo ni sawa na muuaji.

Tunapo tekekeleza maagizo ya Mungu katika kuishi mwanaume na mwanamke inakuwa ni mzunguko (circle) mwanaume ampende mwanamke, mwanamke amtii mwanaume, watoto wawaheshimu wazazi na watu wote wapendane. Hakika kama tungefuata haya wote kwa pamoja usingesikia jambo baya katika jamii zetu. Hiyo kwa ufupi formula tuliyowekewa na Mungu, ni rahisi sana kuifuata kama binadamu akiamua.

Kuhusu 50/50 sikubaliani nayo kwa sababu ina muumiza mwanamke mwenyewe na kuharibu mfumo mzima tuliowekewa na Mungu. Niweke wazi hapa katika 50/50 simaanishi fursa ya jambo fulani kati ya mwanamke na mwanaume kama vile elimu, kazi, afya, umiliki wa mali, biashara, n.k. Mwanamke na mwanaume wote wanahitaji fursa sawa kama nilizo eleza hapo juu.

Ila sikubaliani na MFUMO DUME (Kumyanyasa mwanamke) [emoji777] na pia sikubaliani na kuweka mazingira ya kumfanya mwanamke awe kiburi na jeuri cross [emoji777], haya yanasababisha kutengeneza watoto wasio na heshima, adabu na baadaye kuja kuwa wezi, mafisadi, n.k.

50/50 inayoongelewa na wengi ni kumfanya mwanamke awe juu ya mwanaume hususa katika familia (yaani kuwa kichwa cha familia huku mwanaume akiwepo) jambo ambalo ni kosa [emoji777].
Nafikiri watu wengi wanapotosha hiyo maana ya 50/50 ndio maana kunakuwa na huu mkanganyiko wote, 50/50 haina maana kwamba mwanamke amtawale mwanaume, bali maana yake ni kila mtu ajitawale mwenyewe kusiwe na wa kumtawala mwenzake yani
 
Nina majibu manne kwenye hii paragraph yako.

1.

Majukumu ya nyumbani hayana uhusiano wowote kwenye kufanikisha maendeleo.

Na ndio maana hata tunapo waoa mnatukuta tayari tupo kwenye progress tushafanya achievements kadhaa na hivyo tunaamua kuoa kwa lengo moja tu la kupata familia.

Kwa maana hiyo tunaona jinsi mwanaume alivyoweza kufanya maendeleo hayo pasipo kuwa na mwanamke huyo wa kumsaidia kazi za nyumbani.

Hiyo inatupa tafsiri kwamba uwepo wa mke kufanya kazi za nyumbani haina mchango wowote kwa mume kuweza kufanya maendeleo ambayo baadaye huyo mwanamke naye ahesabike kuwa ni sehemu ya maendeleo.

Hata nyinyi mara nyingi tunawaona vipaumbele vyenu katika kuolewa huwa mnataka muolewe na mtu ambaye tayari amejipata eidha ana pesa au kazi ya uhakika.

Sasa kama majukumu ya nyumbani hayana mchango wowote katika maendeleo yenu kwanini wanaume wengi huwa wanaoa ili wafanyiwe hayo majukumu, yani kuna wanaume wake zao wasipofanya hayo majukumu huwa wanachukia seriously kabisa na wanaweza hata kuwarudisha makwao, utasikia mtu anasema kabisa "acha nioe nimechoka kupika, kuosha vyombo, kufua, kusafisha nyumba nk, na vipi kuhusu suala la kulea watoto nalo mbona hujaliongelea ilihali mgawanyo wa mali kwa asilimia kubwa huzingatia kwamba mwanamke ndiye mlezi wa watoto tangu wakiwa wadogo

Lakini hoja nyingine

2.
Kama kazi za nyumbani ndio kiwe kigezo cha kutaka ulipwe, vipi kama tukisema malipo yako yalifanyika kupitia mali?

Vipi nikisema ile mali ndio thamani yako wewe ambayo wazazi wako walikuthaminisha, na mimi baada ya kutoa hiyo mali ni lazima ufanye majukumu ya nyumbani ili kuifidia ile mali?

Kama ulimaanisha mahari basi kaa ukijua mahari haihusiani kabisa na majukumu anayoenda kufanya mwanamke kwenye ndoa labda nikurekebishe hapo mahari ni kama shukurani na fidia kwa wazazi wa mke, kwa sababu mwanamke anapoolewa familia yake inahesabika imelose while ya mwanaume imegain kwa maana kwamba mke ataenda kuendeleza ukoo wa mume na watoto watatumia majina ya ukoo wa mume, na ndio maana kwenye jamii nyingi wanaopokea hiyo mahari ni wazazi na ndugu wa mwanamke na si mwanamke mwenyewe kwa sababu ni familia yake ndio inahesabika imepoteza hapo

Lakini

3.

Vipi kama nilikuwa mtu wa huruma nisiyependa kukuona ukihangaika na hivyo kuamua kutafuta mfanyakazi wa kukusaidia?

Bado utaendelea kudai 50/50 ya mali kwenye kazi ambazo hufanyi wewe??

Ni wanaume wangapi wanaoweka wafanyakazi bila kutaka wake zao nao wafanye hizo kazi, ningekuelewa kama ungesema ukiweka huyo mfanyakazi basi yeye ndio anatakiwa afanye kazi zote na siyo tena uanze kumuuliza mkeo kwanini hamsaidii mfanyakazi, lakini wanaume wengi wakiona hivyo wanaanza tena malalamiko kwamba mke kajisahau kamuachia kila kitu mfanyakazi na matokeo yake wanaanza kutembea na hao wadada wa kazi kwa hiko kisingizio

4.

Wapo wanawake wenye pesa na kazi zao nzuri waliolewa na wanaume choka mbaya.

Wanaume hao hawana kazi, mke ndio anaye hudumia familia kwa kila kitu.

Huyo mume anaweza akawa anafanya vikazi vidogovidogo pale nyumbani kipindi mke yupo kazini.

Kwa hiyo unavyoona wewe huyo jamaa siku wakiachana na mke wake, anayo hiyo haki ya kudai 50/50 kwa kigezo cha kazi za nyumbani kipindi wife yupo job?

Yeah 100% katika scenario kama hiyo basi mwanaume ana haki zote za kudai 50/50 katika mali zote za mke wake

Sasa kama hilo lipo kwanini ukatae kutangulia mbele kwenda kupambana na jambazi kwa kigezo cha maumbile??

Ni kweli wanawake wanasita sita sana na hiyo kwasababu ya sisi kuwadekeza.

Kumbe udhaifu wa wanawake upo kwenye hesitation.

Hata kwenye mgawanyo wa mali tunapaswa kufanya kila linalowezekana msipate chochote ili tuwape ujasiri wa kutafuta vya kwenu.

Hapana wanawake wanasitasita kwa sababu mnataka kwenye hiyo 50/50 wakubali majukumu tu ila haki wasipewe au wapewe kidogo, mwanamke kutafuta pesa na mali zake siyo shida shida ni pale ambapo mwanaume bado anataka heshima na utii na kutimiziwa majukumu ya nyumbani kutoka kwa huyo huyo mwanamke anayejitafutia vya kwake, na huo ndio utapeli wenyewe ninaousema

Kwanza nataka nijue, nawewe ni mmoja wapo wa hao wanaofanya kazi ngumu??

Halafu kuhusu makomandoo wa kike kuna kitu hukijui.

Hao makomandoo wa kike unafikiri wana hitimu kozi yenye mafunzo sawa na makomandoo wa kiume?

Unafikiri komandoo wa kike ni sawa na komandoo wa kiume?

Hao ni makomandoo wa kike dhidi ya wanawake wenzao ambao walishindwa kufuzu hayo mafunzo.

Unafikiri kwanini kwenye parade za majeshi yote huwaoni makomandoo wakike wakivunja mawe kwa kichwa??

Aliyekuambia kwamba course za ukomandoo zinatofautiana mafunzo baina ya wanaume na wanawake ni nani na ni jeshi gani linalofanya hivyo, suala la kuvunja mawe kwa kichwa hilo wanajua viongozi kwanini hawawapangi wanawake nao wafanye hilo zoezi lakini si kwamba duniani hakuna wanawake wanaoweza kuvunja mawe kwa kichwa, huko kwenye course za ukomando hata wanaume wapo wengi wanaoshindwa kufuzu sasa kwanini ionekane kama vile mwanamke kushindwa kufuzu ni kwa sababu ya jinsia yake tu na si kwa sababu nyinginezo ambazo zinafanya na baadhi ya wanaume nao wasifuzu

Inawezekana ukawa na majukumu mengi kakini yasiwe magumu.

Na mwingine akawa na jukumu moja likawa gumu kuliko hata yule mwenye majukumu mengi.

Mfano wewe upo nyumbani majukumu yako ya kila siku ni usafi wa ndani, kupika, kuosha vyombo, na baadaye kumuandalia mumeo maji ya kuoga.

Ukimaliza hapo kinachofuata ni kuangalia Sinema zetu na kuchati tu kwenye simu.

Hii haiwezi kufanana hata na mtu anayefanya kazi ya zege.

Ni kweli kupigana na jambazi haiwezi kuwa ni jambo la kila siku lakini lilipaswa kuwa katika sehemu ya sera zenu kwenye kunadi 50/50

Hiyo ni kuonesha kuwa 50/50 sio mkakati wa kimaslahi unaodiki kwenye vitu simple bali ni fairness katika kila aspects

Mkuu unatofautishaje na unatafsiri vipi jukumu gumu na jukumu rahisi kwa sababu mimi ninavyojua ugumu au urahisi wa jukumu unategemea na mtu binafsi maana naona umekomaa kuyaita hayo majukumu "vitu simple", hayo majukumu unayoona wewe marahisi kuna watu wanaona ni magumu na hawataki kuyafanya na unayoona wewe ni magumu kuna watu wanaona ni marahisi na wanapenda kuyafanya, hayo majukumu ya nyumbani unayoona rahisi wanaume wengi wanayaona magumu na wako radhi hata washinde shambani wanalima siku nzima kuliko kuyafanya hayo kwa mfano shughuli ya kulea mtoto mchanga kuna mwanaume atakayekubali kuifanya
 
Hii 50/50, imekuwa strategy ya muda mrefu ya mabeberu kusambaza ushoga duniani.
Je, waweza furahi kuona kijana wako wa kiume akijihuaisha na ushoga?
Faida kuu ya mfumo dume ni kuandaa vijana madume kweli kweli.
Siyo kijana wa kiume ajionaye kuwa sawa na Binti Kwa namna yoyote.
Ushoga ulikuwepo toka enzi za Sodoma na Gomora kipindi cha mfumo dume mkuu
 
Nafikiri watu wengi wanapotosha hiyo maana ya 50/50 ndio maana kunakuwa na huu mkanganyiko wote, 50/50 haina maana kwamba mwanamke amtawale mwanaume, bali maana yake ni kila mtu ajitawale mwenyewe kusiwe na wa kumtawala mwenzake yani
Ukifuata nadharia za nchi za magharibi wanataka kuwe na mambo ambayo ni kinyume na maelekezo ya Mungu kupitia 50/50. Inatakiwa kuwa makini sana. Kiuhalisia 50/50 imevuka mipaka na imetumika vibaya kupitisha mambo yasiyo ya kawaida ikiwemo ushoga.
 
Iko hivi mwanamke mwenye pesa kukuzidi au mkalingana huyo kidume mwenzio, hapo ndani kuna njemba mbili, hapakaliki tena.

Mwanamke hapaswi kukuzidi kipato.

Mwanamke hapaswi kukuzidi elimu.

Mwanamke hapaswi kukuzidi umri.

Mwanaume ameumbwa kutii na sio kuheshimu, kuheshimu tunaheshimu mzazi tu labda, ila siwezi heshimu mwanaume mwenzangu. Ndio jeshini ukiona mwanaume anapewa adhabu na anafanya huo ni utii si heshima.

Mwanamke kaumbwa kuheshimu na kutii, amheshimu mumewe na kumtii.

Kwenye ndoa mwanamke apendwe, mwanaume aheshimiwe, hio ni asili huwezi badilisha.

Unachozungumza ni kama kusema wanaume na wanawake wote tufanane maumbile, wote tuwe na misambwanda, wote tubebe mimba, wote tuvae shimizi..

Wanawake hamuwezi haki sawa, mtaongea tu, lakini majukumu usawa kwa usawa na mwanaume yupo hamuwezi, mtaanza kutegea tu.

Mfumo dume uendelee, tena sasa hivi msiajiriwe kabisa mkae nyumbani.
Hata akikuzidi kimo ,utajuta.
 
Sasa kama majukumu ya nyumbani hayana mchango wowote katika maendeleo yenu kwanini wanaume wengi huwa wanaoa ili wafanyiwe hayo majukumu, yani kuna wanaume wake zao wasipofanya hayo majukumu huwa wanachukia seriously kabisa na wanaweza hata kuwarudisha makwao, utasikia mtu anasema kabisa "acha nioe nimechoka kupika, kuosha vyombo, kufua, kusafisha nyumba nk, na vipi kuhusu suala la kulea watoto nalo mbona hujaliongelea ilihali mgawanyo wa mali kwa asilimia kubwa huzingatia kwamba mwanamke ndiye mlezi wa watoto tangu wakiwa wadogo
Wanaume hawaoi kwa ajili ya kufanyiwa hizo kazi.

Wanaoa kwasababu wanataka familia.

Na hizo kazi sio kitu cha kumsumbua mwanaume kwa miaka hii ambayo digital imetawala.

Kama kufua alikuwa anaweza kuwapa nguo madobi wamfulie akawalipa, akawa ameokoa gharama za sabuni na maji.

Angeweza kununua washing machine akawa anafua bila tabu yeyote.

Angeweza kununua hata dish washer akawa anaosha vyombo bila usumbufu wowote.

Angeshindwa kabisa angeweza kumuajiri dada wa kazi ambaye angekuwa anafanya hizo kazi tena kwa malipo nafuu kabisa.
 
Kama ulimaanisha mahari basi kaa ukijua mahari haihusiani kabisa na majukumu anayoenda kufanya mwanamke kwenye ndoa labda nikurekebishe hapo mahari ni kama shukurani na fidia kwa wazazi wa mke
Shukurani hiyo mbona wewe hujaitoa kwa wazazi wangu?

Kwamba wazazi wangu hawastahili shukurani au ni kudharau walicho kizaa kuwa hakistahili kupewa shukurani?
 
kwa sababu mwanamke anapoolewa familia yake inahesabika imelose while ya mwanaume imegain kwa maana kwamba mke ataenda kuendeleza ukoo wa mume na watoto watatumia majina ya ukoo wa mume, na ndio maana kwenye jamii nyingi wanaopokea hiyo mahari ni wazazi na ndugu wa mwanamke na si mwanamke mwenyewe kwa sababu ni familia yake ndio inahesabika imepoteza hapo
Sio kweli kuwa familia ya mwanamke inakuwa ime lose.

Mwanaume ndio anaye lose

Kwasababu mwanaume akioa anakuwa amebeba majukumu yanayohusu familia yake, majukumu ya wazazi wake hadi familia ya wazazi wa mke wake.

Kutumia jina la ukoo hakuna maana kumetokana na malipo ya mali.

Kutumia jina la mume la ukoo ni kutokana na kuweka usawa katika umiliki wa mtoto.

Mama ndio mtu pekee ambaye akizaa mtoto anakuwa wake kwa 100%. Lakini kwa mume hilo kuna walakini inawezekana akawa amesingiziwa

So ili ku balance ndio ikawekwa hiyo principle
 
Ni wanaume wangapi wanaoweka wafanyakazi bila kutaka wake zao nao wafanye hizo kazi, ningekuelewa kama ungesema ukiweka huyo mfanyakazi basi yeye ndio anatakiwa afanye kazi zote na siyo tena uanze kumuuliza mkeo kwanini hamsaidii mfanyakazi, lakini wanaume wengi wakiona hivyo wanaanza tena malalamiko kwamba mke kajisahau kamuachia kila kitu mfanyakazi na matokeo yake wanaanza kutembea na hao wadada wa kazi kwa hiko kisingizio
Kama kufua anafua msaidizi, kupika anapika yeye, usafi wote ni yeye.

Hiyo sehemu ambayo unataka huyo mfanyakazi afanye usafi unataka aingie chumbani kwako?

Yani malalamiko yako sio tena wingi wa kazi bali hutaki kazi yeyote bila kujali udogo wake?

Kazi ya kufagia chumbani kwako ndio hiyo ambayo inakufanya udai 50/50 mkiachana?
 
Hapana wanawake wanasitasita kwa sababu mnataka kwenye hiyo 50/50 wakubali majukumu tu ila haki wasipewe au wapewe kidogo, mwanamke kutafuta pesa na mali zake siyo shida shida ni pale ambapo mwanaume bado anataka heshima na utii na kutimiziwa majukumu ya nyumbani kutoka kwa huyo huyo mwanamke anayejitafutia vya kwake, na huo ndio utapeli wenyewe ninaousema
Na nyie kwenye sera ya 50/50 mbona focus yenu mmeiwekea mambo ya kimaslahi lakini hamjawahi kudai haki za kupambana na majambazi kama hizi??

Sisi tunawaona nyinyi kama wanyonyaji mnaotumia sera ya 50/50 kama fursa ya kutuibia mali zetu, kwasababu tunaona kwenye mambo magumu hiyo sera hamuiongei
 
Dunia inahitaji Equity sio Equality ,mkilitambua hili basi mtaondoa huu upumbavu wenu kichwani.

Yule superpower ,the father of democracy nchi yake na purukushani za kidunia hajawahi kumpa mwanamke aongoze.

Ni mjinga anaweza kukubali usawa wakati hata vikojoleo vipo tofauti
 
Aliyekuambia kwamba course za ukomandoo zinatofautiana mafunzo baina ya wanaume na wanawake ni nani na ni jeshi gani linalofanya hivyo, suala la kuvunja mawe kwa kichwa hilo wanajua viongozi kwanini hawawapangi wanawake nao wafanye hilo zoezi lakini si kwamba duniani hakuna wanawake wanaoweza kuvunja mawe kwa kichwa, huko kwenye course za ukomando hata wanaume wapo wengi wanaoshindwa kufuzu sasa kwanini ionekane kama vile mwanamke kushindwa kufuzu ni kwa sababu ya jinsia yake tu na si kwa sababu nyinginezo ambazo zinafanya na baadhi ya wanaume nao wasifuzu
Ukomandoo wa mwanamke hauwezi kuwa sawa na komandoo wa kiume.

Yapo mazoezi ambayo wanashare kama ABT ambayo yanatolewa kwenye level ya chini ya regular army.

Mwanaume aliyeshindwa kufuzu kwenye ukomandoo ni kutokana na intensity ya hayo mafunzo yalivyokuwa magumu.

Na mwanamke aliyefuzu mafunzo ya ukomandoo haina maana amefuzu hayo mafunzo ambayo huyo mwanaume amefeli.

Ni tofauti kabisa.
 
Mkuu unatofautishaje na unatafsiri vipi jukumu gumu na jukumu rahisi kwa sababu mimi ninavyojua ugumu au urahisi wa jukumu unategemea na mtu binafsi maana naona umekomaa kuyaita hayo majukumu "vitu simple", hayo majukumu unayoona wewe marahisi kuna watu wanaona ni magumu na hawataki kuyafanya na unayoona wewe ni magumu kuna watu wanaona ni marahisi na wanapenda kuyafanya, hayo majukumu ya nyumbani unayoona rahisi wanaume wengi wanayaona magumu na wako radhi hata washinde shambani wanalima siku nzima kuliko kuyafanya hayo kwa mfano shughuli ya kulea mtoto mchanga kuna mwanaume atakayekubali kuifanya
Tofautisha kuyaona magumu kwasababu ni magumu na kuyaona magumu kwasababu ni mvivu.
 
Ukifuata nadharia za nchi za magharibi wanataka kuwe na mambo ambayo ni kinyume na maelekezo ya Mungu kupitia 50/50. Inatakiwa kuwa makini sana. Kiuhalisia 50/50 imevuka mipaka na imetumika vibaya kupitisha mambo yasiyo ya kawaida ikiwemo ushoga.
Mkuu sijui kwanini unakazania hili suala la ushoga kama vile ni jambo geni duniani, ushoga ulikuwepo toka enzi za Sodoma na Gomora ambako kulikuwa na mfumo dume, maovu yote haya tunayoyaona yalikuwepo toka enzi za mfumo dume huo mfumo ulifanya nini kuzuia maovu hayo
 
Wanaume hawaoi kwa ajili ya kufanyiwa hizo kazi.

Wanaoa kwasababu wanataka familia.

Na hizo kazi sio kitu cha kumsumbua mwanaume kwa miaka hii ambayo digital imetawala.

Kama kufua alikuwa anaweza kuwapa nguo madobi wamfulie akawalipa, akawa ameokoa gharama za sabuni na maji.

Angeweza kununua washing machine akawa anafua bila tabu yeyote.

Angeweza kununua hata dish washer akawa anaosha vyombo bila usumbufu wowote.

Angeshindwa kabisa angeweza kumuajiri dada wa kazi ambaye angekuwa anafanya hizo kazi tena kwa malipo nafuu kabisa.

Wewe sasa naona unaleta nadharia kwenye uhalisia hawa wanaume tunaowaona kila siku wanasema wanaoa ili wake zao wawafanyie kazi za nyumbani ni wa wapi, hao wanaume unaosema wananunua hizo mashine za kusimplify kazi au wanawalipa watu wafanye hizo kazi ni wangapi kulinganisha na hawa ambao hadi leo wanaona hayo mambo ni anasa na wengine wanadai hawawezi kuafford, kuna mwanaume hadi leo anawaza kupelekewa maji ya kuoga bafuni na akiambiwa aweke bomba anakuambia sasa nimeoa mke wa kazi gani au labda nikuulize wewe unaweza kukubali kulipa watu wafanye hizo kazi ilihali una mke nyumbani

Shukurani hiyo mbona wewe hujaitoa kwa wazazi wangu?

Kwamba wazazi wangu hawastahili shukurani au ni kudharau walicho kizaa kuwa hakistahili kupewa shukurani?

Ndio maana ya mfumo dume, ukitaka mahari itolewe basi kubali 50/50, hiyo ni shukurani ya familia ya mke kumtoa mtoto wao kwa familia ya mume

Sio kweli kuwa familia ya mwanamke inakuwa ime lose.

Mwanaume ndio anaye lose

Kwasababu mwanaume akioa anakuwa amebeba majukumu yanayohusu familia yake, majukumu ya wazazi wake hadi familia ya wazazi wa mke wake.

Kutumia jina la ukoo hakuna maana kumetokana na malipo ya mali.

Kutumia jina la mume la ukoo ni kutokana na kuweka usawa katika umiliki wa mtoto.

Mama ndio mtu pekee ambaye akizaa mtoto anakuwa wake kwa 100%. Lakini kwa mume hilo kuna walakini inawezekana akawa amesingiziwa

So ili ku balance ndio ikawekwa hiyo principle

Hapana familia ya mke ndio inakuwa imelose kwa sababu kwa kawaida kwenye tamaduni nyingi, mwanamke akishaondoka kwao huwa hatakiwi kuwatembelea wazazi au ndugu zake mara kwa mara, lakini kwa mwanaume ni tofauti yeye wazazi na ndugu zake hata wakitaka kuja kuishi hapo kwake inaonekana sawa tu

Na mwanamke mara nyingi huwa anashiriki kwenye shughuli za upande wa mume kuliko anavyoshiriki kwenye shughuli za kwao, na wakati mwingine mume anaweza hata kumuambia mke akamuuguze mama yake mzazi akiumwa, hivyo ni haki kabisa familia ya mume kuhudumia familia ya mke yani hapo inakuwa ni kama exchange ya huduma

Kuhusu majina ya ukoo sidhani kama baba kutokuwa na uhakika na umiliki wa watoto inahusiana na watoto kutokutumia jina la ukoo la mke, kwa sababu kwa tamaduni za afrika mtoto kutumia jina la ukoo ni heshima kwa upande wa mwanaume kwamba watoto wanaendeleza jina linakuwa halifi hivyo kwa familia ya mke hiyo ni loss, na ndio maana kwenye makabila mengi wababa walikuwa wanachukia kuwa na watoto wa kike wengi kuliko wa kiume sababu kubwa ni hiyo

Kama kufua anafua msaidizi, kupika anapika yeye, usafi wote ni yeye.

Hiyo sehemu ambayo unataka huyo mfanyakazi afanye usafi unataka aingie chumbani kwako?

Yani malalamiko yako sio tena wingi wa kazi bali hutaki kazi yeyote bila kujali udogo wake?

Kazi ya kufagia chumbani kwako ndio hiyo ambayo inakufanya udai 50/50 mkiachana?

Sasa kama wewe na mke wako wote mnafanya kazi na wote mnawahi kuondoka na mnachelewa kurudi ni kipi kinachofanya mwanamke aweze kufanya usafi wa chumbani kwenu ambacho wewe kinakufanya ushindwe, na ndio maana nikasema mnaposema kazi ni rahisi mnatakiwa mjiulize kwanini ninyi mnashindwa kuzifanya na kutegemea mke ndio azifanye kila wakati, halafu siyo usafi wa chumbani tu wanaume wengi hata hizo kazi za kupika na kufua bado hawataki mahousegirl wafanye wanataka wake zao ndio wafanye wanadai hawawezi kula chakula cha housegirl wakati mke yupo

Kwenye theory ndio, ila uhalisia hilo jambo halipo kabisa

Halipo kwa sababu hata hao wanaume uliowatolea mfano kwamba wanafanya kazi za nyumbani kisa wake zao wanatafuta pesa hawapo, wanaume hawawezi kukubali kufanya kazi za nyumbani eti kisa tu wake zao wanatafuta pesa watawaambia watafute wadada wa kazi, na pia wanaume bado huwa wanataka kupewa heshima na utii hata katika scenario kama hiyo ambayo mke ndio anatafuta pesa na kuhudumia nyumba

Na nyie kwenye sera ya 50/50 mbona focus yenu mmeiwekea mambo ya kimaslahi lakini hamjawahi kudai haki za kupambana na majambazi kama hizi??

Sisi tunawaona nyinyi kama wanyonyaji mnaotumia sera ya 50/50 kama fursa ya kutuibia mali zetu, kwasababu tunaona kwenye mambo magumu hiyo sera hamuiongei

Ndio maana nikakuambia mnataka tuongelee kwenye mambo magumu ambayo they are not likely to happen in daily life hizo ni uncertainties tu, 50/50 siyo sera ya kuwaibia mali ndio maana nikasema mgawanyo wa mali mara nyingi huzingatia kwamba ni either mmechuma wote au mwanamke ndiye anayelea watoto, sidhani kama mwanamke anaweza akagawiwa mali za mwanaume nusu ikiwa siyo katika mazingira kama hayo

Ukomandoo wa mwanamke hauwezi kuwa sawa na komandoo wa kiume.

Yapo mazoezi ambayo wanashare kama ABT ambayo yanatolewa kwenye level ya chini ya regular army.

Mwanaume aliyeshindwa kufuzu kwenye ukomandoo ni kutokana na intensity ya hayo mafunzo yalivyokuwa magumu.

Na mwanamke aliyefuzu mafunzo ya ukomandoo haina maana amefuzu hayo mafunzo ambayo huyo mwanaume amefeli.

Ni tofauti kabisa.

Mimi sijui unaongelea jeshi gani mkuu lakini ninachojua ni kwamba mafunzo yote huwa ni sawa hayatenganishwi, halafu kitendo cha wanawake kujaribu tu tayari wameonesha uthubutu suala la kufuzu au kutokufuzu hayo ni matokeo tu kama ambavyo wapo wanaume wanaoshindwa kufuzu, ingekuwa ni suala kama wanawake wangekuwa hawajaribu kabisa ila wapo wengi sana wanaojaribu ila ndio hivyo kufuzu ni matokeo tu

Tofautisha kuyaona magumu kwasababu ni magumu na kuyaona magumu kwasababu ni mvivu.
Oohh kwahiyo wanaume wanapokataa kufanya kazi za nyumbani na kulea watoto maana yake ni wavivu siyo
 
Kwani ye mwanmke hahitaji sex company kutoka kwa mwanaume kwamba mpaka nimlipe ili nimtombe ???

Kama ni hivo aweke dau iwe wazi na sio mahusiano iwe kichaka cha kupewa hela kwasababu nachojua kwenye mahusiano tunahusiana coz tumependana na wote tuna mahitaji sawa ya kihisia ikiwa ni pamoja na sex
Km mnahusiana, bas jua mnaoana, na sio kuoa wala kuolewa.

Hisia za sex kwa mumewe, sio mchumba, km ambavyo wee utampa huduma na mahitaji mkeo.

Hukimbiiii hapa.
 
Kama wote mnahusiana na mnapendana na mna mahitaji sawa ya kihisia kwanini wanaume ndio mnalihitaji sana hilo tendo na mko tayari kuhonga chochote kilicho ndani ya uwezo wenu ili tu mlipate ilihali kwa wanawake haiko hivyo, na je kwanini baada ya kuwa kwenye hayo mahusiano mkishaachana matusi na lawama huenda kwa wanawake kuwa hawajitunzi na hawajiheshimu ndio maana wanaachwa huku wanaume wakisifiwa, na je kwanini kwenye mahusiano mnapozini mwanamke ndio huitwa malaya kwa kuzini bila ya ndoa huku mwanaume akionekana rijali
Nakupendea hapo tyuuh dada angu, [emoji122][emoji122][emoji122]
 
Back
Top Bottom