Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 11,550
- 40,697
Wapi mnakoenda? Na unaenda na nani?Leo tarehe 24 mishahara bado haijalipwa. Ieleweke kwamba vitu kama hivi ndivyo vitakavyopima uwezo wa Rais Samia kama anastahili awamu ya pili au la.
Nachelea kusema kwamba kwa mwezi kama huu (mwisho wa mwaka wa fedha) kufika tarehe 24 mishahara haijalipwa si dalili njema huko tuendako.
... that's even worse!Huo si mpicha, ni video clip ibofye usikilize.
Nafikiri mdau anazungumzia kuchelewa na sio kushindwa kulipa.serikal haijawah kushindwa kulipa mishahara yake.
24 ni mapema sana...
acha kulalamika vitu vya kitoto.
Hata mfanyabiashara huwa anacheleweshwa kupata hela pale ambapo wateja wanakosekana. Mara kumi hata mtumishi wa umma huwa inatabirika, biashara huwa hazitabiriki. Au mmesahau wale waliobaki na mbaazi majumbani mwao juzi tu hapa?...lakin kama pia unaona ni ishu. tafuta biashara kuliko kukaa unasubiria mshahara wa serikal.. halad ulichelewa unalalamika.
boss hanuniwi
Utetezi mwingine wa kipuuzi huu!!Ingawa hali ni mbaya lakini kimahesabu tarehe bado. Kulipwa tarehe 22,23,24,25 ni utaratibu tu uliwekwa kulipwa mapema ila kiuhalisia mwisho wa mwezi ni 30.
Point ya kwakuwa mwezi uliopita ulilipwa 23 eti mwezi huu hiyo 23 imepita basi mama anayumba ni ujinga. Ulilipwa mapema kabla ya tarehe husika (30).
Labda niwaulize kwa mfano ulilipwa 23 halafu tarehe 30 ukawa tarminated kazi vipi utadai siku 7 za kazi ulizofanya mpaka terehe 30?
Watumishi mnadeka sana.. Tarehe 24 unakuja kulia lia humu!Leo tarehe 24 mishahara bado haijalipwa. Ieleweke kwamba vitu kama hivi ndivyo vitakavyopima uwezo wa Rais Samia kama anastahili awamu ya pili au la.
Nachelea kusema kwamba kwa mwezi kama huu (mwisho wa mwaka wa fedha) kufika tarehe 24 mishahara haijalipwa si dalili njema huko tuendako.
Mwenye busara hujibu hoja kwa hoja. Ukiona mtu anajibu hoja kwa matusi kichwani kuna vitu haviko sawa. Hebu tingisha kichwa kidogo unahisi nini?Utetezi mwingine wa kipuuzi huu!!
Mnachotetea hata sikielewi. Mishahara hulipwa hata before 23rd mwezi wa 6 za kila mwaka miaka yote ya JPM akiwa rais. Serikali hulielewa hilo na hulipa mishahara mapema ili kujiandaa kwa ajili ya mwaka mpya wa fedha.Kila mwisho wa mwaka huwa inachelewa jpm ana husika vipi sasa
wakati mwingine ushukuru mtu wa aina hii maana anaachia fulsa wasio na ajira nao waichukue pesa yake maisha yaendelee.Upumbavu wako ndio unakufanya uwe mtumwa wa mishahara
Wekeza kula mazao ya mshahara sio kula mshahara
NB "Kuna marekebisho makubwa ya madaraja na kulipa baadhi ya malimbikizo hivyo mvumilie mpaka jumatatu"
Nimekujibu hivyo kwa sababu hukuwa na hoja ya maana. Mwezi ni siku 30 na siyo tarehe 30. Kimsingi nchi zote zilizostaaribika huwa na fixed date ya kulipa mshahara. Sisi kwetu kwa muda mrefu tumekuwa tukilipwa on 24th hivyo kwenda mbele ya tarehe hiyo inaamsha tahadhari, hasa kipindi hiki.Mwenye busara hujibu hoja kwa hoja. Ukiona mtu anajibu hoja kwa matusi kichwani kuna vitu haviko sawa. Hebu tingisha kichwa kidogo unahisi nini?
Acha kulalamika wewe. Hiyo ni issue ndogo sana ndugu.Leo tarehe 24 mishahara bado haijalipwa. Ieleweke kwamba vitu kama hivi ndivyo vitakavyopima uwezo wa Rais Samia kama anastahili awamu ya pili au la.
Nachelea kusema kwamba kwa mwezi kama huu (mwisho wa mwaka wa fedha) kufika tarehe 24 mishahara haijalipwa si dalili njema huko tuendako.
Yaani nianze kumkumbuka Magu kwa lipi eti kisa mshahara haujalipwa tarehe 24?never never,hata tukilipwa tarehe 30 sina shaka na mh rais Samia,najua na waziri kasema mwezi huu mishahara ya madaraja mapya inaanza kulipwa na ndio sababu ya kuchelewa.Kwahiyo leo watumishi mnamkumbuka Magu jinsi alivyokuwa mwema kwenu?
Hivi watumishi nchi hii mna akili timamu kweli ?
Leo tarehe 24 mishahara bado haijalipwa. Ieleweke kwamba vitu kama hivi ndivyo vitakavyopima uwezo wa Rais Samia kama anastahili awamu ya pili au la.
Nachelea kusema kwamba kwa mwezi kama huu (mwisho wa mwaka wa fedha) kufika tarehe 24 mishahara haijalipwa si dalili njema huko tuendako.