Mizengo Pinda: Tuanze mchakato wa kuwa na Tume huru ya Uchaguzi
"Kuna mambo ambayo sisi CCM kama chama tawala lazima tubebe dhima. Tutoe uongozi. Kwa, mfano hili la Tume Huru ya Uchaguzi kizuizi ni nini? Hili ni jambo ambalo lazima tukubaliane na wenzetu wa upinzani na tuanze mchakato wa kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi"

Chanzo: Darmpya
Haiwezekani yaani CCM imekaa miaka kidogo tu yaani 60 tu bado haijaifaidi nchi eti iondoke! Haiwezekani
 
Tume huru ya uchaguzi lazima ianze na katiba, uwezi kutunga Sheria iliyo kinyume cha katiba. Mzee Pinda atusaidie yeye hiyo tume huru inaundwaje endapo katiba inabaki ileile?

Je hiyo tume itatokana na wananchi au itatokana na wanasiasa? Nadhani kujadili kuwa na tume huru ni makosa na nimchongo wa TCD kupunguza Kasi ya mambo yanayoendelea Sasa. Tumekwama na tumekuwa watu wakulumbana Kwa miaka Sasa, malumbano yalianza baina ya viongozi lakini Sasa yamekwenda Hadi Kwa wananchi wa chini, hakuna mwenye Imani na mfumo wa kisiasa na hata waliopitishwa na mfumo uliopo wa siasa hakuna mwenye uwezo wakusimama mbele ya wananchi kusema walimchagua.

Hoja ibaki moja TU ya katiba mpya, ndani ya katiba mpya mengine yote yatapata ufumbuzi. TCD waache agenda za michongo, wasimame kuhesabiwa kwa kudai Kati mpya SIYO kuitia Katiba viraka.

Mwisho, wanapojadili Tum huru wajiulize bunge lakupitisha hiyo sheria ya kuunda tume huru ni lipi? Bing la Sasa linaweza kupitisha sheria ya Tume huru? Bunge la chama kimoja lipitishe sheria ya kuunda tume huru.....labda wapewe maelekezo.

Tukitaka tume huru tutengeneze bunge jipya la katiba , la sivyo hata bunge la kubadili sheria Kwa sasa halikidhi vigezo vya mabunge ya kidemokrasia
Mna jema nyie? 🙄
 
Mkuu wapiga kura wengi wapo vijijini, na huko vijijini huwaambii kitu kuhusu CCM na kura nyingi huwa wanazoa huko. Huku mijini wazee wa hoya hoya nyingi na kuchangamsha mikutano
Wewe acha uongo bwana, unaongelea Tanzania ya mwaka gani hiyo, sasa hivi kila mtu mjanja teknolojia imebadilisha kila kitu.

Hao wana vijiji unaowasema wengi wao walishakufa sio hawa wa sasa ambao kila mara wanaangalia EPL. Wangekuwa hivyo ccm wangeishakubali hiyo tume huru miaka 20 nyuma.

Endelea kulala, tume huru, uchaguzi huru na haki mtajikuta mna wabunge 20 wa kuchaguliwa. Wewe ccm kukataa tume huru unafikiri wao ni wajinga.
 
"Kuna mambo ambayo sisi CCM kama chama tawala lazima tubebe dhima. Tutoe uongozi. Kwa, mfano hili la Tume Huru ya Uchaguzi kizuizi ni nini? Hili ni jambo ambalo lazima tukubaliane na wenzetu wa upinzani na tuanze mchakato wa kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi"

Chanzo: Darmpya
Asije kuyakana maneno yake kuwa walimnukuu vibaya.
 
"Kuna mambo ambayo sisi CCM kama chama tawala lazima tubebe dhima. Tutoe uongozi. Kwa, mfano hili la Tume Huru ya Uchaguzi kizuizi ni nini? Hili ni jambo ambalo lazima tukubaliane na wenzetu wa upinzani na tuanze mchakato wa kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi"

Chanzo: Darmpya
Anagalau ktk uhai wake japo kwa kuchelewa ameonesha kuguswa na swala la Haki japo mara moja ktk maisha yake.
 
Kamugisha naomba kutofautiana na wewe kidogo hoja kwa hoja kama ifuatavyo;

Tume huru ya uchaguzi lazima ianze na katiba, uwezi kutunga Sheria iliyo kinyume cha katiba. Mzee Pinda atusaidie yeye hiyo tume huru inaundwaje endapo katiba inabaki ileile?

Pinda kasema kuwa "...hata TUME UHURU YA UCHAGUZI tatizo ni nini? Tukae (wao CCM) na wenzetu wa vyama vingine tukubaliane...."

Key word hapa ni "Kukubaliana" ambayo obvious ni process. Na process hii ni pamoja na kuangalia sheria yetu mama (katiba), sheria ya uchaguzi na ya tume ya uchaguzi zinavyoweza kupatana kwa pamoja...

This means kuwa "amendments" ya katiba haiepukiki. Na ku - amend kitu si sawa na kuki - overhaul na kukifanya kipya...
Je hiyo tume itatokana na wananchi au itatokana na wanasiasa? Nadhani kujadili kuwa na tume huru ni makosa na nimchongo wa TCD kupunguza Kasi ya mambo yanayoendelea Sasa. Tumekwama na tumekuwa watu wakulumbana Kwa miaka Sasa, malumbano yalianza baina ya viongozi lakini Sasa yamekwenda Hadi Kwa wananchi wa chini, hakuna mwenye Imani na mfumo wa kisiasa na hata waliopitishwa na mfumo uliopo wa siasa hakuna mwenye uwezo wakusimama mbele ya wananchi kusema walimchagua.

Hapana. Tukianza na TUME HURU YA UCHAGUZI is a good step kwenda kwenye KATIBA MPYA. Binafsi sioni tatizo....

Tukumbuke kuwa hawa CCM ni chama cha siasa na lengo lao kama "chama cha siasa" linabaki lilelile la kama vyama vingine, yaani KUONGOZA DOLA..

Wao ndiyo wenye dola sasa. Miaka yote hii, wametumia njia OVU na za HILA kushinda chaguzi na kutusababishia shida hizi tunazopitia sasa...

Sasa kitendo cha kukubali na kuanza kuachia kidogo kidogo baada ya pressure kwa maoni yangu ni hatua nzuri kuelekea kwenye utengamano halisi, na maana yake ni hii, akili njema hao CCM inaanza kuwarudia...!
Hoja ibaki moja TU ya katiba mpya, ndani ya katiba mpya mengine yote yatapata ufumbuzi. TCD waache agenda za michongo, wasimame kuhesabiwa kwa kudai Kati mpya SIYO kuitia Katiba viraka.

Katika siasa Beatrice sometimes ni ngumu kupata yote kwa mpigo. Na kama ukitaka kupata yote at a go, basi you have to pay a big price...

Hebu tukubaliane twende na hili kwanza maana ni zuri kwa kuanzia. Hii haina maana ya kuwa madai ya katiba mpya yatakufa..

Na kumbuka kuwa, ili kuipata NEC mpya HURU pekee kutakwenda sambamba na mabadiliko makubwa ya katiba ili ku - accommodate huo "UHURU WA HIYO TUME.."


Mwisho, wanapojadili Tum huru wajiulize bunge lakupitisha hiyo sheria ya kuunda tume huru ni lipi?

Ndiyo maana ya wito huu wa kukutana na kujadiliana jinsi ya kuipata hiyo NEC guru..

This means that, hayo yatakuwa considered na wote kuamua the right way to go....
Bing la Sasa linaweza kupitisha sheria ya Tume huru? Bunge la chama kimoja lipitishe sheria ya kuunda tume huru.....labda wapewe maelekezo.

Inaweza isiwe kama tutarajiavyo sote. Lakini twendeni kwenye huo wito majadiliano tutaona huko. Kama ni kuwapa "benefit of the doubt ", tutawapa...

Lakini wakumbuke kuwa, kuamua mustakabali wa kiutawala na kiaiasa wa nchi/taifa ni lazima kila mdau ashiriki kwenye maamuzi hayo...
Tukitaka tume huru tutengeneze bunge jipya la katiba , la sivyo hata bunge la kubadili sheria Kwa sasa halikidhi vigezo vya mabunge ya kidemokrasia
"Bunge la katiba" kwa ajili ya NEC huru pekee, ni ngumu. Badala yake tunaweza kutengeneza tume ndogo itakayoshirikisha stake holders wote i.e vyama vya siasa, NGOs, taasisi za dini nk nk wakapendekeza maeneo ya kufanyiwa amendments kwenye katiba na muundo wa NEC HURU yenyewe utakuwaje...

Kama kuna "nia njema" kwenye hili, kila kitu kinawezekana kwa njia ya majadiliano...!!
 
Asante. Sina la kuongeza nisiharibu ulichokisema.
Hili suala la tume huru ya uchaguzi ni suala la msingi sana.

Kilichotokea 2020 hakikuwa na afya kwa nchi yetu ipo siku kutaiangamiza nchi.

2008 kenya waliuana law sababu ya tume ya uchaguzi kufanya upumbavu.

2010 Zimbabwe wakauana kwa sababu ya tume ya uchaguzi kufanya upumbavu.

Ivory coast waliuana kwa sababu ya tume ya uchaguzi.

Tunataka mpaka nini kitokee ndiyo tujue umuhimu wa tume ya uchaguzi.
 
Kumbe kunauwezekano wa kuwapata wanaccm wenye akili!!
Tatizo ccm wanajua ikiwepo tume huru ya uchaguzi, wangi wao hawata toboa
No alikuwa wapi huyu crocodile inawezekana katumwa baada international pressure kutamalaki
 
Hili suala la tume huru ya uchaguzi ni suala la msingi sana.

Kilichotokea 2020 hakikuwa na afya kwa nchi yetu ipo siku kutaiangamiza nchi.

2008 kenya waliuana law sababu ya tume ya uchaguzi kufanya upumbavu.

2010 Zimbabwe wakauana kwa sababu ya tume ya uchaguzi kufanya upumbavu.

Ivory coast waliuana kwa sababu ya tume ya uchaguzi.

Tunataka mpaka nini kitokee ndiyo tujue umuhimu wa tume ya uchaguzi.
Kwa yaliyotokea 2019 na 2020,tume ya uchaguzi ilipaswa iwe imeshajiuzuru

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Sio wa kwanza yeye, hata Mkapa alisema hilo kwenye kitabu chake.
 
Muda wa kutengeneza katiba mpya na tume upowakusha tatizo nini
 
Lakini kama anania ya Dhati na ya kweli kuhusu Tume basi tumuunge mkono.
Nia anayo, ili kuridhisha wanasiasa wapinzani, yote hii ni kukwepa katiba mpya.

Usifikiri katoa maoni haya kutoka hewani, naamini baada ya serikali kubinywa, wameona solution ni kuwapa wapinzani wait kisiasa tume huru, ili wakae kimya. Waachane na suala la katiba mpya.

Kwa jicho la mbaliii, naona Mbowe akiachiwa Kwa sharti la kuachana na suala la katiba mpya Kwa kua Alisha Hongwa tume huru.

Inaeleweka, kizungumkuti kwenye katiba mpya ni Masuala ya Muungano.
Hali ni tete hivo Basi ni afadhali Tume huru kuliko Muungano kuwa dhaifu,
Ukizingatia n 1 wa Sasa akipata nafasi au sababu anaweza egemea kuleeeee.
Na ikawa ndo mwisho wa Kila kitu.
 
Back
Top Bottom