Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

Jamani hebu tumieni akili kidogo nanyie, hili nalo kweli linahitaji "msaada" wa serikali? Acheni aibu na uwoga, hutaki kuchanga weka wazi kabisa "mimi huwa sichangii harusi", ukiwajibu hivyo wataacha wenyewe kukufuata, then elekeza kipato chako cha ziada kwenye kuwasaidia wenye shida zaidi yako. Mimi hata skumbuki mara ya mwisho kupewa kadi ya mchango wa harusi ilikuwa lini.
Nimeupenda ujumbe wako mkuu. Hata mm msimamo wangu kama wako tu ila harusi za ndugu huwa nachangia kwakweli ila kitchen party sichangi wala send off hata kama ni ndugu
 
Mkuu nipo Latin-America niliwahi kuwasimulia ndugu zetu hawa walatino process ya kuoa nyumbani walishangaa mno na hata kusema ni nani atayaweza hayo?
Mbaya zaidi imekuwa kama ugonjwa kuanzia kwa wazazi mpaka kwa watoto. Mwaka juzi nikiwa likizo nilimkuta mama anawaza namna ya kujazia pesa ya harusi ya mdogo wangu. Niliangalia uwezo wa familia na majukumu yaliyopo nikayalinganisha na bajeti ya harusi kisha nikashauri baadhi ya vitu vitolewe na harusi isiachie familia madeni; wacha kabisa karibu nitolewe macho aisee.
Kama nawaona vile walikushambulia kama nyuki
 
Bado hujawekwa ktk loud speaker unaulizwa pledge yako"tuko kikaoni hapa tumekuweka ktk loud speaker, enhe unapledge ngapi"
 
Michango ya Harusi:

jambo hili linachosha sana mathalan kwa miezi hii baada ya Easter unakuta mtu una card zaidi ya tano (mimi binafsi nnazo saba) ,minimum mchango ni TZS 50,000 na unatakiwa kwenda kwenye wedding utatumia extra cost minimum TZS 40,000
 
Mimi hilo jambo ni raisi sana. Nawaambia sina bajeti hiyo kwa sasa, nina majukumu ambayo ni kipaumbele kwangu. Nami nimeshajipanga kisaikologia sitakuja kuomba michango kwa mambo ya sherehe labda kwa familia yangu.
 
Mhubiri wa "Hatimaye maisha"yanayorushwa mubashara kutoka Mbeya alisikika akizungumzia kidogo suala la kujiepusha na gharama za arusi na kuangalia suala la elimu zaidi.
Nampongeza kama kiongozi wa kiroho kuzungumzia hilo,lakini alisema kidogo sana kuhusu aina hiyo ya "ujinga" ambao umekuwa ugonjwa wa wa Tanzania hasa wa imani ya kikristo.
Arusi zimekuwa ni kitu cha kuoneshana ufahari na mashindano ya matumizi makubwa ya pesa kwa ulevi na fahari za muda tofauti kabisa na uhalisia wa maisha ya walio wengi wanaoshiriki arusi hizi.

Ujinga unakuwa mkubwa zaidi pale mtu anapokuwa tayari kuchangia zaidi ya laki saba hadi milioni kwa mwaka kwa ajili ya arusi halafu anakataa kuchangia matibabu ama elimu kwa watoto wenye uhitaji.

Nawapongeza wakenya tangu enzi zile za mwl.Nyerere utasikia matangazo radioni "mbunge wa nyeri anaalika harambee ya kuchangia wanafunzi siku ya jumamosi"...

Matangazo hayo nikikumbuka japo nilikuwa mdogo,yanaonesha umakini wa wakenya katika suala la elimu.

Nilipokuwa mdogo nikisikia salamu katika vipindi vya watoto walikuwa na msemo " na maziwaa..ya watoto wa nyayo"

Viongozi waliona umuhimu wa lishe kwa watoto ili wawe makini na elimu.

Vipi suala la gharama hizi za arusi lisijadiliwe kwa kina na kubadilisha mind set za wa Tanzania kutoka kuchangia arusi na kufikiria kusaidia katika suala la elimu.

Bahati mbaya baadhi ya viongozi wa dini ya kikristo wanahimiza matumizi mabovu ya arusi za kifahari na wakati huo ndoa zinazofungwa nyingine hazidumu.

Imefika wakati wa kila mmoja wetu aanze kuangalia upya iwapo tunahitaji arusi za kifahari wakati tunakabikiwa na umaskini na ujinga ambao hatuungani kuutokomeza kama tunavyoungana wakati wa arusi.
KWELI MDAU TUNAPASWATUAMKE TOKA USINGIZINI TUBADILIKE TUEPUKANE KUSHIBISHA FUNZA CHOONI BALI TUANGALIE MABADILIKO YATAKAYO LETA TIJA KWA JAMII SASA NA SIKU ZIJAZO.
 
Ndoa za mwendokasi zimekuwa ni nyingi sana skuizi, vijana wamekuwa wanamuamko wa ajabu kuowa bila kujiandaa mwishowe wanakuja kusumbua watu, Alafu unapewa kadi ya mchango yenye kiwango cha mwisho kabisa cha mchango yaani unaambiwa usitoe chini ya 100,000.

Nimeshawachangia mabest zangu wengi nilisoma nao miaka ya nyuma, nakumbuka nishawachangia mabest zangu kama 40 hivi na kati ya hao 15 ndoa zao zimeshavunjika tena ndani ya mda mfupi tu tokea wafunge ndoa

Na wengine wamekuwa ni matapeli kama yule mzee Kokobanga wa kule Instagram, wanaomba michango ukishawachangia wanaingia mitini na ndoa hamna hela wanakula, ifike mahali sasa kila mtu apambane na hali yake, ukitaka kuowa nenda kanisani au msikitini na mpenzi wako kimya kimya fungeni ndoa yenu na maisha yaendelee, mambo ya michango michango yamekuwa mengi alafu ndoa zenyewe hazidumu mnachezea hela za watu tu
 
Ndoa za mwendokasi zimekuwa ni nyingi sana skuizi, vijana wamekuwa wanamuamko wa ajabu kuowa bila kujiandaa mwishowe wanakuja kusumbua watu, Alafu unapewa kadi ya mchango yenye kiwango cha mwisho kabisa cha mchango yaani unaambiwa usitoe chini ya 100,000.

Nimeshawachangia mabest zangu wengi nilisoma nao miaka ya nyuma, nakumbuka nishawachangia mabest zangu kama 40 hivi na kati ya hao 15 ndoa zao zimeshavunjika tena ndani ya mda mfupi tu tokea wafunge ndoa

Na wengine wamekuwa ni matapeli kama yule mzee Kokobanga wa kule Instagram, wanaomba michango ukishawachangia wanaingia mitini na ndoa hamna hela wanakula, ifike mahali sasa kila mtu apambane na hali yake, ukitaka kuowa nenda kanisani au msikitini na mpenzi wako kimya kimya fungeni ndoa yenu na maisha yaendelee, mambo ya michango michango yamekuwa mengi alafu ndoa zenyewe hazidumu mnachezea hela za watu tu

Umegonga ikulu mkuu....michango inasumbua sana.....me huwa nikiona hizo text za michango napiga kimya tu maisha yenyewe yako wapi
 
Ndoa za mwendokasi zimekuwa ni nyingi sana skuizi, vijana wamekuwa wanamuamko wa ajabu kuowa bila kujiandaa mwishowe wanakuja kusumbua watu, Alafu unapewa kadi ya mchango yenye kiwango cha mwisho kabisa cha mchango yaani unaambiwa usitoe chini ya 100,000.

Nimeshawachangia mabest zangu wengi nilisoma nao miaka ya nyuma, nakumbuka nishawachangia mabest zangu kama 40 hivi na kati ya hao 15 ndoa zao zimeshavunjika tena ndani ya mda mfupi tu tokea wafunge ndoa

Na wengine wamekuwa ni matapeli kama yule mzee Kokobanga wa kule Instagram, wanaomba michango ukishawachangia wanaingia mitini na ndoa hamna hela wanakula, ifike mahali sasa kila mtu apambane na hali yake, ukitaka kuowa nenda kanisani au msikitini na mpenzi wako kimya kimya fungeni ndoa yenu na maisha yaendelee, mambo ya michango michango yamekuwa mengi alafu ndoa zenyewe hazidumu mnachezea hela za watu tu

starehe yake yeye sie ndio tugharamikie....upuuzi mtupu. tena anaweka na kiwango kabisa. ukiomba mchango wa ada za shule wanasema oh mbona ulizaa kama ulikuwa hujajiandaa...basi kama nawe unaoa jiandae
 
Back
Top Bottom