MJADALA: Kwanini pale alipo mtu mweusi hali ya uchumi huwa ni tete? Nini chanzo cha umasikini?

MJADALA: Kwanini pale alipo mtu mweusi hali ya uchumi huwa ni tete? Nini chanzo cha umasikini?

Gwa
Issue kubwa kwa mtu mweusi inayo fanya awe nyuma kimaendeleo kulinganisha na watu weupe ni ubnafsi .Aliye bahatika kupata nafasi nzuri ya kutumikia sehemu flani ata hakikisha iwe kwa udi au uvumba anaweka watu wake hata kama hawana uwezo. Kingine mtu anaenda shule kusoma lakini lengo sio kupata maarifa ili aya tumie lakini lengo ni kupata cheti ili awe promoted akae kwenye AC africa msomi ni yule anaye jua kukariri na anaye jua kujieleza lakini lakini kiutendaji hamna kitu.Ili tutoke hapa tuweke watu wenye uwezo husika bia kujalisha ni mtoto wa nani wa mjini au kijijini kutumika sehemu husika alafu hoja ya Gwajima ya kuwa na long term plan ni ya kuizangatia sana nchini kama watu au sehemu ni productive kwa kitu flani ndio tuwekeze nguvu kubwa huko kwa miundo mbinu wezeshi ili kuleta matokeo makubwa:
Gwajima was right sema kuna watu wakamzushia Sukuma gang na vitu kama hivyo kumnutralize ionekane ana msema mama hana maono. Siasa tabu sana.
Nchi zote zilizoendelea kuna mambo ya msingi hata aje nani hawezi kuyabadirisha. Wakisema Osama mbaya hata regime ya 4 itaendelea kumtafuta Osama. Wakisema Hiyo hata kwa individuals hatuna consistency ndio maana mambo yetu ni bahati na sibu. Nilijiuliza kwa nini serikali isichukue engineering graduates wapelekwe china wakajifunze viwanda vidogovidogo hao ndio wangekuwa wanabeba uchumi. Wangekopa benki kujiendesha na ingeongeza mzunguko wa hela na kupunguza importation. Nilienda India nikakuta wazee na vijana wana workshop ambayo inatengeneza AC kuanzia scratch yaani wanaanza na bati hadi mwisho.
 
[emoji23]
Inategemea ni ugali wa kitu gani.. kama sembe ni shida.
Lkn kama ni mixer ya muhogo, mtama, ulezi, uwele, nk.. iQ inakuwa juu zaidi ya wastani
Havitakiwi kuchanganywa hivyo vitu, cocktail nikwaajili ya vinywaji tu kama juisi, hata uji wa mtoto Ili apate afya pika kimoja peke yake alafu ongeza butter original siyo blue band uone iQ na afya ya mtoto inakwenda vizuri.
 
Chanzo cha Afrika (Tanzania) kuwa maskini ni..

1. Mfumo mbovu wa elimu.

2. Usalama wa taifa/TISS mbovu (hiki ndio chanzo kikuu).

3. Viongozi wabovu ambao hawajaandaliwa (refer magufuli alipo sema ameokota parachichi chini ya mwarobaini).

4. Kutotumia rasilimali zetu vizuri (refer gesi ya mtwara).
Challenge kweli. Elimu inazungumzwa kuwa chanzo mara nyingi. TISS wameaminiwa lakini hamna weledi, Viongozi wabovu ni elimu na ubinafsi, Kutotumia rasilimali ni ubinafsi tena mtu anapewa rushwa kuuza rasilimali za taifa. Solution Katiba mpya?
 
Wa
Pia watu weusi tunatatizo la kuvumila shida badala ya kuzitatua. Mtu anashida kibao eti anaamuachia Mungu kweli!!

Common Phrases Tanzania
1. Sa nitafanyaje? - ukukashika tama
2. Hamna namna
3.Tumuachie Mungu nk.
Wakoloni walipotuletea dini ndio walitumaliza kabisa. Mwafrika anajiona yuko karibu na Mungu kuliko hata yule aliyemletea. Haha hukuti mkoloni anashinda kanisani siku nzima.
 
Watu weusi sisi ni malaya. Malaya kutoboa ni kazi sana.
Na ukitaka tufanikiwe uwe mkali kuchukua maamuzi magumu yaaani kama viboko kwa punda bila kuwa hivyo watu watajiendea vibaya kuleta matokeo ya hovyo hovyo alafu iwe lawama kwa utawala, baba, mama na mtoto akili zinalingana na mkubwa anategemea mdogo ndo atoke amuokoe ila yeye mkubwa anaendekeza uvivu na kuchezea muda tu na huyu wa chini akikua anategemea wa chini yake ndo aje kumkwamua Sasa circle inakwenda hivyo hivyo.
 
Mkuu maji ya mvua na mto si salama hata kidogo. Hapo tukubaliane kwa sababu yanakusanya taka zote unazozijua na hazichujwi. Mbali na kutokuwa hayachujwi nikiwa shule tulifanya mambo ya ku grow bacteria. Unaambiwa tu weka finger print kwenye plate halafu ikifanyiwa incubation unapigwa na butwaa vitu tunavyokuwa navyo kwenye mikono hata kama unaiona ni misafi. Mmasai hanywi maji salama. Ukiicheck clear water katika slide ya darubini utaona namaanisha nini.
Unajua neno contamination ? Sasa kama mazingira hayajaharibiwa kama western countries au mito na natural springs hazijaharibiwa alafu mtu akachukua hayo majo na kuyachemsha na kuyanywa utasema sio salama sababu hayajawa chlorinated kama public water ? Point yangu hizi jamii zilikuwa na utaratibu kwenye mto kuna sehemu zimetengwa sehemu ya maji ya kunywa inakuwa mwanzo kule mwisho ndio sehemu ya mifugo all in all ni avoiding contamination.., Pili kulingana na watu kuishi kwenye mazingira hayo wanakuwa wagumu na ku-build natural immunity tofauti hata hizo hospitals za ulaya unaweza kwenda ukapata kitu kinaitwa super bugs (kutokana na hospital kuwa so clean..., kuna bugs wamesha-adapt madawa mpaka wamekuwa sugu wa kutupwa (sisemi watu wasiende hospitals najaribu tu kukwambia all is not rosy) and we need kuboresha sio huku tu hata huko....
Matibabu ni kigezo cha maendeleo, ukianguka na pikipiki utapata huduma? je dawa zipo? Bima sawa lakini basic ipo? na je unapokuwa na bima ma specialist unaweza kuwaona na wapo? Mama akitaka kujifungua kwa operation huduma ipo? ukizungumzia mizizi na appreciate sana ni muhimu lakini kuna mambo haifanyi.
Kuboresha ndio maendeleo..., wamasai wameweza kuishi na dawa zao, na kila jamii kila sehemu kuna dawa zao ingawa sijasema wasiboreshe, bali waendelee kuboresha na specialist maana yake ni mtu aliyespeacilize na kubobea kwenye jambo fulani (kila jamii ilikuwa na inayo ma-specialists wake hivyo cha maana ni kuboresha) ila point yangu ilikuwa unaweza ukawa States unakaa jirani na specialist lakini usimuone sababu huduma zake sio kwa everyone (masikini hawezi kuzipata)
 
Challenge kweli. Elimu inazungumzwa kuwa chanzo mara nyingi. TISS wameaminiwa lakini hamna weledi, Viongozi wabovu ni elimu na ubinafsi, Kutotumia rasilimali ni ubinafsi tena mtu anapewa rushwa kuuza rasilimali za taifa. Solution Katiba mpya?
Katiba mpya inaweza kuwa solution lakini hata ikiwepo na tukandelea kuwa na viongozi kama tulio nao je kuna jipya?

Mimi nadhani solution ni katiba lakini pamoja na katiba mpya ni lazima kuanza kuifumua TISS na kuhakikisha inafanya kazi kwa weledi. Maana TISS ikisimama hutaona mikataba ya hovyo wala viongozi wa hovyo hovyo wakiingia kwenye uongozi.
 
Botswana mnayoitolea kama mfano ni nchi kubwa iliyo tupu..wana resources sawa lakn ina idadi ya watu sawa na zenji..GDP yao na yetu ni almost alike.lakn wakt sisi tupo milion 60, wao ni wachache, ni 1.5m including foreigners.
 
Botswana mnayoitolea kama mfano ni nchi kubwa iliyo tupu..wana resources sawa lakn ina idadi ya watu sawa na zenji..GDP yao na yetu ni almost alike.lakn wakt sisi tupo milion 60, wao ni wachache, ni 1.5m including foreigners.
Ukiona watu hawazai ovyo jua wana akili
 
Nimesema hayo au wewe ndio umesema ?!!!!

Ngoja nikupe mifano mingine Kiafya kipi kinafaa Choo cha Kukaa (Wester) au cha Kuchuchumaa (Eastern)

Pia Wajapan na utamaduni wao wa kukaa kwenye matress chini wakati wanakula na shughuli nyingine ni Ushamba au inawasaidia ki-afya ??

To each his / her own...., tatizo umejengewa kwamba kila kinachofanywa au kiliochofanywa ni ushamba na kukosa ustaarabu na kila unacholetewa ndio usasa (ndio maana tunahangaika kuweka tiles kwenye madarasa yetu kwa pesa ya mkopo kabla hata hatujaboresha maktaba, vitabu wala waalimu (eti ndio usasa)
Jinga kabisa wewe tambelea vijijin huko watu hawana hata vyoo wanajisaidia kwenye vyanzo vya maji na maporini!
 
Challenge Kikwete akiwa London alisema kuzaliwa Africa peke yake ni challenge. Upbringing yetu. Mfano mtu unakua unalala chini, income ya kwanza badala ya kuinvest unaanza kuwaza kitanda, nyumba ya kuishi na kwa sababu unakuwa ushapigwa sana na maisha unaanza kunywa na bia ambayo ulikuwa hu afford. Mtu akizungumzia investment ni maili nyingi sana kichwani.
Na kimsingi kwa asili yetu watu weusi tuna ubinafsi mwingi sana na hapa utaona watu hawapo tayari kutumia akili zao kuwaza na kwa nafasi walizo nazo kutumika kwa mapana kwa ajii ya jamii nzima.....watu wenye mentality kama Mwl. Nyerere, Nelson Mandela, Nkwame Nkurumah ni wa kutafuta kwa tochi miongoni mwa watu weusi.
 
Mkuu Ufugaji Wa Kuhama Kama Hao Masai Ng'ombe Hawezi Kuwa Na Afya Nzuri kwanini Wasiwekewe Sehemu Nzuri Waletewe Chakula Kuliko Kuwatembeza Kwenye Jua?

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
Nimesema wanachofanya sio sustainable kama wingi wao ukiongezeka (ila point yangu ni kwamba kwa jamii yao, maisha yao na wakati wao husika wao sio masikini) kwahio inabidi wabadilike (nilichofanya ni comparison ya hawa na wale wadau ambao unaweza ukasema ni matajiri sababu tu ya perception yako wakati kumbe mmasai ni better off na ana peace of mind)
 
Mkuu tufanye nini kwa sababu hizi ndio sababu zinazotuchelewesha. Haya mambo hata kwa wazungu lakini yakaisha je ni elimu watu waelimishwe?
Katiba, Sheria za kujijenga jamii na kuirekebisha inapokosea ndo msingi wa Kila kitu, Leo hii kama kusingekuwa na Sheria za kulazimisha watoto wapelekwe shule tungekuwa na watu wengi wasiosoma kama zamani, Leo hii wazazi wasingelazimishwa kutunza watoto wanaozaa Sasa tungekuwa na watoto wanaojilea wenyewe tangu wadogo, hata hizi chaguzi za Nchi zote ni katiba na Sheria zilizotungwa kipindi hicho zinaongoza jamii na Nchi, Sasa nini kifanyike kubadili hii jamii ya teknologia mpya ni kuweka katiba mpya na Sheria mpya zitakazofatwa na kizazi hiki cha teknologia mpya Ili jamii ibadilike na iwe ya kisasa.
 
Botswana mnayoitolea kama mfano ni nchi kubwa iliyo tupu..wana resources sawa lakn ina idadi ya watu sawa na zenji..GDP yao na yetu ni almost alike.lakn wakt sisi tupo milion 60, wao ni wachache, ni 1.5m including foreigners.
Alafu unaona umeandika point kweli.
 
Jinga kabisa wewe tambelea vijijin huko watu hawana hata vyoo wanajisaidia kwenye vyanzo vya maji na maporini!
Kwako choo ni nini ? na kuna aina ngapi za vyoo ?

Je unaona ni sahihi na sustainable kwa sehemu za vijiji vyenye ukame kuwa na flushing toilet au ni kama jamii hizo walivyojiwekea a dry toilet ili kuweza ku-conserve maji ? Hata huko ulaya wameshaona kwamba pa kuelekea ni kutumia water recycling...

Wewe uliopo mjini unadhani hujisaidii kwenye vyanzo vya maji..., ushaona waste water zinavyokuwa dumped kwenye vyanzo vya maji au haujui kuna meli huwa zinakuja na industrial wastes kutoka huko ili kuzileta huku na kuzi-dump (juzi tu kuna meli ilishikwa Kenya ikiwa inaelekea huku)

Moral of the story ni kwamba kutokuendelea kwetu kupo kwenye fikra kwa sasa na sio kwenye ngozi (kutawaliwa kwetu kumesababisha kuona kwamba suluhisho ni wale wanavyofanya na sio sisi kuweza kuboresha kile wanachofanya au mababu zetu walichofanya)
 
Inategemea

Naanza kutetea hoja

Mkuu wazo lako la kuwa panapo mtu mweusi hali ya uchumi inakuwa tete nalipinga
1 your too general
Kikanda au kieneo flani kama vile nchi, mkoa nk waafrika wengi kiukweli ni maskini ila kuna baadhi yao wana ahueni

2 uchumi wa mwaafrika mmoja mmoja
 
System za uongozi ni mbovu mbaya
Uongozi unaanza ngazi ya familia mkuu

Unafata kwenye jamiii

Familia nyingi za kiafrika ni uchawi na huamini maendeleo yapo tu

Hapa unakuta familia haina strategy za kujikomboa kiuchumi yenyewe kwanza

Hata serikali ikipambana kumuinua mwananchi lakini kama mwananchi mwenyewe hana strategy za kujiinua kiuchumi lazima aiponde

NB Usiilaumu serikali je ngazi ya familia inakuongoza vipi kwenye kujikwamua kiuchumi?
 
Naomba Kuuliza Kwanini Tunasoma Elimu ya Mkoloni Tangu Enzi Na Enzi,Kwa Mfano Mtu Kamaliza Form Four Amekariri What Is Biology Hata Haiwezi Ikamtoa Wenye Umasikini?

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Inategemea

Naanza kutetea hoja

Mkuu wazo lako la kuwa panapo mtu mweusi hali ya uchumi inakuwa tete nalipinga
1 your too general
Kikanda au kieneo flani kama vile nchi, mkoa nk waafrika wengi kiukweli ni maskini ila kuna baadhi yao wana ahueni

2 uchumi wa mwaafrika mmoja mmoja
Mwafrika akipata pesa haitamsaidia yeye wala jamii inayomzunguka.
 
Back
Top Bottom