Mjini Mipango: Unaweza kuanza hii biashara hata kwa mtaji usiozidi bei ya iPhone moja latest

Mjini Mipango: Unaweza kuanza hii biashara hata kwa mtaji usiozidi bei ya iPhone moja latest

Uko sahihi nkoi. Sio WaTZ tu, ni karibu Wafrika wote ni wavivu, hatupendi kazi, tuna visingizio sana na si waaminifu. Nimeona hii kwa nchi kadhaa za Afrika nilizofika.

Ukienda nchi zilizoendelea ndio utajua sisi ni wavivu na hakuna wakati tutawafikia wenzetu. Hata tubadilishane wahamie Afrika, twende kwao, baada ya miaka michache watatupita tena.

Hii jamii yetu ya wavivu wengi pia inakwamisha wachache wenye bidii. Unaajiri vijana, wanakusumbua hadi uwasimamie hasa. Na ukiwasimamia wanakimbia. Huwezi fungua biashara ukasafiri au ukashinda kwenye majukumu mengine inakufa.

Ndio maana matajiri wengi Afrika wenye makampuni makubwa wasimamizi wao wa kazi ni Wazungu au wa-Asia. Tazama Mo, Bakhresa, Mengi, Dangote, Patel na hata makampuni mengi yanayokuwa.
Actually watanzania siwaweki kwenye kundi la wavivu kivile. Malawi, S. Africa, Swaziland, Congo, Zambia...hao baadhi niliwahi kuishi nao, wavivu balaa...wabongo wakiwa majuu wanapiga mzigo balaa.
 
Mimi niliwahi kukodi marine board,acha kabisa.moja inakodiwa Kwa 13,000-15,000.na dukani moja ni tzs40,000+.Kwa hiyo,zile ambazo fundi atatumia nzima ni bora kukodi,na ambazo atahitaji vipande,unanunua nzima ili akate.
Unaweza ukaona jamaa wanapata sana,ila niliwauliza,kuna kipindi wanaweza kukaa hata miezi sita hawajapata mteja wa kuhitaji kukodi,na kuna kipindi wanapata sana wateja mpaka havitoshelezi.
 
Hii mbona ipo sana, wala haina shida ni biashara kama biashara nyingine
Hapana kuna sheria za visima , dawasa wakikustukia wanakupiga faini za kibabe haswa
Sema wanakuwa wagumu kuikomalia hii sheria maana kuna baadhi ya sehemu maji ya staili hii ni muhimu
 
Hapana kuna sheria za visima , dawasa wakikustukia wanakupiga faini za kibabe haswa
Sema wanakuwa wagumu kuikomalia hii sheria maana kuna baadhi ya sehemu maji ya staili hii ni muhimu
Wakomalie sehemu zenye mtandao wao wa maji. Sehemu nyingine hazina kabisa maji yao watu wafanye nini?
Mimi nimeunganisha kwa jirani yangu namlipa 15,000 kila mwezi. Nimepiga hesabu kuchimba kisima ni kama 3.5m. Mwaka mzima nalipia maji 180,000 hio 3.5m ni maji ya miaka 20 nikaamua wacha ninunue kwake tu.
 
Mtoa mada 40+ age So imemchukua miaka 40+ yeye kukodi mbao.

Mathematically:
kwa mteja kukodi inachukua muda wa miaka 40 utakuja muona tena baada ya miaka 40+
Tangu nimeamka asbh, hii ndo pumba ya kwanza naisoma leo.
 
Nitoe ushuhuda wangu,

Hii kazi ya kukodisha vifaa vya ujenzi Eg, mbao za lenta, mirunda, fox, nguzo za chuma, majukwaa nk. Ni nzuri kwakuwa nami naifanya japo changamoto zipo ndogo ndogo
Eg, mbao kukatwa na mafundi, mteja kuchelewa kurudisha vifaa kama mlivyo kubaliana nk.

Hata hivyo pamoja na changamoto hizo bado inalipa. Binafsi nina miaka3 tangu nianzishe biashara hii, nakumbuka nilianza na mbao20 ila kwa sasa zimefika mbao 600 na nimefungua branch office

Lakini sikuishia hapo nilianzisha na biashara ya kuuza vifaa vya ujenzi kwakuwa ni biashara zinazoendana.

Kwa sasa namshukuru Mungu kile kilio cha ajira kwangu kimeisha kwa sasa naagalia namna gani ya kutanua biashara yangu

Haikuwa rahisi kiivyo kupiga hatua but kujituma na kuwa na nidhamu ya pesa ndio mambo muhimu.

Vijana wenzangu tupambanie ndoto zetu coz wazee wameishamaliza majukumu yao kutuleta duniani. Asanteni wote

Karibu nikuuzie rangi za Nyumba
Silk
Emulsion
Weathrguard
Drewa
Na Terrasit kwa Bei ya Agent
 
Hapana kuna sheria za visima , dawasa wakikustukia wanakupiga faini za kibabe haswa
Sema wanakuwa wagumu kuikomalia hii sheria maana kuna baadhi ya sehemu maji ya staili hii ni muhimu
Kumbe.....
Ninakoishi mie hakuna maji ya dawasa ni visima wameunganisha mabomba, na mita zipo wanakuja kusoma na kuijia bill mwisho wa mwezi, sasa kama sio halali wamewezaje hadi kuungalisha mita kwenye mitaa?
 
Wakomalie sehemu zenye mtandao wao wa maji. Sehemu nyingine hazina kabisa maji yao watu wafanye nini?
Mimi nimeunganisha kwa jirani yangu namlipa 15,000 kila mwezi. Nimepiga hesabu kuchimba kisima ni kama 3.5m. Mwaka mzima nalipia maji 180,000 hio 3.5m ni maji ya miaka 20 nikaamua wacha ninunue kwake tu.
Sheria yenyewe ina mapungufu kibao ,na ndio sababu hata wao inawawia vigumu kuisimamia
Imagine wanataka uombe kibali na kulipa tozo kabla hata hujachimba kisima chenyewe,
Kwenye mambo ya visima kuna mengi, unaweza kuchimba na usipate maji, au ukapata maji yenye chumvi isiyovumilika , au ukapata maji ambayo hayatadumu
@ 3.5 mil huko ulipo ni nafuu sana sijajua uhakika wa kupata maji upoje , huku nilipo nilipo visima kama hivyo vinaenda hadi 10 mil na unaweza ukayakosa maji , na chances za kupata maji matamu ni very slim to none
 
Kumbe.....
Ninakoishi mie hakuna maji ya dawasa ni visima wameunganisha mabomba, na mita zipo wanakuja kusoma na kuijia bill mwisho wa mwezi, sasa kama sio halali wamewezaje hadi kuungalisha mita kwenye mitaa?
Dawasa sehemu ambazo hawajafika wanakuwa wapole , na siku wakifikisha maji , hao waliosambaza maji, wataanza kusumbuliwa kuna sheria kabisa ya visima, na ina adhabu zake pia zipo
 
Sheria yenyewe ina mapungufu kibao ,na ndio sababu hata wao inawawia vigumu kuisimamia
Imagine wanataka uombe kibali na kulipa tozo kabla hata hujachimba kisima chenyewe,
Kwenye mambo ya visima kuna mengi, unaweza kuchimba na usipate maji, au ukapata maji yenye chumvi isiyovumilika , au ukapata maji ambayo hayatadumu
@ 3.5 mil huko ulipo ni nafuu sana sijajua uhakika wa kupata maji upoje , huku nilipo nilipo visima kama hivyo vinaenda hadi 10 mil na unaweza ukayakosa maji , na chances za kupata maji matamu ni very slim to none
Kigamboni maji yapo karibu sana na mazuri sana.
 
Ulimkata vibao ama[emoji23][emoji23][emoji23]maana majamaa wanakera kwa kiwango cha juu

Unaweza kufika site unaona kabisa hapa nimepigwa

Hahahaaaa hapana nilimchana tu aache kuniibia manake hela inapatikana Kwa shidaa

Akakasirika akasema namuona mwizi akaacha na kazi[emoji23][emoji23]
 
Kumbe.....
Ninakoishi mie hakuna maji ya dawasa ni visima wameunganisha mabomba, na mita zipo wanakuja kusoma na kuijia bill mwisho wa mwezi, sasa kama sio halali wamewezaje hadi kuungalisha mita kwenye mitaa?
Huko mpo advanced...hadi Mita kabisa.
 
Nimekuwa kwenye sekta ya ujenzi kwa muda mrefu sana kwasababu mzee wangu yupo huko.

Nakwambia hakuna watu wabaya kama mafundi.

Fundi lazima atakuibia utake usitake na ukimbana sana anakuachia kazi yako anaondoka.

Wewe ni boss, kazi ya fundi ni kutekeleza. Ukimpa nafasi akupe ushauri kuhusu mambo ya fedha utamuachia hela nyingi sana.

Wewe sikiliza utaalamu wake, kama una make sense tekeleza tena kwa njia yako na sio njia yake.

Ila mafundi wanapiga wateja jamani
Kuna muda mpaka unamuonea huruma
 
Watu wa hardware wanapiga sana pesa kwenye hii biashara na ukipasua mbao yake unailipa..!!!
Mno. Nina jamaa yangu anakodisha mbao zilizotengenezwa spesho kwa kusimamishia nguzo za zege (beams). Anakuletea mpaka site. Mjini kuna wabunifu wengi sana
 
Back
Top Bottom