Mkataba (MoU) kati ya Serikali na Kanisa Katoliki na Taasisi nyingine za Kidini

HIVI KWANINI SISI WAISLAM HATUNA SHUKRANI???
HOSP ZA WENZENTU PERAMIHO, KCMC, BUGANDO HOSP PAMOJA NA ST AUGUSTINE UNIVERSITY, TUMAINI UNIVERSITY NA VINGINE ZILIJENGWA WAKIWA NA WATAALAMU WAO AMBAO WANGEWATOSHELEZA...LAKINI HAWAKUTUBAGUA, WALITUHUDUMIA WOTE BILA KUANGALIA KAMA MIMI NI ASHA AU ANNA!
SERIKALI KWA KUONA MCHANGO WAO MKUBWA IKAAMUA KUSIGN MoU ILI KUBORESHA HUDUMA ZILIZOKUA ZINATOLEWA KWA WATANZANIA WOTE !!!!
JE MLITAKA NA SISI TUSIGN MoU KWA KIPI TULICHOKUA NACHO AMBACHO KILIKUA NA MANUFAA KWA JAMII YOTE BILA KUJALI ITIKADI??? NKISEMA MADRASA MTAKUA MNAKOSEA NDUGU ZANGU
ISITOSHE SASA TUMEZAWADIWA CHUO KIKUU AMBACHO ILKUA CHUO CHA HUDUMA ZA UMMA NA SIJASIKIA WAKRISTO WAKILALAMA KAMA SISI
KWANINI TUNAKUA NA ROHO MBAYA NA UNAFKI KIASI HIKI??? LAITI WAKRISTO WANGETUBAGUA SIJUI TUNGEKUA WAPI??
DAH ALIYETULOGA AMEKUFA SIJUI???!!!!!
 


TUMIA AKILI YA KUZALIWA KUCHAMBUA MAMBO MKUU, HATA KAMA DARASANI HUJAENDA TAFAKARI MoU ISINGEKUEPO HAWA WAKRISTO WAKAJITOSHELEZA NA KUTUMIA HIZO HUDUMA WENYEWE HALI YETU INGEKUAJE???
TUACHE UNAFKI BANA KWANZA ZAIDI YA 90% YETU WAISLAM TUNAPONEA KWENYE HUDUMA ZA AFYA NA ELIMU BORA KWA WAKRISTO
 


Unaandika hovyo ukiwa dsm..nina wasiwasi hata kama umewahi fika mail moja tu hapa....hujui shida wanazopata ndugu zetu vijijini...hujui kiasi gani hospitali za makanisa zinavyoto huduma...hujui Ikonda...Hujui peramiho....hujui Ilembula kaa kimya!!!!!
 
Unaandika hovyo ukiwa dsm..nina wasiwasi hata kama umewahi fika mail moja tu hapa....hujui shida wanazopata ndugu zetu vijijini...hujui kiasi gani hospitali za makanisa zinavyoto huduma...hujui Ikonda...Hujui peramiho....hujui Ilembula kaa kimya!!!!!

Asante Makete Kwetu yaani ni ukweli mtupu!!!
Natamani wakristo watunyime hizo huduma ndio tutajua kwamba wao ni msaada kiasi gani kwetu!
Waislam tusiwe wanafki jamani...huu unafki wetu na wivu ndio vinatufanya tuwe waropokaji badala ya kumshukuru Mungu
 
mama D ,chukua tano . . . . . . . . . . !!
 
Last edited by a moderator:
Makubaliano kama haya ni mojawapo ya mikataba ya kifisadi inayolenga kupora uchumi wa nchi na kuupeleka ktk taasisi zinazonufaika na mikataba hiyo huku serikali ikidhohofisha uwezo wake wa kutoa huduma hizo za kijamii. Huu ni uhujumu wa uchumi.
 
Makanisa si ndo wajanja, wasomi, na wanajua umuhimu wa mikataba.
Baada ya utaifishaji wa kipind cha nyuma kutokea so mambo ndo yanabidi kupelekwa kisheria tu no way out.... Wacheni kulia lia tu...
 

bravo mkuu natumia simu ningekugonga like
 

Aga Khan ni taasisi ya kidini (na si ya Kikristo) ila inapata the same treatment kama hospitali nyingine zinazomilikiwa na makanisa. Na hilo unalisemea vipi?
 
Makubaliano kama haya ni mojawapo ya mikataba ya kifisadi inayolenga kupora uchumi wa nchi na kuupeleka ktk taasisi zinazonufaika na mikataba hiyo huku serikali ikidhohofisha uwezo wake wa kutoa huduma hizo za kijamii. Huu ni uhujumu wa uchumi.

Hebu jaribu kusoma hoja mkuu!!!
 
Habari za asubuhi wandugu,

Nilivoona heading nimeshawishika kuufungua uzi huu ili nionekilichomo na kuchangia pale ikibidi. Nimeona, kama ambavyo wenzangu mmeona, kilichomo ndani ya MoU ambayo kimsingi imewekwa katika mlengo ambao haupo kwenye mizania. Wengi wamemfahamisha mleta mada kuwa angekua amefanya justice kama document yote ingeletwa humu.

Mawazo yangu juu ya hili ni kama ifuatavyo;

MoU ilisainiwa 1992, commander in chief wa wakati huo alikua Ali Hassan Mwinyi. Wote mnafahamu imani yake na ukweli kwamba nchi haina dini. Nimeanza hivi ilikuonesha kuwa hata mkuu wa nchi alijiridhisha mantiki ya ombi la TEC na CCT kuwa hapakuwa na nia ovu katika kuomba mashirikiano haya. Kwanza aina ya huduma ni za kijamii hususan elimu na afya (consumption of social services the principle of non-exclusivity holds). Maana yake ni kwamba hamna namna ya kumzuia mtu ku-access huduma ya kijamii kwa msingi mwingine wowote ule nje ya utu na haki ya mtu kuishi.


Naomba nimuulize mleta mada hivi katika taasisi za afya madhalani, kanisa liliomba waiver ya kodi na kusaidiwa wataalam na mishahara ikibidi. Kwa kuwa huduma zinatolewa kwa misingi ya utu na haki ya kuishi, si kwa imani zao, naona MoU haikua na tatizo ikiwa unalitazama jambo hili objectively. Ninavyofaham kuna combination ya waajiriwa wa taasisi husika na waajiriwa wa Wizara ya Afya. Ivi kunaushahidi wowote kuwa ajira chini ya Wizara ya Afya zipo ktk misingi ya kidini? hapana binafsi siamini na sina ushahidi. Ukienda Bugando, KCMC, Mbeya Referal Hospital nk hutakuta watumishi wa imani moja lakini hizi taasisi ni za madhehebu ya kidini hii inaonyesha kuwa hizi fikra mfu na incitement zinazojaribu kujengwa ni watu wenye akili ndogo tu ndo wanaweza kuafiki hoja ambazo hazina mashiko. Pia fanyeni utafiti kwny registers za haya mahospitali wagonjwa wanaotibiwa kama majina yao ni ya dini fulani pekee ama vinginevyo! Na kama utafiti utadhihirisha beyond reasonable doubt kwamba huduma zinatolea kibaguzi then hoja itakua na mashika. Utafiti huu hauhitaji PhD hata asiye jua kusoma na kuandika ila akawa anajua majina ya dini zetu atakuja na genuine findings katika hili.


Pia najiuliza ivi watu wa imani zingine hawakuwepo na kama walikuwepo hawakusikia hata tetesi ya kilichokuwa kinaendelea ktk maombi ya CCT + TEC kuhusu MoU? Je, mtazamo wa watu wa imani zingine bila kusahau wapagani walilionaje jambo hili kwa wakati huo? Je, ni kweli kwamba MoU iliratibiwa chini ya Carpet? Je, tangu wakati huo wanufaika ni kundi fulani la kiimani? Je, mtu wa imani nyingine ukienda kutibiwa treatment ni tofauti? Ukiwa katika taasisi hizo unalazimishwa kufuata imani ya kikristo? Nadhani ukifanya uchambuzi wa dodoso langu utakuja kugundua kuwa mada hizi zinaanzishwa si kwa nia njema. Maana unavoleta mada jaribu kufanya japo utafiti mdogo ili hoja iwe na uzito zaidi.


Mimi ni mkristo, siandiki haya kwa kuzingatia imani yangu ila najaribu kutazama objectively. Nimesoma shule iliyokuwa na mchanganyiko wa imani tumesoma vizuri, tulikua na group discussions based on our programs na sio imani, nimarafiki zangu wa karibu kabisa ila ni waimani tofauti na yangu lakini ni marafiki si wakinafiki. Nashangaa leo kila jambo tunataka kulipa mlengo aidha wa ukristo ama uislam. Napenda niwakumbushe Watanzania wenzangu kuna jambo tunalisahau kuwa nchi hii hakuna imani mbili pekee, ukristo na uislam. Kwa mfano mimi ni mkristo kwa kuwa nimezaliwa ktk imani/familia hiyo, wewe ni muislam kwa kuwa umezaliwa ktk familia/imani ya kiislam. Wengine wanamajina ya kikristo lakini si waumini wa ukristo ama ya kiislam lakini sio waumini wa uislam. Tunawaweka wapi watu hawa ktk mijadala yetu. Na wanahaki ya kuishi, kuheshimiwa, kuto bughudhiwa wala kudharauliwa kwa kuwa hawana ufuasi wa wa dini tunazozijua.

Kwa mfano, tunawaganga wa jadi (kienyeji) wenye majina yanayoshabihiyana na imani zetu lkn shughuli zao ni tofauti na mafundisho ya imani zetu. Ikumbukwe mganga wa jadi amesajiliwa na mamlaka za nchi hii. Hawa tunawaweka wapi kwenye huu ujinga tunaoukuza bila sababu. Utulivu wa nchi hii unatakiwa uwe chachu ya maendeleo kwa mtu mmoja mmoja na nchi kwa ujumla na si vinginevyo. Naamini lengo la dini ni kudumisha amani na upendo na si vinginevyo. Sitaki kuamini kama dini zinamaanisha chuki, uadui, fujo na aina nyingine za fujo. Tumekua wandugu tudumishe udugu wetu. Na kwa wale waliochoka utulivu wakae kimya kwa faida ya tuliowengi!
















 
aliyeleta MOU kakosa cha kuleta?Serikali ilipotoa chuo cha TANESCO zawadi kusaidia Muslim University huko MORO nani alilalamikia?Leteni hoja msipike mawe hayatatoa supu!
 
Mimi bado sijauona ubaya wa wa negotiations za namna hii baina ya serikali na asasi yoyoe, iwe ya kidini au binafsi kwani serikali haina uwezo wa kupeleka huduma kama za maji, umeme, afya, elimu n.k. kila mahali nchini. Haya ni mapatano baina ya serikali na asasi zinazotoa huduma kwa wananchi ambao serikali ndiyo ilikuwa na jukumu la kuwahudumia na ambayo kutokana na sababu kadhaa imekuwa na uwezo mdogo kufanya hivyo; sasa kuna ubaya gani ikifanya mapatano na mtu binafsi au taasisi inayotoa huduma hiyo kuwapunguzia mzigo wanaotoa huduma hizo? Mikataba kama hiyo haihusu asasi za kikristo pekee; nazifahamu asasi binafsi na za kiislamu zinazohudumia wananchi zenye mikataba ya namna hiyo. Kwa kweli MoU zimesaidia wananchi kupata baadhi huduma bora kabisa kwa bei nafuu au bure katika Hospitali bora kabisa kama Agha Khan, Ifakara, Bugando, KCMC, na Hospitali kadhaa za taasisi za kidini. Na mapatano yenyewe mara nyingi ni jinsi serikali itakavyozipunguzia mzigo asasi hizo katika majukumu yao ya kutoa huduma kwa wananchi wenye haki ya kuhudumiwa na serikali yao; sasa ubaya uko wapi hapo?
 
Mama D, do you really know the History of this nation? Dont you know that Muslims were the first to support decolonization process? kimsingi,lengo la brother kuleta hoja hii with such memorandom ni kutaka kuitanabahisha jamii kuwa waislam hawana chuki na dini nyngn.the problems have been engineered by the govt it self.
 
Sasa kama watu wana maphd ya ukweli wanajua kuplan mambo yao kisomi sio hajabu kuwa na protecction ktk investment zao,

nafikiri ni bora dini nyingine pia zikatafuta namna ya kupata memorandum kama hii,
 
huwa napata kichefu chefu kusikia watu wanasema eti Makanisa yalikuwa yakisaidia serikali kabla ya MOU, na eti serikali ndo ikadandia huduma za makanisa , amazing!
Hivi hawa watu wamekwenda kwenye hizi hospitali? wamepewa huduma wakalinganisha na some other normal pure private hospital?
Mimi binafsi nimekwenda , najua kujifungua katika hospitali za serikali ni bure kwa wakati ule 2008 sijui sasa, nikaenda hospital ya KCMC kumpeleka mke wangu nikafikiri kwa kuwa ni private yenye subsidy kutoka serikalini mambo yatakuwa nafuu, OOOPH nikashanga mbali na huduma zoote, kujifungua kwa kawaida kabisa ni sh 20,000 kumbuka ni 2008 hiyo! ,niliguna kidogo, dada mmoja pale reception akaniambia kaka KCMC ni private hospital! nilikuwa nalijua hilo lakini sikutegemea.
Hospitali za kanisa ni wafanyabiashara kama ilivyo kwenye mashule yao, kielelezo ni ada kubwa wanazotoza ! ni mfumo kristo tu ndo utakubaliana na hali hiyo, jenga picha eti ruzuku inayokwenda hospitali za kanisa ni zaidi ya inayokwenda kwenye hospitali za serikal, sasa serikali inashindiwa nini kujenga hospitali zake!
 
Hakuna sababu ya kulumbana kwa sababu ya MoU hiyo. Huduma inayotolewa ni kwa Watanzania wote. Wenye kutaka kuingia MoU kama hiyo au nyingine iliyobora zaidi kwa manufaa ya Watanzania wote wafanye hivyo. Tutawashukuru kuliko kulalama kwa mazuri waliyofanya wengine. Huo ni wivu usiojenga. Tushirikiane tujenge nchi yetu tusifarakane.
 
Kaka toa ushauri wako, je ulitaka wakatoliki waingie mkataba na waisilamu? Serikari ndio Baba na ndiyo mwenye pesa na mamlaka katika nchi hii, hivyo basi kila Taasisi inawajibu wakumshawishi baba/ Serikali kwa namna inavyoona ina kuwa inafaa, hata waisilamu munakaribishwa kufanya mikataba ilimradi iwe na tija kwa jamii ya watanzania. Hata hivyo mkataba huo hauna ubaya, tatizo hapo ni shule/ Elimu ni duni wapendwa, someni elimu dunia kwa nguvu zote.
 
Jamani shule ni tatizo, hata kwenye hii mitandao anajitokeza ustaadhi mmoja mmoja kweli, tumnawakaribisha kusoma kwa bidii.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…