Mkuu, huyo mtoto wa mtu unayelala nae kimya kimya siku asipoamka hakuna mtu atakuelewa hapo mtaani

Umemsanua ndugu yako.
 
Mkuu noma sana hii ilimtokea mshkaji wangu. Mtoto kafunga shule kafikia kwake kabla ya kwenda kwao. Siku ya 1, 2 asubuhi mtoto haamki. Kumbe kafa. Jamaa alikimbia...
Mimi ilitaka nitokea mtoto kaja geto mara kazima. Yani nilidata si kidogo nilidata balaa
 
 
Iliishaje mkuu?
 
Iliishaje mkuu?
Ya jamaa au yangu?
Jamaa alidakwa, akasota ndani kwa muda mrefu pasipo kesi kusikilizwa. binti alikuwa anasoma uganda sasa aliporudi, alikuwa anasoma form 6, akafikia kwake akae siku 3 ndo aende kwao ndipo akafa. so jamaa alikimbia kisha akapiga simu kwa jirani kumwambia ndani kwake kaacha maiti. Alikaa sana zaidi ya miaka 7 ndani kesi hata haisikilizwi. Ila kwa sasa yuko uraiani japo sijui yuko wapi ni muda sana nimesikia taarifa zake.
Mimi alikuja kwangu. Tumekaa kaa tumefanya yetu. Baadae nimekwenda sebuleni narudi namkuta kazima. Haitiki, hajitingishi. Nikimtikisa anaguna tu. Wee asikwambie mtu nilitaka kudata. Nikaanza kumtikisa anaguna tu mapigo yake ya moyo yako chini kabisa.
Nikamkokota hadi bafuni nikamwagia maji, wapi. Nikataka kuwaita majirani, nikaona jau maana hakuwa kavaa. Nikamvisha kwanza. nikatoka nje nikaona isiwe tabu. Nikarudi ndani nikamkokota nikamwingiza kwa gari, hapo nawaza nimpeleke hsptal. shida sikuwa na pesa ya kutosha, na nikawaza nipige simu kwao. Familia zetu zilikuwa family friend lakini hawakuwa wanajua kama mimi natoka na mwenzangu ilikuwa siri kubwa baina yetu.
Mwisho ilibidi nipge simu kwao maana nilimpeleka hsptal akalazwa kapgwa drip za kutosha, pimwa kila kitu kuanzia presha, sukari sijui nini na bado hawakuona tatizo. Alianza stabilize baada saa nane usku toka saa mbili nilipomfikisha hospital.
Kwao walifika hapo na nashukuru Mungu hawakuniuliza nimemtoa wapi, nadhani walijiongeza na bill mzee wake akalipa na wala hakunihoji.
Nilikuwa bado chalii ndo nina mwaka nimemaliza chuo. Baada ya hapo nilikuwa namwogopa kama ukoma.
 
Mkuu inawezekana huyo wako alikua na tatizo la kiafya na yaweza kuwa ni siri ya familia kwa maana ya kwamba familia yake tu ndio wanajua ndio maana hawakukuliza chochote..
Mshukuru sana Mungu na pia usimtenge. Sitisha mahusiano naye lakin usimkatae kinamna hiyo kwa kumuona kama ukoma.

Ni mambo tu ya maisha, hakupenda kuzaliwa hivyo.
 
Kifo kifo tu, iwe wa kwako au sio lazima kiwake

Kama unajidanganya eti kisa akiwa mke wako ndio simu moja tu, kesho matanga kesho kutwa unaanza kusaka mwengine hakuna kitu kama hiko, lazima uchunguzi wa kina ufanyike

Hivyo potelea pote, mtoto akiutaka anaupata
 
Kitambo kidogo mkuu ashaolewa kwa sasa na ana watoto wawili ila huwa tunawasiliana mara moja moja akinikumbuka ananipgia simu kwanza tuko mikoa 2 tofauti yuko a city mimi niko dsm.
Huenda alikuwa na shida mkuu sikuulizwa swali lolote. Mama yake alikuwa analia tu daah nilikuwa najiona mwenye hatia nakaza mfuko nina buku 12 tu hata haiwezi nunua chochote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…