Fredwash
JF-Expert Member
- Oct 27, 2009
- 1,400
- 2,010
Iran amekuwa wazi ya Israeli ni uovu usiokubalika na wao kama nchi hawatakuwa watazamaji.
Israel kaamuriwa na baba yake, hakuna kuivamia Gaza isije kuwa taabu Bure! Aachie maji na mafuta haraka kwenda Gaza. Kisha wote wajipange upya. Yasije yakawa makubwa, maana madogo yana nafuu.
Kwamba Blinken aliyekuwa kadai wataiunga Israel kwa lolote, inabidi Sasa kuyameza matapishi yake.
Hali ya uwanja imebadilika, gia lazima kubadilika. Nani anataka kufa?
Kwa hakika hii ni kwa mkwara tu wa Iran sembuse ingekuwa makombora mawili matatu ya maana? Mbona manduli hawa wanapigika? Mbona mwisho wa uvamizi wa Israel ulikuwa uwe huu?
Waarabu kwa ujinga wao kutotambua uwezo mkubwa wa nguvu ya idadi ya watu wao, ni tatizo kubwa zaidi kuliko la Israel kwa uvamizi.
Ndugu yangu tatizo unaliangalia hili kishabiki aidha kiimani au rangi ya ngozi sababu hupendi walichofanya israel.. hata mie siungi mkono kabisa tena asilimia 1000 wanachofanya israel..
Ila unasahau kuwa tuko kwenye dunia ya kibepari na sheria moja ya kibepari ni unafiki.. yaan ukaribu wangu na ww inategemea nanu faikaje bila kujali tuhashare imani
Au rangi ya ngozi .. hao Iran unaowasema amin nakwambia hata israel aichukue gaza hawatarusha hata baruti..
Sio kwasababu wanaiogopa israel hapana ila wanajua kuwa nguvu yoyote atakayoitumia itamuathiri kiuchumi .. nini maana yake...? maana yake akiathirika kiuchumi ndo amewapa karata dume wapinzan wake maana. Yake watauangusha utawala wake kutokea ndan.. rejea kumbukumbu za sadam, gadafi nanhata Misri sasa hv mataifa yote makubwa ya naliana timing ukijifanya kuingia mazima mgogoro wa j
Rafiki au jiran.. utajikuta unatetereka kiuchumi maana yake utahitaj mda wa kujikusanya.. na hapo adui zako hawakupi mda wataingiza mamluki kwako waanze kupiga spana.. hujakaa sawa watu wako mtaan Wanataka muachie madaraka maana maisha magumu..mara vikundi vy kupinga serikali vinaanza sabotage.. kdg adui zako wanakupiga pin ya kiuchumi kwa Kisingizio Unaua raia wako
Kuja kushtuka washakutoa madarakan kwa kisingizio cha kulinda aman ya Nchi
C unaona Misri algeria kipind kile cha Arab spring.. bashir Syria kaponea sababu aliamua achague kumtumikia mkubwa mmoja (mrusi) wakat marekan yuko na wale waasi
We c unao a vita ya ukraine.. mrusi anajua analiwa timing sio apigwe mabomu hapana ila ana subiriwa aporomoke kiuchumi Watu wagawane urusi.. ndo
Maana hao mabest wake iran na china wanaunga mkono urusi ila hata silaha wanamuuzia.. maana na wao wanauma na kupuliza kote.. na ulaya wanamsapot ukraibe ila wanampigwa mkwala vita asiingize urusi.. kwao hio vita ikiendelea hata 10 yrs ni faida
Hata upande wa ukraine angalia misaada anayopokea inavyotolewa kila Nchi ila baada ya matamko wakikaa pamoja na wanachangia huyu mara huyu mie silaha hakuna anayesema
Anaeingia mazima.. maana wanajua ukishuka umepoteza nafasi yako na wenzio wataanza kukugeuza mtaji.. so usione misri na iran anavyoliendea hili jambo wamejifunza
DUNIA YA MBWA MWITU UKITEGUKA AU UKAVUJA DAMU TUNAWEZA KUKUGEUZA ASUSA