Mmiliki wa Shule za Tusiime jitafakari na uwalipe wafanyakazi stahiki zao

Mmiliki wa Shule za Tusiime jitafakari na uwalipe wafanyakazi stahiki zao

Hakuna shule ambayo inafukuza walimu kama tusiime.
Wala hakuhitaji hata kuhamisha yeye alitakiwa asiguse walimu angehangaika na non core function staff ambao sio walimu aongee nao the way forward politely .Lakini walimu no no no.

Walimu hawakutakiwa waguswe kabisa alitakiwa at any time awe na akiba hata ya miezi sita ya kuendelea kulipa walimu hata Kama shule itafungwa kwa corona au kwa kukosa wanafunzi ili alinde walimu wazuri wasije ondoka .Hana retention policy endelevu kwa teachers itamgharimu Sana

Ameshajenga jina anataka kubomoa .Kurudisha jina sio kazi rahisi .Ku build brand sio easy task kubomoa one day inatosha.Aachane kusumbua walimu brand builders waliomjengea tusiime Brand

Serikali huwa na akiba ya dharura ,mkulima pia ana akiba ya kiangazi ya chakula taasisi kubwa Kama Tusiime haina akiba ya kiangazi ? Very bad and hopeless financial management .Aajiri wataalamu aache ubahiri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Walimu wanatakiwa kujua kuwa wanalipwa kutokana na ADA za wazaz wanazolipia watoto wao. Sas kwa mda huu wazaz hatulipi sabab watoto wetu hawapati huduma. Wafanyakaz wajue WAAJIRI wa ndo wenye stress zaidi. Wengine wamejenga hizo shule kwa mikopo ya shule. Sas hakuna marejesho ya mikopo. Mabenk hayajui excuse ya Covid 19 watakwambia tafuta plan B tuletee marejesho..Waajili hawawafanyii mtima nyogo ni mtikisiko wa dunia ndo chanz. Vumilieni

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dharura naongelea mishahara ya wafanyakazi wake siongelei mtu kashikwa kipindu pindu serikali iwe na hela ya kumtibia kuharisha kwake mfululizo non stop!!

Tusiime siongelei hella ya dharura ya tiba ya Corona naongelea hela ya wafanyakazi core staff walimu
Umesikia serikali inachangisha ipate mishahara au posho za kulipa wabunge?
Tusiime ina source moja tu ya mapato ambayo ilishafungwa tangu tuna cases 3 tu.
Serikali ina sekta kibao bado zinafanya kazi na kodi zinalipwa.
Huwezi force vitu vifanane na kama serikali unasema haijakopa hela kwa ajili ya kutibu wagonjwa sijui wabunge, si inataka mkopo kwa ajili ya matatizo ya kiuchumi yanayokuja. Tusiime wakope benki gani itakayokubali sasa.
 
Hata stimulus package ambazo serikali za ulaya na matekani hutoa private sector huangalia survival time sio corona imekuja Leo kesho unataka stimulus package !!!!!
Naona umeniletea tena mambo ya stimulizi, embu kuwa kama mtu mwenye akili... nimeuliza hivi...

"Unaposema ya muda mfupi unajua hii hali itaisha lini?"

Naomba majibu.
 
Kwa kile ambacho hakikutarajiwa na wengi Ni suala la wamiliki wa Shule za Binafsi ikiwemo Tusiime ambayo inamiliki Tusiime nursery, primary na secondary kukaidi kulipa mishahara ya watumishi wake wakiwemo walimu.

Mmiliki wa Tusiime aliitisha kikao na wafanyakazi mnamo tarehe 17/4 kwa nia ya kuwaeleza wafanyakazi wake wote Nia yake ya kupunguza wafanyakazi, kuvunja mikataba pamoja na kutolipa mishahara kwa mwezi April na kuendelea.

Watumishi walipinga vikali ajenda hiyo na akaamua kupendekza ajenda ya wafanyakazi 500 kuwa na wawakilishi 50 ambao watakaa kikao kingine ili kujadili na kuamua hatma ya stahiki za watumishi

Vikao vyote alihakikisha anakua na mwanasheria ambae atatetea maslahi yake na hakuwapa wafanyakazi nafasi ya kuwa na mwanasheria au kiongozi wa chama Cha wafanyakazi.

Katika kikao Cha pili aliwashawishi wafanyakazi wasiokua walimu kukubali na ajenda yake ya kutolipa mishahara na kuwataka kuchukua likizo Bila malipo, kwa kutumia ushawishi huo watumishi (auxiliary) ambao wengi ni wahaya wakaunga mkono na hivyo hatma ya wafanyakazi kuamuliwa kwa Kura.

Walimu wa sekondari hawakuridhia uamuzi huo na kuamua kukutana ili kupata mastakabali wao. Baada ya Taarifa hizo kumfikia Ndugu Albert (Mmiliki) aliomba polisi wa kutuliza ghasia kutoka kituo Cha Staki Shari ili kuwadhibiti walimu hao wasikusanyike ili kunadiliana kuhusu mustakabali wao katika eneo lilokubaliwa na kwa bahati nzuri walimu hawakukutana!

Baada ya hapo ameandaa fomu maalum ya likizo Bila malipo na kuwaita wafanyakazi kimya kimya ili wasaini huku akiwapa malipo ya tsh laki Moja na nusu(rushwa) ambao watakubali!

Ikumbukwe kwamba baada ya agizo la kufungwa Shule kwa siku 30 wafanyakazi walitakiwa kujaza fomu za likizo, je inawezekana kisheria ndani ya mwezi mmoja kuwe na likizo, halafu likizo Bila malipo?

Walimu Hawa wanalipa PAYE Kila mwezi, walimu Hawa wanatoa mchango kwa serikali katika utoaji elimu Kama sekta Binafsi.

Serikali na vyombo vyake vimwagize Mr Albert Katagira alipe mishahara ya mwezi April na May haraka! Na pia vikao vyote alivyofanya viamuliwe Ni batili kisheria!

Baada ya hapo aone Ni namna gani atahakikisha wafanyakazi wake wanaishi katika kipindi hiki Cha Covid

Serikali imfanyie ukaguzi katika mapato na matumizi yake kwani hi ni Tusiime holdings kwa maana hiyo Ni group of companies. Kabla uchafu wake mwingine haujaanikwa hadharani. T
Mkuu,mambo mengi muda mchache,Vipi wanafunzi bado wanalipa ada katika kipindi hichi?Serikali inabidi sasa ianze kulipa mishahara hio maana yeye kashindwa
 
Naona umeniletea tena mambo ya stimulizi, embu kuwa kama mtu mwenye akili... nimeuliza hivi...

"Unaposema ya muda mfupi unajua hii hali itaisha lini?"

Naomba majibu.
Analazimisha mfanyabiashara awe na akiba lakini mwajiriwa asiwe nayo.
Mwajiriwa akikopa milioni 2 benki, mwajiri anaweza kopa milioni 900 kuendeleza uwekezaji. Watu wanahesabu hela zinazoingia tu utadhani ni rahisi hivyo.
 
Yes mkuu shule inawanafunz zaid ya elf mbili wa primary sijajua wa secondary

Walimu

Wapishi

Madreva wa school bus makonda

Cleaners

Bursers

Walinz

Huenda wanafika

Sent using Jamii Forums mobile app


Akili hana
Kama makampuni yanaoyoingiza mabilion Kwa siku kama voda na Tigo..hayaajiri madereva na cleaners..

Yeye ilikuwaje akaajiri Hadi cleaners?
Why asitumie basi za kukodi?

Anatakiwa kuajiri walimu wasiozidi 50 na wapishi Tu ..

The rest ni matatizo ya kujitakia
 
Tatizo taasisi binafsi wanachukua mapato yao kuwekeza kwenye biashara nyingine ambazo nyingi hazirudishi fedha na faida.
Wanachukua mikopo mabenki kwa kutumia dhamana na kipato cha biashara mama na kununulia amana/mali (asset) zingine ambazo hazizalishi kitu au zinatia hasara tu. Nyingi ya asset hizo huwezi kufanya Liquidity ya haraka na kurudisha pea sawa au zaidi ya uliyowekeza kwa haraka ukaenda kurudisha kuokoa kampuni mama inapokuwa katika msukosuko wa kiuchumi kama huu wa sasa wa COVID-19 au recession.

Kwa mfano wamiliki wengi wanaingia tamaa ya kuwekeza miundombinu mipya ya kudumu kama majengo mapya, shule na vyuo vipya ambavyo bado virudishi pesa haraka kama shule mama.

Kama pale St. An*e Mar*e naona majengo mapya kila kukicha unafikiri ada pekee zitaweza kujenga vile na bado wakalipa wafanyakazi kwa wakati na kutunza akiba itakayo saidia wakati wa dharula kama sasa?
Huenda kuna mikopo mikubwa wanachukua. Hawa wanataka pesa yao ya robo muhula siku mwanao anaripoti shule kwa robo muhula husika vinginevyo hapokelewi hadi ombi maalum, hivyo tusingetegemea kuyumba kirahisi hivyo angalau mishahara ya mwezi March, na nusu mshahara wa mwezi April, kisha likizo bila malipo au robo mshahara mwezi May.

Mambo ndiyo hivyo karibu biashara zote binafsi ilitakiwa serikali isimamie vizuri mifumo ya kifedha, mahesabu ya mapato, na mikopo ya taasisi binafsi kama wanavyo dhibiti taasisi za kifedha binafsi na za umma. najua wanajaribu kudhibiti hivyo lakini pia kuna udanganyifu kwenye mambo ya kifedha unafanywa na baadhi ya hizi taasisi wanapochukua mikopo na kufanya hesabu zao.

Inatakiwa tuige mifumo kama ya kwenye soka ya FIFA Financial Fair Play taasisi zisikwame kirahisi na kudhulumu au kutesa waajiriwa wao.

Ningeshauri kwa sasa serikali iwasaidie mikopo isiyo na riba hizi shule kama kuzifanyia BAIL OUT walipe nusu mishahara kipindi hiki au wawalipe kama theluthi mbili (two thirds) ya kima cha chini cha mishahara ya waalimu wa serikali wa ngazi husika. Waanze kulipa huo mkopo miezi miwili baada ya kufunguliwa shule lakini malipo yote ya shule hizo yapitie account maalum za serikali siyo za shule ili kulinda fedha za walipa kodi wasije kusumbua kulipa.
Serikali na wenye shule wapige hesabu gharama za uendeshaji shule kisha wajue kiasi gani serikali itawapa pesa zao hizo shule toka kwenye hayo malipo ya ada.

Hawa waalimu ni wachche sana serikali inaweza, taasisi binafsi sekta ya elimu ni kama ya afya wanaisaidia serikali kutoa huduma muhimu ya kijamii. mbona kwenye afya serikali inazisaidia taasisi binafsi kama Bugando, KCMC na nyinginezo?

CC: Prof Ndalichako , Dr. Mpango, Mh. Jafo, BOT, Waziri Mkuu, Mh. Raisi.
ujumbe wako utawafikia
 
Tusiime ina source moja tu ya mapato ambayo ilishafungwa tangu tuna cases 3 tu.
Serikali ina sekta kibao bado zinafanya kazi na kodi zinalipwa.
Huwezi force vitu vifanane na kama serikali unasema haijakopa hela kwa ajili ya kutibu wagonjwa sijui wabunge, si inataka mkopo kwa ajili ya matatizo ya kiuchumi yanayokuja. Tusiime wakope benki gani itakayokubali sasa.
Hapa ni kukaa chini muajiri/muajiriwa na kuja na win win situation. Mwalimu anadai alipwe mshahara wakati hajaingia darasani kufundisha na mwajiri anadai hana pesa ya kumlipa kwa sababu chanzo chake cha mapato kimesimama. Wote wapo sahihi. Mwalimu anafikiri mwajiri ana pesa nyingi za ziada lazima amlipe hizo na au akakope bank ili amlipe. Ila ni mara chache kumpata mfanyabiashara mwenye excess capital kwa ajili ya kusubiri majanga kama corona (ingawa kwa jicho la mwalimu linaona huyu jamaa ni tajiri sana ila hajui source of capital yake ni ipi na anaifinace kivipi)). Na wala hakuna benki itakayomkopesha bila kuwa na business plan inayo onyesha atalipaje hilo deni. Kwanza haijulikani huku kufungwa kwa shule kutaisha lini. Hata angeweza kulipa nusu mshahara (ambao kwa atitude ya hao walimu sidhani wanawesa kuukubali) atalipa hadi lini kama siyo kudrain accounts. Kwa mwajiri priority ni kulinda capital ili baada ya corona biashara iendelee. Kwa mwalimu hajali kama bishara itafungwa baada ya corona ili mradi amelipwa mshahara hata kama mtaji utatumika kumlipa maana ataenda kutafuta ajira kwingine. Kila upande unazo sababu za kulinda upande wake na zote zina mashiko.

Ila sasa mwisho wa siku ni lazima muafaka ufikiwe baina ya pande zote mbili. Lazima wote wajue hili ni janga na halijulikani mwisho wake na pande zote hazijahusika na ujio wa janga. Wajue kila upande una changamoto zake na wachore mstali unao wafanya wote waishi katika kipindi hiki. Mwisho wa siku mwenye shule hawezi kulipa zaidi ya uwezo wake. Ni serikali tu yenye uwezo wa kuwalipa wafanyakazi hata katika mazingira haya. Suala la stimulus package kwetu ni ndoto. Marekani Raisi kaidhinishiwa US2.5 trilion kwa tatizo kama hili na vile vile wana unemplyoment benefit . Nasikia hili neno linaimbwa na NSSF na wenzake. Hapa ndo pangekuwa na jibu badala ya kumbana mwajiri na mabo yangekuwa shwari. Basi kaeni mzungumze mkubaliane na mwajiri. Options ni mbili zenye maamuzi magumu kwa pande zote.
1. Termination of the contract by either party - Worse case scenario; itamfilisi mwajiri na kuwafanya waajiriwa kupoteza ajira
2. Kuwa na retention arrangement, walimu wakubali likizo bila malipo ila mwajiri atoe chochote kwa jina watalokubaliana nalo hata kama ni kidogo kuwezesha kuishi wakati utaratibu wa kufungua shule ukisubiriwa. Walimu wakubali kuwa this is not life as usual na wafunge mikanda kama ilivyo kwa secta zingine kama utalii, usafiri, baa,mahoteli nk. Kote kumepigwa.
 
[Tusiime ajiongeze taasisi yake Ni household name pesa zote anazopata anapeleka wapi huwa anakula zote? Aajiri investment manager au financial controller ammsaidiae jinsi ya kuwekeza au atafute investment consultant s mbona wahaya wenzie wako kibao tu wamsaidie.
Walimu ndio capital yake kubwa asicheze nao.Mtaji wake sio pesa ,mijengo au migari ya shule Ni walimu

Napinga kwa nguvu zote kitendo Cha yeye kugusa walimu.Mtaji mkuu wa shule Ni walimu.Hata tuition nyingi mfano mwenge dar watoto wengi huenda kwenye vibanda umiza vya hovyo lakini vyenye vijana walimu wa kutisha wenye uwezo wake kufa mtu kwenye kufundisha masomo ya sayansi

Tusiime be careful with teachers hao Ni producers wa hela za tusiime sio consumers

Haiwezekani taasisi kubwa Kama Tusiime iyumbe na ipate economic shock muda mufupi hivi .

Ada akilipwa akishatoa matumizi huwa anazipeleka wapi? Zote anazifanya dividend yake au?
Wamiliki wengi wa mashule hawatambui haya.

Haiwezekani shule ishindwe kuwalipa mishahara walimu ndani ya mwezi mmoja tu.

Je, Corona isipoisha ndani ya mwaka mzima?

Si atakufa na familia yake?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Achen kulaumu hawa mamiliki.


Ni vema serikali ifanye kitu kwaajili ya kulinda Ajira za sekta binafsi hususani hawa walimu.


Kwan wazazi wote mmelipa Ada ya mwaka mzima wa masomo??..wapo wanaolipa kwa mafungu....


Sasa kama nayeye uchumi umeyumba afanyaje ??


Serikali itoe fungu, angalau nusu kisha wamiliki waongezee, ili Watu walindiwe ajira zao.





Sent using Jamii Forums mobile app
Serikali ipi unayoiongelea?

Hii inayokula rambirambi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo St Anne Marie mshahara wa March miaka yote huwaga ni shida mshahara wa December nao ni shida wanalipwa robo robo mpaka shule zikifunguliwa.
Sasa pata picha kipindi hiki.
Wamiliki wengi wa mashule hawatambui haya.

Haiwezekani shule ishindwe kuwalipa mishahara walimu ndani ya mwezi mmoja tu.

Je, Corona isipoisha ndani ya mwaka mzima?

Si atakufa na familia yake?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom