Mnaomshambulia RC wa Arusha, mnafurahia kiongozi wetu kutukanwa?

Mnaomshambulia RC wa Arusha, mnafurahia kiongozi wetu kutukanwa?

Mkuu,

Hata ikiwa Kenya kweli wametoboa baada ya katiba mpya (this is debatable, but lets grant that for the sake of argument), ule utamaduni wao wa kutaka mabadiliko, kutaka katiba mpya, kutaka kuishi kisheria zaidi ndiyo umewapa hiyo katiba mpya.

Kwa maneno mengine, utamaduni wa Wakenya ndio umewapa katiba mpya, na kupelekea huko kutoboa unakokusema.

Katiba mpya haikuwapa Wakenya utamaduni wao.

Sisi mara nyingine tunataka kufanya vitu backwards. Tunafikiri tukiwa na katiba mpya katiba mpya itamaliza matatizo yetu.

Ni kama vile tuna uvivu fulani wa kufikiri na kutatua matatizo, tunapenda kutoa jibu rahisi kwa kila tatizo. Jibu la tatizo lolote ni "katiba mpya" tu.

Katiba mpya itamalizaje matatizo ikiwa kuna tatizo la kiutamaduni la kutoheshimu katiba iliyopo na hata hiyo mpya watu hawataiheshimu na hawataitumia?

Don't get me wrong. Katiba mpya ni muhimu, hata mimi naitaka.

Lakini, utamaduni wa watu kusimamia haki zao za kikatiba ni muhimu zaidi. Bila huu utamaduni katiba mpya haitakuwa na maana.

Kwanza hamuwezinhatabkupatabkatiba mpya nzuri. Mkioata mpya mtagundua mapungufu na kudai mpya zaidi. Kwa sababu hata hiyo mpya hamtaipata kwa umakini, kwa sababu ya kukosa utamaduni wa kuishi kikatiba.

Lets say maximum efficiency ya katiba ni 100%. Tuiite katiba inayofikia hii maximum efficiency katiba A.

Let's say katiba yetu ya sasa, katiba B, haifiki hiyo 100% maximum, maximum efficiency ya katiba yetu sasa, katiba B, ni 50% ya katiba A.

Tukiweza kuitumia katiba yetu B kwa 100% efficiency tutapata 50% efficiency ya katiba A.

Katiba B si nzuri sana, ina efficiency ya 50% tu, lakini tumeweza kuitumia hiyo hiyo mbaya fully, tukapata efficiency 50%.

Halafu, watu wanaotumia katiba A, yenye potential efficiency ya 100%, wanaitumia kwa level ya efficiency 20% tu.

Hapo utaona hao wenye katiba bora maradufu zaidi yetu wanaitumia vibaya na kupata efficiency ya 20%, wakati sisi tuna katiba mbaya zaidi yao lakini tunaitumia vizuri zaidi na kupata efficiency ya 50%.

Kwa hivyo, mabadiliko ya katiba ni muhimu, tunayahitaji, lakini kitu muhimu zaidi ni uwezo wa watu kuisimamia katiba, utamaduni wa kuheshimu na kuisimamia katiba ni kitu muhimu zaidi ya kuwa na katiba mpya tu.
👏💐👑🛡️
 
Dp world washaanza kazi ,vingunguti nyumba zimeshawekwa x na zile zenye migogoro mahakamani zimeachwa kwanza pale patakuwa bandari kavu yao
 
Dp world washaanza kazi ,vingunguti nyumba zimeshawekwa x na zile zenye migogoro mahakamani zimeachwa kwanza pale patakuwa bandari kavu yao
Wanaibua HOJA dhaifu Ili tuachane na HOJA za msingi.
 
Nitaendelea kulia na wafanya maamuzi wa hii nchi hasa wale wasioonekana Kwa public!!

SIASA IWE KAZI YA KIZALENDO SIO KAZI YA MAPESA MENGI NA KUTAJIRIKIA KAMA ILIVYO SASA!!

TUNATAKA MATAJIRI WATOKANE NA KILIMO CHA KISASA,BIASHARA,UELEDI KATIKA ELIMU NA UTAFITI NA SIO SIASA!!

NANI ASIMAMIE HILI NDUGU ZANGU!!?

NANI ATUTOE KWENYE HILI JANGA!!?

NANI ASHUSHE MISHAHARA NA POSHO PLUS ANASA SIASANI!!?SIO MIMI!!?NANI MWINGINE!!?
WABUNGE WAPOKEE ROBO YA MSHAHARA WA SASA NA POSHO ZAO!!SIASA IWE KAZI YA KUJITOLEA NA SIO KAZI YA MAPESA!!

MUNGU IBARIKI Tanzania!
Na hii ndosolution no. One katika hatma ya nchi hii. Vijana wanauana kushinda Kwa waganga kupata chance za siasa kwakua ni mapesa. Zishushwe daraja na kuwa kazi ya kawaida Kabisa ili ifisishe hio dhana. Na Si tuu siasa posho zote nchini zisizo na tija zifutwe kazi ziwe level yenye gap dogo, italeta equality na hapo ndo mwisho wa vita. Chanzo kikuu Cha hila ni inequality ya society.
 
KATIBA inahusika vilivyo.

Mamlaka makubwa ya Rais yanatoa mwanya Sanduku la kura kuchezewa na viongozi wasio na Maadili ambao wao wako tayari kufanya lolote kufanikisha agenda zao.

Mawaziri wangekuwa hawatokani na wabunge ,Bali mchakato wa Taasisi huru na Imara isiyoingiliwa na rais, tusingekuwa na mawaziri ambao chama kimewahi kuwatia MIZIGO!!

Matatizo ya nchi yetu, Yana mahusiano ya Moja Kwa moja na Katiba ya nchi.
Chadema mnafeli sana Kila mkiongelea katiba mpya mnaongekea tume huru ya Uchaguzi na kuhusu kuibiwa kura

Kwahiyo mnadai katiba mpya Kwa maslahi ya matumbo yenu
 
Kwa hiyo na wewe unaamini kuna watendaji na washauri wa karibu wa Rais (Mawaziri) wanamtukana Bosi wao! Kama ni kweli basi inawezekana huyo Bosi wao atakuwa ana mapungufu mengi ya kiuongozi bila shaka.
Mbona ni kitu cha kawaida . Hakuna Kiongozi anaweza kupendwa na wote.Tunawasimanga na kuwateta baba na mama zetu iweje kwa mtu ambaye si mzazi wako. Atatetwa,atapewa majina mbali mbali, ili mradi tu muhusika asijue. Kama unataka kupotosha kwa ajili ya siasa hilo ni jambo lingine
 
Wanajua sana kuhamisha mijadala!!
Wameshajua watanzania wengi ni bendera kifata upepo na ndio sababu wanaendelea kufanya ufisadi na Kila baya kwa kadri wanavyo penda kwa sababu udhaifu wetu wanao mikononi kwao
 
Chadema mnafeli sana Kila mkiongelea katiba mpya mnaongekea tume huru ya Uchaguzi na kuhusu kuibiwa kura

Kwahiyo mnadai katiba mpya Kwa maslahi ya matumbo yenu
Wanaoibiwa kura Si CHADEMA ni wananchi.

Mwananchi anapochagua kiongozi Fulani, Kisha ushindi akapewa mwingine,

Aliyeibuwa ni Mwananchi,

HAKI yake ya kuchagua kiongozi amtakaye imeporwa.

Nikuulize wewe, unapata faida Gani kuiba kura?

Kwa kumalizia, register ya CDM Jina Rabbon halipo.
 
Umejiuliza kwanini Nape na Makamba hawakumshambulia au kumkemea mtukanaji Kwa wakati ilhali wao ndio wenye dhamana katika jambo Hilo?

Wao kesi yao ni mbali kabisa, ishu ya huyu Mwehu ni nyengine, mana sio mara ya kwanza. Ufahari wa maisha yake ni kudhalilisha watu
 
Aliyekuwa Katibu Mwenezi ambaye ni RC Arusha sasa, aliteuliwa siku DP World wanasaini HGA.

Ndipo uone, mtu huyu anatumika kuzima mijadala muhimu ya kitaifa isijadiliwe ipasavyo.

Tustuke.
Dp world washaanza
Picha linaanza walinzi getini wako wachina,wahindi,wasomali
Sijaambiwa nmeona kwa macho yangu

Ova
 
Back
Top Bottom