Mnaopokea salary take home chini ya milioni moja, huwa mnawezaje kutoboa mwezi mzima?

Mnaopokea salary take home chini ya milioni moja, huwa mnawezaje kutoboa mwezi mzima?

Mie nasema ukweli nilikuwa napokea 5,00000 Kwa mwezi haijakatwa kitu ila nilikuwa namaliza mwezi Wala simwombi mtu hata kumi , laki Moja na 30 ni nauli ya Kwa mwezi kwenda kazini na kurudi home , chakula laki Kwa mchana tu , hapo laki mbili zimebaki , halafu 1 laki ni pamba na 50 vitu vya jumla na 50 ndio akiba yangu benki , ila sio kila mwezi nanunua pamba Kwa hiyo ni laki nanusu naweka benki . Kwa hiyo ndio hivyoo.
 
Kuna mwalimu wa sekondari anae pokea hiyo pesa kweli?
Walimu ndo walikufundisha ushoga? Mbona mmekomaa sana na Walimu hadi mnaonekana wajinga? Kwani mleta mada kajitaja yeye ni Mwalimu?

Turudi kwenye swali lako. Unajua Mwalimu wa ngazi ya mshahara TGTS H ana take home ya sh. ngapi?
 
Hicho kitu hakipo kwa sasa labla huko 2014 kushuka chini hata hivyo miaka hiyo mishahara ya Ualimu ilikuwa haijafika huko. TGTS D1 ilikuwa 630K.

Kuanzia 2015 watu wamekaa miaka 8 wengine 7 bado wapo TGTS D1, Samia ndio kawapandisha 2022 kwenda TGTS E1.

Kwa kifupi ...

Kufika TGTS F1 ndani ya miaka kumi itategemea na factor nyingi mno wengi uwachukua hata miaka 15.
2015 kabla ya uchaguzi mishahara ilikuwa 716,000 kwa D1
 
Ni kuanzia 2020 kurudi chini Ajira za mwisho za Magufuli zile za December 2020 ndio Walimu wa Sayansi na sanaa zilitofautiana.

Sayansi TGTS D3 na

Sanaa TGTS D1
Hili nalifahamu ndio maana nikaandika 2022 kurudi chini, mishahara ilikuwa sawa
 
Huna udhibitisho kiongozi, huo mshahara kwa mwalimu mbona wa kawaida kuna walimu wamekaa tu miaka 10 na kuendelea wanakunja 1,300,000, TGTS F, akianzia degree
Nadhani wewe unachanganya na certificate

Unabishana na jinga. Achana nalo. Kuna walimu wanakunja zaidi ya Milioni 2 na Hilo halijui
 
Hivi mnaopokea salary baada ya mwezi huwa mnaishi vipi asee?

Mimi nishazoea kuingiza pesa kila siku kisha naitumia nitakavyo sasa sijui wenzetu mnasavaivu vipi kudadadeki

Yaani unafanya kazi siku 30 kisha ndo unashika hela !!!!!!!

Hapana asee nilishashindwa hiyo staili ya maisha

Kwan ukishapokea mshahara si unaweza kuutoa wote na kuuweka ndani then unagawa jumla ya pesa kwa siku 30 unakua unapata per day then ukitoka job unachukua kiasi hicho Cha per day unaweka mfukoni hivyo hivyo mpk mweizi unaisha. Si kujiwekea tu utaratibu.
 
Nimekushangaa sana unawezaje kuishi mwezi mzima ukaumaliza kwa mshahara wa 1.2M ?

Haya Sasa na wewe jieleze kama ulivyotaka wenzako wanaolipwa chini ya 1M wajieleze maana mimi nisingetoboa na huo mshahara wako siku 3
 
Mwalimu wa sekondari au msingi hadi anastaafu hawezi kuwa na TAKE HOME ya 1.29M hapo kafanya kazi 35 years ana degree yake, meanwhile kuna mtu kaanza kazi pake TANAPA ana mwezi mmoja kazini ana certificate tuu anakunja take home ya zaidi ya 1.3M per month.
Unauhakika?
 
weka ushahidi
Nina dogo yupo TANESCO ana certificate ya VETA mwezi mmoja kazini ananionyesha salary slip.
Basic 800k
Responsibility allowance 130k
Housing allowance 150k
Posho ya mazingira magumu 120k.
Hapo bado zile bahasha za pale ofisini kukiwa na over tym na safari.
Almost 1.3M
 
Suluhisho ya haya ni PM majaliwa kasimu kuitoa ripoti ya tume ya ku harmonize mishahara, aliiunda miaka ya 2018's hivi hadi leo ripoti haijawekwa hadharani na recomendations zake ukute hazifanyiwi kazi.
 
Back
Top Bottom