Uchaguzi 2020 Mnyika: Sakata la Wabunge wa Viti Maalum limehusisha mfumo wa Serikali kufifisha ajenda ya 'Uchaguzi haramu'. Ahoji Nusrat kuteuliwa akiwa gerezani

Uchaguzi 2020 Mnyika: Sakata la Wabunge wa Viti Maalum limehusisha mfumo wa Serikali kufifisha ajenda ya 'Uchaguzi haramu'. Ahoji Nusrat kuteuliwa akiwa gerezani

Wanasiasa wote wa Tz iwe opposition or chama tawala wanapambania matumbo yao,huwa nashangaa watu humu mishipa inawatoka kisa hayo mavyama lakini wananufaika wengine,jinga kabisa......poleni mliovuliwa nguo......hata Shangazi anayejifanya mwanaharakati,leo akiteuliwa kuwa DC au RC atakubali na mtaishia kushangaa tu
 
sasa kinachokuliza humu kuwa ni haki yako ni haki yako ni nini? tulia wewe ulichelewa kutambua kuwa chadema ni kampuni tena ya mtu binafsi utaumia sana huku wenyewe wanakula maisha wewe endelea kudai haki wakati unatambua kabisa haki zote zimehifaziwa.
Haki kuifadhiwa haizuii haki hiyo kuendelea kupiganiwa.Hata wakoloni waliifadhi haki za waafrika ila mwisho wa siku waliziachia.
 
Kweli wazazi waliuza ng'ombe ili wapeleke ng'ombe Shule. Hivi wewe huoni kinyaa serikali nzima inashiriki uhalifu wa kugusbi nyaraka na kudanganya umma?
Yote haya juu ya nini?
Ndugu yangu tumia akili angalau kidogo...jifunze kupambanua mambo...usikariri tu mambo...kwa mawazo yako serikali imefoji...hivi Mdee na wenzake wanaweza kukubali serikali ifoji halafu wao waapishwe?

Kama ni kufoji kwanini usifikirie kuwa pengine baadhi ndani ya Chadema wamefoji saini za kiongozi wao na kuwasilisha majina bungeni?!

Halafu hivi unadhani Mdee na wenzake wanaweza kwenda kuapishwa Bila baraka za uongozi wa juu wa Chadema? Mimi nawasikitia Sana Chadema kwa kweli...mkiaminishwa kuwa kulikuwa na wizi kwenye uchaguzi na nyie mnaimba hivyo hivyo...Lissu akiimba huu siyo uchaguzi Bali ni uchafuzi na nyie mnakuja na msamiati huo huo..yaani mnachezewa Kama mazezeta...hamuwezi kutumia akili zenu na kuchambua mambo...mnapelekeshwa tu...uchaguzi huu ulikuwa ni uchaguzi halali.

Kibaraka na msaliti alishindwa kihalali kabisa...hakukuwa na wizi wa kura..nyie mitandaoni na kwenye vichwa vyenu ndio mnaoamini kuwa ulikuwepo wizi. Sasa akina Mdee happy bungeni wamewaacha na wamekwenda kupata milioni tano kwa mwezi.

Lissu amekwenda kwa mabwana zake ulaya...mtaaminishwa sijui ICC, nakuthibitishia hakutakuwa na ICC Wala mjomba wake...Tanzania pia haitakatiwa misaada...endeleeni kuteseka na kusononeka kwa mawazo...Na hakuna Mtanzania atakayeandamana.
 
Kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi na kanuni zake orodha ya wabunge watarajiwa wa viti maalumu yanapaswa kupelekwa lini NEC na vyama vya siasa?

Je, ni kabla ya tarehe ya uchaguzi mkuu au baada?

Nakumbuka uchaguzi wa 2015 Esther Bulaya alikuwa kwenye orodha ya wabunge wa viti maalumu watarajiwa kabla hajamshinda mzee Wassira jimboni Bunda.

Tusimlaumu Dobi kaniki ni rangi yake.

Maendeleo hayana vyama!
 
Hongera kwa kuandika pepa. Sijasoma chochote humo.
Kwa mujibu wa tamko la Kimataifa kuhusu haki za Binadamu la mwaka 1948 ambalo lilibainisha msingi wa kutokubaguliwa kifungu cha (2)kinakariri
’kila binadamu ana haki sawa na uhuru bila kubaguliwa kwa misingi ya rangi utaifa jinsia lugha na itikadi za kisiasa’
Vile vile mkataba wa Kimataifa wa kutokomeza aina zote za ubaguzi dhidi ya wanawake wa mwaka 1979 unasisitiza kwamba
‘Ubaguzi dhidi ya wanawake ni ukiukwaji wa haki zao za msingi hususani haki ya kuheshimu utu wao na haki zao za msingi.’

Pia katika tamko la shirika la maendeleo kusini mwa Afrika SADC(2005) ambayo Tanzania ni mwanachama liliweka kiwango cha jinsia chini ya uwakilishi wawanawake kutoka kuwa asilimia 30%na baadae kupandisha hadi kufikia 5O%.

Kwa utanguizi huo hapo juu ni wazi kuwa jamii inapaswa kuelimishwa na kuoneshwa umuhimu wa wanawake kushiriki katika uongozi kutokana na umuhimu wa kundi hili ndani ya jamii na kupiga vita wale wote wanaotumia hila na nyadhifa zao kuwadhalilisha na kuwanyima haki zao wanawake.
Hivi sasa tatizo la udhalilishaji na rushwa ya ngono kwa wanawake kwenye vyama vya upinzani limekua kubwa kiasi cha kuwanyima fursa wanawake kushiriki katika uongozi ndani na nje ya vyama vyao.Ni wanawake wachache wanaoshiriki siasa nchini bila kukutana na vikwazo hivi kutokana na misimamo yao mikali ndani ya vyama vya upinzani.Hii inapelekea ushiriki wa wanawake ndani ya vyama vya upinzani kuwa mdogo ukilinganisha na ushiriki wao ndani ya chama tawala Chama cha Mapinduzi (CCM).
Katika uchaguzi uliomalizika hivi karibuni,yapo mambo kadhaa ambayo yalifanyika ndani ya uongozi wa vyama vya upinzani yanayodhihirisha uwepo wa rushwa ya ngono na udhalilishaji mkubwa wa kundi hili muhimu la wanawake ndani ya vyama hivi.Miongoni mwa mambo haya ni kama yafuatayo:

1.Ucheleweshaji wa haki za wanachama wanawake
Baada ya uchaguzi mkuu wa Octoba 2020 Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kilitakiwa kwa mujibu wa sheria kupeleka majina ya wanawake viti maalumu kuwakilisha chama na wanawake bungeni.Ucheleweshaji wa haki hii kwa wanawake waliostahiki umegubikwa na udhalilishaji na viashirishi vya rushwa ya ngono kwa wanawake waliostahili kupewa nafasi hizi.Mzozo unaoendelea hivi sasa ndani ya CHADEMA ni matokeo ya msimamo mkali wa wanawake waliokataa kudhalilishwa na viongozi wachache ndani ya chama.

2.Uteuzi ndani ya Vyama vya Upinzani
Ili uweze kugombea ndani ya Chama chochote ni lazima chama kikupitishe ndipo jina lako likubalike kwa ajili ya kugombea.Uteuzi ndani ya vyama vya upinzani kwa mwaka 2020 uligubikwa na usiri mkubwa na hujuma ambazo baadhi yake zilihusiha udhalilishaji mkubwa wa wanawake na rushwa ya ngono.Haya yaliwekwa pia wazi na Chama Cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) katika ripoti yake ya vitendo vya rushwa katika uchaguzi.

3.Gharama za uchaguzi
Kutokana na mfumo dume wa kurithi wa kiafrika ambao ulimpa mali mwanaume na kumnyima mwanamke ni wazi kuwa idadi kubwa ya wanawake wanaotaka kushiriki siasa kipato chao kinakuwa kidogo.Hivyo kuhitaji msaada ndani ya vyama au familia ili kumudu uchaguzi ambao unakua na gharama kubwa.Gharama za uchaguzi ndani ya Chadema zimekua zikitolewa kwa maamuzi ya viongozi wachache ambao wamekua wakitumia nafasi zao kutekeleza matakwa yao binafsi yakiwemo ya ngono na udhalilishaji wa wanawake.

4.Vitendo vya udhalilishaji katika uchaguzi
Viongozi wa juu wa Chadema wamekua wakiwatumia wanawake kwa kuwadhalilisha ili jamii na mataifa ya nje yaone kuwa Tanzania inawadhalilisha wanawake.Mfano,tukio la kutengeneza la kura za jimbo la Kawe ambalo lilipelekea Mh Halima Mdee kudhalilika kwa kujua kura zilizoletwa na waliotengeneza tukio na kuondosheka zililetwa na mgombea wa CCM.

5.Kuwatumia wanawake kuvunja sheria
Viongozi wa juu wa Chadema wamekua wakiwatanguliza mbele wanawake katika matukio mbalilmbali ya uhalifu kuwakabili polisi na kusababisha taharuki huku wao wakiwa nyuma,hii imepelekea mara kadhaa wanawake ndani ya vyama hivi kuanguka na kuvunjika mkono kutokana na matukio ya kutengeneza ya viongozi wao.
Zipo sababu nyingi zinazothibitisha udhalilishaji na rushwa ya ngono iliyokithiri ndani ya CHADEMA na umuhimu wa serikali kufanya uchunguzi juu ya tuhuma hizi kwa lengo la kuwalinda wanawake na jamii ya Kitanzania kwa ujumla.
 
Sio uongozi wa chama....
Nchi hii inaendeshwa ki dikteta.. Unafikiri hao Covid 19 wameapa kwa hiari?
Kuna mwingine alikua jela Uhuru wake unatakana na kukubali ubunge
Halima baada ya kukubali kesi Zake zote zimefutwa.. Kama nchi taasisi zote kubwa zipo kisiasa unategemea nini
Mahakama..TRA.JESHI LOTE.. TAKUKURU.. USALAMA WA TAIFA
Hizi idara zote zipo kisiasa sana... Sasa unategemea maajabu gani?
 
Sio uongozi wa chama....
Nchi hii inaendeshwa ki dikteta.. Unafikiri hao Covid 19 wameapa kwa hiari?
Kuna mwingine alikua jela Uhuru wake unatakana na kukubali ubunge
Halima baada ya kukubali kesi Zake zote zimefutwa.. Kama nchi taasisi zote kubwa zipo kisiasa unategemea nini
Mahakama..TRA.JESHI LOTE.. TAKUKURU.. USALAMA WA TAIFA
Hizi idara zote zipo kisiasa sana... Sasa unategemea maajabu gani?
Punguza stress mkuu utakufa bure kunywa maji kidogo. Hebu angalia mwenye chama alivyo tweet hapa chini!!

IMG-20201125-WA0019.jpg
 
Kwa mujibu wa tamko la Kimataifa kuhusu haki za Binadamu la mwaka 1948 ambalo lilibainisha msingi wa kutokubaguliwa kifungu cha (2)kinakariri
’kila binadamu ana haki sawa na uhuru bila kubaguliwa kwa misingi ya rangi utaifa jinsia lugha na itikadi za kisiasa’
Vile vile mkataba wa Kimataifa wa kutokomeza aina zote za ubaguzi dhidi ya wanawake wa mwaka 1979 unasisitiza kwamba
‘Ubaguzi dhidi ya wanawake ni ukiukwaji wa haki zao za msingi hususani haki ya kuheshimu utu wao na haki zao za msingi.’

Pia katika tamko la shirika la maendeleo kusini mwa Afrika SADC(2005) ambayo Tanzania ni mwanachama liliweka kiwango cha jinsia chini ya uwakilishi wawanawake kutoka kuwa asilimia 30%na baadae kupandisha hadi kufikia 5O%.

Kwa utanguizi huo hapo juu ni wazi kuwa jamii inapaswa kuelimishwa na kuoneshwa umuhimu wa wanawake kushiriki katika uongozi kutokana na umuhimu wa kundi hili ndani ya jamii na kupiga vita wale wote wanaotumia hila na nyadhifa zao kuwadhalilisha na kuwanyima haki zao wanawake.
Hivi sasa tatizo la udhalilishaji na rushwa ya ngono kwa wanawake kwenye vyama vya upinzani limekua kubwa kiasi cha kuwanyima fursa wanawake kushiriki katika uongozi ndani na nje ya vyama vyao.Ni wanawake wachache wanaoshiriki siasa nchini bila kukutana na vikwazo hivi kutokana na misimamo yao mikali ndani ya vyama vya upinzani.Hii inapelekea ushiriki wa wanawake ndani ya vyama vya upinzani kuwa mdogo ukilinganisha na ushiriki wao ndani ya chama tawala Chama cha Mapinduzi (CCM).
Katika uchaguzi uliomalizika hivi karibuni,yapo mambo kadhaa ambayo yalifanyika ndani ya uongozi wa vyama vya upinzani yanayodhihirisha uwepo wa rushwa ya ngono na udhalilishaji mkubwa wa kundi hili muhimu la wanawake ndani ya vyama hivi.Miongoni mwa mambo haya ni kama yafuatayo:

1.Ucheleweshaji wa haki za wanachama wanawake
Baada ya uchaguzi mkuu wa Octoba 2020 Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kilitakiwa kwa mujibu wa sheria kupeleka majina ya wanawake viti maalumu kuwakilisha chama na wanawake bungeni.Ucheleweshaji wa haki hii kwa wanawake waliostahiki umegubikwa na udhalilishaji na viashirishi vya rushwa ya ngono kwa wanawake waliostahili kupewa nafasi hizi.Mzozo unaoendelea hivi sasa ndani ya CHADEMA ni matokeo ya msimamo mkali wa wanawake waliokataa kudhalilishwa na viongozi wachache ndani ya chama.

2.Uteuzi ndani ya Vyama vya Upinzani
Ili uweze kugombea ndani ya Chama chochote ni lazima chama kikupitishe ndipo jina lako likubalike kwa ajili ya kugombea.Uteuzi ndani ya vyama vya upinzani kwa mwaka 2020 uligubikwa na usiri mkubwa na hujuma ambazo baadhi yake zilihusiha udhalilishaji mkubwa wa wanawake na rushwa ya ngono.Haya yaliwekwa pia wazi na Chama Cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) katika ripoti yake ya vitendo vya rushwa katika uchaguzi.

3.Gharama za uchaguzi
Kutokana na mfumo dume wa kurithi wa kiafrika ambao ulimpa mali mwanaume na kumnyima mwanamke ni wazi kuwa idadi kubwa ya wanawake wanaotaka kushiriki siasa kipato chao kinakuwa kidogo.Hivyo kuhitaji msaada ndani ya vyama au familia ili kumudu uchaguzi ambao unakua na gharama kubwa.Gharama za uchaguzi ndani ya Chadema zimekua zikitolewa kwa maamuzi ya viongozi wachache ambao wamekua wakitumia nafasi zao kutekeleza matakwa yao binafsi yakiwemo ya ngono na udhalilishaji wa wanawake.

4.Vitendo vya udhalilishaji katika uchaguzi
Viongozi wa juu wa Chadema wamekua wakiwatumia wanawake kwa kuwadhalilisha ili jamii na mataifa ya nje yaone kuwa Tanzania inawadhalilisha wanawake.Mfano,tukio la kutengeneza la kura za jimbo la Kawe ambalo lilipelekea Mh Halima Mdee kudhalilika kwa kujua kura zilizoletwa na waliotengeneza tukio na kuondosheka zililetwa na mgombea wa CCM.

5.Kuwatumia wanawake kuvunja sheria
Viongozi wa juu wa Chadema wamekua wakiwatanguliza mbele wanawake katika matukio mbalilmbali ya uhalifu kuwakabili polisi na kusababisha taharuki huku wao wakiwa nyuma,hii imepelekea mara kadhaa wanawake ndani ya vyama hivi kuanguka na kuvunjika mkono kutokana na matukio ya kutengeneza ya viongozi wao.
Zipo sababu nyingi zinazothibitisha udhalilishaji na rushwa ya ngono iliyokithiri ndani ya CHADEMA na umuhimu wa serikali kufanya uchunguzi juu ya tuhuma hizi kwa lengo la kuwalinda wanawake na jamii ya Kitanzania kwa ujumla.
Wewe bongo yako hamna kitu kabisa. Unafikiri hayo ya ngono na mambo mengine hayapo kwa CCM?
Yaani watu wengine mnatia aibu, kama hujui siasa kaa kimyaaa.
 
Punguza stress mkuu utakufa bure kunywa maji kidogo. Hebu angalia mwenye chama alivyo tweet hapa chini!!

View attachment 1634586
Halima hana jinsi tangu jiwe kaingia madarakani Leo Ndio mara ya kwanza kalala bila kesi
Sina ubaya nao pia naamini alikua hana jinsi
If you can't fight them just join them
Huyu bint kweli kateseka sana
Kuanzia leo hutamuona tena mahakama ya kisutu
 
Chadema wasikurupuke.

Kuna jambo wanapaswa kufikiria sana kabla ya kwenda hatua anazosema Mnyika...

Nimeona kule twitter Heche anasema atashiriki Kamati Kuu. Ni vizuri wakikaa kama kamati kuu waangalie mahala pa kurekebisha kabla hawajatimuana kwani ot will be loong battle from to within.

HIVI LILE TAMKO LA KUTOTAMBUA MATOKEO YA UCHAGUZI LILITOKANA NA UAMUZI WA KAMATI KUU?
 
Shetani akisisitiza ufanye jambo fulani, jiulize mara mbili.

Waliosema wapinzani ni wa kuwafutilia mbali, leo wanalalamika kwanini hawaendi Bungeni.
 
Back
Top Bottom