Mohammed Shabiby: Namna ya kupunguza bei za mafuta kwa 50% ya bei za sasa

Mohammed Shabiby: Namna ya kupunguza bei za mafuta kwa 50% ya bei za sasa

Huu ushauri ni mzuri lkn suala la mafuta hata nchi kubwa zinapata taabu je nao wanauziwa na bandari yetu au
Nchi gani kubwa hizo zinazopata taabu na suala la mafuta?

Na nini hasa maana ya "nchi kubwa" na "nchi ndogo?" na uhusiano wake na hiki tunachojadili hapa?

Kuna nchi kama Luxembourg, Israel, Quatar, Austria nk ni nchi dogo sana lakini ni nchi zenye chumi imara na nchi zenye maisha nafuu sana kwa wananchi wao..!

Na kwa taarifa yako mambo haya hayako hivyo unavyofikiri..

Haya mambo ya uendeshaji wa uchumi wa nchi kwa manufaa nafuu ya maisha kwa wananchi ni suala la SERA na MIPANGO BORA..

Huwezi kuwa na mipango na sera bora bila kuwa na MFUMO BORA wa UTAWALA unaozalisha VIONGOZI BORA wenye kutumia bongo zao vizuri na wasio WABINAFSI (Selfish)..

Tatizo la nchi yetu ya Tanzania wala hata haliko huko unakofikiri wewe..

Tatizo liko kwenye ubinafsi wa viongozi wetu. Na viongozi hawa hutumia matatizo kama haya kujinufaisha kisiasa kwa gharama ya wananchi..!!
 

Shabiby atoa mwarobaini kupanda bei mafuta​


MBUNGE wa Gairo Mohammed Shabib ameitaka Serikali kuruhusu kampuni binafsi kuagiza mafuta wenyewe bila kutumia uagizaji wa pamoja.

Shabiby ametoa ushauri huo leo Jumatano tarehe 6 2022 bungeni jijini Dodoma wakati akichangia hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu.

Amesema mfumo wa uagizaji wa pamoja unafanya kutokuwepo kwa ushindani wa bei na hivyo bei inapopanda kwenye soko ambalo mafuta yanaagizwa kunakuwa hakuna mbadala.

“Leo hii mkiruhusu kampuni binafsi ziagize mafuta na kama mtu anaona kuna unafuu kwenye uagizaji wa pamoja afanye hivyo na kama ataona haina unafuu alete yeye,” amesema.

Ameongeza kuwa zimekuwa zikitolewa hoja za upotoshaji kwamba uagizaji wa mtu mmoja mmoja unasabisha ukwepaji wa ushuru.

“Meli zote zinashusha kwenye mita wanakwepaje ushuru? Hii kazi waachieni TRA utasikia TRA wanakula dili lakini ukiangalia tangu huu mfumo wa uagizaji wa pamoja mita imekufa mara nyingi kuliko kipindi cha uagizaji binafsi,” amesema.

“Naombeni sana turuhusu hayo na bei ya mafuta itashuka kuliko tulivyotarajia na wala tusidanganyane watu kwamba Serikali inaweza kutoa kodi kwenye mafuta, haiwezekani kodi ndiyo inayolipa mishahara na kununua madawa,” amesema Shabiby.
View attachment 2178669
Ili mafuta yapungue bei tuazimie viongozi wote wanaopata mafuta bure kwa magari yao iondolewe kwani mishahara yao inajitosheleza watumie magari wakiwa kazini na si kwa matembezi binafsi. Kodi za nyumba, umeme maji entertaiment allowance zifutwe wabaki kama wananchi au wafanyakazi wa kawaida. Wastaafu wote wenye marupurupu haya yatolewe kwani wanalipwa pensheni inayojitosheleza. Hakuna haja ya kujengea nyumba viongozi kwani wana mishahara mikubwa waishi kama wafanyakazi wengine. Ikifanyika hivi tutasave hela nyingi sana
 
Bulk procurement faida yake ninayoiona ni control ya kodi.

Ila faida ya kuacha watu waagize wenyewe ni ushindani wa bei hapa ananufaika mlaji wa mwisho.

Sasa ni jambo la kuchagua kati ya hayo mawili.

Kodi kwa serikali au faida ya soko huria.
Hakuna mwagizaji binafsi atakayeweza kukwepa kodi.
 
Nchi gani kubwa hizo zinazopata taabu na suala la mafuta?

Na nini hasa maana ya "nchi kubwa" na "nchi ndogo?" na uhusiano wake na hiki tunachojadili hapa?

Kuna nchi kama Luxembourg, Israel, Quatar, Austria nk ni nchi dogo sana lakini ni nchi zenye chumi imara na nchi zenye maisha nafuu sana kwa wananchi wao..!

Na kwa taarifa yako mambo haya hayako hivyo unavyofikiri..

Haya mambo ya uendeshaji wa uchumi wa nchi kwa manufaa nafuu ya maisha kwa wananchi ni suala la SERA na MIPANGO BORA..

Huwezi kuwa na mipango na sera bora bila kuwa na MFUMO BORA wa UTAWALA unaozalisha VIONGOZI BORA wenye kutumia bongo zao vizuri na wasio WABINAFSI (Selfish)..
Tafakari
IMG-20220405-WA0074.jpg
 
Yaan hao wezi na majambazi ndio huwa wanamtukana JPM.Na pia ndio wanashangilia kifo cha JPM.Kipara na Msoga katika ubora wao.
Huyo unayemwita Kipara ndiye aliyechangia pakubwa ushindi wa Magu. Sasa walishindana wapi wanajuana wenyewe. Magu alivyokuwa mtu wa visa sidhani kama hata ubunge angeupata huyu kama angejua madhambi yake.
 
Tatizo ni wenye dhamana wana maslahi mapana na mifumo iliyopo, Bwana Shabiby ujumbe mzuri ila take it back hakuna wa kukuelewa.
 
Kumbe Russia ni giant
Kabana mafuta kidogo dunia nzima inatetema kama Mayele..
Mafuta ya Russia yanarandaranda bahari kuu hamna wanunuzi- hofu ya kukiuka masharti ya vikwazo iliyowekea urusi inazuia nchi nyingi kununua mafuta ya Vladimir dikteta Putin.
 

Shabiby atoa mwarobaini kupanda bei mafuta​


MBUNGE wa Gairo Mohammed Shabib ameitaka Serikali kuruhusu kampuni binafsi kuagiza mafuta wenyewe bila kutumia uagizaji wa pamoja.

Shabiby ametoa ushauri huo leo Jumatano tarehe 6 2022 bungeni jijini Dodoma wakati akichangia hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu.

Amesema mfumo wa uagizaji wa pamoja unafanya kutokuwepo kwa ushindani wa bei na hivyo bei inapopanda kwenye soko ambalo mafuta yanaagizwa kunakuwa hakuna mbadala.

“Leo hii mkiruhusu kampuni binafsi ziagize mafuta na kama mtu anaona kuna unafuu kwenye uagizaji wa pamoja afanye hivyo na kama ataona haina unafuu alete yeye,” amesema.

Ameongeza kuwa zimekuwa zikitolewa hoja za upotoshaji kwamba uagizaji wa mtu mmoja mmoja unasabisha ukwepaji wa ushuru.

“Meli zote zinashusha kwenye mita wanakwepaje ushuru? Hii kazi waachieni TRA utasikia TRA wanakula dili lakini ukiangalia tangu huu mfumo wa uagizaji wa pamoja mita imekufa mara nyingi kuliko kipindi cha uagizaji binafsi,” amesema.

“Naombeni sana turuhusu hayo na bei ya mafuta itashuka kuliko tulivyotarajia na wala tusidanganyane watu kwamba Serikali inaweza kutoa kodi kwenye mafuta, haiwezekani kodi ndiyo inayolipa mishahara na kununua madawa,” amesema Shabiby.
View attachment 2178669
Hii itakuwa nzuri sana, bata mimi nitajitoa kwenda kununu mafuta ya urusi maana bei yake iko chini
 
very sensible.
P

Shabiby kuna kitu hajakisema vizuri kuhusu uagizaji wa mafuta wa mtu mmoja mmoja, ubora wa mafuta unakuwa substandard sana, wengi wanafanya mix za uhuni, wanaleta mafuta with low Octane rating, alafu wanatuulia gari zetu.

Shabiby ana point, ila waagizaji binafsi wengi sio waaminifu, wanaleta mafuta with low quality, alafu wanahonga watu wa vipimo, mafuta yanapita alafu yanaua engine zetu

 
Hayo mafuta yaliyowekewa vikwazo na mafuta ya wizi (black market oil) serikali haiwezi kuonekana inahusika kuyanunua maana itawekewa vikwazo. Labda serikali iwaachie wafanyabiashara binafsi wayaingize kama bidhaa za magendo halafu wayauze ndani ya nchi. Na hao wafanyabiashara binafsi sidhani kama watapunguza bei sana, watawalangua na kuwapiga tuu wananchi.
 
Shabiby kuna kitu hajakisema vizuri kuhusu uagizaji wa mafuta wa mtu mmoja mmoja, ubora wa mafuta unakuwa substandard sana, wengi wanafanya mix za uhuni, wanaleta mafuta with low Octane rating, alafu wanatuulia gari zetu.

Shabiby ana point, ila waagizaji binafsi wengi sio waaminifu, wanaleta mafuta with low quality, alafu wanahonga watu wa vipimo, mafuta yanapita alafu yanaua engine zetu

Tatizo la watanzania ni ubinafsi. Hivi mtu umeajiriwa una mshahara unakubalije kupokea rushwa? Yani sisi wananchi tunalipa gharama ya watu wachache ambao sio waaminifu. Shabiby yupo sahihi kabisa, watendaji wa mamlaka ndio wenye matatizo.
 
Siku zote sheria za protectionism huwa zinaharibu Sana uchumi na haya yote yalitungwa enzi za mwendazake,Dunia hii imebadilika tuache soko lipange bei.

Ona sasa hayo ya matreka unawapa watu wa serikali wanafanya wizi wakati unge float tender na kutoa specifications wafanyabiashara wenyewe wangeleta vitu Bora..
Naunga mkono hoja, kusema ukweli, japo Blaza wangu kuna vitu alisaidia, ila pia kuna vitu aliharibu, sisi wasema kweli, hatukunyamaza, tulisema...
P
 
Ole wako Mmarekani ajue umeenda kununua mafuta Urusi, nakuambia utayarudisha ulikoyatoa mwenyewe,
Hapa ndo namkumbuka Magufuli, angekuja hadharani na kusema hapangiwi na mabeberu tungenunua mafuta Russia kwa bei ya chini
 
... hao wahuni watatengeneza cartel; wata-collude kuwaumiza wananchi. Sidhani kama huo ushauri una msaada wowote maana siku za nyuma ilikuwa hivyo "wakashindikana" ndipo serikali ikaja na wazo la bulk procurement kujaribu kuondoa tatizo. Asitake kuturudisha kule.
kweli , lakini EWURA si wapo? inatakiwa wawadhibiti.
 
Back
Top Bottom