Monalisa apata presha mtoto wake aliye Ukraine kimasomo, vita ya Urusi yamvuruga mama mtu

Monalisa apata presha mtoto wake aliye Ukraine kimasomo, vita ya Urusi yamvuruga mama mtu

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Muigizaji mkongwe wa Bongo Muvi, Monalisa ameelezea jinsi ambavyo mgogoro wa Urusi na Ukraine unavyompa hofu kwa kuwa mwanaye yupo nchini Ukraine.

Rais wa Urusi, Vladimir Putin alitangaza kuanza oparesheni ya kijeshi katika baadhi ya maeneo ya Ukraine baada ya mvutano wa muda mrefu baina ya mataifa hayo mawili.

Monalisa ameandika: “Tumbo linanicheza kama mzazi. Ukraine! Hakuna ndege, nampataje mwanangu? Mungu wasimamie watoto wetu.”

Ameandika maandishi hayo katika ukurasa wake wa Instagram akiambatanisha na picha moja ikionyesha moto katika moja ya maeneo inayodhaniwa kuwa ni Ukraine.

Binti huyo, Sonia inaelezwa kuwa anasoma katika Chuo Kikuu cha Sumy State kilichopo katika Mji wa Sumy akisomea kozi ya Uhasibu na Ukaguzi (Accounting and Auditing) kwa kipindi cha miaka minne.

Sonia mwenyewe aliwahi kunukuliwa akisema: "Sababu ya kuchagua kwenda kusoma nchi hiyo ni kwanza wametutangulia kiteknolojia kwa hiyo tunapoenda huko kusoma tunaweza hamisha teknolojia kwa njia ya elimu kuja hapa Tanzania.

"Kitu kingine Ukraine na Urusi ni nchi ambazo zina fursa nyingi za utalii hivyo tunavyoenda huko kusoma ni nafasi yetu kuwaambia Tanzania kuna nafasi nyingi za Uwekezaji, kuna Mlima Kilimanjaro, Tanzanite na mengine mengi ambayo Tanzania tunajivunia," amesema Sonia.

MONALISA2.jpg


Ukraine.jpg
 
Baada ya Urusi kuonyesha nia ya dhati kabisa ya kuishambulia Ukraine, mataifa mengi Duniani yalichukua hatua za kuwarudisha raia wake nyumbani.

Wale ambao hawakuwa na nauli Serikali zao ziliwatumia nauli.

Na baadhi ya nchi kama Israel na Germany walituma ndege kabisa kubeba raia wao.

Wakati hayo yakijiri, Tanzania ilikuwa kimya utadhani hakuna mtanzania yoyote Ukraine.

Baada ya Urusi kutangaza kuyatambua majimbo ya Donetsk,Donbass na Lugansk yaliyoasi kutoka Ukraine na kujitangaza Jamhuri,ndipo Serikali ya Tanzania ilipotoa ushauri tu,na siyo msaada kuwataka Watanzania waliopo Ukraine warudi nyumbani.

Yaani ni ushauri tu,na si kwamba Serikali haikujua kwamba ni lazima vita iwepo, hapana, Serikali ilijua yote kuwa vita ipo kwa sababu kila kitu kilikuwa wazi ktk uso wa Dunia.

Ila kwa sababu ya kutokuwa na Desturi ya kupenda watu wake ndo sababu haikuchukua hatua zozote kuokoa watu wake.

Mmoja Kati ya Watanzania wenye majonzi na hili janga la Ukraine ni msanii wa Bongo movie,Monalisa, anadai kwamba amepoteza mawasiliano na Bintiye anayesoma Ukraine na hajui hatima yake hadi sasa hivi.

Kulikuwa na ugumu gani Serikali kuchukua hatua mapema za kuokoa watu wake kwa gharama yoyote ile?

Huwa tukisema kwamba Serikali ya CCM imechoka na imechakaa kifikra na kiutendaji tunaonekana watu wabaya sana.

Tuendako tutaongea lugha moja,sasa hivi mipaka ya Ukraine imefungwa,na anga limefungwa, hairuhusiwi ndege yoyote ya kiraia kuruka kwenye anga la la Ukraine.

Rais wa Ukraine amewataka raia wote kwenda kwenye kambi za kijeshi kuchukua silaha za kujihami.

Hatima ya Watanzania waliopo Ukraine hadi sasa haijulikani itakuwaje.
 
Mimi ingekua mwanangu yupo huko ningetafuta uongozi wa chuo wanipe muongozo, wazir wa wizara ya mambo ya nje na kama kuna ubalozi hapo itabidi nideal nao.
Yaani ubalozi wa Tanzania nje za nchi ni wabinafsi mno, sijui kama wanaweza msaidia. Yeye kama anahela asepe zake tu nchi zingine. Pia kwa nature ya ubaguzi atapata tabu.

Hivi kingine hiyo nchi mbona imechapika alimepeleka kujiuza kama kahaba? Maana sioni sababu kwenda nchi ambayo mi naifahamu imechapika na wabaguzi
 
Back
Top Bottom