Moshi: Mzazi ampiga na kumjeruhi mwalimu shuleni kwa kosa la kumuadhibu mwanae

Moshi: Mzazi ampiga na kumjeruhi mwalimu shuleni kwa kosa la kumuadhibu mwanae

Na katika hili unaweza kujifunza na kubaini mtu mwenye shule kiasi kichwani na asie na shule kichwani.

Moja anachochewa na mihemko, ghadhabu na hasira bila kutathmini wala kujua hatari na madhara mbeleni....

Mwingine anaamua kuchukua hatua kwa hekima na utulivu sana tena baada ya kutathmini kwa kina, madhara ya yanayoweza tokea huko mbeleni ikiwa ataamua vinginevyo...

Nadhani mzazi angemwendea kwa upole Mwalimu,yeye pamoja na mwanae wangesaidika vizuri zaidi kwenye suala la malezi.
Hata kama kijana alichapwa na kuumizwa bado ingekua faida kwake kwa siku za usoni, kuliko kumjengea mwanae ujasiri na kiburi dhidi ya anayoelekezwa na walimu na pengine jamii baadae..
Haitamsaidia...

Mjengee mwanao malezi na ujasiri wa kumsadia, sio kumbomoa na kupambana na wanaomzunguka, huo sio upendo katika malezi.
πŸ‘πŸ‘ŒπŸ‘πŸ™πŸŽπŸ’
 
Mtoto wa darasa la 5 ni ngumu kumgomea mwl kufanya usafi shilikisha ubongo kidogo, huyo mwl amempa adhabu ya kikatiri huyo mtoto na kusema kakataa kufanya usafi ni kisingizio tu.

Kivyovyote mama wa mtoto alivyoenda hapo shuleni lzm kulikua na maongezi waliposhindwa kuwekana sawa ndo wakafikia hatua ya kupigana. Kikubwa ninacho wahasa walimu acheni ukatiri kwa watoto wadogo, unapiga mtoto mpaka anashindwa kutembea alafu unataka mzazi nikuchekee??
 
Siku moja nilitoa kichapo kwa mwanafunzi mmoja wa kike wa darasa la kike baada ya kukataa kunipikia chai asubuhi. Baada ya kumchapa viboko kadhaa kwa ubishi wake alikimbia nyumbani kwao kumleta baba yake. Mzazi alikuja amefura hasira mpaka nyumbani kwa walimu eneo la shule akakosa mwalimu yupi amshambulie kwa kuwa walimu tulichanganyikana huku wengine wakiwa ni watu wazima na wenye miili mikubwa iliyojazia. Mzazi alirudi nyumbani kwake huku akitoa ole wake huyo mwalimu aliyemchapa mtoto wake angepigana naye. Tangu siku hiyo niliona isiwe taabu kuwatumia wanafunzi kwenye shughuli zangu binafsi. Kuna mkuu mmoja wa shule ni wa kike alikuwa ni mbabe, mzazi akijitia kiherehere kwenda shuleni kuleta fujo alikuwa anamkwida na kumzabatua makofi na ngumi huku akimuambia anampeleka polisi. Wazazi wengine shuleni hawaji ila watatengeneza manuever kumkomoa mwalimu aliyechapa watoto wao. Mwalimu anaweza kujikuta katundikwa juu ya mti kalala huko usiku wote kimazingara. Wengine hufanyiwa vitendo vya kishirikina usiku
Unaona mialimu mlivyo mi
jinga!!! Unamlazimisha mtoto akupikie chai amekua mke wako huyo??? Shenzi kabisa!
Alafu unajisifu eti nilitia kichapo!
Walimu kama nyie Mimi ndo nawataka sasa
 
Hali ya taharuki imetokea katika shule ya msingi Narumu, katika Kijiji cha Narumu wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, baada ya mama mmoja ajulikanae kwa jina la Valentina kweka, kuingia ofisi ya walimu na kumpiga Mwalimu.

Mwalimu huyo ambaye ni wa kike (jina limehifadhiwa) alijeruhiwa hivyo Kupelekea kutoka damu puani kwa kile kinachodaiwa kuwa ni mwalimu huyo kumchapa mwanafunzi huyo wa darasa la tano fimbo moja kwa kosa la kukataa kudeki darasa.

Mtoto huyo alienda kusema kwa mamake huku akilia ndipo mzazi huyo alipochukua jukumu la kwenda hadi shuleni na kumpiga mwalimu huyo na kumjeruhi.

Aidha mwenyekiti wa kijiji hicho Bwana Ismael Urassa pamoja na diwani wa kata hiyo wamethibisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa tukio hilo limefika ofisi ya kata na linashughukiwa.
Wazazi wa aina hii wangekuwepo shule kama Loleza na nyinginezo
Walimu wangekuwa wamenyooka maana wanatesa mno watoto wa watu kwa fimbo kali mno na adhabu zinazokiuka haki za binadamu.
 
Hali ya taharuki imetokea katika shule ya msingi Narumu, katika Kijiji cha Narumu wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, baada ya mama mmoja ajulikanae kwa jina la Valentina kweka, kuingia ofisi ya walimu na kumpiga Mwalimu.

Mwalimu huyo ambaye ni wa kike (jina limehifadhiwa) alijeruhiwa hivyo Kupelekea kutoka damu puani kwa kile kinachodaiwa kuwa ni mwalimu huyo kumchapa mwanafunzi huyo wa darasa la tano fimbo moja kwa kosa la kukataa kudeki darasa.

Mtoto huyo alienda kusema kwa mamake huku akilia ndipo mzazi huyo alipochukua jukumu la kwenda hadi shuleni na kumpiga mwalimu huyo na kumjeruhi.

Aidha mwenyekiti wa kijiji hicho Bwana Ismael Urassa pamoja na diwani wa kata hiyo wamethibisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa tukio hilo limefika ofisi ya kata na linashughukiwa.
Walimu wanaweza kukuulia mtoto hivihivi yaani fimbo moja wanatuona sisi mafala ninii
 
Huo ni ujinga wangu nliwapa waalimu ruksa staff room wakiwa wote mpaka mwanangu, kama amekosa piga tu bora usiue kama ana kosa. Toka nitoe taarifa ile mwana akiskia uniform huwa safi na kupaswa kila muda, homework vilevile humalizwa on time, yaani alinyooka kabisa.
 
Kuna watu vichaa kumbe nchi hii eti KAZI ya usafi ni ya mwalimu khaa,
Huyo chalii namuombea mungu baadae katika pambana zake za maisha aangukie jkt atajua alifanya kosa kubwa Sana kutokutii amri ya kufanya usafi ya mwalimu
 
Walimu achaneni na watoto wa watu , wewe angalia mshahara na kutimiza wajibu ! Ingia darasani piga pindi sahihisha madaftari yako hajafanya kazi zako ulizompa mwite ongea nae , kesho likirudiwa tena kosa msipigane mafimbo , wewe sahihisha daftari zitakazokuja tu nnachoamini darasa zima kuna watu wanajituma , kuna wasiojituma na wavivu !! Hii inachangiwa pia na malezi nyumbani kwao ! Wewe hakuna unachoweza kurekebisha hapo zama zimebadilika Deal na wanaojituma na anayetaka tu kuelekezwa ! Imeisha hiyo

Serikali haitakufukuza kazi kwa ajili ya wanafunzi kufeli au kuwa na tabia mbaya zaidi tu utahamishwa au kupigwa beat, lakini ukimpiga mtoto akavimba hata mkuu wako atakukana utaenda jela au utaishia kufukuzwa kazi , na kudhalilika !

Malezi ni triangle,inaanza na Wazazi au Walezi kisha Mwalimu na Mtoto mwenyewe ! Ikitokea mmoja ameacha wajibu wake mzigo utakua mzito kwa waliobaki !

Pole mwalimu kwa ngumi.
 
Angenikuta mimi hakika angejuta huyo mama ningemung'oa taya right away, wazazi wabadilike, shule zinaendeshwa kwa utaratibu na kufuata sheria za nchi, mimi kumchapa mtoto naruhusiwa baada ya kupewa idhini na mkuu wa shule, ambapo viboko visizidi vitatu kwa kila kosa.


Pili wazazi watambue kuwa shule ni sehemu salama kwa mtoto kujifunza mitaala ya ziada,mfano kulima,kufanya usafi na kumfanya mtoto ajue mazingira ya kujitegemea,sasa chukulia mtoto nyumbani kazi zote zinafanywa na house girl ,je yeye atajua lini haya majukumu!?

Kingine naona baadhi ya member wanaraumu mtoto kufanyishwa usafi hasa huyu member FaizaFoxy na Islam005 sasa kwa akili ya kawaida mwalimu ndo afanye usafi mazingira ya shule!? Shule zetu za serikali zinajulikana ni supana mkononi,kama hutaki mtoto afanyishwe kazi peleka shule za kulipia kama feza.
Tunakoelekea ni kubaya sana
 
Una uhakika ni kweli alikataa kudeki akachapwa fimbo moja tu? Kabla ya kutoa laana upande mmoja hebu jiridhishe kidogo nini kilitokea.

Nakupa mfano mmoja mdogo, mtoto wa jirani yangu alikuwa mgonjwa wa pumu na alitakiwa asifanye kazi ngumu kwa muda aliokuwa anatumia dozi fulani na taarifa mzazi alipeleka shuleni.

Akaja mwalimu fulani mgeni akaintroduce program ya kukimbia asubuhi kama mazoezi, so kwakuwa yule dogo alikuwa ana kamwili fulani yule mwalimu akajua dogo mzembe tu na akamlazimisha akimbie ili apungue, mzazi alivyoskia vile bado kidogo aje ale kichwa cha yule mwalimu ndio waalimu wengine wakaomba msamaha.

Kumbuka mtoto hawezi kujieleza vizuri ni jukumu la mwalimu kumuelewa haraka kwanini hataki kazi fulani na kuchukua hatua stahiki ila sio kukimbilia kuchapa mtoto kama punda. Rudia tena kutoa comment kistaarabu
Mtoto wa darasa la 5 asiweze kujieleza vizuri huyo kzazi alikurupuka angefika shuleni aulize kilichotokea.
 
Back
Top Bottom