Mpina: 05/2021 Symbion ililipwa bilioni 350 bila kutozwa kodi

Mpina: 05/2021 Symbion ililipwa bilioni 350 bila kutozwa kodi

Bilioni 350 bila kutoza kodi, huku mimi nikituma 30,000/= kijijini kwetu nakatwa tozo.

Haya mambo kama Samia hayajui, au anayajua na kuamua kuyafumbia macho makusudi ndio yanamfanya aonekane alivyo Rais dhaifu.

Kwasababu hata kama kweli hayajui, anapopata taarifa kama hii toka kwa Mpina hakuna anachofanya zaidi ya kukaa kimya na kulea huu wizi, huku wao wakiwaza jinsi ya kumshughulikia mtoa taarifa za wizi.

Mpina kwa sasa ndie mbunge anayejitambua kule bungeni, nampongeza kwa kuamua kwake kujitofautisha na walamba asali wengine bila kuhofia nafasi yake kwenye bunge lijalo, inshort, Mpina ameushinda utumwa wa tumbo unaosababisha kujipendeza.
Raisi anaachaje kujua hilo? Yani Signatory wa mwisho BOT asijue hela ndefu imelipwa vipi ilihali yeye alishasimikwa uraisi?
 
Nchi ina matatizo hii...! Hapana aisee!

Ni lini viongozi wetu wataumizwa na hali mbaya za watu wanaowaongoza

Wananchi wanakufa kisa wamekosa huduma bora hospitalini, Majii safi, njaa, ajali zinazosababishwa na miundombinu mibovu

Ni lini hawa viongozi wataanza kuthamini maisha ya wengine na kwamba pazia linalotuzinga Ni zile nafasi tu, lakini sote Ni binadamu na tuko sawa!!.

Ni Kwa nini tunapomkumbuka JPM kunakuwepo mashambulizi makali saana???

Ni lipi sasa kwenu mmefanya ili basi tumsahau mnayedhani hakufanya kitu?

Ndo kutuongezea mzigo wa kodi?

Ndo kutunyima maji na umeme?

Ndo kutuongezea malipo ya kuingiza umeme majumbani?

Aaaah! Semeni, ni lipi sasa?

Tulizoea kuona kila aliyehusishwa na wizi, alitumbuliwa na wengine kufikishwa mahakamani, Kwa sasa kinafanyika nini sasa.?
Kwa sasa nchi inafunguliwa mkuu, mafisadi wanalipwa na kuondolewa magerezani na wengine kupewa vyeo nafasi nyeti 😂,,,utasikia dume zima linaropoka "Nani kama mama!"
 
Leo nimesikia bungeni kuna kampuni x ilipewa tenda bandarini ya 104 billion na yenyewe ikauza hiyo tenda kwa kampuni x kwa 40 billion wakabaki na 64 billion hizo pesa zimeenda kwa wajanja wakagawana wakavimbisha vitambi vyao kana kwamba nchi hii ya mababu zao..
 
Leo nimesikia bungeni kuna kampuni x ilipewa tenda bandarini ya 104 billion na yenyewe ikauza hiyo tenda kwa kampuni x kwa 40 billion wakabaki na 64 billion hizo pesa zimeenda kwa wajanja wakagawana wakavimbisha vitambi vyao kana kwamba nchi hii ya mababu zao..
Kiongozi anayekenua meno kwa mambo ya aina hio ndio haswa anapendwa huko NEC na CCM utawala kwa ujumla. Ukizuia haya tu unaitwa dikteta unayeua uchumi.
 
Jamaa anahangaika na Tozo na muda mwingine utawaona TRA wamejibanza wanakamata watu wasio na Risiti wakati yapo majambazi tena yanapewa na maji ya kunywa kabisa na kodi hayalipi na hakuna atakaeongea hizo mambo unakutana nazo kwenye Ripoti ya CAG ambayo pia ni taarifa tu ila haina nguvu ya kuwawajibisha wakosaji na wezi kama hao yaani wao wanaishauri tu Serikali isiendelee kuibiwa..
 
Sasa mtu anayesimamia Tanesco ndio huyo Makamba, tutegemee maumivu zaidi
conflict of interests hazijawahi kuisha hapa nyumbani Tanzania....... si bado tunamkumbuka yule kiongozi shujaa aliyewaita watengeneza ndege na kukaa nao chumbani bila kufuata sheria yeyote ya manunuzi?
50% ya ndege moja ni shilling ngapi? tulihoji kwann sheria ya manunuzi haijafuatwa au TULIKUBALI KUJINGISHWA NA KUSHANGILIA MINDEGE ILE?
Leo twahoji kwasababu ni kina January Makamba?
 
Magufuli hakugusa mwizi hata mmoja wa maana, alikua anadeal na vidagaa kwa kelele nyingi, lakini hakuna fisadi hata mmoja alimgusa. Kamkamata Singa na Rugemalira, lakini kawaacha wanasiasa wenzake ambao ndio walikuwa watoa maamuzi. Inshort alikuwa ni mpenda sifa za bei rahisi.
Bora huyo alijaribu hata kuwagusa kina Singa singa na hayo malipo hungeweza kuyasikia enzi zake lakini siyo hawa wapendwa wako
 
m

na ile ya kununua ndege ili sainiwa wapi na lini? kulifuatwa sheria gani za manunuzi kwenye ununuzi wa zile ndege? ujenzi wa uwanja wa chato kuna sheria yeyote ya manunuzi ilifuatwa?
mbona hamkukenua midomo yenu na kusema? acheni nongwa sukuma gaang wapumbavu
Naona mvaa kobazi una mtetea sana huyu bibi yako mpendwa katika imani.

Waone huruma wazazi wako wanaoliwa na umasikini basi! Uchawa wako kwa bibi hauwasaidii kitu
 
Mbunge Luhaga Mpina amehoji ni kwa nini kampuni ya Symbion ililipwa pesa zaidi ya bilioni Mia tatu bila kutozwa kodi ya Serikali?

Amehoji pia ni kwa nini mkataba wa symbion uliokuwa unakoma 2015 ulihuishwa September 2015 bila kufuatwa taratibu na ajabu Serikali kwa uharaka ilikubali kuilipa Symbion Mei 2021 na bila kutozwa kodi?

Amehoji inakuwaje C.A.G ameshasema mkataba ule uliingiwa kimakosa na kwa nini aliyeuingia kimakosa hawajibishwi na matokeo yake Symbion amelipwa pesa za Watanzania maskini pasipo kufuatwa utaratibu?

Mtasikia rushwa na habari za rushwa huko na huko. Msifadhaike, kwamaana siku zao zitaendelea kufupishwa.
 
conflict of interests hazijawahi kuisha hapa nyumbani Tanzania....... si bado tunamkumbuka yule kiongozi shujaa aliyewaita watengeneza ndege na kukaa nao chumbani bila kufuata sheria yeyote ya manunuzi?
50% ya ndege moja ni shilling ngapi? tulihoji kwann sheria ya manunuzi haijafuatwa au TULIKUBALI KUJINGISHWA NA KUSHANGILIA MINDEGE ILE?
Leo twahoji kwasababu ni kina January Makamba?
Unawatetea kwavile ni wenzako katika imani?

Mpumbavu kweli wewe!
 
Bilioni 350 bila kutoza kodi, huku mimi nikituma 30,000/= kijijini kwetu nakatwa tozo.

Haya mambo kama Samia hayajui, au anayajua na kuamua kuyafumbia macho makusudi ndio yanamfanya aonekane alivyo Rais dhaifu.

Kwasababu hata kama kweli hayajui, anapopata taarifa kama hii toka kwa Mpina hakuna anachofanya zaidi ya kukaa kimya na kulea huu wizi, huku wao wakiwaza jinsi ya kumshughulikia mtoa taarifa za wizi.

Mpina kwa sasa ndie mbunge anayejitambua kule bungeni, nampongeza kwa kuamua kwake kujitofautisha na walamba asali wengine bila kuhofia nafasi yake kwenye bunge lijalo, inshort, Mpina ameushinda utumwa wa tumbo unaosababisha kujipendekeza.
Ninakubaliana na wewe kwa yote uliyoandika hapa, isipokuwa hilo moja la kumfanya Samia awe pembeni mwa mchezo wenyewe, huku yeye ndiye akiwa nahodha.
Huwa nashindwa kuelewa kwa nini watu wenye uelewa mzuri kabisa wa mambo kama wewe, inapofika sehemu ya kulaumu anayestahili lawama huwa inawawia vigumu sana kufanya hivyo.
Badala yake mnabaki kupapasa tu pembeni.
 
Mbunge Luhaga Mpina amehoji ni kwa nini kampuni ya Symbion ililipwa pesa zaidi ya bilioni Mia tatu bila kutozwa kodi ya Serikali?

Amehoji pia ni kwa nini mkataba wa symbion uliokuwa unakoma 2015 ulihuishwa September 2015 bila kufuatwa taratibu na ajabu Serikali kwa uharaka ilikubali kuilipa Symbion Mei 2021 na bila kutozwa kodi?

Amehoji inakuwaje C.A.G ameshasema mkataba ule uliingiwa kimakosa na kwa nini aliyeuingia kimakosa hawajibishwi na matokeo yake Symbion amelipwa pesa za Watanzania maskini pasipo kufuatwa utaratibu?
Daaaaaaaaaah.
 
Unawatetea kwavile ni wenzako katika imani?

Mpumbavu kweli wewe!
imani yangu na upumbavu wangu vimeingia vipi hapo? huw naogopa kujenga hoja mbele ya mtu mwenye ujinga wa kihalaiki kama wewe. jenga hoja MATUSI HAYATAKUSAIDIA
Nimetukanwa tangu nukiwa tumboni mpaka vyuo vikuu lakini sijawa MJINGA WA KIHALAIKI usiyejipa muda wa kutafakari kama wewe
 
Back
Top Bottom