Mrejesho: Biashara ya Nyumba za Kupangisha Vs Nyumba za Kulala Wageni

Mrejesho: Biashara ya Nyumba za Kupangisha Vs Nyumba za Kulala Wageni

Hiyo line yako ya mwisho kuna wengine wateja hawapendi pulukushani za kelele sasa ukishaanza kuuza Pombe, supu, chakula hiyo sasa inakua sio lodge hata mazingira wateja wanaweza kimbia wale wastaarabu. Alafu ukiweka hivo vitu inakua lodge ya wahuni shortime, uchafu. Labda aweke ki bar nje ya lodge huko ambapo mteja akiitaji chakula inakua sio mbali kukifata na kelele za watu/miziki haziingii lodge.

Maana kuna logde zingine zenye bar ni kelele sana likipigwa "IN DA CLUB" la 50 cent unaweza hisi umo ndani chumbani kitanda kina dance imagine mziki huo mpaka saa saba au nane usiku huko na unataka kulala.

Lodge wewe weka vitu vya kawaida pale reception kama miswaki, maji, dawa ya mswaki, vitu vile vitakavomvutia mteja maana ni wa kulala na kuondoka.

Ukianza kuweka sijui chakula, pombe, mziki e.t.c hiyo sio lodge ni bar wateja utakaopata ni wahuni na kukuharibia lodge yako.

Muhimu kujali wateja wako. Wateja wengine asubuhi wanakula breakfast, saa nne wanakutana na washikaji wanaongea kidogo wanaenda kumaliza dili huko.

Wakirudi saa tisa, kumi wanakamilisha maongezi yao. Hapo wanaweza kuomba supu, nyama choma, nk wanaachana saa kumi na mbili. Ila mziki ni hapana. Hautakiwi kabisa.
 
Hizo hidden camera watakuwa hawazioni Kwa uwazi kama hizo camera nilizokwisha kuzifunga? Zinakuwaje?
Hawawezi kuzijua, tena unawaambia kabisa hiki ni kifaa cha kujua kukiwa na moshi, moto, vingine ni kama taa au saa za ukutani.
1706801063391.png

1706800680190.png

1706800870276.png
 

Attachments

  • 1706801027211.png
    1706801027211.png
    37.9 KB · Views: 6
Daah hii mtu anaweza kuweka akawa anapiga chabo wateja wake..not good! Watu wawe makini sana wanaweza kuchukuliwa matukio bila kujijua

Ni ukweli, hivyo vimefanyika sana nchi zingine halafu wanauza video. Wengine wakiingia chumbani wanakagua kila kitu TV, taa, electonics gaps zozote zisizoeleweka kwa nini vipo pale.
 
Ni kweli ulichosema kuwa Layman wengi huwa ni risk taker kwenye Uwekezaji.

Ila pamoja na hivyo, lakini wanakuwa na watu proper wenye taaluma kwenye maeneo tofauti.

Ndiyo maana Bills of Quantities (BoQ) inajazwa na wataalamu ili kuona price anayokoti basi itamlipa.

Huwezi kufanya Mradi bila kujaza Bill zako, kupitia hiyo ndiyo utajua anapata Faida ama laa

Na mara nyingi kama Mradi hauna Faida Wakandarasi wengi huwa hawaombi.

Mimi pia nipo kwenye hii Sekta ya Ujenzi
Wasomi ni waoga sana wa kutake risk, wao wanacalculate risk kabla hawajatake risk, huku Mgodini tuna Msukuma mmoja aliuza kila kitu ili kuhudumia duara lake mpaka mke alitaka kumkimbia, but toka mwaka Jana mwezi wa sita hadi Leo shimo lake linatema na anauza mawe mfuko wa azam wa kilo 25 anauza sh.700,000, kwa wiki anaingiza zaidi ya mil 160.
 
Wasomi ni waoga sana wa kutake risk, wao wanacalculate risk kabla hawajatake risk, huku Mgodini tuna Msukuma mmoja aliuza kila kitu ili kuhudumia duara lake mpaka mke alitaka kumkimbia, but toka mwaka Jana mwezi wa sita hadi Leo shimo lake linatema na anauza mawe mfuko wa azam wa kilo 25 anauza sh.700,000, kwa wiki anaingiza zaidi ya mil 160.
Ni kweli Mkuu, sifa Moja wapo ya Mjasiriamali ni kuwa na uwezo wa kutake risk.

Kuna jamaa alikopa Mkopo Benki Kwa dhamana ya mshahara wake kisha kuacha kazi na kuingia kwenye Ujasiriamali.

Kwasasa ana Ukwasi wa zaidi ya bilioni 5 hadi 10 maana alijikita kwenye biashara ya kuagiza vifaa nje na kuja kuviuza Bongo
 
Faida ya kusajiri kampuni ni nyingi. Lakini hata kama huna kampuni (sole trader) gharama zote ulizotumia na risiti unazitunza. Baadaye unaziweka kama expenses. Vitu vingi sana vinaingia kwenye expenses. Mishahara yote, umeme, maji, gharama nyingine. Ukarabati wowote, hadi mafuta ya gari, nauli, chakula zikiwa na mahusiano ya kazi. Zinawekwa kwenye gharama (expenses). Zinapunguza kodi pakubwa.
Shukrani Kwa Madini yako Mkuu

Hapo jambo la kuzingatia kumbe ni kutunza risiti, Wacha nikazitafute zote kuanzia zile za kununua Mabati/Malumalu n.k

Ishu ya Mafundi itabidi niandike nao Mkataba sio?
 
Ni kweli Mkuu, sifa Moja wapo ya Mjasiriamali ni kuwa na uwezo wa kutake risk.

Kuna jamaa alikopa Mkopo Benki Kwa dhamana ya mshahara wake kisha kuacha kazi na kuingia kwenye Ujasiriamali.

Kwasasa ana Ukwasi wa zaidi ya bilioni 5 hadi 10 maana alijikita kwenye biashara ya kuagiza vifaa nje na kuja kuviuza Bongo
Mzee Graham's ninampango wa kuja huko chunya kuchukua karasha nadhani nitaangaza angaza lodge mpya ya 30k nilale humo may be ikawa yenyewe.
 
Sio waaminifu kuanzia receptions hadi walinzi hata wamasai siku hizi labda professional companies kama Suma Jkt. Wasipokuibia mapato watawaibia wateja sana.

Kuna trick wanafanya mfano madirisha huwa hayawi locked. Usiku umeme ukikatika walinzi wakishirikiana na vibaka kwa kutumia kama fimbo hivi ndefu ya chuma wanachukua nguo na begi hasa kama vipo karibu na dirisha.

Nyingine ni kuwaambia wateja wakitoka nje waache funguo reception, halafu wanapitia vitu vyao.

Dawa ni kuwa na umeme 24/7 na mfumo thabiti wa CCTV kuizunguka nyumba pande zote, reception na corridors. Unaweza kuwa na mifumo miwili mmoja hata wafanyakazi wote hawaujua ni wewe tu unaojua unakuwa kama taa za kawaida lakini ni camera na mwingine wanaoujua.
✅ noted
 
Uzi nzuri Sana ..naomba kuongezea...

Kuhusu wizi tumia technology..nenda jukwaa la IT wakueleze kuhusu vitasa vya card. Na software zake iwe chumba kikipata Tu mgeni unapata notifications hapo hapo...hata kama wa short time.....

Kwingine since wewe ni mpya kwenye biashara nashauri Fanya research ya lodge zilizo kufa au kukosa soko ikiwezekana uzi Kodi upige hela ..

Wengi wanashindwa maintenance Tu...sasa badala ya wewe kutumia hela nyingi kujenga zingine ...jaribu kukodi Kwa mkataba mrefu ..itakusaidia vitu viwili....kwanza utapunguza competition since competition umeinunua...pili utantumia hela ndogo for expansion...

Unaweza amini kkoo kuna hotel inakodishwa Kwa milioni 4 Tu Kwa mwezi wakati ni jengo la ghorofa 8..?

kisa muasisi kafa na watoto wanakula hela yote hawafanyi maintenance..

All in all nakutakia all the best miaka miachache kutoka sasa uwe na lodge hata tano...
Great idea 👏👏
 
Mzee Graham's ninampango wa kuja huko chunya kuchukua karasha nadhani nitaangaza angaza lodge mpya ya 30k nilale humo may be ikawa yenyewe.
Karibu sana kwenye biashara ya Uchimbaji.

Ukiwa na bahati huwezi kukosa millioni millioni, muhimu Kwa miezi ya awali uwe na funds za kukuwezesha ku-run biashara walau miezi 6 hadi 12 bila kutegemea fedha ya duarani.
 
Lodge zina hela sana, kuna moja mchana inajaa waiba wake za watu na usiku inajaa bei ni 30000 kwa 35000.
Hahaha.....eti Waiba wake za watu 😜

Huoni wanapunguziana majukumu na Mume mwenza....maana Wanawake Wanacheza sana Vikoba hivyo wanakuwa na watu wa kuwasaidia kulipa 😜🏃🏃🏃🏃

Ni biashara nzuri na inalipa hasa, ukipata sehemu nzuri, utajikuta Kila Siku inajaa tu
 
Back
Top Bottom