Mrejesho: Biashara ya Nyumba za Kupangisha Vs Nyumba za Kulala Wageni

mkuu kama itakupendeza nitumie picha dm yangu maana mimi nilikuwa mbioni kujenga lodge baada ya wapangaji kunisumbua sana ila mimi nilitaka kuweka mfumo wa slab ili ikikuwa naongea kwa juu tu
Kujenga Kwa mfumo huo angalia kwanza uimara wa nguzo zako kama wali-design kubeba mzigo huo.

Vinginevyo bomoa uanze upya ama kufanya underpinning ili ku-stablize jengo lako ili kuruhusu hicho unachopanga kufanya.
 
kwa kweli mkuu umenipa moyo sana maana nyumba za kupanga ni usumbufu mkubwa sana na bado itachukua muda mrefu sana kurudisha garama zako
Nina nyumba nimepangisha, kutokana na gharama nilizotumia kujenga nimebaini itachukua miaka 15 Hela yangu kurudi.

Hata hivyo naiacha as naitumia kupata ada za Vijana wangu Kwa uhakika
 
Asante Mkuu

Watanzania wengi sio waaminifu

Baada ya kuichezea Camera saivi analeta hela anayojisikia maana anasema Leo wamelala wateja 7 kumbe wamelala 9

Nimetengeneza mara 3 lakini baada ya muda inaharibika Tena.

Nina hakika ningekuwa nakaa mwenyewe huenda Payback period ingeshuka hadi miaka 2

Maana nahisi napoteza Mapato mengi Kwa Wizi wao Hawa Vijana
 
Umesema sahihi Mkuu

Tuendelee kukomaa tu
 
Kwa pesa hiyo ungeanzisha Restaurant ya maana na kupata wapishi wazuri ungepata faida na pesa zako zingerudi haraka na faida kubwa
Mwanzo unakuwa mgumu lakini baada ya muda utaona faida.
Inategemea pia eneo la biashara na mzunguko wa pesa.
Restaurant ukiweza kuiendesha vizuri hukosi laki 3 mpaka 5 kila siku.
Nafanya biashara hiyo Arusha
 
Asante Mkuu, ila Benki zinasumbua sana kwenye kutoa Mikopo Kwa biashara mpya.

Kuna haja Wizara ya Fedha/Benki Kuu wakalegeza masharti kwenye hizo Taasisi za Kibenki

Vinginevyo ndoto za Wajasirimali wengi zinakufa
Hongera sana mkuu suala la benki jaribu kuongea vizuri na meneja Tanzania hakuna kinachoshindikana
 
Asante Mjukuu

Wanasema Mwanzo mgumu ila ukitia nia unaweza kufanikisha japo unaweza kuchukua muda

Kuna Siku nilipata Wageni dizaini hiyo unayosema ya watu 8 na walikaa wiki 1.

Unakuta Kila Siku mzigo unasoma SIM banking 😅
 
Biashara ya chakula nitaifanya iambatane na Vinywaji.

Nataka nijenge dizaini ya Kitambaa Cheupe ama Bambalaga
 
Tuwekee na ramani ya hiyo project mkuu!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…