Mrejesho: Faida nilizopata baada ya kuwatoa watoto wangu shule ya English Medium na kuwarejesha kayumba

Mrejesho: Faida nilizopata baada ya kuwatoa watoto wangu shule ya English Medium na kuwarejesha kayumba

Ila maisha yanaenda haraka sana, kipindi chetu tunaingia sekondari miaka ya themanini mwishoni, kusoma private ilikuwa aibu maana ni kwa wale waliofeli, leo kusoma huko ni fahari, kisa kiingereza na ada kubwa. Tumejiwekea social classes kutumia hizi shule, ambaye hana uwezo naye anajifaragau aoneka yumo wakati huo anateseka. Mwisho wengine wanakuja kuuza baa na vikiingereza vyao. Shule mtoto anatakiwa apige vizuri Hisabati na masomo ya sayansi yakiwemo ya uchumi na biashara hayo ndiyo maisha siyo lugha ya watu, bado ni utumwa tu.
Inategemea private zipi ilikuwa aibu shule kama shaaban robert, aga khan mzizima hizi nazo ilikuwa aibu?
 
Miezi michache iliyopita nilianzisha Uzi hapa jf wenye title" Tunao watoa watoto wetu shule za English Medium na kuwarejesha kayumba njooni tufarijiane hapa"

Lengo la Uzi lilikuwa kupata watu watakao nipa " faida" nitakazo zipata kwa kuwarejesha watoto wangu Kayumba plus maneno ya kunifariji ambayo yatasaidia kujustify uamuzi wangu.

Sababu ya kuwarejesha kayumba wanangu ni kuyumba kiuchumi. Nilipata maoni mengi mazuri. Miongoni mwa maoni niliyopata hapa JF ni pamoja na:

1. Itanisaidia kuokoa pesa ambayo ninaweza ku invest katika maeneo mengine muhimu kama vile kuwanunulia viwanja na kuwajengea nyumba watoto wangu so that wanapo fika level ya chuo at least kila mtu awe na nyumba yake moja.

2. Sintokuwa na stress za ada plus mbaya kuliko zote( ile stress maalumu ambayo mzazi unaipata wakati mtoto wako amerudishwa nyumbani ada, wakati wenzake plus jirani zako wanao soma kayumba wanaenda shule.


Nje ya JF nilipata ushauri kutoka kwa

1. Binti yangu ( yeye yupo form three shule ya kayumba pia. Nilimsomesha English Medium kuanzia la kwanza. Anasema daddy kuna watoto wamesoma shule za kiswahili lakini wapo vizuri sana darasani kuliko walio soma shule za kiingereza.

3. Brother wangu wa mtaani ambae na yeye kawarudisha watoto wake kayumba.. (huyu kasomesha hadi chuo but still bado ana watoto wa primary. Alikuwaga kichaa wa shule za English medium.

Anasema mdogo wangu mtoto wako umsomeshe kayumba au English Medium mwisho wa siku wote watakufa watazikwa" anataja jina la makaburi ya mtaani kwetu"

Akaongeza: Tofauti ya kayumba na English Medium ni lugha tu lakini mwisho wa siku wote wanaandaliwa kuajiriwa..


Kingine siku hizi watoto wanaharibika sana so hakuna guarantee mtoto wako atakuja kuwa nani hapo baadae.

Akaongeza " shule nyingi za English Medium zinawafanya wanafunzi hasa watoto wa kiume kuwa watoto walaini laini ( ana experience na watoto wake mwenyewe na rafiki zake)

Halafu haziwafundishi watoto kuhusu uhalisia wa maisha zaidi ya kuwakaririsha masomo so bora umpeleke kayumba akapambane na kukomaa huko.


MIEZI MIWILI BAADA YA KUFANYA UAMUZI.
Nimenunua kiwanja nje ya mji ( ilala rural/ mvuti) kwa sh.laki tisa na mwezi ujao Insha'allah nitapiga msingi( fundi wangu yupo kinondoni ambae alinijengea nyumba yangu ya kwanza utaratibu wake wa kazi huwaga ni" wewe ukiwa na hela yoyote hata laki TANO niite kwa lako TANO hiyo hiyo nitafanya kitu . Next time ukipata laki tatu niite. Hadi nyumba yako itakamilika. Huyu ndo alinifanya nikajenga nyumba yangu ya kwanza. Tukiwa Kino garden au hananasif tunaangalia ndondo anapokea simu za watu anao wajengea nyumba anasema ' huyu anauza mchicha' huyu mama lishe, etc. Nikawa inspired.

Kuhusu somo la kiingereza: nimenunua vitabu na cds ambayo madogo watakuwa wanajifunza wakiwa home plus tuition ya nguvu ya kiingereza.

Mungu akinipa uhai nitafanya vitu vikubwa sana kwenye familia yangu.

Kama uwezo wako mdogo, unaishi nyumba ya kupanga uswahilini, uchumi wako umeyumba, sikushauri uhangaike na English medium.

Mpeleke mwanao kayumba wewe upambane kutafuta hela.
Umefanya la maana,mimi pia nimewashauri wengi kufanya hivyo.Bora kwajengea watoto nyumba zakuwasaidia.Hata we.we hizo nyumba,zitakusaidia.
Unakaa nyumba ya kupanga,halafu unalipa mamilioni ya ada za shule.Wenye shule wanajenga majumba,wewe unabakia na mavitabu ndani ya nyumba.Kila mwaka wanataka ununue vitabu vipya,ukiwa na watoto wanne,wanasoma private,lazima upate presha tu.
 
Hata mimi kipato kilipokata nikatoka kwenye steki na soseji nikaingia kwenye dagaa wale wanaokaangwa barabarani, nikawasifu sana kwa utamu wake na ubora wake kwa kurumangia dona.
Safi sana hamna kukaa kinyonge🤣😂
 
Fanya kitu kulingana na uwezo wako. Pia calculate risks kabla ya kufanya kitu chochote. Jiulize mpango wako wa fedha ukoje kwa miaka 7 ijayo ya mwanao huko English medium. Ukiona huelewi peleka St Kayumba. Kusema kwamba English Medium wanatoa watoto mayai ni zile stori za sizitaki mbichi hizi...
 
Nyerere, Mwinyi, Mkapa na Kikwete walisoma silabasi ya uingereza na mitihani ilitoka Kembriji, ilisahihishwa Kembriji na matokeo yalitokea Kembriji.
.
Sahihi Wengine humu wanajifariji wanadhani hao maraisi walisoma kayumba walisoma shule za private msingi tena za kulipia kama za private za sasa hivi
 
Hapana, hazikuwa za praiveti bali mfumo wa elimu enzi hizo ulikuwa ni wa uingereza.
Zikikuwa private za dini za katoliki, Anglican ,Agha Khan nk serikali ya kikoloni haikuwa na shule za Serikali ilileta tu syllabus na mitihani ya Cambridge

Mkoloni hakuwa na shule hata moja ya serikali
 
Naunga mkono hoja asilimia mia.
Shida inapokuja unataka kuishi kama tajiri wakati ni masikini. Una fake maisha.
Shule za wenye hela, na wewe unapata vihela vihela unataka upeleke shule ya wenye hela matokeo yake unaishia kwenye madeni na kuwarudisha nyumbani.
Kuna watoto wazazi wao wanasowasomesha Fedha boys, akimaliza anaenda kusoma chuo nje ya nchi.
Tusifake maisha, ishi kwa uhalisia wako. Ukimpeleka za wenye hela lazima siku moja uumbuke.
Usijifariji kwasababu umepata faida, sema hauna hela. Kuna watu watoto wao wako kwenye shule za hela, na maendeleo anafanya na hakopi wala hawawazi ada. Amini hilo
 
Umefanya la maana,mimi pia nimewashauri wengi kufanya hivyo.Bora kwajengea watoto nyumba zakuwasaidia.Hata we.we hizo nyumba,zitakusaidia.
Wazazi wengi wenye mawazo yako walijikuta mbele wanakwama Ohh nawajengea hizi nyumba wanangu hapa kijijini

Watoto wanapata kazi mikoa au wilaya nyingine au mikoa mingine au nje ya nchi na hawana mpango wa kurudi kwenye hivyo vijumba viko chini ya kiwango cha kisasa vilivyoko kijijini au nje ya mji huko visivyo kwenye fashion ya kisasa viwe vighorofa nk

Watoto somesha vizuri the rest watajaza wenyewe mbele ya safari kama nyumba wao ndio wajenge nyumba wapi ndani ya nchi au nje ya mjini au kijijini ya kiwango gani na fashion ipi kwa wakati wao watakao kuwa nao

Huwezi kubeba hadi maamuzi yao ya future .Wewe kazana kusomesha elimu nzuri tena mno .Future waachie wenyewe Usiingilie hadi huko
 
Kwa dunia ya leo hakuna sehemu salama kwa watoto ila kusema kweli Kayumba ni hatari zaidi jamani.
Kwanza shule nyingi za Kayumba zina watoto wengi kiasi kwamba kuna watoto wanatoa makwao ila wanaishia vyooni na njiani darasani hawafiki na mwalimu hajui.Mtoto anaweza kaa mwaka hajaingia class.
Kayumba watoto wanafanyana vitu vibaya chooni na njiani.

Kayumba mwanao anacheza na watoto wanaotembea umbali mrefu kwenda na kurudi shule na huko njiani wanajifunza mambo mengi mabaya.

Kayumba tupeleke watoto ikiwa hakuna namna ila kama ka uwezo kapo tafuta shule nzuri ya kulipia fanyia research tabia za watoto wa hapo ukiridhika mtoto asome hapo.
Muache mtoto ajichanganye na watoto wengi ili wampe changamoto. Kuna baadhi ya shule za private darasani kuna wanafunzi wanane mtoto anakuwa bwege halafu anakuwa bored pia.


Dunia ni mbaya na ina watu wabaya. Huo ndio uhalisia wa dunia. Kumuweka private kwa sababu hutaki akutane na uhalisia wa dunia ni kufanya kama mbuni, anajificha macho ili asimuone adui yake halafu anaacha matako wazi.

Akitoka shule atakuja kukutana na huo uhalisia ambao ulikuwa hutaki au experience ilhali wenzake tayari wamesha u experience

Muache mtoto ajifunze kuhusu uhalisia wa maisha yeye mwenyewe. Kuna jamaa mtoto wake kaanza kupanda mwendokasi yupo darasa la kwanza anatoka kimara anaenda gerezani.
 
Kumbe? 🙌 Ni hatari aisee
Unajua sisi masikini huwa tunajifariji sana tusionekane tumeshindwa au hatuna hela. Utasikia yeye anaishi kwenye ghorofa mimi kwenye nyumba ya kawaida ila usingizi ni ule ule.
Hapa duniani kuna watu wanaishi na wengine wanapambana ili waishi.
Kuna watu watoto wao wanasoma kwenye shule za hela, maendeleo anafanya, akimaliza mtoto anaenda kusoma nje ya nchi km Canada. Sisi masikini ukipata hela, una fake maisha ili uonekane na wewe una hela.
Kuna watu wanakaa hoteli ya nyota 5 mwaka mzima akifanya shughuli zake yaani kifupi hela kwake siyo tatizo.
Huyu bwana hakuwa na hela ila alifake maisha aonekane na yeye ana hela matokeo yake akarudi kwenye uhalisia.
Kuna watu wanahela na hela kwao siyo tatizo.
 
Shida inapokuja unataka kuishi kama tajiri wakati ni masikini. Una fake maisha.
Shule za wenye hela, na wewe unapata vihela vihela unataka upeleke shule ya wenye hela matokeo yake unaishia kwenye madeni na kuwarudisha nyumbani.
Kuna watoto wazazi wao wanasowasomesha Fedha boys, akimaliza anaenda kusoma chuo nje ya nchi.
Tusifake maisha, ishi kwa uhalisia wako. Ukimpeleka za wenye hela lazima siku moja uumbuke.
Usijifariji kwasababu umepata faida, sema hauna hela. Kuna watu watoto wao wako kwenye shule za hela, na maendeleo anafanya na hakopi wala hawawezi ada. Amini hilo


Uko sahihi sana watu wanalazimisha shule sio za level zao.

MO DEWJI alosomeshwa IST sababu ndio uwezo wa familia yao utajiri mkubwa ulikuwa upo kwenye familia yao. Hakuwai kusimamishwa asiende shule kisa ada.

Na wala baba yake hakuwai kwenda kukopa hela ya Ada ili amlipie Mo dewji IST.

Mo dewji hakuwai kuzunguka na bahasha kutafuta ajira ama kazi

MO DEWJI WAKATI YUPO A LEVEL ( HIGH SCHOOL ) baba yake alikuwa ananunua shirika la National milling kutoka kwa serikali kwa mabilioni ya pesa.
 
Unajua sisi masikini huwa tunajifariji sana tusionekane tumeshindwa au hatuna hela. Utasikia yeye anaishi kwenye ghorofa mimi kwenye nyumba ya kawaida ila usingizi ni ule ule.
Hapa duniani kuna watu wanaishi na wengine wanapambana ili waishi.
Kuna watu watoto wao wanasoma kwenye shule za hela, maendeleo anafanya, akimaliza mtoto anaenda kusoma nje ya nchi km Canada. Sisi masikini ukipata hela, una fake maisha ili uonekane na wewe una hela.
Kuna watu wanakaa hoteli ya nyota 5 mwaka mzima akifanya shughuli zake yaani kifupi hela kwake siyo tatizo.
Huyu bwana hakuwa na hela ila alifake maisha aonekane na yeye ana hela matokeo yake akurudi kwenye uhalisia.
Kuna watu wanahela na hela kwao siyo tatizo.
wataje hao watu so that we be sure ur not talking about ghosts
 
Back
Top Bottom