Mrejesho: Nimepata mume kutoka Jamiiforums

Mrejesho: Nimepata mume kutoka Jamiiforums

Mkuu, jaribu kutoonyesha hiyo rafudhi ya kikurya
Wara = wala
Hatujari = hatujali
Tunasubiri = tunasubili
Kumradhi.
=Tunasubiri
Mkuu nilimsahihisha mtu then nikamtania kwa hiyo lafudhi. Niko mbali sana na hayo matamshi.
 
nisitie neno hapa ngoja nipite na zangu. Mtu yupo kwenye mchakato wa ndoa lakini keshajua aliyenae ni mume bora.... Hii ndio jf bhana Jimena wangu angalia hapa
Lakini kaka Ibra mbona unataka kumuogopesha mwenzio?
 
Less than a year mmeshafahamiana vya kutosha mpaka kutaka kufunga ndoa. Mtoa mada joined JF June 2015 Kila la heri wapendwa! Yawezekana kumbe
Wapo wanaokaa hata miaka 5 baadae wanamwagana hiyo haina formula kabisa mkiridhikana mnaoana siyo mambo ya kupotezeana muda baadae mnapigana chini kimasihara. Mimi mwenyewe natafuta nikimpata hata kesho natangaza ndoa nshapoteza muda sana.
 
Habari zenu,

Nilileta habari ya kutafuta mume soma; Nimechoka kumsubiri, nahitaji kuolewa Napenda kuwashukuru wale wote milojitokeza kwa nia nzuri au mbaya na kubwa namshukuru Mungu wangu kwa nikipatia mume bora, kutoka hapahapa JamiiForums, nilimpata mume na karibuni tutafunga ndoa. Mtakaribishwa tena kwenye harusi yetu.

Asanteni wote
Mkuu hongera sana japo wapo wanaobeza lakini naamini wengi ni wivu tu na kukata tamaa hawaamini kama unaweza kumpata mme au mke hapa jf au kumpata kwa haraka kihivyo kutokana na maigizo waliyoyazoea. Kukaa na mtu miaka 2, 3, 4 eti mnachunguzana ndo chanzo cha kupotezeana muda na kuachana kwa sababu rahisi sana na wala haijalishi kwamba ndo lazima muoane, wengi wamepotezewa muda nikiwemo mimi na baadae unaanza na moja sasa utumie tena miaka 4 kudate na mwingine?. Nawashauri vijana wenzangu akitokea mdada/mkaka kakupenda na anahitaji kuoa/kuolewa usipoteze muda mrefu kuchunguzana miezi mitatu hadi sita inatosha sana hujamkubali ndani ya muda huo achana nae sio kila siku unaextend probation. Ata mchunguzane miaka 10 siyo tiba ya kumpata mwenza bora kwanza ni dalili ya mashaka mashaka na huyo mtu labda kama umri wako haujatimia. Kuna tabia nyingine zinaibuka kutokana na wakati na mazingira cha muhimu ni nyinyi kurekebishana na kutanguliza mapenzi.
 
Nadhani mpaka mlipofikia hakuna haja ya kuficha ID yake,ungeiweka hadharani maana JF hii ni pana kuliko uijuavyo.
Unaweza ona umepata kumbe kuna wenzio wanadanganywa hivyohivyo huko PM's na kujiona wamepata.

Na hasa ogopa ID's mpya...JF ya sasa wageni ni wachache,wengi ni walewale ila wana ID's zao mpya au za kazi zao maalum.

Huu ni ushauri tu,take it or leave it....
Kila la kheri.
Atakuwa ni kaka yako aliye tukuka...Teh Teh..sipati picha..
 
Atakuwa ni kaka yako aliye tukuka...Teh Teh..sipati picha..
Ha hahahahaaa aisee nimecheka sana.
Wewe muache,hii ndio JF bwana.
Isijekuwa ndio maana popoma haonekani siku hizi kama kawaida yake,kumbe yuko busy na Le Mbebez.....
 
Mapenzi ni sawa na maua........popote huchanua! Hongera sana mamy.
 
Kukuuliza swali ndo unijie moto kama mwiko wa pilau, kwa haya majibu unaonekana jinsi ulivyo empty huko kichwani......na hata huyo unayemuita mume bora yuko anakuchora tu jinsi 'mke bora' ulivyo na majibu ya chooni. Good luck.
naona mtoa mada anakua mkali endapo atakosolewa au mtu akimzingua kidogo
kwa attitude hii ndoa inaweza kua chungu, maana kuishi na mtu huyohuyo kwa miaka 30+ chini ya paa moja kunahitaji tolerance sana
 
Back
Top Bottom