Msaada: Kichwa kinawaka moto kwa mawazo, nakosa usingizi

Msaada: Kichwa kinawaka moto kwa mawazo, nakosa usingizi

Nahisi unamatatizo ya afya ya akili,waone wataalamu wakusaidie,kupata supplementary sidhani kama ni tatizo kubwa la kufanya ufikirie kijiua hasa Kwa tuliopita vyuo ni jambo lipo la kawaida.Nikushauri pia jitahidi kusocialize na watu usipende kukaa mwenyewe na kujifungia,jichanganye japo maskani za hapo mtaani kwenu piga story na washkaji ongea Cheka relax,tafuta mwanamke mwingine awe karibu yako atakutoa upweke(proved).pole sana usiruhusu hiyo hali itawale maisha yako.

Hyo hali ilinianza kubla ya kuishi na huyu binti baada ya kupata supplementary 2018
 
Nilimuacha dem wangu dar pisi kali kinoma nikaja mkoani kujitafuta siku zilivyokua zinazidi kwenda mawasiliano yakawa yanapungua inaweza pita siku hatujawasiliana, nikajiongeza nikaamua kumfungia vioo nayeye akafanya the same nikawa naview status zake za mafumbo baadae nikaamua kuacha na kuangalia status zake tho naumia coz nilimpenda ila maisha ndio yametutenganisha uwezo wa kumuhudumia sasa mimi sina bado najitafuta, ni mwanamke mzuri lazima atapata mtu mwenye uwezo, G nilikupenda ila nimeamua nijitenge ili kuepusha mengi, haya maisha kama huna hela mapenzi weka pembeni. Am out.
 
Nimekuwa nikipitia changamoto ya kukosa usingizi, kutaka kujiua toka mwaka 2018 nikiwa chuo baada nikaanza kunywa madawa ya usingizi zaidi ya aina 15 bila kupona, nimeenda sehemu za maombezi pia ila bado haiponi.

Mwaka 2020 nilipata mchumba ambae nae mwaka huu kaenda JKT nimejikuta ninaishi kwa mawazo sana, maana huyu mwanamke nilikuwa nampenda sana.

Kiufupi kwa sasa nimekosa direction, maana pamoja na kusoma sina kazi, sipati usingizi na kuna roho ya kutaka kujiua inanisumbua kila siku.

Naombeni msaada.
Hiyo roho inayokujia dili nayo Mkuu

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Nimetibiwa Muhimbili miaka yote hyo amna kitu
Tafuta mkoa wenye ardhi nzuri ya kilimo uende huko upate walau ekari 3 uwe bize masaa yote na kazi za shamba. Uhakikishe unashiriki physically kiasi kwamba jioni uko hoi, lazima usingizi utakuja na baadae utavuna mazao na kupata pesa.
 
Nimekuwa nikipitia changamoto ya kukosa usingizi, kutaka kujiua toka mwaka 2018 nikiwa chuo baada nikaanza kunywa madawa ya usingizi zaidi ya aina 15 bila kupona, nimeenda sehemu za maombezi pia ila bado haiponi.

Mwaka 2020 nilipata mchumba ambae nae mwaka huu kaenda JKT nimejikuta ninaishi kwa mawazo sana, maana huyu mwanamke nilikuwa nampenda sana.

Kiufupi kwa sasa nimekosa direction, maana pamoja na kusoma sina kazi, sipati usingizi na kuna roho ya kutaka kujiua inanisumbua kila siku.

Naombeni msaada.
Hebu cheki na Chid Benz kwanza.
 
Kama uko dar tembelea sinza Mori Kuna ajent pale wa kazi za nje ya hii nchi anaitwa competitive manpower limited.

Ngoja nikutaftie namba zao kwa mdau kwnza. Kuna jamaa humuhm jf amepata mchongo hapo juzi juzi tu
Mkuu naiomba hiyo namba Tafadhali
 
Dah pole Sana mkuu, hali hiyo ni mbaya Sana Nina ushuhuda rafiki yangu alipata Hali kama iyo na sasa Iv dah inauma Sana amechanganyikiwa. wakati tunamaliza chuo kila mmoja alikuwa na matarajio makubwa Sana,binafsi sikurudi nyumban nilitafuta mkoa mwingine wa mbali sana, kijijini nikajichanganya na kilimo na biashara ndogo ndogo uku marafiki zangu Wakinibeza wao walirudi nyumban kusubiria Ajira, kifupi nilikula msoto haswaa lakini nilikaa kwenye mstari hapo baadae, kwa upande wao mambo yalikuwa tofauti Sana mategemeo Yao yakawa tofauti, ikafika mahali mawasiliano yalipotea nakuja kurudi nyumban kusalimia, nikasema niende na kwao maana ninapajua asee nilichokikuta dahh inauma Sana jamaa amechizika full na akuwahi kutumia madawa yeyote, nakushauri Hama sehemu uliyopo, tafuta Mishe yeyote ufanye, jiamini unaweza, mapenzi usiyapekipaumbele Sana, usikae peke yako Mda mrefu, usione aibu kujaribu fursa utakayoifikiria, uku ukiendele kutafuta Ajira, mwisho wa siku Mungu ndio mpaji, onyesha jitihada utafanikiwa.
 
Dah pole Sana mkuu, hali hiyo ni mbaya Sana Nina ushuhuda rafiki yangu alipata Hali kama iyo na sasa Iv dah inauma Sana amechanganyikiwa. wakati tunamaliza chuo kila mmoja alikuwa na matarajio makubwa Sana,binafsi sikurudi nyumban nilitafuta mkoa mwingine wa mbali sana, kijijini nikajichanganya na kilimo na biashara ndogo ndogo uku marafiki zangu Wakinibeza wao walirudi nyumban kusubiria Ajira, kifupi nilikula msoto haswaa lakini nilikaa kwenye mstari hapo baadae, kwa upande wao mambo yalikuwa tofauti Sana mategemeo Yao yakawa tofauti, ikafika mahali mawasiliano yalipotea nakuja kurudi nyumban kusalimia, nikasema niende na kwao maana ninapajua asee nilichokikuta dahh inauma Sana jamaa amechizika full na akuwahi kutumia madawa yeyote, nakushauri Hama sehemu uliyopo, tafuta Mishe yeyote ufanye, jiamini unaweza, mapenzi usiyapekipaumbele Sana, usikae peke yako Mda mrefu, usione aibu kujaribu fursa utakayoifikiria, uku ukiendele kutafuta Ajira, mwisho wa siku Mungu ndio mpaji, onyesha jitihad a utafanikiwa.
Best advice. Mtoa mada hukua hili... Hapo ulipo hama kwanza! Huko utakapoenda patakupush japo utaanza moja.
 
Pia badilisha ID hiyo sijui Mafanikio muda wote unawaza mafanikio kwani unadaiwa lazima ufanikiwe ? Chukulia maisha very simple ila unatakiwa upambane kila kitu utapata kwa wakati wake...
 
Ila ukiwa jobless au kipato kidogo jitahidi kutojihusisha na mapenzi kabisa.
Hata nyeto usipige, komaa kutafuta hata vibarua tu.

Kujihusisha na mambo ya ngono vitakuletea sonona zaidi.

Usilaumu watu kwa kufeli kwako, tathmini makosa na ulipokosea na utafute soln.

Sonona ni mbaya sana, faraja na furaha yako i ndani yako, usimtegemee mpenzi, ndgu au rafiki akupe furaha.

Mimi nilikua najitahidi nipate bundle tu, madem nikaachana nao kabisa na wala sikua natongoza kabisa(mpaka leo).

Mkuu usitegemee demu wako akupe furaha, jitafute wewe mwenyewe. Ridhika na ulichonacho, usitake kua kama fulani, jitafute.

Ulikosea wapi?? Rekebisha, muda unao, nguvu unazo, wao wana nini na wewe ushindwe.

Ni mwiko na marufuku kukata tamaa.
Kwa nini asipige nyeto mkuu?
 
Unahitaji kazi ambayo itakufanya kuwa busy mpaka ukose muda wa kufikiria about harming yourself,Mungu akujalie.
 
Pole mkuu nahitaji kukuandikia mengi on how you can overcome that challenge.

Check on me +255658124288 via WhatsApp then I will share with you A lot about negative emotions.

Naomba na MTU mwingine ambaye yupo na msongo Wa mawazo anicheki
KAMA upo Dar njoo pm nikupe namba ya daktari bingwa wa magonjwa ya akili,huyu jamaa atakusaidia Ila tu ,dawa ni bei kidogo kwenye maduka ya mtaani Kwa town bei ni rahisi Tu,ila utapona na kurudi sawa as per doctor instructions

Sent from my 21061119AG using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom