Msichana wa Kitanzania akipata mchumba na kufunga ndoa anajiona amepata degree (Hons)!

Msichana wa Kitanzania akipata mchumba na kufunga ndoa anajiona amepata degree (Hons)!

Hio status mama yake alikuwa nayo wakati unamuoa? 😂😂😂
Of course mama yake ni PhD holder, humu ndani nyie kila siku huwa mnapiga mikelele ati mabinti wamezidi kuwaomba pesa. Leo hii wazazi tunajitahidi ili mabinti zetu wasiwe tegemezi (status) mnapinga, tuwaeleweje?

Of course, haikubaliki kuoa mwanamke ambaye anakuzidi umri, kipato au ilimu. Hivyo wakati mwingine mnajihami tu
 
Mawazo haya yananitia uchungu sana!!!! Nina binti yangu (now 31 yrs) naona hili jambo linamfanya asianze PhD programme ati kila siku kwenda kusali. Inaniboa saaana ingawa sina la kufanya. Naamini kuolewa kupo na ukiolewa ukiwa na status ndiyo inakuwa bora zaidi au nakosea kama mzazi
Hivi kumbe wee ni kakijeba eehh????🤔🤔🤔🤔🤔!! 31 years dohh!!
 
Of course mama yake ni PhD holder, humu ndani nyie kila siku huwa mnapiga mikelele ati mabinti wamezidi kuwaomba pesa. Leo hii wazazi tunajitahidi ili mabinti zetu wasiwe tegemezi (status) mnapinga, tuwaeleweje?

Of course, haikubaliki kuoa mwanamke ambaye anakuzidi umri, kipato au ilimu. Hivyo wakati mwingine mnajihami tu
Kwahio umenipanga mzee. Amini kwamba mkubwa hapangwi.
 
tatizo zama hizi watu wana oana bila kupima UKIMWI mara 3 kama inavyo shauriwa, yaaani watu wanajuana leo baada siku chache wanaoana!!! maambukizi ya UKIMWI yanaenea. hatari kubwa.

UKIMWI bado ni ugonjwa hatari sana duniani.
 
tatizo zama hizi watu wana oana bila kupima UKIMWI mara 3 kama inavyo shauriwa, yaaani watu wanajuana leo baada siku chache wanaoana!!! maambukizi ya UKIMWI yanaenea. hatari kubwa.

UKIMWI bado ni ugonjwa hatari sana duniani.
Acha uphaler wewe ukimwi gonjwa la kawaida kabisa hilo
 
Mawazo haya yananitia uchungu sana!!!! Nina binti yangu (now 31 yrs) naona hili jambo linamfanya asianze PhD programme ati kila siku kwenda kusali. Inaniboa saaana ingawa sina la kufanya. Naamini kuolewa kupo na ukiolewa ukiwa na status ndiyo inakuwa bora zaidi au nakosea kama mzazi
Mleta mada yuko sahihi.
lakin wewe hauko sahihi sana.
Faida ziko pande mbili lakin anayekuwa amelamba karata dume ni ke.
Mwanamme anamiliki public parts lakin mwanamke anamiliki private parts. Itakaa hivyo until further notice and Father notices!
......ALWAYS NATURE PREVAILS!
 
Ningependa aolewe lakini asubiri kwanza amalize mambo muhimu ya maisha......kuoelewa sio maisha. Soma andiko langu lote utanielewa mkuu.
Hayo mambo muhimu ya maisha ni kama yapi tukitoa ndoa?! [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Maana nicheke kwanza.

Yaani ni sawa na kusema mtu aanze ujenzi kwanza kabla hajatafuta plot, swali linakuja ujenzi utafanyika wapi sasa?!

Mnawadanganya sana watoto wakike. Maisha ya Ndoa ni ya kitaasisi sio kitu kidogo cha kuamua tu kuanza muda wowote.

Ndio maana mila na desturi zetu za jamii ya mwafrika ukienda popote zilitambua hilo kwa kuwaandaa vijana katika umri wa balehe na mabinti wanapovunja ungo. Maana kuanzia pale ndio muda wa kuwaingiza katika ndoa waendelee nayo hadi utu uzima.

Umri unavyokwenda ndivyo akili inazidi kuhama na kuingiwa na kila aina ya uchafu wa dunia na kushindwa kushika misingi ya Ndoa.

Ndio maana leo kitu cha ajabu eti kuna mwanamke anaamini anaweza kuwa nje ya nyumba yake tokea saa 12 asubuhi hadi saa nne usiky halafu anaita yupo kwenye ndoa. Hapo unaishi kisela sio Ndoa.

Au unakuta kuna mwanamke ana amini kuwa ana uhuru au haki ya kulala na mwanaume nje ya ndoa yake na si tatizo.

Au atapuyanga tokea akiwa sekondari hadi chuo kisha atakapomaliza then atatokea mwanaume wa kumpenda na history yake la kulala na wanaume tofauti wakimkunja na kumpiga mashine na madudu yao ya yuyu ya size tofauti tofauti.

Haya na mengineyo ni matokeo ya kuwapotosha mabinti wasijue kuwa muda wao wa kuinvest katika ndoa ni umri kati ya miaka 16 hadi 25. Kuanzia 26 hadi 35 ni kukosa uelekeo sasa na 35 kwenda juu haina maana tena kwa mwanamke kuingia ndoani. Maana kuna mengi umepoteza.

Kama unabisha njia nzuri ni kujaribu kwa matendo kama umri bado.
 
- Sielewi kwa nini wanawake wanaongelewa sana, kulingana uwiano wa Ke na Me kwenye matokeo ya sensa, kama wanawake hawaolewi inamaanisha kuna wanaume hawajaoa. Thamani ya ndoa ipo kwa wote ME na KE. Mwanaume pia kama hana mke huonekana hana thamani bila kujali elimu, pesa wala umri.
Nadhani kuna mambo ambayo jamii ya sasa ni vema ikayaelewa. Hapa kuna asili ya maisha ya mwanadamu na kuna aina ya maisha tunayoishi sasa. Ni vema kuwe na balance.

Kwa nilichokiona, mwanamke anayesoma hadi kufika elimu ya juu, hajakatazwa kuolewa na wala si kwamba haiwezekani yeye kuolewa na akasoma vizuri tu na kumaliza elimu ya juu na siky ya graduation mumewe, watoto na familia wakaja kusheherekea nae. Haya yapo na tumewaona wanawake wa hivi.

Shida inaanza na mitazamo. Mabinti wanapokuwa shule wanakatazwa na wazazi kuwa na mahusiano ila je ni kweli huwa hawana mahusiano? Tena wanakuwa na mahusiano na wanaume hata sita. Wote hawa wanamla mwanamke mmoja.

Sasa wazazi hili wanaliona wanapiga kimya ila waanapiga kelele na kumtisha binti yao asiolewe huku akiendelea na mambo yake ya elimu, shida ipo wapi.

Kwann mnataka kuona ni sawa mtoto wa mtu wa kiume aoe binti ambaye huko chuo ameishi na kijana kinyumba kama mume na mke na wameachana baada ya kumaliza chuo. Hii imekaaje?

So nadhani muhimu sana kama jamii tulitazame hili upya kuwalinda mabinti zetu. Wakiwa ndani ya ndoa wanalinda heshima yao, kwakuwa na mume wake ambaye wataweza kuwa nae maisha yote lakini pia wataweza kutuliza vichwa wakiwa darasani wakijua kuwa wapo kwenye ndoa na wanatakiwa kuziheshimu.

Pia mfumo wa elimu upunguze miaka hii ya kusoma ni mingi sana. Miaka 7 primary, 6 sekondari,chuo maiam 3 kuendelea hii kwa mabinti inawaharibia sana.

Na tuongee ule ukweli. Wanapomaliza chuo ni wangapi wana ajiriwa na wakipata ajira mishahara huwa inatosha kuendesha maisha yao ya kila siku, maisha yenyewe wanafanya na nani sasa ?!

Wanaume hawana interest na mwanamke aliyekwenda shule sana sababu wengi huwa hawana uwezo wa kujishusha kuwa mke wa mtu kwa maana ya kusikilizana na mwanaume wake. Sio wote, wapo mabinti ni wastaarabu, wamesoma adabu ipo mbele hadi raha.

Tuna mengi ya kurekebisha katika jamii yetu especially katika eneo hili. Mabinti ndio ambao wapo katika wakati mgumu. Kijana atasoma, ata hangaika na ajira akikosa ataenda fanya biashara akija toboa hata ana miaka 35 kwenda juu ana uhakika wa kupata binti chini ya miaka 25 na wakayajenga maisha na utulivu ukawepo.

Hawa mabinti mnaowapotosha hadi wanakuja stukia wapo na miaka 30 wanatanga tanga tu, maisha hakuna, ajira hakuna , pesa ngumu, maisha gharama zipo juu, miili inazeeka na wengine masikini wameshazalishwa watoto wawili hivi wanaishia na nani?!

Nani atawasitiri hawa. Na mshawajaza akili za kimasikini kuwa akiwa na elimu kubwa maisha yake yatabadilika,atakuwa na kazi ya mshahara mzuri,ataishi kama wazungu, ataolewa na meneja wa benki akishamaliza shule. Atamudu maisha kwa urahisi. Je, hii ni kweli?!

Hivi maisha mnayachukuliaje kwa mfano?!
 
Back
Top Bottom