Mstaafu wa Jeshi atuhumiwa kuua kwa risasi kisa mgogoro wa mipaka

Mstaafu wa Jeshi atuhumiwa kuua kwa risasi kisa mgogoro wa mipaka

tupinge uuzwaji wa viwanja vya 20 kwa 20.. mara nyingi hivi ndio vinamadhara makubwa sana ya ugomvi.. sidhani kama case inakua the same kwenye viwanja vya kuanzia sqm 1000+..na mara nyingi hio unakuta mtu anakiwanja kikubwa ila anataka akikate apate vipande vingi bila kuweka mipaka vzuri.
mwisho wa siku mji ukikua wale waliouziwa viwanja wakija kuanza kujenga ndo anaona reality kiwanja chake kidogo..inaleta ugomvi huku aliewauzia keshasahau
 
Hadi akamiliki silaha alikuwa mtu mkubwa jeshini
Na ukubwa wake Sheria itamnyoosha tu,kule Hai Sabaya alimuamuru Captain mstaafu aliyekua anazingua mambo ya ardhi aachie hio ardhi au akizingua ashughulikiwe.Mzee akawa mpole ardhi ikarudi kwa wenyewe fasta tu.
 
Haya masuala ya mipaka ardhi ukiyachunguza kwa undani ni tamaa, upumbavu, ujinga, ubinafsi, wivu, uwelewa mdogo na roho mbaya tu kati ya mtu na mtu na wala hayahusiani na kazi, kabila, dini wala elimu ya mtu.

Kuna rafiki yangu mmoja wapo familia mbili jirani (mojawapo ni ya rafiki yangu) wamejenga wamefuatana lakini barabara ya kufika kwao inapita ubavuni kwenye kiwanja cha jirani yao ambaye ni kijana wa makamo tu ambaye ameenda shule vizuri na mkristo safi anatokea kanda ya Ziwa na mkewe anatokea kanda ya Kaskazini. Japo hizo familia mbili ndio zilizotangulia kujenga na kuhamia jamaa alipofika akajenga halafu akaweka ukuta kwenye usawa kabisa wa barabara. Jamaa ndani ya ukuta wake akaweka vyumba vya kupanga halafu akatoboa milango kwenye ukuta kwa hiyo mpangaji akifungua tu mlango kutoka nje yupo barabarani kabisa. Kama haitoshi akaongeza vijibaraza vya ngazi barabarani kiasi wakikaa nje gari ikipita inawabidi wainuke ili gari ipite. Barabara ilikuwa kubwa ya kupishana gari mbili sasa inapitisha gari moja tu hamna kupishana. Na ujinga wa kutamani kiwanjani chake kitanuke wakati ardhi haitanuki kajenga geti lake la kuingilia mwishoni kabisa mwa kiwanja matokeo anakuja kujenga kile kipaa kikawa kichekesho kimeingia kabisa barabarani ili kisigongwe na magari ikabidi akiinue juu kabisa kama mti wa mnazi.

Siku moja rafiki yangu alijaribu kumuuliza jirani yake kama anaona anachokifanya ni sahihi maana alikuwa ameweka tofali zake barabarani magari yakawa yanapita kwa shida. Jamaa akaja juu sana rafiki yangu akaachana naye sio kwa kumuogopa bali jama yangu ameshika sana dini na hapendi kabisa ugomvi. Na siku zote msemo wake ni kuwa ukitaka ushindi wa muda mfupi na laana ya muda mrefu basi dhulumu mtu ardhi hata hatua moja tu.

Kiukweli watu wengi wanaponunua hivi viwanja ndio uwezo wao kwa wakati huo. Lakini wakija kupata pesa zaidi baadaye badala ya kutumia akili wakanunue maeneo makubwa zaidi nje ya mji wanatamani eneo lile walipo liongezeke wakati ardhi haitanuki ndipo hapo sasa ugomvi wa mipaka na majirani unapoanzia.
 
tupinge uuzwaji wa viwanja vya 20 kwa 20.. mara nyingi hivi ndio vinamadhara makubwa sana ya ugomvi.. sidhani kama case inakua the same kwenye viwanja vya kuanzia sqm 1000+..na mara nyingi hio unakuta mtu anakiwanja kikubwa ila anataka akikate apate vipande vingi bila kuweka mipaka vzuri.
mwisho wa siku mji ukikua wale waliouziwa viwanja wakija kuanza kujenga ndo anaona reality kiwanja chake kidogo..inaleta ugomvi huku aliewauzia keshasahau
Ni ustaarabu tu. Watu wanadhulumiana mipaka kwenye viwanja vya sqm 1000 na wengine 20*20 wanaishi kwa amani. Ukipakana na hawa wanajeshi/askari au watu wasioenda shule ni shida sana. Nashukuru eneo nililopata sasa hivi kuna viwanja vya 20*20(wengi wananunua viwili au vitatu vinaunganishwa) ila watu wameenda shule,tena vijana wadogo mimi kaka yao kwa mbali sana.
 
masuala ya mipaka ni hatarii ndugu tu viwanja vya urithi wanaweza kuuana
 
Kupakana na askari yeyote wa jeshi la Tanzania ni changamoto kubwa sana. Wale wanao pakana nao nikiwemo mimi tulio wengi itakuwa tunajuta sana. Japo si wite, ila walio wengi wao wanajifanya wababe sana.
Asakari hata akiwa kwenye Ukoo wenu na hata kama hana pesa,bado atajifanya mbababee wa familia,achelewi kukutishia chuma au kukulaza lockup mkitofautiana kimtazamo wa kifamilia!!!
 
Asakari hata akiwa kwenye Ukoo wenu na hata kama hana pesa,bado atajifanya mbababee wa familia,achelewi kukutishia chuma au kukulaza lockup mkitofautiana kimtazamo wa kifamilia!!!
Unamsema mjomba etu mmoja hivi 😀😀😀😀😀😀
 
Ameua bila kukusudia atahukumiwa kifungo Cha nje ataendelea kukaa kwenye kiwanja chake
Hasara kwa marehemu
Alikusudia kuwa ndiyo maana akaenda ndani na kutoka na silaha! Labda uniambie Soja alifutwa lindoni akiwa na silahaa yake,hapo tunaweza kaa na kujadili kidogo!! Lakini mwisho wa siku kazi yote inabaki kwa Wasimamizi wetu wa Sheria kusimamia haki kwa kila moja!!!
 
Unajua kesi za jinai Tanzania zinavyokuwa...Ametumia silaha Kaka hapo na alikuwa Ndani utampata state attorney gani aitoe kwenye murder aiweke kwenye manslaughter!!!
Upelelzi kukamilika hapo ni Mwaka
Kuanza kusilikiza kesi miaka miwili
Ardhi Tanzania bado IPO kubwa Sana...Hapo alipo anajuta sana.
Leo hii akifa anaenda kuzikwa kwenye shamba la magereza...
Soja mzima kashindwa kujua kua kuna mabaraza na Mahakama za Aridhi kwa ajili ya migogoro ya Aridhi!!? Dah! Kweli na Mshukhuru sana Mdingi wangu kwa kunipa elimu na maarifa ya kuishi na Wanadamu wa kila aina!! RIP DAD!!!
 
Back
Top Bottom